Naomba msaada wa maelekezo kwa waliowahi kusafiri nje ya nchi au kwa yeyote anayefahamu

euca

JF-Expert Member
Apr 6, 2015
3,734
4,075
Habari za asubuhi wana jamiiforums

Bila kupoteza muda ni kwamba nina sister wangu huwa anasafiri kwenda southafrica na akifika huko huwa anakaa kwa miezi mitatu au chini ya hapo but mwezi wa 9 alisafiri hadi huko na akawa huko mpaka mwezi huu tarehe 20. Hivyo alivyofika hapo uwanjani wakati anakuja bongo kwenye ofisi za uhamiaji baada ya kutoa passport ikapigwa mhuri na akapewa barua au form ambayo nimeweka chini hapo

Mimi na yeye hatupo vizuri kwenye hiyo lugha ya malikia lakini nahisi kama anakosa fulani. Kwa yeyote anaelewa au aliyewahi kupatwa na issue kama hyo anipe maelekezo kuhusu hiyo form au barua na kitu gani kinapaswa kufanyika maana yeye ni mtu wa kwenda sana huko south.
Capture%2B_2019-12-27-08-46-52.jpeg
Capture%2B_2019-12-27-08-49-38.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sidhani kama mtu atakaeweza kusoma hayo maandishi. Tafadhali piga tena picha vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Muwe mnakula samaki achaneni na matembele...

Na joke mkuu.

Ila kwa ufupi mdada alizidisha siku za kukaa SA tofauti na alizopewa...hiyo barua imempiga ban kuingia SA hadi tarehe 20 December 2020..hivyo kuanzia tarehe 21 anaweza akaingia.
 
Dada yako amezidisha siku za kukaa SA kwa siku moja, hivyo amepewa adhabu ya kutoingia SA mpaka tarehe 20-12-2020.

Ila kama anahisi ameonewa, anayo fursa ya kukata rufaa kwa director general wa Immigration au waziri wa mambo huyo kule SA
 
Sasa nn kifanyike ili arudi kabla ya huo muda maana ni mbaali sana huko 20 Dec 2020?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo ni nchi ya watu kama mmezoea uswahiliswahili hapo mtakuwa mmekwama! Hakuna namna, dawa ni kutii maagizo tu! Ameambiwa anaweza kukata rufaa, sasa aangalie kama anaweza kukata rufaa!
 
Mambo gani hayo ndugu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Alitakiwa ajue ame overstay...hapo angeweza kwenda na kujisalimisha angelipa pesa hati yake ikawa safi.

Kama anaweza abadili hati na akiweza atoe herufi kwenye jina kama haitaathiri chochote kwenye maisha yake. Mfano anaitwa Fatma anaweza akaandika Fatima. Hii inategemea kama waliweka kila kitu kwenye system.

Ila muda mwingi Wasouth ni wazembe hawaangalii ukienda na pass mpya unapita tu.
 
Alitakiwa ajue ame overstay...hapo angeweza kwenda na kujisalimisha angelipa pesa hati yake ikawa safi.

Kama anaweza abadili hati na akiweza atoe herufi kwenye jina kama haitaathiri chochote kwenye maisha yake. Mfano anaitwa Fatma anaweza akaandika Fatima. Hii inategemea kama waliweka kila kitu kwenye system.

Ila muda mwingi Wasouth ni wazembe hawaangalii ukienda na pass mpya unapita tu.
Lakn mbona kwenye hati yake anasema amegongewaa ule muhuri wa kawaida ambao kila akisafiri huwa unagongwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakn mbona kwenye hati yake anasema amegongewaa ule muhuri wa kawaida ambao kila akisafiri huwa unagongwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo wamerecord sasa... si jina lake lipo kwenye system (computer) siku anaingia wanalitafuta watakutana na ban ya kutokuingia.

Anyway nisiwe kama afisa wa SA...ila nimeona watu walioverstay wanafanya hivyo nilivyoeleza hapo juu.

Kama nilivyosema inategemea na mambo mengi. Anafanya nini? Anaingia mara ngapi kwa mwaka? Kuna shughuli haziwezi kukuruhusu uingie kimaghumashi ila zingine zinaruhusu. Zingine haziwezi ruhusu ubadili hata herufi kwenye hati.

Kila la kheri hiyo rufaa wala usiifikirie maana kwanza ishapita na utaulizwa maswali mengi utakayoshindwa kuyajibu.
 
Ukizidisha siku za kukaa ukala burn....km unataka kurudi mapema ...lipa zile siku ulizokuwa umezidisha !! Nenda ofice za imagration

Pia pasport yake inawezekana aliomba ya utalii ambayo huwa inakuwa fixed days

Km anafanya kule ....ambatanishe na work permit ili imagration offisor ambadilishie pasport yake asiwe anakula burn

Sent using i phone x
 
Ukizidisha siku za kukaa ukala burn....km unataka kurudi mapema ...lipa zile siku ulizokuwa umezidisha !! Nenda ofice za imagration

Pia pasport yake inawezekana aliomba ya utalii ambayo huwa inakuwa fixed days

Km anafanya kule ....ambatanishe na work permit ili imagration offisor ambadilishie pasport yake asiwe anakula burn

Sent using i phone x
Haujaeleweka kabisa mzee../mama/baba.

Nimeelewa tu kama umezidisha nenda kalipe siku ambazo ulizidisha. Lakini wameshampa barua ya ban na yupo Tz kwasasa ataendaje kulipa ofisi za SA?
 
Nadhani waliochangia hapo juu washakueleza tatizo.Sasa kwa kifupi tu nenda ubalozi wa South Africa watakusiidia .

Sent using Damu ya Yesu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom