Naomba msaada wa kuelekezwa ni wapi naweza kupata HDD SATA CABLE

Nina wasi wasi na huu ujanja wakuunganisha alioshauri pamjela kwasababu

kwa uelewa wangu Data cable ikikatika haiungiki (sijui kama nipo sahihi) na kama

ukiunganisha hutoweza pata Data ila ule waya/cable utapitisha umeme tu.

Nimejaribu mara kadhaa kuunganisha USB za simu zinazo support data read

ila nikiunganisha simu inachaji tu ila ule waya hauwezi tena kusoma data.

Hii nadhani hata kwenye TV ule waya wakutoka kwenye dish to decoder huwezi unganisha

na kama ukiunganisha Tatizo la signal kupotea halitoisha,ndio mana Dish waya wake

kutoka juu mpk kwenye decoder huwa ni direct,kampuni za ving'amuzi kwa kulijua hilo

wanatoa nyaya refu ili kuepusha usumbufu wa kuunganisha waya,Tukirudi kwenye case

yetu ya Kuunga SATA CABLE na ika support data hilo sina uhakika nalo labda Chief-Mkwawa

unisaidie hapo kama linawezekana au lah,maana mimi kuunga naungaga Power cable tu na si Data cable.
 
Chief-Mkwawa kuna mashine moja nimeichukua motherboard yake ina SATA port mbili tu

ila nyaya za power zipo 3 maana yake hapa ilipo nmeweka Hard Disk mbili,(sata zimeisha)

hii power cable iliyobaki imekosa SATA cable,ambayo nilikua nataka hii sata ya tatu niunganishe

DVD/CD ROM sasa ktk kufikiria nmewaza nikaona hapa nahitajika kutafuta SATA SPLITTER

Nmetafuta k.koo kona zote nimekosa hii cable,nadhani unaifahamu ni kama hiii👇

View attachment 1484137

Swali langu ni kwamba chief,Hii cable naweza ipata kwa hapa au mpk niagize?

Na je ninachokifikiria niko sawa au itakua kazi bure,maana motherboard ina 2sata port

mashine ninayotaka iongezea sata cable ni hii HP i3-3220,point yangu ni kwamba

nataka mashine ifungwe Hard Disk Mbili + 1 DVD ROM,tofauti na sasa nmefunga

Hard Disk tu ila MLANGO upo umekaa tu umekosa cable,Naomba ushauri wako Boss!!
Hizi cable zipo nyingi sana used, nenda kwa mafundi wa computer mjini au mitaani, au wauza scraper za vifaa vya computer pale K/Koo karibu na mtaa wa Uhuru round about.
Au Samora Avenue Posta karibu na Computronics, au ukitoka Samora unaenda RITA karibu na Bookshop hapo zipo kibao kwa mafundi.
 
pamjela
Chief-Mkwawa

waya ninaouzungumzia ni huu,kwenye picha nilikosea kumbe

ule ulikua power,mimi nataka huu wa sata (data) wa aina hii

Screenshot_1.png
 
Hizi cable zipo nyingi sana used, nenda kwa mafundi wa computer mjini au mitaani, au wauza scraper za vifaa vya computer pale K/Koo karibu na mtaa wa Uhuru round about.
Au Samora Avenue Posta karibu na Computronics, au ukitoka Samora unaenda RITA karibu na Bookshop hapo zipo kibao kwa mafundi.
Chief alinielekeza na wewe pia unanielekeza tena Asante boss

kesho naingia town ntazitafuta maeneo hayo,asante kwa msaada.
 
Chief nimekosa huu waya Titicomb ndugu yangu nmezunguka sana kutafuta huu waya nmeukosa kabisa,sasa nilikua nina swali kwako Chief-Mkwawa katika zunguka zangu huko

nimekutana na case ya Hard Disk kubwa hizi za ndani ya mashine hiyo case ni kama inavyoonekana kwenye picha,hii picha nmeichukua online ila ndio case hii hii niliykutana nayo town

SATA-Hard-Case.jpg


kwa sababu lengo langu ni kupata waya wa sata,nimeona ile harddisk iliyo ndani ya mashine niinunulie case ikae nnje then ule waya wa sata wa ndani ya mashine niurudshe kwenye DVD ROM.

swali langu ni: Hii case nataka weka ndani HDD ya 4TB lakini nimesoma juu ya case nmeona speed ya port ni 2.0 je hii Case itasoma Data vizuri bila tatizo? speed yake ya kupokea data itakua nzuri kama ilivyokua ndani ya computer?

Je hii case ina madhara yyte katika Hard Disk endapo nitaitumia? nisije ua Hard disk kwa uzembe,maana naogopa ogopa,nilishaua 6TB nakumbuka ilikua bado kidogo nife ile siku (NIMEKOMA SITAMANI ILE MOMENT IJIRUDIE)

kabla ya kwenda fata hii case kuna nini cha kuzingatia kabla sijanunua?

pamjela mawazo yako ktk hili mkuu.
 
huu waya @Titicomb ndugu yangu nmezunguka sana kutafuta huu waya nmeukosa kabisa
Kuna jamaa walikuwa karibu na KVD wanaitwa something Princess ... sikumbuki jina vizuri. Ni duka la jumla na rejareja vitu vya ICT.
Sina hakika kama bado wapo, hao jamaa kila cable au kitu chochote cha mambo ya computer unaweza pata hapo. Hii cable watakuwa nayo tu, ukikosa nenda hapo KVD nao wanaweza kuwa nayo .

Wapo karibu sana na makutano ya Makunganya Street na Mkwepu Street, mlango wa pili au wa tatu toka kwenye kona fuata Makunganya Street kama unaenda India Street. Jamaa wanatazama Puma Petrol Station (BP) iliyo nyuma ya Ext Telecom Building. Ukitoka duka lao unapita mlango mmoja unafika KVD.
Kuna machinga wanapanga nguo hasa trouser jirani yake. Ukitoka RITA vuka kabisa roundabout ya Mkwepu/Makunganya.
 
Kuna jamaa walikuwa karibu na KVD wanaitwa something Princess ... sikumbuki jina vizuri. Ni duka la jumla na rejareja vitu vya ICT.
Sina hakika kama bado wapo, hao jamaa kila cable au kitu chochote cha mambo ya computer unaweza pata hapo. Hii cable watakuwa nayo tu, ukikosa nenda hapo KVD nao wanaweza kuwa nayo .

Wapo karibu sana na makutano ya Makunganya Street na Mkwepu Street, mlango wa pili au wa tatu toka kwenye kona fuata Makunganya Street kama unaenda India Street. Jamaa wanatazama Puma Petrol Station (BP) iliyo nyuma ya Ext Telecom Building. Ukitoka duka lao unapita mlango mmoja unafika KVD.
Kuna machinga wanapanga nguo hasa trouser jirani yake. Ukitoka RITA vuka kabisa roundabout ya Mkwepu/Makunganya.
CONTROLA check duka la princess hapo kwenye picha ya ramani chini.
Princess-Shop.PNG
 
Chief nimekosa huu waya Titicomb ndugu yangu nmezunguka sana kutafuta huu waya nmeukosa kabisa,sasa nilikua nina swali kwako Chief-Mkwawa katika zunguka zangu huko

nimekutana na case ya Hard Disk kubwa hizi za ndani ya mashine hiyo case ni kama inavyoonekana kwenye picha,hii picha nmeichukua online ila ndio case hii hii niliykutana nayo town

View attachment 1496883

kwa sababu lengo langu ni kupata waya wa sata,nimeona ile harddisk iliyo ndani ya mashine niinunulie case ikae nnje then ule waya wa sata wa ndani ya mashine niurudshe kwenye DVD ROM.

swali langu ni: Hii case nataka weka ndani HDD ya 4TB lakini nimesoma juu ya case nmeona speed ya port ni 2.0 je hii Case itasoma Data vizuri bila tatizo? speed yake ya kupokea data itakua nzuri kama ilivyokua ndani ya computer?

Je hii case ina madhara yyte katika Hard Disk endapo nitaitumia? nisije ua Hard disk kwa uzembe,maana naogopa ogopa,nilishaua 6TB nakumbuka ilikua bado kidogo nife ile siku (NIMEKOMA SITAMANI ILE MOMENT IJIRUDIE)

kabla ya kwenda fata hii case kuna nini cha kuzingatia kabla sijanunua?

pamjela mawazo yako ktk hili mkuu.
kwa ilivyoandikwa hapo juu na huo waya wa nje hio ni zile hard disk kubwa za 3.5 inch, sababu zinatumia umeme mwingi ndio maana zina external power supply.

kusoma data itasoma ila speed haziwezi kuwa sawa, port ya ndani ni sata ambayo inapitisha data hadi 6gbps usb 2.0 inaweza pitisha labda around 500mbps

na hdd ikishakaa nje mkuu kuilinda inakuwa ngumu sana, HDD zinadumu muda mrefu ila pia zinakuwa dhaifu sana ikipata mtikisiko mkubwa kama vile ukiidondosha.

unaweza piga picha ya motherboard ukifungua case?
 
kwa ilivyoandikwa hapo juu na huo waya wa nje hio ni zile hard disk kubwa za 3.5 inch, sababu zinatumia umeme mwingi ndio maana zina external power supply.

kusoma data itasoma ila speed haziwezi kuwa sawa, port ya ndani ni sata ambayo inapitisha data hadi 6gbps usb 2.0 inaweza pitisha labda around 500mbps

na hdd ikishakaa nje mkuu kuilinda inakuwa ngumu sana, HDD zinadumu muda mrefu ila pia zinakuwa dhaifu sana ikipata mtikisiko mkubwa kama vile ukiidondosha.

unaweza piga picha ya motherboard ukifungua case?
Kuhusu kudondosha mkuu nina uhakika na hili 81% nipo salama,ila hofu yangu labda hdd ikikaa kwenye case uhai wake unapungua kuliko ikikaa ndani ya mashine,hapo ndio nina wasi wasi napo.

kuhusu speed Chief unasema speed itakua sawa tu na kama hdd ingekua ndani?

unaweza piga picha ya motherboard ukifungua case?

Hii picha ipi unamaanisha chief? motherboard ya hiyo HP inayonisumbua au case ya hiyo ex.hdd?
 
Kuhusu kudondosha mkuu nina uhakika na hili 81% nipo salama,ila hofu yangu labda hdd ikikaa kwenye case uhai wake unapungua kuliko ikikaa ndani ya mashine,hapo ndio nina wasi wasi napo.

kuhusu speed Chief unasema speed itakua sawa tu na kama hdd ingekua ndani?



Hii picha ipi unamaanisha chief? motherboard ya hiyo HP inayonisumbua au case ya hiyo ex.hdd?
Motherboard tuangalie arrangement yake, au weka full model ya pc niangalie motherboard online.

Na Hio HDD itapungua speed, ila kama sio Main HDD haina neno.
 
chief ni hii hapa

HP COMPAQ PRO 4300 SFF
pdf ya manual
http://h10032.www1.hp.com/ctg/Manual/c03550774

seems mkuu hio njia ya kutumia hdd ya nje sio mbaya, haka ka desktop kako full packed hakuna hata nafasi ndani.

kuna idea nyengine nimeipata ya port ya 3 ambayo hutumika kama multimedia reader, angalia huu mchoro wa motherboard yako
mobo.PNG

hio namba 4 ni kwa ajili ya card reader, ambayo inakaa chini ya mlango wa cd, na kutokezea nje kwa ajili ya kuchomeka vitu kama memory card, ila zipo card reader zinazosoma hdd ndogo za laptop kama hivi
HTB1PPk1X.LrK1Rjy1zbq6AenFXae.jpg

hio waya wake unaingia kwenye 4 kwenye picha ya motherboard sio cable ya sata, inamaana kwa njia hii unaweza pata extra hdd.

naiona online hapa dola 5 inauzwa sijajua kama uhuru kwenye mitumba pale unaweza kuipata.

uzuri wa njia hii hdd pia unachomeka na kuchomoa kama cd.
 

Attachments

  • 1593950639674.png
    1593950639674.png
    24.3 KB · Views: 4
pdf ya manual
http://h10032.www1.hp.com/ctg/Manual/c03550774

seems mkuu hio njia ya kutumia hdd ya nje sio mbaya, haka ka desktop kako full packed hakuna hata nafasi ndani.

kuna idea nyengine nimeipata ya port ya 3 ambayo hutumika kama multimedia reader, angalia huu mchoro wa motherboard yako
View attachment 1498293
hio namba 4 ni kwa ajili ya card reader, ambayo inakaa chini ya mlango wa cd, na kutokezea nje kwa ajili ya kuchomeka vitu kama memory card, ila zipo card reader zinazosoma hdd ndogo za laptop kama hivi
HTB1PPk1X.LrK1Rjy1zbq6AenFXae.jpg

hio waya wake unaingia kwenye 4 kwenye picha ya motherboard sio cable ya sata, inamaana kwa njia hii unaweza pata extra hdd.

naiona online hapa dola 5 inauzwa sijajua kama uhuru kwenye mitumba pale unaweza kuipata.

uzuri wa njia hii hdd pia unachomeka na kuchomoa kama cd.
Nashukuru chief,acha nikienda kwenye hii mashine nikaikague tena

kama nitaona nitafurahi sana kwani kuna kitu umenifungua hapa nilikua

hata sijui kama kuna sehemu ya namna hiyo,Acha nifate kwanza hii ext.case.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom