Mfahamu mdudu kunguni (bedbugs) na jinsi ya kumuangamiza

Mkuu mi sijawah kuwa hata na nzi wala mbu geto kwangu wala mende, na nilikua bishoo ila najua kuna mpuuzi mmoja tu alikuja nao tuu maana siwez kujua ntawazalishaje mwenyewe na niliishi home fresh tuu tangu nazaliwa ndo nije kuwa nao ukubwani, theory ya uchafu ni uongo, maana nakumbuka utotoni sikuwa msafi, na boarding nimesoma sijawaona, na chuo hosteli sijawaona ndo nimekuja kuwaona baada ya kupanga uswazi na kukaribisha washkaji tu wanachill wanacheki muvi nini wanaenjoy mara haaaooo,

Sent from my TECNO W1 using JamiiForums mobile app
Soma vizuri mkuu nilichoandika, unaweza ukawa msafi ila kuna wachafu wengine wametumika kuzalisha kunguni na ndio maana wakawa transfered kutoka kwa washikaji wako kuja kwako maana kama wangekuwa wanajielewa wewe usingewapata...ni sawa na tunapoambiwa ukiugua kipindupindu ni kwamba umekula mavi na sio wote wanaougua kipindupindu wamekula mavi directly bali alisalimiana na mgonjwa ama katika kumhudumia mgonjwa akajikuta ameukwaa ugonjwa kwa bahati mbaya. Ndivyo na kunguni hivyo hivyo kuna watu wamejenga mazingira ya kunguni kuwa sehemu ya maisha yao na mwisho wa siku wanafanya kuwahamisha...kunguni akiwepo ndani kwanza shuka tu zinachoka na kama mtu amekaa nao mpaka anakuletea wewe unadhani hilo gheto lake likoje mkuu kama sio chafu (uchafu sio lazima kuoga kila siku hata kurundika nguo, kuweka viatu ovyo nakadhalika
 
Naombeni mnisaidie dawa itakayo maliza kunguni maana wamevamia chumba changu
na pia nimeckia ile dawa ya RUNGU spray yaweza ua kunguni je hii ni kweli?

Msaada please namna ya kuwatoa hawa wadudu!
View attachment 801832


Baadi ya michango ya wadau;






KUFIKIA katikati ya karne ya 20, ilionekana kwamba wanadamu wamefaulu kuwadhibiti kunguni. Watu fulani walifahamu kunguni kupitia tu wimbo wa zamani wa Kiingereza ulioimbwa na watoto wa shule za nasari (au chekechea) uliosema: “Usiwaache kunguni wakuume.” Hata hivyo, katika miaka ya 1970, nchi nyingi ziliamua kupiga marufuku matumizi ya dawa ya DDT—iliyokuwa dawa kuu ya kuua kunguni—kwa kuwa ilikuwa yenye sumu na iliharibu mazingira.

Hata hivyo, kemikali nyingine zilipotumiwa ilionekana kwamba kunguni walikuwa sugu na hazikuwaua. Pia watu walianza kusafiri mara nyingi zaidi na bila kujua walihama pamoja nao. Matokeo yakawaje? Ripoti moja ya mwaka wa 2012 kuhusu kuwadhibiti wadudu hao inasema: “Katika miaka 12 ambayo imepita kunguni wameanza kuonekana tena nchini Marekani, Kanada, Mashariki ya Kati, nchi kadhaa za Ulaya, Australia, na katika sehemu fulani za Afrika.”

Huko Moscow, Urusi, katika mwaka mmoja hivi karibuni, ripoti za kutokea kwa kunguni ziliongezeka mara kumi kuliko ilivyokuwa hapo awali. Wakati huohuo, upande ule mwingine wa ulimwengu, huko Australia, kumekuwa na ongezeko la asilimia 5,000 la kunguni tangu mwaka wa 1999!

Watu fulani hubeba kunguni bila kujua wanapoenda dukani, kwenye kumbi za sinema, au hotelini. “Upende usipende utabeba kunguni,” anasema meneja fulani wa hoteli nchini Marekani. “Maadamu hoteli inapata wateja lazima kunguni wataendelea kuwapo.” Kwa nini ni vigumu kiasi hicho kuwamaliza kunguni? Unaweza kujilindaje? Kunguni wanapovamia nyumba yako, unaweza kuchukua hatua gani zinazofaa ili kuwaondoa na kuwazuia wasirudi tena?

Wadudu Wasiokufa kwa Urahisi

Kwa kuwa wadudu hao ni wadogo kama mbegu ya tofaa na wana mwili bapa, kunguni wanaweza kujificha mahali popote pale. Wanaweza kujificha katika godoro lako, fanicha zako, sehemu ya ukutani ya kuunganishia vitu vya umeme, au hata kwenye simu yako. Kwa kawaida kunguni hupenda kujificha mita tatu hadi sita kutoka kwenye vitanda na maeneo ya kuketi. Kwa nini? Ili wawe karibu na chakula chao, yaani, wewe!*

Mara nyingi, kunguni huwauma watu wanapolala. Hata hivyo, watu wengi hawahisi wanapoumwa kwa sababu mdudu huyo humdunga mtu kitu kinachogandisha kinachomwezesha kuendelea kula kwa dakika kumi hivi bila kukatizwa. Na ingawa kunguni wanaweza kula kila juma, imesemekana kwamba wanaweza kuendelea kuishi bila kula kwa miezi mingi.

Tofauti na mbu na wadudu wengine, inaonekana kwamba kunguni hawaenezi magonjwa ya kuambukiza. Hata hivyo, wanapomuuma mtu wanatokeza mwasho na baadaye sehemu hiyo inavimba, na watu wengi huathiriwa kihisia. Watu walioumwa na kunguni wanaweza kupoteza usingizi, kuaibika, na hata kufikiri kwamba kunguni amewauma muda mrefu baada ya wadudu hao kutoweka. Jarida moja nchini Sierra Leone linasema kuwa kunguni “ni wasumbufu sana na wanawakosesha watu usingizi” na linaonya kuhusu “aibu inayohusianishwa na kunguni.”

Kuwadhibiti Kunguni

Kunguni wanaweza kumsumbua mtu yeyote. Ni rahisi kuwadhibiti ukitambua mapema kwamba wapo. Kwa hiyo, jifunze kutambua ishara za kwamba wapo nyumbani na unaposafiri. Chunguza fanicha zako na vitu vingine vya mbao pamoja na mizigo, uone ikiwa kuna mayai madogo yanayofanana na mbegu ndogo nyeusi au alama za damu. Tumia tochi unapowatafuta kunguni ili uweze kuwaona.

Usiruhusu kunguni wawe na sehemu nyingi za kujificha. Ziba nyufa zote ukutani na kwenye viunzi vya milango. Ingawa kunguni hawaletwi na uchafu, itakuwa rahisi zaidi kuwatambua na kuwadhibiti ikiwa unasafisha nyumba kwa ukawaida na kupunguza vitu vilivyorundamana. Ukiwa hotelini, unaweza kupunguza uwezekano wa kubeba kunguni kwa kuepuka kuweka masanduku yako sakafuni na kitandani.

Kunguni Wanapovamia Nyumba Yako

Ukipata kunguni nyumbani au hotelini, huenda ukawa na wasiwasi au hata ukaaibika. Dave na mke wake waliumwa na kunguni walipokuwa likizoni. Dave anasema: “Tuliaibika sana. Tulijiuliza tutawaambia nini watu wa familia na marafiki tutakapofika nyumbani? Je, wakati wowote wanapojikuna au kupatwa na mwasho wa ngozi wangejiambia ni kwa sababu walitutembelea?” Hata ingawa ni kawaida kuwa na maoni kama hayo, usiache aibu ikuzuie kutafuta msaada. Wizara ya Afya ya Mwili na Akili ya New York City inatoa uhakikisho huu: “Ni vigumu, lakini inawezekana kuwaangamiza kunguni.”

Chunguza uone kama kuna kunguni kisha uchukue hatua za kuwazuia wasijifiche nyumbani kwako
Hata hivyo, usifikiri kwamba ni rahisi kuwamaliza kunguni. Kunguni wakivamia nyumba yako, unaweza kupata msaada kutoka kwa mtaalamu wa kuwadhibiti wadudu wasumbufu. Ingawa kemikali zilizotajwa awali hazitumiwi tena, wataalamu hao hutumia mbinu kadhaa zinazofaa ili kuwaangamiza kunguni. Dini M. Miller, mtaalamu wa wadudu anasema hivi pia: “Kuwadhibiti kunguni kunahitaji ushirikiano mkubwa sana kati ya wakaaji wa nyumba, wamiliki wa nyumba yenyewe, na kampuni ya kuwadhibiti wadudu wasumbufu.” Kwa kufuata mwelekezo wa mtaalamu na kuchukua tahadhari zinazohitajika, unaweza kutimiza sehemu yako na ‘kutowaacha kunguni wakuume’!
Jumla DAWA ya LARVA
 
hao jamaa kunguni - land rover 109, wako fasta ajabu.....yaani utoe kila kitu nje ndio upulize dawa....wanaenea kwa kasi ya ajabu..
 
jamani kunguni wamekuwa tishio nyumbani kwa miaka 10 sasa, nimetumia dawa nyingi za poda (sevin dudu dust, aerial powder), diazoni, ngao, kuchemsha maji, povu la sabuni, rungu spray na chaki ya kuchora lakini wapi! Ivyo wanajamvi kwa yeyote anayeweza kunishauri (dawa) nini cha kufanya naomba sana msaada wenu binadamu wenzangu. Asanteni!
Mkuu kanunue ddt ndio kiboko yao hutakaa uwaone tena maishani mwako. Cha kufanya ni hiyo dawa na vipimo vyake unaua hadi mayai kwishney hutawasikia tena hapo unapokaa. Kama wamezidi sana hiyo dawa paka kwenye hizo conner za vitanda na kabati kavu usidilute na maji paka hivyo hivyo habari yao utaimaliza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wakuu!. Naomba msaada kwa anayejua dawa ya kumaliza kunguni kwa haraka.

Msicheke nafanya usafi wote lakini bado nimepulizia rungu wapi, na sijui niliwatoa wapi nina wasiwasi na kwenye basi moja la mkoani.

=========

1596372903834.png



Kunguni ni wadudu wadogo wa familia Cimicidae katika oda Hemiptera ya nusungeli Pterygota (wenye mabawa). Mara nyingi huishi katika mazingira ya kificho na yenye mlundikano wa uchafu utokanao na taka mwili, hasa vitanda ambamo hufyonza damu ya watu au wanyama kama chakula chao, hasa usiku.

Spishi
Spishi muhimu sana ni kunguni wa Ulaya (Cimex lectularius). Inatokea duniani kote mahali ambapo watu wanaishi. Katika Afrika kuna spishi nyingine muhimu, kunguni wa Afrika (Cimex hemipterus). Spishi ya tatu, kunguni magharibi (Leptocimex boueti), inatokea Afrika ya Magharibi na Amerika ya Kusini na hupendelea damu ya popo, lakini hufyonza damu ya watu pia mara nyingi.

Biolojia
Kunguni hujilisha damu tu, lakini wanaweza kuishi mwaka mzima bila kula. Wapevu ni wa rangi ya hudhurungi hadi kahawianyekundu, wana umbo la duaradufu bapa na hawana mabawa ya nyuma. Mabawa ya mbele hayafanyi kazi na yamepunguzwa kwa miundo kama pedi. Wapevu hukua hadi urefu wa mm 4-7 na upana wa mm 1.5-3.

Wadudu hao wana hatua tano za maisha kama tunutu na hatua ya mwisho ya upevu. Huambua ngozi yao mwishoni mwa kila hatua, wakitupa kiunzi chao cha nje. Tunutu wakitoka mayai ni wangavu, wenye rangi isiyoiva na wanakuwa kahawia kadiri wanapoambua ngozi na kufikia upevu. Kunguni wanaweza kudhaniwa kuwa wadudu wengine, kama vile chawa-vitabu, mende wadogo au mbawakawa-zulia, lakini wakipata joto na kufanya shughuli, mwendo wao ni ule wa sisimizi, na, kama kunguni-mgunda wengi, wakisetwa hutoa harufu bainifu inayononga.

Kwa sababu kunguni ni wafyonza damu shuruti, wana sehemu za kinywa ambazo zinakeketa ngozi na kuingiza mate yenye dutu dhidi ya mgando na viondoa maumivu. Kiwango cha hisia cha wanadamu kinatofautiana kutoka athari mbaya ya mzio hadi kutokuwepo kwa athari yoyote (karibu 20%). Kwa kawaida umo hutoa uvimbe bila doa nyekundu, lakini wakati kunguni wengi hujilisha kwenye eneo dogo, madoa mekundu yanaweza kuonekana baada ya uvimbe kupungua. Kunguni hupendelea ngozi wazi, haswa uso, shingo na mikono ya mtu aliyelala.

Kunguni huvutiwa na vidusiwa wao kwa dioksidi ya kaboni hasa, kisha kwa joto, na pia kwa kemikali fulani. Kunguni wa Ulaya hujilisha kila siku tano hadi saba tu, ambayo inadokeza kuwa hatumii muda mrefu sana wa maisha yake kutafuta kidusiwa. Kunguni akiwa na njaa, huondoka makazi yake na kutafuta kidusiwa. Anarudi kwenye makazi yake baada ya kujilisha vizuri au ikiwa anakabiliwa na mwanga. Kunguni wa Ulaya hujumuika kwa hatua zote za maisha na hali za kukomaa. Kunguni wanachagua kujumuika labda kwa sababu ya umbuai, nguvu kinzi dhidi ya ukaushaji na fursa zaidi za kupata mwenzi. Feromoni zinazotumwa na hewa zina jukumu la jumuiya.

Mweneo

Uingiaji wa kunguni mahali papya husababishwa na ukosefu wa usafi mara chache tu. Kwa kawaida uhamisho kwa maeneo mapya huwa katika vitu vya binafsi vya wanadamu ambapo wanajilisha. Makazi yanaweza kuingiliwa na kunguni kwa njia tofauti, kama vile:
  • Wadudu na mayai yaliyoletwa kutoka kwa makazi mengine yaliyokuwa nayo kwenye mwili wa mgeni au mavazi au mizigo yake;
  • Vitu vilivyo na kunguni (kama vile samani, haswa vitanda na kochi, mavazi au shanta) vinavyoletwa katika nyumba au jengo la biashara;
  • Ujirani wa makazi yaliyo na kunguni, ikiwa njia rahisi za kupitia zinapatikana, k.m. mifereji au dari bandia;
  • Wanyama-mwitu (kama vile popo au ndege) walio na kunguni au spishi ndugu kama kunguni-popo.
Ingawa kunguni watajilisha juu ya wanyama vipenzi nafasi ikitukia, hawaishi au kusafiri kwenye ngozi ya vidusiwa wao na wanyama vipenzi hawafikiriwi kuwa sababu ya kuenezwa kwao.

Ishara na dalili

Ngozi
Athari za binafsi za maumo hutofautiana na kwenda kutoka kutokuonekana kwa athari (20-70%) hadi madoa madogo na hata vivimbe pamoja na mwasho mkali unaoweza kudumu siku kadhaa. Maumo yapo katika safu mara nyingi. Doa la kati litoalo damu linaweza kuwapo kwa sababu ya kufeleti kwa dutu dhidi ya mgando katika mate ya mdudu.

Dalili labda hazionekani mpaka siku kadhaa baada ya maumo kutukia. Athari zinakuwa kali zaidi baada ya maumo mengi kwa sababu inawezekana kama protini katika mate ya kunguni huhisisha ngozi. Athari ya ngozi hutukia kwa kawaida katika eneo la umo ambalo mara nyingi sana ni mikono, mabega na miguu kwa sababu imefiduliwa usiku kwa kawaida. Maumo mengi yanaweza kusababisha ugonjwa wa mabaka ngozini.

Elimunafsia
Uwepo wa mashambulio tele na ya kudumu yanaweza kusababisha wasiwasi, dhiki na kukosa usingizi. Inawezekana mtu aanze kufikiri kwamba vidusia wapo lakini hawapo kwa kweli, kwa sababu anafikiria sana kunguni kila wakati.

Nyingine
Dalili nyingine kadhaa zinaweza kutukia kwa sababu ya maumo ya kunguni au kusikia harufu yao. Anafilaksisi iliyosababiswa na uingizaji wa protini za mate ya kunguni imeripotiwa kwa nadra. Kwa sababu kila umo linachukua kima kidigi cha damu, uwepo wa kudumu wa kunguni wengi unaweza kusababisha anemia.

Ambukizo la ngozi na bakteria linaweza kutukia kwa sababu kujikuna kunaweza kufungua ngozi na hii inaweza kusababisha kusumu damu kote ikiwa kuna maumo mengi sana.

Kusikia harufu ya kunguni kunaweza kuchokonoa shambulio la pumu kwa sababu ya vizio katika hewa, ingawa ithibati ya mwungano huu ni ndogo.

Hakuna ithibati ya kwamba kunguni wanaeneza magonjwa ya kuambukiza, hata ingawa wanaonekana kuweza kubeba pathojeni na uwezekano umechunguzwa. Umo lenyewe linaweza kuleta uchungu ambao unasababisha usingizi mbaya na utendaji mbaya wa kazi.

Mithili ya wanadamu, wanyama wa kipenzi wanaweza kuumwa na kunguni pia. Ishara zilizoachwa na maumo ni sawa na kisa ya watu na dalili zinafanana (kuwasha ngozi, kujikuna n.k.).

Utambuzi
Utambuzi dhahiri wa athari za kiafya zinazosababishwa na kunguni unahitaji kutafuta na kuona wadudu katika mazingira ya kulala kwani dalili siyo maalum ya kutosha. Kwa kawaida kunguni hufanya safu ya maumo yanayoitwa kimazungumzo "kiamshakinywa, chakula cha mchana na chakula cha jioni". Pia kwa nadra hujilisha kwenye kwapa au nyuma ya magoti ambayo inaweza kusaidia kuwatofautisha na wadudu wengine wanaouma.

Dalili hizi zinaweza kuchanganywa na hali za afya zifuatazo: upele (unaosababiswa na matitiri ya watu na ya ndege), athari za mzio, maumo ya mbu na buibui, tetekuwanga na maambukizo ya ngozi yanayosababishwa na bakteria.

Ugunduzi
Kunguni wanaweza kuweko peke yao, lakini huwa hukusanyika ikiwa wamelowea. Ingawa ni vidusia madhubuti, hutumia sehemu ndogo tu ya maisha yao wakishikamana kimwili na vidusiwa. Mara kunguni akimaliza kujilisha, huhamia mahali karibu na kidusiwa anayejua, kwa kawaida katika au karibu na vitanda au kochi kwenye vikundi vya wapevu, wachanga na mayai, ambapo bingwa wa wadudu huita maeneo ya bandari au bandari tu ambapo mdudu hurudi baada ya kujilisha akifuata nyayo za kemikali.

Maeneo haya yanaweza kutofautiana sana katika muundo, pamoja na mizigo, ndani ya magari, katika samani, katikati mparaganyo kando ya vitanda, hata ndani ya soketi za umeme na katika tarakilishi za karibu. Kunguni zinaweza kukaa pia karibu na wanyama ambao wameweka kiota ndani ya makazi, kama vile popo, ndege au panya. Pia wanaweza kuishi juu ya paka na mbwa wa kipenzi, ingawa binadamu ndiye kidusiwa anayependelewa na kunguni wa Ulaya.

Ikiwa idadi katika nyumba ni kubwa, harufu tamu na chungu inaweza kusikiwa ambayo inafanana na harufu ya rasiberi zinozooza. Mbwa wagundua kunguni hufunzwa ili kuonyesha mahali kamili pa uwepo wao, ambayo ina kiwango cha ugunduzi kati ya 11% na 83%.

Uzuiaji
Ili kuzuia kuleta kunguni nyumbani, wasafiri wanashauriwa kuchukua tahadhari baada ya kutembelea mahali palipoathiriwa: kwa ujumla hii ni pamoja na kuangalia viatu wakati wa kuondoka mahali hapa, kubadilisha nguo nje ya nyumba kabla ya kuingia na kuweka nguo zilizotumiwa katika kikausha nguo nje ya nyumba. Wakati wa kutembelea nyumba mpya ya kulala, inashauriwa kukagua kitanda kabla ya kuleta masanduku katika eneo la kulala na kuweka sanduku juu ya jukwaa ili kupunguza uwezekano wa kuingia ndani kwa kunguni.

Inapaswa kutundika nguo au kuziacha katika sanduku na kamwe kuziacha kwenye sakafu. Mwanzilishi wa kampuni iliyojitolea kuangamiza kunguni alisema kwamba 5% ya vyumba vya hoteli alivyochukua vilikuwa vimeathiriwa. Alishauri watu wasikae chini kwenye usafiri wa umma, wakague viti vya ofisi, viti vya ndege na magodoro ya hoteli, na waangalie vizuri vitanda vya nyumbani na kuvipigia kivuta vumbi mara moja kwa mwezi.

Udhibiti
Tiba inahitaji kuzuia mtu asiumwe tena na tena na labda kutumia antihistimini na kortikosteroidi kidalili (ama kwa mahali au kupitia mfumo wa damu). Lakini hakuna ithibati kwamba dawa zinaleta matokeo mazuri zaidi na kwa kawaida dalili zinaisha bila matibabu katika wiki 1-2.

Kuzuia maumo kunaweza kuwa ngumu, kwa sababu kunahitaji ukomeshaji wa kunguni katika nyumba au ofisi. Hii ni ngumu mno kwa vitendo na kwa kawaida inahitaji mchanganyiko wa njia za viuawadudu na njia bila viuawadudu. Vile vilivyoonwa kufaa zamani vinajumuisha piretroidi (dawa zifananazo na pareto), dichlorvos na malathion, lakini nguvu ya kukinza dawa imezidi sana sasa na matumizi yao yana athari mbaya kwa afya. Sikuhizi hakuna kiuawadudu kinachofaa.

Njia za umakanika, kama vile kutumia kivuta vumbi na kuwekea magodoro joto au kuyafunika kabisa, zinafaa mara nyingi. Muda wa saa moja kwa nyuzijoto ya 45ºC au zaidi ama muda wa masaa mawili kwa chini ya -17ºC unaua kunguni. Kikausha nguo cha nyumbani au stima ya kibiashara zinaweza kutumiwa. Kuwanyimia kunguni chakula hakufanyi kazi kwa sababu wataendelea kuishi muda wa siku 100 hadi 300 kulingana na nyuzijoto.
 
Mkuu dawa ya kunguni sio dawa za kununua madukani... hawa wadudu hawarespond na hizo dawa hata kidogo.

Solution ni kuchemsha maji ya motoooo then mwagia chaga na kitanda chote kwa ujumla.

Then chukua godolo ulipige pasi(ule moto wa mwisho kabisa) .
Then fua mashuka kwa maji ya motooo sana..

Rudia hio procesure kil weekend kwa mwezi mmoja utakuwa umewamaliza kunguni woote
 
Habari wakuu!. Naomba msaada kwa anayejua dawa ya kumaliza kunguni kwa haraka. Msicheke nafanya usafi wote lakini bado nimepulizia rungu wapi, nasijui niliwatoa japo nna wasiwasi na kwenye basi moja la mkoani.
Nunua mafuta ya taa weka kwenye chupa tupu ya maji,toboa pale juu halafu nyunyuzi kila eneo unaloona watakuwa wamejificha kitandani kwenye Kona toa godoro pia uangalie kama ni mayai yapulizie,Fanya hivyo kila asubuh angalau Kwa siku 3 uangalie matokeo
 
Habari wakuu!. Naomba msaada kwa anayejua dawa ya kumaliza kunguni kwa haraka. Msicheke nafanya usafi wote lakini bado nimepulizia rungu wapi, nasijui niliwatoa japo nna wasiwasi na kwenye basi moja la mkoani.
Mkuu wakati mwingine kabla hujaanzisha thread ebu jaribu kusearch kwa kichwa cha habari kinachofanana na thread yako uloikusudia, kwa sababu unaweza kuona kama unaleta thread mpya kumbe imejadiliwa mda mwingi huko nyuma.

Search thread ya kunguni ipoo humu utajifunza mengi huko..
 
Mkuu dawa ya kunguni sio dawa za kununua madukani... hawa wadudu hawarespond na hizo dawa hata kidogo.

Solution ni kuchemsha maji ya motoooo then mwagia chaga na kitanda chote kwa ujumla.
Then chukua godolo ulipige pasi(ule moto wa mwisho kabisa) .
Then fua mashuka kwa maji ya motooo sana..

Rudia hio procesure kil weekend kwa mwezi mmoja utakuwa umewamaliza kunguni woote
Hiyo kazi kubwa dawa yao mafuta ya taa
 
Mkuu dawa ya kunguni sio dawa za kununua madukani... hawa wadudu hawarespond na hizo dawa hata kidogo.

Solution ni kuchemsha maji ya motoooo then mwagia chaga na kitanda chote kwa ujumla.
Then chukua godolo ulipige pasi(ule moto wa mwisho kabisa) .
Then fua mashuka kwa maji ya motooo sana..

Rudia hio procesure kil weekend kwa mwezi mmoja utakuwa umewamaliza kunguni woote
Kuna bobi aliwahi kusema haya mafuta ya kula haya.

Unayapaka kwenye sehemu unapohisi wapo mkama kitandani unapaka kama unapiga banish vileeee.

Hapo unawaondoa kabisa
 
Habari wakuu!. Naomba msaada kwa anayejua dawa ya kumaliza kunguni kwa haraka. Msicheke nafanya usafi wote lakini bado nimepulizia rungu wapi, nasijui niliwatoa japo nna wasiwasi na kwenye basi moja la mkoani.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom