Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Aisee hongera mkuu ndo kitu nataka nijifunze pia nione utofauti japo najua nitachelewa kufika tofauti na basi!Nilisafiri mwaka 2001 kwa treni ya Tazara, nilienda kwa free pass , KUSAFIRI na Treni ni raha sana, aswaa ukate ticket ya first class, tulikula bia na wadada wa kizambia, tuli-Enjoy ile safari kwakweli
Kwa maelezo haya nishaiona sfr yangu vile itakuwa nashukuru Sana mkuu umefafanua vzr Sana Sana ubarikiwe na Imani na wengine wasojua wamepata kitu pia!Usafiri wa train ni usafiri ninaoupenda sana...ni usafiri wenye risk ndogo na wa uwakika ukilinganisha na bus.
Kuhusu train via TAZARA zipo za aina mbili.
1. Train ya mizigo
2. Train ya abiria
~ Train ya abiria zipo za aina mbili
1* Express train...hii ni train ya route ndefu safari yake huanzia Zambia to Dar,sifa ya train hii Ina speed,inasimama vituo muhimu tu,inamuinekano mzuri kwa ndani,inabeba mizigo kwa limit, pia nauli yake imechangamka kidogo...
Ina madaraja matatu.
First....ni kachumba chenye vitanda vinne au viwili vya kukunja na kukunjua na meza moja..ni daraja lililo karibu na sehemu ya vinywaji na chakula, system charging na feni ipo na vyoo vyake vipo vzur sana.
Ni daraja lenye Bei ya juu kuliko class zote,ukipanda daraja hili hutojutia safari yako.
Second class..ni daraja la kati kuna seat ambazo zpo comfortable (super seat) na zpo seat zengne zinafanana tu na third class,kila behewa Lina system charging moja...kila behewa Lina feni 6,vyoo vyake vipo poa.
Bei yake ya kawaida tu,kama utapanda second class kata ticket ya super seat hutojutia safari yako.
Third class...halina tofauti sana na second class. Na Bei yake ndogo kulinganisha na first na second.
2* Ordinary train....hii train huanzia mbeya to Dar,ni train ambayo huchukua muda mrefu ktk safari zake,husimama kila ktuo ata porini as long as kuna huduma maalumu inahitaji kufanyika.
Nayo Ina class tatu, first.. second..na third.
Nauli yake hupishana elfu 2 adi elfu 5 na express.
Ukipanda ordinary sikushauri ata kidogo upande third class.
Asante bujibujiTickets and Reservations | TAZARA
We advise you book your seat in advance at any of the following stations (Please note that reservation enquiries will only be attended to during working hours, i.e. 07:30 – 17:00hrs (CAT and EAT) from Monday to Friday): In Tanzania Dar es Salaam: Senior Passenger Services Officer: Mr Loningo...www.tazarasite.com
Pole sana mkuu ata hvyo ulijitahidi mana mi nawaza kutokula chochote nisije rudisha chenji SFR ya Kwanza Kwa huu usfr inabidi niwe mtulivuKna cku natka dar naenda moro ,nakumbuka nilikula tungi(pombe) njia nzima mpka kufika ifakara hoi hoi al manusura nipitilize kituo...ila nilichana mdomo cku iyo baada ya kuanguka kisa tungi, mbna nilikoma
kupanda treni Raha sana nilitumia usafiri huu Alhamis ilopita From Mngeta, Ifakara to Dar full raha yani Full kupombeka hutojutiaAsanteni kwa michango yenu familia mbarikiwe Sana tuombeane heri Tu nikifanikiwa ntawajulisha pia hapa hapa asanteni
Naona kama nachelewa mnanitamanisha Sana mana tangu nizaliwe ndo itakuwa mara yangu ya Kwanza kutumia usfr huo ila inaonekana watu wana enjoy gambe Sana mkuu!!kupanda treni Raha sana nilitumia usafiri huu Alhamis ilopita From Mngeta, Ifakara to Dar full raha yani Full kupombeka hutojutia
Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
KaribuAsante RFK
Kabsa, kuwa mtulivu aiseePole sana mkuu ata hvyo ulijitahidi mana mi nawaza kutokula chochote nisije rudisha chenji SFR ya Kwanza Kwa huu usfr inabidi niwe mtulivu
Accommodation kwenye treni au kwa mkoa wa Mbeya
Kwa mkoa mpenzi...Accommodation kwenye treni au kwa mkoa wa Mbeya
Oohh kwa Mbeya hotels nzuri jaribu Desderia, Tughimbe, Hills View, Peace of Mind, Mbeya Hotel na UsungiroKwa mkoa mpenzi...
Ila kama unajua train fare kwa chumba kizima cha first class naomba kujua.