Naomba msaada wenu wa haraka kuhusu NMB App

kiboboso

JF-Expert Member
Sep 17, 2013
9,174
12,268
Nilidownload app ya Nmb mobile account na nikafungua account bila kwenda bank, pesa nikawa naweka kama kawaida. Yaani nilikuwa nafanya kuhamisha hela zilizoko mpesa naweka NMB mobile account. Sasa leo asubuhi nikapita kwa wakala wa nmb ili nitoe tsh 200,000. Nimefanya huo muamala lakini maajabu pesa imetoka lakini sijapokea sms yoyote na wakala nae hajapata sms yoyote pia pesa nayo haijafika.

Nimejaribu kuwasiliana na NMB huduma kwa wateja kupitia njia ya simu nikawapa maelekezo yote, waliponichosha ni pale waliponiuliza number ya account.

Kiukweli mimi number ya account sina... Na sijui hiyo number ya account naipataje. Pia wakati najiunga na hiyo app hiyo number ya account sikupewa, nilikuwa natumia number ya simu kuingia.

NISAIDIENI PLEASE...
 
Kabla hatujakujibu na Sisi pia tunakuomba Msaada wa haya maneno yako ya 'Msahada' na 'nilidownload' je, ni maneno ya Kiswahili na yako sahihi?
Unajua Gentamycine...HIVI Kinachokushinda kuangalia content...ukamsaidia Kama Unaweza..unaanza kutoa vikasoro kwenye bandiko...kilikushinda Nini kupika kimya kimya..

Ndio nyie hata Jambo liwe zuri Vipi...mtakomaaa na kakosa kadogo na kuacha lile Jambo la msingi..

UPOPOMA wako Ni wakiwango Cha juu Sana.
 
Mkuu nakushauri kitu kimoja nenda tawi la nmb lililo karibu nawe wakuthibitishie Kama hio app ni yao au ni scammer wakisema yao Basi pesa yako iko salama maana utakuwa na authority ya kuwashtaki Ila Kama sio yao imekula kwako
 
Punguwani wewe. Mwenzio anauliza kitu cha msingi wewe unaleta upumbavu.
Alafu eti Lidoctor...Doctor gani JINGA NAMNA HII...Yaani jitu zima linaangalia vitu visivyo namaana.....Kuna vitu Sio material..unapotezea.
Huyu akiwa boss...atakomaa na wewe hujaweka koma...kwenye sentensi wakati ulivyopresent Ni nondo..

HUKO SHULE HUA MNASOMAGA NINI?
 
Unajua Gentamycine...HIVI Kinachokushinda kuangalia content...ukamsaidia Kama Unaweza..unaanza kutoa vikasoro kwenye bandiko...kilikushinda Nini kupika kimya kimya..

Ndio nyie hata Jambo liwe zuri Vipi...mtakomaaa na kakosa kadogo na kuacha lile Jambo la msingi..

UPOPOMA wako Ni wakiwango Cha juu Sana.
Jamaa huwa anajikuta sana,yaani anajiona mjuvi wa kila kitu,harafu huwa najaribu kuwaza umri wake namchukulia kama Dada wa miaka 17 ,kwa sababu unaweza kuta mtu kauliza hoja ya màana harafu analeta ujuaji wake wa nanjilinji,
 
Unajua Gentamycine...HIVI Kinachokushinda kuangalia content...ukamsaidia Kama Unaweza..unaanza kutoa vikasoro kwenye bandiko...kilikushinda Nini kupika kimya kimya..

Ndio nyie hata Jambo liwe zuri Vipi...mtakomaaa na kakosa kadogo na kuacha lile Jambo la msingi..

UPOPOMA wako Ni wakiwango Cha juu Sana.
Inanekana una Hasira sana na Mimi hapa JF na ukizipata nafasi kama hizi huwa unapenda Kuzitumia. Hivi 'Kumkosoa' Mtu tu ni Kosa Wewe Juha?
 
Mkuu nakushauri kitu kimoja nenda tawi la nmb lililo karibu nawe wakuthibitishie Kama hio app ni yao au ni scammer wakisema yao Basi pesa yako iko salama maana utakuwa na authority ya kuwashtaki Ila Kama sio yao imekula kwako
Unaweza kufungua account kwa kutumia app ya benki? Sijawahi kusikia hili jambo. Account ya benki siyo lazima uende benki na vitambulisho upewe na account number? Kuna uwezekano jamaa fedha zake zimepigwa na matapeli
 
Ndio mkuu.
Nenda bank.ndo msaada ulipo na uwaonyeshe app ulotumia
Unatakiwa ufungue acc ya bank kule halafu ndo uje ujisajili kwenye app kwa namba yako na namba ya acc yako ya bank ndipo uanze kutumia.
MF unatoa tigopesa kwenda bank kuna kipengele unajaza namba ya acc ya bank halafu ukituma pesa inaingia.
Na kutoa pia
 
Kama unaitaj account number mbona ni simple tu kwenye app
Kama ulitumia NMB MKONONI APP

account number yako ni namba iyo ya simu ulitumia

na utakua na uwezo wakupata massage endapo utakwenda kuregester namba iyo kwenye ATM

na zaidi kama ni account uliongeza kuna kipengele cha. More account upande wa juu kulia namba utaikuta uko na info zote

Au uchukue iyo apo inayoonekana kushoto kwenye UI home menu tu

Ila utaitajika kuenda benk kuboresha taarifa za account yako ikiwemo kupata na atm card
 
Unaweza kufungua account kwa kutumia app ya benki? Sijawahi kusikia hili jambo. Account ya benki siyo lazima uende benki na vitambulisho upewe na account number? Kuna uwezekano jamaa fedha zake zimepigwa na matapeli
Skuizi inawezekana ila ataitaj kwenda benk akipata mda kuboresha taarifa zake
 
Inanekana una Hasira sana na Mimi hapa JF na ukizipata nafasi kama hizi huwa unapenda Kuzitumia. Hivi 'Kumkosoa' Mtu tu ni Kosa Wewe Juha?
Sina hasira na wewe...nashangaa NI MTU WA AINA GANI...hivi mtu akileta bandiko anahitaji msaada..na Umeelewa alichouliza..kusahihisha Kama kaweka R badala ya L...ndo lengo la bandiko..umesoma bandiko kusaidia au kukosoa Uandishi?..

Ifike mahala ujue wapi kukosoa Kuna tija na wapi msaada unahitajika..?
Unaonekana Kuna skills unalack Kama mtu mzima.
 
Sina hasira na wewe...nashangaa NI MTU WA AINA GANI...hivi mtu akileta bandiko anahitaji msaada..na Umeelewa alichouliza..kusahihisha Kama kaweka R badala ya L...ndo lengo la bandiko..umesoma bandiko kusaidia au kukosoa Uandishi?..

Ifike mahala ujue wapi kukosoa Kuna tija na wapi msaada unahitajika..?
Unaonekana Kuna skills unalack Kama mtu mzima.
Skill ninayokosa labda ni ya 'Kukubandua' tu vizuri.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom