Naomba mwenye vitabu na material mengine kwa kujifunzia ufundi magari na pikipiki anisaidie

Jitu Kabeja Diggala

Senior Member
Apr 12, 2015
164
182
Mambo vipi wakuu,

Jamaa yenu hapa ninayo shauku kubwa ya kujifunza kutengeneza magari pamoja na pikipiki kwani maisha niliyo nayo mara baada ya kutoka chuo hayasomeki hivo nimeona ni vema zaidi nikapata japo ufundi stadi ambao utaniwezesha kupata riziki ya kuishi wakuu.

Lengo langu ni kupata materials au source zozote zitakazoniwezesha kujifunza ufundi huo theoretically kwanza halafu baadae ndo nakuwa nasogea gereji napractice polepole mpaka kitakapoeleweka. Mwenye kuweza kunisaidia kwa hilo anakaribishwa sana wakuu

Asanteni.
 
kujifunza kutengeneza magari
Kutengeneza magari kwa ujumla wake itakuwa ni ndoto.

Gari ina mifumo mingi.

Kuwa specific unataka ubobee kwenye ujuzi wa mfumo upi wa gari:-
- Umeme
- Engine
etl

Sehemu sahihi ya kuanzia ni VETA au DIT au NIT, ila sio kwa huo utaratibu wa kuanza na theory, mafanikio itakuwa ni kidogo au hakuna kabisa, Ujuzi husika ni too practical, na sio kinadharia, Kumbuka wahitimu wa vyuo vikuu wanafundishwa kushika spana na mafundi/ vijana wenye ujuzi wengi wao hata chuo hawajafika.

Iwapo hauko tayari kwenda vyuo rasmi kupata huo ujuzi basi fanya tafiti na upate gereji kubwa inayojishughurisha na magari / piki piki, Ongea na wamiliki na watakupa utaratibu wao wa wewe kuanza kujifunza, Gereji hakuna maswala ya notice za kusima.
 
Piga uwa ni lazima uwende kwanza gereji ama chuo cha ufundi,kwenye ufundi kusoma vitabu bila vitendo(practical) jnatwanga maji kwenye kinu.
Afadhali uanze kwanza gereji au chuo kisha uanze kutafuta vitabu taratiibu kulingana na jinsi unajifunza.
 
Ingia google, search for the most popular books on the subject

Leta orodha hapa tutakusaidia kudownload
 
Mkuu Kama uko Sirius basi fanya hivi,

Tafuta geregi ya ufundi wa magari "MVM" kwa kuanzia Kisha fanya prack kwa miezi kazaa"Baada ya hapo utakuwa uko tayari kupiga short course ya Motor Vehicle Mechanic,M.V.M.
 
Back
Top Bottom