Naomba msaada toka kwa rais wangu mh. dr. Jakaya Mrisho Kikwete

optimistic1

Member
Jun 10, 2013
5
1
RAISI WANGU MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE
Raisi wangu naomba nikupe pole kwa majukumu ya kila siku ya kitaifa, naona misukosuko mingi inajitokeza Tanzania mfano Mtwara Mungu azidi kuisaidia Tanzania na kuidumisha amani.

Raisi wangu nimekua ni mtu ambaye nafuatilia kujua wewe ni raisi wa namna ipi, nimeridhika na raisi wangu. Hata leo najitokeza kuadika ujumbe huu kwako raisi wangu nikiomba msaada wako wa dhati.

Mimi ni kijana ninayetoka katika familia ya kimasikini, kusoma kwangu kulikua kwashida sana. Namshukuru mungu nimemaliza elimu yangu ya juu ktk chuo kikuu kimoja hapa nchini mwaka mmoja uliopita. Katika mlolongo wa shule nilizo soma ni zile shule za wengi ambazo masikini wengi wanaweza kumudu. Katika maisha yangu nimekua nikiamini kua elimu ndio ukombozi wangu katika kujikwamua katika ugumu wa maisha, pia bado naamini hivyo kwani kwakusoma kwangu nimeondoa ujinga na kugain vitu vingi ambavyo ni msaada kwangu.

Raisi wangu sijaona njia ambayo ningeweza fikisha ombilangu kwako zaidi ya hapa nilipo tumia pia naamini lazima maombi yangu yangu yatafika kwako.

MAOMBI YANGU KWAKO RAISI WANGU
Raisi wangu naipenda nchi yangu nabado sijafikia pointi ya kuilaumu nchi yangu. Ninasifa za kuajiriwa na kufanya kazi, lakini bado nashuudia watu wakiajiriwa na mimi nikiendelea kuapo mitaani. Raisi wangu naamini kua wewe ndio TOP katika nchi hii, naomba unisikilize mimi mtanzania ninaye omba msaada wako siku hii ya leo, ninaamini kwa msaada wako raisi wangu wakati wowote na saa yoyote naweza pata ajira katika nchi yangu ya Tanzania.

RAIS WANGU NAOMBA UNISAIDIE MWANANCHI WAKO NIWEZE PATA AJIRA.

Laiti ningekua na uwezo ningeweza fika ikulu au ningeweza simamisha msafara wako kwaajiri ya kuomba msaada wako, na wengi waweza ona nimekurupuka na nimefanya ujinga ukweli ni kwamba nimejaribu kutafuta kazi kwa kadri ya uwezo wangu wote bila hata MAFANIKIO. Raisi wangu sikia kilio na ombi langu.

Raisi wangu naomba kwa Mungu ujumbe huu ukufikie kwani naamini ujumbe huu ukifika kwako lazima raisi wangu utanisaidia mwananchi wako nisiyekua na msaada wowote. Pia nakumbuka umeisha wasaidia watu wengi sana katika nchi yako, nitazame na mimi leo hii.

Raisi wangu nashukuru sana kwa yote , pia naamini kua ujumbe wangu utakufikia na msaada nitaupata toka kwako.

MWISHO
Namuomba Mungu wangu azidi kukupa afya njema na maisha marefu zaidi, pia Mungu azidi kukuzidishia hekima katika kuliongoza taifa la Tanzania.


Optimistic1980s@gmail.com
 
Pole kijana , Pamoja na kuomba msaada wa kupatiwa ajira lakini Kumbuka kuwa kwa sasa vyuo vikuu vinatoa wahitimu wangapi kwa mwaka, na ajira zinazotolewa na serikali ni kiasi gani. Hapo ndio utajua ajira za serikali ni chache mno, ila sekta binafsi ikiwemo kujiajiri mwenyewe kwa ujuzi wowote ule ambao haupingani na sheria za nchi ndio fursa zilizojaa nchini.

Ukiwa mchagua kazi utasota sana, lakini ukijichanganya bila kujali maslahi kwanza utaishi tu. wengine walianza kwa kuuza machungwa na pension wakati wanasubiria kupata pale ambao wanaona panawafaa maishani mwao.
 
Mkuu mleta uzi, kwanza nikupe hongera kwa kubahatika kuwa mmoja ya wasomi wachache wa ngazi ya chuo kikuu hapa nchini..pili nikupe pole kwa changamoto ya kutafuta ajira...tatu naomba nikushauri kwamba ni vyema utoe details zako ikiwa ni pamoja na degree uliyosoma, specialisatn,chuo na mwaka ikiwezekana ht jina then kuna jukwaa la kazi na tenda uwe unapitia sana pale kuna nafasi za kazi watu wana post kila siku kila idara serikali na private...pia umetumia fursa mhm kufikisha yaliyo moyoni mwako yanayokukera tatizo ni wana jf wengi kukosa ustaarabu wa kupeana mawazo...hatua uliyopo sasa wengi wanaipitia na huwa na challenges sana..kikbwa uvumilivu,subira na kutokata tamaa
 
Ni vyema pia uende google angalia namna ya kuandika cv,namna ya ku appear/ jibu maswali common yanayoulizwa kwenye interview, interest za waajiri na requrement za interviewer ili hata ikatokea ukaitwa kwenye interview uwe na abcs...jitahidi uwe na soft copy ya cv yako mana now days appl. Nyingi zinafanyika online...jitahidi pia kupita kwenye maofisi peleka cv yako hata kama hawajatangaza ....and last kwa level ya graduate tafuta hata temporary job kwenye maofisi usikae tu nyumbani kuangalia tv kula na kulala itakuwa msiba kwako.
 
Tatizo la vijana wanasoma degree ambazo wakimaliza hawauziki. Ungesomea ualimu leo hii JMK angekuwa n sababu ya kwenda kuomba walimu Malaysia? Hata kama hukusomea ualimu unaweza kurudi tena chuoni ukasoma PGDE kwa mwaka mmoja na ukawa na uhakika wa ajira.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
aisee mkuu haya mambo yanaisha.. na kaz utapat.. sema hi ki2 ya kumuomba JK ajira unakosea mkuu... ungeomba ushaur wadau tukuonesh njia hiv.. hi ki2 inakushushia p kidog ujue.. achana na JK weka mamb hadharan, wapo walioanza na sifur humu humu jf mpk leo wana zaid ya mia!
 
me cio JK lakni kama ulisoma sayans Alevel na BSc. ni tumie text (ni pm)..
 
Mkuu optimistic1,

Ni nani aliye kuambia nchi hii ina amani ?
Possibly hujui tofauti kati ya amani na utulivu........

Refer mistari ya Roma Mkatoliki 2030 upate funguka, siyo kusikiliza taarab masaa yote.
 
mkuu ww ni mmoja kati ya wale mnao penda kumsema vibaya raisi then comments nyingi, sijakosea he is my president.

Hakuna anayemsema vibaya.. Akichemka tunamkosoa!... Hata malalamiko yako ni sehemu ya ukosoaji huo, kuwa serikali yake imeshindwa kutengeneza ajira.
 
RAISI WANGU MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE
Raisi wangu naomba nikupe pole kwa majukumu ya kila siku ya kitaifa, naona misukosuko mingi inajitokeza Tanzania mfano Mtwara Mungu azidi kuisaidia Tanzania na kuidumisha amani.
Raisi wangu nimekua ni mtu ambaye nafuatilia kujua wewe ni raisi wa namna ipi, nimeridhika na raisi wangu. Hata leo najitokeza kuadika ujumbe huu kwako raisi wangu nikiomba msaada wako wa dhati.
Mimi ni kijana ninayetoka katika familia ya kimasikini, kusoma kwangu kulikua kwashida sana. Namshukuru mungu nimemaliza elimu yangu ya juu ktk chuo kikuu kimoja hapa nchini mwaka mmoja uliopita. Katika mlolongo wa shule nilizo soma ni zile shule za wengi ambazo masikini wengi wanaweza kumudu. Katika maisha yangu nimekua nikiamini kua elimu ndio ukombozi wangu katika kujikwamua katika ugumu wa maisha, pia bado naamini hivyo kwani kwakusoma kwangu nimeondoa ujinga na kugain vitu vingi ambavyo ni msaada kwangu.
Raisi wangu sijaona njia ambayo ningeweza fikisha ombilangu kwako zaidi ya hapa nilipo tumia pia naamini lazima maombi yangu yangu yatafika kwako.

MAOMBI YANGU KWAKO RAISI WANGU
Raisi wangu naipenda nchi yangu nabado sijafikia pointi ya kuilaumu nchi yangu. Ninasifa za kuajiriwa na kufanya kazi, lakini bado nashuudia watu wakiajiriwa na mimi nikiendelea kuapo mitaani. Raisi wangu naamini kua wewe ndio TOP katika nchi hii, naomba unisikilize mimi mtanzania ninaye omba msaada wako siku hii ya leo, ninaamini kwa msaada wako raisi wangu wakati wowote na saa yoyote naweza pata ajira katika nchi yangu ya Tanzania.
RAIS WANGU NAOMBA UNISAIDIE MWANANCHI WAKO NIWEZE PATA AJIRA.
Laiti ningekua na uwezo ningeweza fika ikulu au ningeweza simamisha msafara wako kwaajiri ya kuomba msaada wako, na wengi waweza ona nimekurupuka na nimefanya ujinga ukweli ni kwamba nimejaribu kutafuta kazi kwa kadri ya uwezo wangu wote bila hata MAFANIKIO. Raisi wangu sikia kilio na ombi langu.
Raisi wangu naomba kwa Mungu ujumbe huu ukufikie kwani naamini ujumbe huu ukifika kwako lazima raisi wangu utanisaidia mwananchi wako nisiyekua na msaada wowote. Pia nakumbuka umeisha wasaidia watu wengi sana katika nchi yako, nitazame na mimi leo hii.
Raisi wangu nashukuru sana kwa yote , pia naamini kua ujumbe wangu utakufikia na msaada nitaupata toka kwako.

MWISHO
Namuomba Mungu wangu azidi kukupa afya njema na maisha marefu zaidi, pia Mungu azidi kukuzidishia hekima katika kuliongoza taifa la Tanzania.
Optimistic1980s@gmail.com
Muone KALA JEREMIAH unaweza kutoka na single kali ya kumpa JK maflag ya kufa mtu!...
 
mkuu mimi nataka nijue namna nitakavyokupata,kama hautajari weka namba ya simu ili tuweze kuwasiliana na kushauriana vema nasuburi majibu yako mkuu.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom