omboklo
Member
- Mar 9, 2020
- 69
- 86
Habari za majukumu wakuu, natumai tunaendelea kuchukua tahadhari zote ili kujikinga na janga hili la corona.
Ningependa kuelewa sheria inaweza kufanyaje kazi katika jambo hili lililoweza kumkabili mzazi wangu.
Ilikua mwaka 2018 mwishoni baba yangu alipata wazo kutoka kwa binamu yangu kuwa wafungue Chuo cha Udereva na kwa namna alivyoelezewa ilimpa hamasa sana ya kuinvest pesa zake akiamini kua ni ndani ya miezi miwili pesa zake alizotoa zitakua zimerudi na wataanza kutengeneza faida, katika kipindi hiki chote hakuwahi kutushirikisha watoto wake tumekua tukipata taarifa tu kupitia kwa mama yetu.
Taratibu za kusajili zilianza na kipindi chote yeye alikua akituma pesa kwa binamu yangu ili aanze michakato, alifanikiwa kukamilisha kwa koasi kikubwa na mwaka 2019 mwezi wa pili chuo kilianza kutoa masomo mambo yalikuwa vizuri na mawasiliano yalikua mazuri ila ndani ya mwezi mmoja hali ilibadilika baada ya pesa kutokuoneka nikimaanisha kua kazi inafanyika ila pesa zilikua zikiingia kwenye akaunti ya huyo binamu yangu.
Baba aliweza kuomba kujua hesabu na ikiwezekana pesa iwekwe kwenye akaunti ya kampuni lakini jambo hilo halikuwezekana ulitokea mvutano mkubwa kiasi kwamba ndugu waliingia kusuluhisha lakini halikuwezekana jambo lolote na hadi leo ni mwaka sasa umepita mzee hajawahi pata return yoyote kutoka kwa hiyo biashara na hajui namna inavyoendelea.
NB: katika usajil binamu alitumia jina lake kwahiyo nyaraka zote zinamuonesha yeye ndio mmiliki ingawaje pesa zilitoka kwa baba.
Ninapenda kujua je ni namna gani sheria inaweza kutusaidia ili tuweze angalau kurudisha pesa hizo zilizopotea (ushaidi uliopo ni slip za benki ambazo alikua akimuwekea pesa benki kwa ajili ya kuanzisha hiyo kazi).
Natanguliza shukrani.
Ningependa kuelewa sheria inaweza kufanyaje kazi katika jambo hili lililoweza kumkabili mzazi wangu.
Ilikua mwaka 2018 mwishoni baba yangu alipata wazo kutoka kwa binamu yangu kuwa wafungue Chuo cha Udereva na kwa namna alivyoelezewa ilimpa hamasa sana ya kuinvest pesa zake akiamini kua ni ndani ya miezi miwili pesa zake alizotoa zitakua zimerudi na wataanza kutengeneza faida, katika kipindi hiki chote hakuwahi kutushirikisha watoto wake tumekua tukipata taarifa tu kupitia kwa mama yetu.
Taratibu za kusajili zilianza na kipindi chote yeye alikua akituma pesa kwa binamu yangu ili aanze michakato, alifanikiwa kukamilisha kwa koasi kikubwa na mwaka 2019 mwezi wa pili chuo kilianza kutoa masomo mambo yalikuwa vizuri na mawasiliano yalikua mazuri ila ndani ya mwezi mmoja hali ilibadilika baada ya pesa kutokuoneka nikimaanisha kua kazi inafanyika ila pesa zilikua zikiingia kwenye akaunti ya huyo binamu yangu.
Baba aliweza kuomba kujua hesabu na ikiwezekana pesa iwekwe kwenye akaunti ya kampuni lakini jambo hilo halikuwezekana ulitokea mvutano mkubwa kiasi kwamba ndugu waliingia kusuluhisha lakini halikuwezekana jambo lolote na hadi leo ni mwaka sasa umepita mzee hajawahi pata return yoyote kutoka kwa hiyo biashara na hajui namna inavyoendelea.
NB: katika usajil binamu alitumia jina lake kwahiyo nyaraka zote zinamuonesha yeye ndio mmiliki ingawaje pesa zilitoka kwa baba.
Ninapenda kujua je ni namna gani sheria inaweza kutusaidia ili tuweze angalau kurudisha pesa hizo zilizopotea (ushaidi uliopo ni slip za benki ambazo alikua akimuwekea pesa benki kwa ajili ya kuanzisha hiyo kazi).
Natanguliza shukrani.