Mfahamu mdudu kunguni (bedbugs) na jinsi ya kumuangamiza

Hapana mkuu sio kweli, mi kuna sehemu nilihamia ikawa sijawah kuwaona kunguni, ila baada ya wageni mbalimbali kuja kutembelea home nilipopanga nikaanza kuskia nawashwa kila nikikaa kwenye kochi, nilipiga makochi yote maji ya moto, kisha nikanyunyiza dawa tena nikayaacha nje km miezi miwili hv hadi yakauke, wakaisha, nikawa sikaribishi watu ndani tena, baada ya muda si nikaachia tena watu waingie na kupiga stori na nini, wakarudi upya,

So kunguni sio uchafu, wanaishi sehemu yoyote ile ambayo inamaficho, km kwenye kona za kuta, kona za makochi, kitanda, sehemu zote ambazo kawaida hazisumbuliwi sana na hazipigwi na mwanga sana,

Ni wagumu kufa kwa Rungu, ila kuna dawa moja niliwah kuiona yan ikimgusa tu ananyoosha miguu juu anadondoka sekunde hiyohiyo, jina silijui maana nlipewa tu na watu wanaotembeza dawa. Wale wadudu omba wasikupate, uwe msafi haijalishi wale sio minyoo au funza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizo sehemu zote ndo uchafu wenyewe maana kwenye kona za kuta maana yake usafi wa mara kwa mara haufanyiki na kwa upande mwingine pia mazingira ambayo kunguni anakaa ni kwenye nyumba yenye vitu vingi kwenye chumba kimoja hasa ukizingatia Watz wengi wanaishi stoo, chumba kina kitanda na viroba vya mahindi uvunguni na kwenye pembe za kuta kuna makwanja na majembe.

Kimsingi wakati watu wanapambana na kunguni, wakumbuke kuondoa mazingira rafiki ya kunguni kuishi kwenye nyumba zao kwa kupunguza makorokoro na kukumbuka kupiga kuta rangi na kuruhusu mwanga wa kutosha kuingia ndani vinginevyo utawaua kunguni ipo siku tena watarudi (kila mtu anajitetea kuna wageni walikuja wakawaleta)
 
Hizo sehemu zote ndo uchafu wenyewe maana kwenye kona za kuta maana yake usafi wa mara kwa mara haufanyiki na kwa upande mwingine pia mazingira ambayo kunguni anakaa ni kwenye nyumba yenye vitu vingi kwenye chumba kimoja hasa ukizingatia Watz wengi wanaishi stoo, chumba kina kitanda na viroba vya mahindi uvunguni na kwenye pembe za kuta kuna makwanja na majembe.

Kimsingi wakati watu wanapambana na kunguni, wakumbuke kuondoa mazingira rafiki ya kunguni kuishi kwenye nyumba zao kwa kupunguza makorokoro na kukumbuka kupiga kuta rangi na kuruhusu mwanga wa kutosha kuingia ndani vinginevyo utawaua kunguni ipo siku tena watarudi (kila mtu anajitetea kuna wageni walikuja wakawaleta)
Sio kila mtu anajitetea, ni kweli mimi sikuwah kuwaona kunguni hadi nilivyotoka home kwenda kupanga mtaani, na nilikuwa bachela msafi sana tuu ila walikuja baada ya washkaji weengi kuingia na kutoka, nilivyopiga dawa nikamwingiza mama mtu geto washkaji hawakuja tena na wadudu sikuwaona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sio kama najisifia mimi msafi saana, lakini ni msafi kwa hakika natamani hata nikupigie picha tu uangalie angalau mazingira utaona hakuna hata moja ya uliotaja hapo, madirisha makubwa ya kutosha chumbani nina kitanda na kabati dogo tu la nguo
Sebuleni kuna set ya kochi na meza ya kioo friji na tv ukutani, sebule kubwa haswa

Kuhusisha kunguni na uchafu labda iwe kwa maana wachafu hawajali uwepo wa kunguni na wanishi nao hivyo hivyo na kusababisha waendelee kuwepo na kusamba

Nakihakikishia wewe msafi ukija kubeba kunguni ukaingia nao ndani kwako utajua ninalojaribu kukueleza hapa
Kunguni sio sawa na nzi au mende wanaokula uchafu, hawa wahuni wanakula damu yako tuu hata uwe msafi vipi as long as wamepata access ya kuingia kwako utajuta
Hata uwe mchafu kiasi gani kama hawajaingia kwako utakua salama

