Naomba msaada wa tatizo la mwili kupigwa shoti

lossoJR

JF-Expert Member
Oct 11, 2012
2,711
2,382
Habari wakuu, nimekua na tatizo la kupigwa shoti mwilini hasa nishikapo materials tofauti(kasoro plastic) bt aluminium,chuma bt hata vitasa vya gari au gari yenyewe, hali hii hunitokea mara moja kwa muda husika, ila nikishika tena sipatwi na tatizo hilo, cha ajabu ikipita masaa kadhaa nikajisahau nikaegemea kitu kimoja wapo napigwa tena,sasa imekua shida.

NOTE; pindi nipatapo hali hii na nikawa napeana mkono na mwingine basi nae hupigwa shoti.

Msaada zaidi tafadhali.
 
Mwili wako utakuwa na electrons za ziada au kuna mazingira yanakusababishia kuwa na electrons za ziada. Unapaswa kufanyiwa uchunguzi maana ni hali ya kutatanisha kwa sababu kuondokana na umeme huo wa ziada ni rahisi na mazingira ya kila siku yanawezesha kuondokana na umeme wa ziada bila hata kujitambua sasa kinachofanya ukung'ang'anie sijui ni nini.
 
Kama unakaa jirani na mitambo ya kinyerezi I na kinyerezi II hiyo hali ni ya kawaida kwa utaalamu hiyo tunaita kreptomania, ni hali ya mwili kuwa na electrons kiwango sawa na waya wa live kusababisha amagamation kati ya mwili na waya, hasa kama huo waya ni high voltage/ high tension.

Unachotakiwa kufanya, Kama huna mpango wa kuhama kinyerezi hakikisha unajenga mahusiano chanya na plastiki, tilia mashaka kila kitu chenye material ya chuma.

BTW nipm for mo info.
 
Mimi nina hali inataka kufanana na yako lakini mimi si kwa kushika vitu hunitokea tu from no where nahisi mishipa ya shingo ma mikono inapgwa kishoti flan na ni mara moja moja yan inaweza nitokea mara moja kwa miezi miwili
 
Kama unakaa jirani na mitambo ya kinyerezi I na kinyerezi II hiyo hali ni ya kawaida kwa utaalamu hiyo tunaita kreptomania, ni hali ya mwili kuwa na electrons kiwango sawa na waya wa live kusababisha amagamation kati ya mwili na waya, hasa kama huo waya ni high voltage/ high tension....
Duuh we mkali
 
Mimi huwa napata joto flani linaanzia maeneo ya tumboni na linasafiri kwa kasi mpaka mabegani, likifika mabegani napata msisimko mpaka kutikisika mwili, nikishatikisika hilo joto huuacha mwili. Hali hii hunitokea karibu mara tatu kila siku
 
habari wakuu, nimekua na tatizo la kupigwa shoti mwilini hasa nishikapo materials tofauti(kasoro plastic) bt aluminium,chuma bt hata vitasa vya gari au gari yenyewe, hali hii hunitokea mara moja kwa muda husika,ila nikishika tena sipatwi na tatizo hilo, cha ajabu ikipita masaa kadhaa nikajisahau nikaegemea kitu kimoja wapo napigwa tena,sasa imekua shida,
NOTE; pindi nipatapo hali hii na nikawa napeana mkono na mwingine basi nae hupigwa shoti.
Msaada zaidi tafadhali.
Naomba uhame Kinyerezi tafadhari.
 
Mkuu umejaribu kushika umeme uone kitatokea nini?!

Isije Kuwa umeukalia utajiri bure.
 
huwa inatokea mara moja moja ila hasa nikienda kijijini niliko zaliwa Sijui kwanini....
 
Watu wanafanya utani, sijapenda !
Kifupi mimi pia ni shida hiyo, haswa mlango wa gari
 
Mimi ikiwa wakati wa usiku
Nikigusa na mtu ngozi kwa ngozi basi hapo kuna nahisi shoti

Bado najifanyia uchunguzi maana ni miaka miwili sasa tangu nianze uchunguzi hii nigundue mwenyewe endapo kama mwili wangu utaweza kuwasha hata kurunzi.
 
Back
Top Bottom