Samcezar
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 13,096
- 22,627
Hili ndio tatizo la watoto wa kike siku hizi. Wanaume wasio na malengo na ninyi mnahangaika nao..... Ila ambao wana malengo na ninyi mnawaona kero au hawana hadhi ya kuwa na nyinyi.Toka tunakutana alikua open sana kuongea masuala ya ajira ajira, japo hasemi direct mpaka nikawa nishamsoma shida ni nini na nikawa nafanya tu kumpa moyo na kubadilisha mada ili asiwe na mawazo.
Kuna muda alikua ndio mood ina change namuambia haupo sawa leo anajibu ndio, namuelewesha pia apunguze kuwaza japo sio rahisi as wanaume ndo mnakuwaga na stress mara 100 zaidi kuliko sisi wanawake.
Saivi ndo naona mood off kabisa.
Sishangai kwann idadi ya Ma'single mother inaongezeka ni kwasababu watoto wa kike the more mnapewa uhuru wa kufanya maamuzi binafsi na kuelimishwa ndio mnazidi kuwa vilaza wa kufiriki na kutumia hekima.
Wewe hapo nikikuuliza unachosubiria muujiza gani utokee utanambia?!
Hapo unasubiri akupe ujauzito halafu akupe makavu live kuwa hakuwa na time na wewe bali ulimlazimisha kuwa na wewe, halafu uanze kulaumu kuwa wanaume hawana mapenzi ya kweli..... NO.... Ni wewe hautumii akili....
Toka hapo kwa huyo jamaa achana nae.... Vijana wanaotafuta wasichana wa kufanya nao maisha wapo kibao.... Mwanamke hauna jukumu la kuchagua mwanaume bali mwanaume ndie anachagua mwanamke. Ikitokea umebahatika aliyekuchagua na wewe umempenda then u are lucky....
Ikitokea unaevutiwa nae hajavutiwa na wewe bali anakutumia then usipoteze muda shuka kituo kinachofuatia usubiri basi lingine.
Hapo unapoteza muda.... Miaka 27 unaleta habari za it might be you....?! Acha uzembe wewe dada..... Nenda katafute mwanaume achana na mtu ambaye ameshakuonyesha fungu lako ni la kukosa..... Wewe bado unatoa toa macho kama nyumbu anasubiria mamba amrukie ziwani wakati wa kunywa maji.
Achana na huyo mtu.... Tuliza kichwa tafuta mwingine..... Achana na huyo mtu.... Achana na huyo mtu.... Umri umekwenda, miaka 27 ni mwanamke mkubwa sio binti mtoto....