Ubaya mwingine kasi yao kuzaliana ni balaa yani ukiona mayai kwenye kitanda godoro makochi ni sehemu ambazo usafi wa kawaida hauwagusi kabisaa
Baada ya maoni ya wadau ilibidi ni google..... aisee hawa jamaa ni janga la dunia
Hizo sehemu zote ndo uchafu wenyewe maana kwenye kona za kuta maana yake usafi wa mara kwa mara haufanyiki na kwa upande mwingine pia mazingira ambayo kunguni anakaa ni kwenye nyumba yenye vitu vingi kwenye chumba kimoja hasa ukizingatia Watz wengi wanaishi stoo, chumba kina kitanda na viroba vya mahindi uvunguni na kwenye pembe za kuta kuna makwanja na majembe.

Kimsingi wakati watu wanapambana na kunguni, wakumbuke kuondoa mazingira rafiki ya kunguni kuishi kwenye nyumba zao kwa kupunguza makorokoro na kukumbuka kupiga kuta rangi na kuruhusu mwanga wa kutosha kuingia ndani vinginevyo utawaua kunguni ipo siku tena watarudi (kila mtu anajitetea kuna wageni walikuja wakawaleta)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na wakiwa hajajiandaa kutoka nduki ukiwamulika taa wanazuga km wamekosea njia wanavyohangaika kutafuta chochoro

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa wadudu wana akili kweli.
I think sumu ya wadudu iitwayo fiprofam (haina harufu ila ni sumu) ikipigwa sehemu husika (kingo za kuta, kitanda, shelves watateketea tu). Care should be taken kuepusha madhara kwa binadamu.
 
Mkuu sio kama najisifia mimi msafi saana, lakini ni msafi kwa hakika natamani hata nikupigie picha tu uangalie angalau mazingira utaona hakuna hata moja ya uliotaja hapo, madirisha makubwa ya kutosha chumbani nina kitanda na kabati dogo tu la nguo
Sebuleni kuna set ya kochi na meza ya kioo friji na tv ukutani, sebule kubwa haswa

Kuhusisha kunguni na uchafu labda iwe kwa maana wachafu hawajali uwepo wa kunguni na wanishi nao hivyo hivyo na kusababisha waendelee kuwepo na kusamba

Nakihakikishia wewe msafi ukija kubeba kunguni ukaingia nao ndani kwako utajua ninalojaribu kukueleza hapa
Kunguni sio sawa na nzi au mende wanaokula uchafu, hawa wahuni wanakula damu yako tuu hata uwe msafi vipi as long as wamepata access ya kuingia kwako utajuta
Hata uwe mchafu kiasi gani kama hawajaingia kwako utakua salama

Ubaya mwingine kasi yao kuzaliana ni balaa yani ukiona mayai kwenye kitanda godoro makochi ni sehemu ambazo usafi wa kawaida hauwagusi kabisaa
Baada ya maoni ya wadau ilibidi ni google..... aisee hawa jamaa ni janga la dunia

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu sijasema mie msafi na hakuna Mtanzania ambae haja experience kunguni ila ukweli unabaki palepale kunguni anasababishwa na uchafu na mazingira flani flani ya hali nyumba kuwa na giza hivyo wakiingia ndani na mwenye nyumba akawachukulia poa hapo ndio chanzo cha tatizo na ndio maana mpaka dakika hii uzi umefika page kadhaa maana inaonyesha tatizo bado lipo na mazingira ya uchafu bado yapo na ndio humo wanapozaliana ambapo wakienda kutembelea ndugu zao wanahama na kuwahamisha (kama nyumba ipo kama yako ulivyoielezea maana yake hapo wamepita na zoezi la kuwaondoa nadhani limekuwa simple tofauti na nyumba ambayo nimeielezea mie. (mie Mtanzania mzawa nyumba zetu nazijua tuliowengi unakuta kochi set 3 ndio maana akiingia mdudu unashituka wameenea)

Nawafahamu vizuri kunguni mkuu na magodoro yetu ya zamani yalikuwa hayana foronya na wenyewe wanajificha kwenye vile vitobo vya godoro, nilichokisema mie ni solution tu yaani zoezi la kuwaondoa liende sambamba na kuweka mazingira ya nyumba kuwa na mwanga wa kutosha na nyumba isiwe na makorokoro mengi, na hiyo ni kwa wadudu wadogo wadogo wote wakiwemo mende hata mbu.
 
Naombeni mnisaidie dawa itakayo maliza kunguni maana wamevamia chumba changu
na pia nimeckia ile dawa ya RUNGU spray yaweza ua kunguni je hii ni kweli?

Msaada please namna ya kuwatoa hawa wadudu!
View attachment 801832


Baadi ya michango ya wadau;






KUFIKIA katikati ya karne ya 20, ilionekana kwamba wanadamu wamefaulu kuwadhibiti kunguni. Watu fulani walifahamu kunguni kupitia tu wimbo wa zamani wa Kiingereza ulioimbwa na watoto wa shule za nasari (au chekechea) uliosema: “Usiwaache kunguni wakuume.” Hata hivyo, katika miaka ya 1970, nchi nyingi ziliamua kupiga marufuku matumizi ya dawa ya DDT—iliyokuwa dawa kuu ya kuua kunguni—kwa kuwa ilikuwa yenye sumu na iliharibu mazingira.

Hata hivyo, kemikali nyingine zilipotumiwa ilionekana kwamba kunguni walikuwa sugu na hazikuwaua. Pia watu walianza kusafiri mara nyingi zaidi na bila kujua walihama pamoja nao. Matokeo yakawaje? Ripoti moja ya mwaka wa 2012 kuhusu kuwadhibiti wadudu hao inasema: “Katika miaka 12 ambayo imepita kunguni wameanza kuonekana tena nchini Marekani, Kanada, Mashariki ya Kati, nchi kadhaa za Ulaya, Australia, na katika sehemu fulani za Afrika.”

Huko Moscow, Urusi, katika mwaka mmoja hivi karibuni, ripoti za kutokea kwa kunguni ziliongezeka mara kumi kuliko ilivyokuwa hapo awali. Wakati huohuo, upande ule mwingine wa ulimwengu, huko Australia, kumekuwa na ongezeko la asilimia 5,000 la kunguni tangu mwaka wa 1999!

Watu fulani hubeba kunguni bila kujua wanapoenda dukani, kwenye kumbi za sinema, au hotelini. “Upende usipende utabeba kunguni,” anasema meneja fulani wa hoteli nchini Marekani. “Maadamu hoteli inapata wateja lazima kunguni wataendelea kuwapo.” Kwa nini ni vigumu kiasi hicho kuwamaliza kunguni? Unaweza kujilindaje? Kunguni wanapovamia nyumba yako, unaweza kuchukua hatua gani zinazofaa ili kuwaondoa na kuwazuia wasirudi tena?

Wadudu Wasiokufa kwa Urahisi

Kwa kuwa wadudu hao ni wadogo kama mbegu ya tofaa na wana mwili bapa, kunguni wanaweza kujificha mahali popote pale. Wanaweza kujificha katika godoro lako, fanicha zako, sehemu ya ukutani ya kuunganishia vitu vya umeme, au hata kwenye simu yako. Kwa kawaida kunguni hupenda kujificha mita tatu hadi sita kutoka kwenye vitanda na maeneo ya kuketi. Kwa nini? Ili wawe karibu na chakula chao, yaani, wewe!*

Mara nyingi, kunguni huwauma watu wanapolala. Hata hivyo, watu wengi hawahisi wanapoumwa kwa sababu mdudu huyo humdunga mtu kitu kinachogandisha kinachomwezesha kuendelea kula kwa dakika kumi hivi bila kukatizwa. Na ingawa kunguni wanaweza kula kila juma, imesemekana kwamba wanaweza kuendelea kuishi bila kula kwa miezi mingi.

Tofauti na mbu na wadudu wengine, inaonekana kwamba kunguni hawaenezi magonjwa ya kuambukiza. Hata hivyo, wanapomuuma mtu wanatokeza mwasho na baadaye sehemu hiyo inavimba, na watu wengi huathiriwa kihisia. Watu walioumwa na kunguni wanaweza kupoteza usingizi, kuaibika, na hata kufikiri kwamba kunguni amewauma muda mrefu baada ya wadudu hao kutoweka. Jarida moja nchini Sierra Leone linasema kuwa kunguni “ni wasumbufu sana na wanawakosesha watu usingizi” na linaonya kuhusu “aibu inayohusianishwa na kunguni.”

Kuwadhibiti Kunguni

Kunguni wanaweza kumsumbua mtu yeyote. Ni rahisi kuwadhibiti ukitambua mapema kwamba wapo. Kwa hiyo, jifunze kutambua ishara za kwamba wapo nyumbani na unaposafiri. Chunguza fanicha zako na vitu vingine vya mbao pamoja na mizigo, uone ikiwa kuna mayai madogo yanayofanana na mbegu ndogo nyeusi au alama za damu. Tumia tochi unapowatafuta kunguni ili uweze kuwaona.

Usiruhusu kunguni wawe na sehemu nyingi za kujificha. Ziba nyufa zote ukutani na kwenye viunzi vya milango. Ingawa kunguni hawaletwi na uchafu, itakuwa rahisi zaidi kuwatambua na kuwadhibiti ikiwa unasafisha nyumba kwa ukawaida na kupunguza vitu vilivyorundamana. Ukiwa hotelini, unaweza kupunguza uwezekano wa kubeba kunguni kwa kuepuka kuweka masanduku yako sakafuni na kitandani.

Kunguni Wanapovamia Nyumba Yako

Ukipata kunguni nyumbani au hotelini, huenda ukawa na wasiwasi au hata ukaaibika. Dave na mke wake waliumwa na kunguni walipokuwa likizoni. Dave anasema: “Tuliaibika sana. Tulijiuliza tutawaambia nini watu wa familia na marafiki tutakapofika nyumbani? Je, wakati wowote wanapojikuna au kupatwa na mwasho wa ngozi wangejiambia ni kwa sababu walitutembelea?” Hata ingawa ni kawaida kuwa na maoni kama hayo, usiache aibu ikuzuie kutafuta msaada. Wizara ya Afya ya Mwili na Akili ya New York City inatoa uhakikisho huu: “Ni vigumu, lakini inawezekana kuwaangamiza kunguni.”

Chunguza uone kama kuna kunguni kisha uchukue hatua za kuwazuia wasijifiche nyumbani kwako
Hata hivyo, usifikiri kwamba ni rahisi kuwamaliza kunguni. Kunguni wakivamia nyumba yako, unaweza kupata msaada kutoka kwa mtaalamu wa kuwadhibiti wadudu wasumbufu. Ingawa kemikali zilizotajwa awali hazitumiwi tena, wataalamu hao hutumia mbinu kadhaa zinazofaa ili kuwaangamiza kunguni. Dini M. Miller, mtaalamu wa wadudu anasema hivi pia: “Kuwadhibiti kunguni kunahitaji ushirikiano mkubwa sana kati ya wakaaji wa nyumba, wamiliki wa nyumba yenyewe, na kampuni ya kuwadhibiti wadudu wasumbufu.” Kwa kufuata mwelekezo wa mtaalamu na kuchukua tahadhari zinazohitajika, unaweza kutimiza sehemu yako na ‘kutowaacha kunguni wakuume’!
 
Kunguni ni mdudu ambae hafi kirahisi sana hivyo basi usitegemee kuweka dawa siku moja tu haitotosha kuwamaliza,chakufanya kila wiki weka dawa kwa muda wa wiki tatu au nne mfululizo bila shaka watapotea kabisa.
 
Hawa wadudu wana akili kweli.
I think sumu ya wadudu iitwayo fiprofam (haina harufu ila ni sumu) ikipigwa sehemu husika (kingo za kuta, kitanda, shelves watateketea tu). Care should be taken kuepusha madhara kwa binadamu.
Kosa moja kubwa sana ambalo wengi wetu tunalifanya ni kutumia nguvu nyingi sana kumuangamiza kunguni mwenyewe, mimi naamini bado tunakuwa hatujaondoa tatizo.
Kwa kuwa kunguni kama kunguni ni rahisi sana kumuua, mfano chukua sabuni ya unga changanya na maji ukimwagia kunguni anakufa au maji ya moto au juani anakufa mara moja.
Lakini mpaka hapo bado tutakuwa hatujaondoa tatizo kwa kuwa wengi wetu tunasahau mayai yake! hili ndio janga halisi.
Huwezi kuangamiza mayai yake juani au kwa maji ya moto ni lazima yatabaki, kwa hiyo utakapo anika juani au kutia maji moto ni sawa na kuyaweka kwenye INCUBATOR na baada ya siku tatu au nne vitaibuka vitoto kibaaao na hivi vikija utakoma, maana vinakuwa ni vikali sana.

USHAURI:
Usianike au kutumia maji moto kuwamwagia kwa maana utawauwa kunguni na wakati huohuo unazalisha wengine, cha kufanya tafuta sumu ya kuwauwa na uipulizie humohumo mdani bila kuhamisha chochote, kwa maana kitendo cha kuhamisha hamisha vifaa ni kuawasambaza, piga dawa chumbani pqmoja na godoro na kitanda usisahau madirishani na milangoni na kutani na kwenye matundu na nyufa zote.
Hili tendo lirudiwe zaidi ya mara mbili ili kuhakikisha mayai yote na kunguni wameangamia.
Nimepata ufahamu huo baada ya kunisumbua sana, nilianika juani haikufaa, nlitia maji moto haikufaa, nilitia mafuta taa hola niliwachoma na hair dryer haikufaa nilitumia mchanganyiko wa sabuni na jik kunguni wenyewe wanakufa fasta lakini mayai ni tatizooo mpaka upate sumu ya uhakika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko Kenya matatu (sawa na daladala hapa kwetu ).ilivamiwa na kunguni mapaka abiria wakaogopa kuitumia . Kuna siri gani ya hawa kunguni ? Naomba Mshana atueleze katika ulimwengu wa roho .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bedbugs...
hata ulaya wapo, wakishaingia ndani kuwatoani Vita.... Watu wameshauri njia mbalimbali hizo zote zinapunguza tu maaana likibaki hata yai moja baaada wikiwanakuwa buku kadhaa......
Permanent solutions choma Kama Ni kuwahi Kama Bado hawajasoma Sana ndani(wapo kitandani pekeee) Ni kufungua kitanda mwagia maji ya Moto kweli kweli, shuka na blanket avichemshe..... GODORO ALICHOME MOTO, narudia Tena GODORO ALICHOME MOTO maana halichemshiki, na awahi kabla hawaja sambaa Hadi kwenye Kochi maana nazenyewe Moto utazihusu hasa Kama nihizi sofa....

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo BITO ni Aka Tu
 
Mkuu sijasema mie msafi na hakuna Mtanzania ambae haja experience kunguni ila ukweli unabaki palepale kunguni anasababishwa na uchafu na mazingira flani flani ya hali nyumba kuwa na giza hivyo wakiingia ndani na mwenye nyumba akawachukulia poa hapo ndio chanzo cha tatizo na ndio maana mpaka dakika hii uzi umefika page kadhaa maana inaonyesha tatizo bado lipo na mazingira ya uchafu bado yapo na ndio humo wanapozaliana ambapo wakienda kutembelea ndugu zao wanahama na kuwahamisha (kama nyumba ipo kama yako ulivyoielezea maana yake hapo wamepita na zoezi la kuwaondoa nadhani limekuwa simple tofauti na nyumba ambayo nimeielezea mie. (mie Mtanzania mzawa nyumba zetu nazijua tuliowengi unakuta kochi set 3 ndio maana akiingia mdudu unashituka wameenea)

Nawafahamu vizuri kunguni mkuu na magodoro yetu ya zamani yalikuwa hayana foronya na wenyewe wanajificha kwenye vile vitobo vya godoro, nilichokisema mie ni solution tu yaani zoezi la kuwaondoa liende sambamba na kuweka mazingira ya nyumba kuwa na mwanga wa kutosha na nyumba isiwe na makorokoro mengi, na hiyo ni kwa wadudu wadogo wadogo wote wakiwemo mende hata mbu.
Mkuu mi sijawah kuwa hata na nzi wala mbu geto kwangu wala mende, na nilikua bishoo ila najua kuna mpuuzi mmoja tu alikuja nao tuu maana siwez kujua ntawazalishaje mwenyewe na niliishi home fresh tuu tangu nazaliwa ndo nije kuwa nao ukubwani, theory ya uchafu ni uongo, maana nakumbuka utotoni sikuwa msafi, na boarding nimesoma sijawaona, na chuo hosteli sijawaona ndo nimekuja kuwaona baada ya kupanga uswazi na kukaribisha washkaji tu wanachill wanacheki muvi nini wanaenjoy mara haaaooo,

Sent from my TECNO W1 using JamiiForums mobile app
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom