Naomba msaada wa tatizo la kikwapa

Biashara Mtaji

JF-Expert Member
Aug 19, 2016
324
288
Nina umri wa miaka 23 sikuwahi kuwa na tatizo hili katika makuzi yangu huu ni mwezi wa tatu nasumbuliwa na tatizo hii, Kama ni usafi ninajitahidi kwani mpaka kwa siku nabadilisha na kuoga Mara 2 .

Msaada kwa jukwaa hili na wana JF kwa ujumla member wote

1. Je nifanyeje kuepukana na hali hii
2. Kuna dawa au ndia ya kutoa hii
3. Kwa yeyote mwenye ufumbuzi please
 
Kwa haraka haraka fanya mazoezi ufungue hizo tezi,pia jitahidi kuvaa nguo za pamba kipindi cha jua na joto kali
Ahsante sana mkuu kwa ushuri wako, Mazoezi nafanya na huwa muda mwingi nikiwa nyumbani huwa kifua wazi, sema hapo kwenye nguo ngoja niingie kwenye soko la mitumba pamba mwanzo mwisho
 
Pole sana kijana mwenzangu, fanya hv kabla ya kuoga jisugue na majivu weka maji kidogoo then jisugue makwapani kwa sec 30 mpka 45 au unaweza tumia limao kujisugilia kwenye kwapa. Baada ya hapo pakaa deodarant unaweza tumia ya nivea for men na products nyingine. Hakika tatizo lako linaweza kuisha au kupungua kwa kiasi kikubwa.
 
tumia deodorant isiyo na manukato kabisa, zipo ziko kama maziwa ziko cool hazinukii ni nzuri sana.
 
Pole sana kijana mwenzangu, fanya hv kabla ya kuoga jisugue na majivu weka maji kidogoo then jisugue makwapani kwa sec 30 mpka 45 au unaweza tumia limao kujisugilia kwenye kwapa. Baada ya hapo pakaa deodarant unaweza tumia ya nivea for men na products nyingine. Hakika tatizo lako linaweza kuisha au kupungua kwa kiasi kikubwa.
Mkuu ahsante sana hiyo Nivea ndio kuna mtu pia kaniambia nitumie na je unaweza pia kutumia zote pamoja na Deodorants?
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom