Naomba msaada kwa kwenu wataalamu

bongo man

JF-Expert Member
Dec 26, 2016
1,053
2,327
Habari nzenu ndugu .

Natumaini hamjambo na mnaendelea vizuri na majukumu yenu ya kila siku bila shaka naleta hili jf ili mnisaidie naamini hapa jf hakishindikani kitu.

Mwaka juzi kuna rafiki yangu tu tuliingia nae mkataba wa masuala ya kusuply mzigo ( siri ila wa halali) wenye gharama 1.5 mil. Yule jamaa tulifanya nae kazi kwa uaminifu kwa muda wa kama miaka miwili hivi sasa sijui ilikuwa aje siku ya kumpa hela huyu jamaa ndo ikawa ndo ntolee mazima kwakweli aliniacha katika wakati mgumu sanaa ikizimgatia kuwa mzigo huu ulikuwa wa kampuni ninayoifanyia kazi .

Basi baada ya kumtafuta kwa muda mrefu takribani mwaka mzima na nikietembea na RB zijampata yani anatoka eneo moja kwenda eneo jingine yani hatulii kwakweli nikaamua kukopa kwenye taasisi flani nikalipa deni kwani ofisi imishaanza kunitilia shaka kwakweli taasisi ile ina riba kubwa ila ikanibidi deni ambalo nalilipa hadi sasa .

Kesi nilishafungua

RB ninayo .

Mikataba yote ninayo .

Huyu jamaa mara moja moja simu yake ukipiga inaita ila hapokei na hata akipokea anajifanya kama umekosea namba yanii mchezo ndio huo .

Kwa helufi kubwa .NAOMBA MNISASIDIE HUYU JAMA NIWEZE KUMPATA KANITESA SANAA NAOMBA KUWAKILISHA.
 
Pole mkuu. kama kesi ipo na RB ipo hukohuko police wanaweza mtrace wakamdaka akatiwa nguvuni. ila huko police kwenye kumtrace ndio uandae hela sasa, na unaweza toa hela na usifanikiwe.

Cha msingi lipa deni na usonge mbele
Hilo nimeshafanya sanaa hadi nimeona napoteza hela bure tu kila siku polisi ni sound tu hakuna jipya .
 
Haya mambo yanaumiza sana,
Pole sana ndugu, mimi nimemtia ndani best friend hakuna anayeamini mpaka leo hii.

Narudia, pole, usawa huu kulizwa pesa si kitu kidogo.
Bora kutia ndani majitu kama hayo..mie bro toto la aunt limekimbia na 19m ! Nikaenda police geita uwii nikawatoa mpunga mzuri tu..mara wakuambia ndug yako yuko tabora anatumia mtambo no 2 tupe mafuta tukamfate unawapa..wanakaa hata wiki kimya ukiuliza wanasema amehama yuko singida tupe hela madame tumfate . Nikasema nhiii!
Nimewaeleza wazazi wake ama zangu ama zake
 
Bora kutia ndani majitu kama hayo..mie bro toto la aunt limekimbia na 19m ! Nikaenda police geita uwii nikawatoa mpunga mzuri tu..mara wakuambia ndug yako yuko tabora anatumia mtambo no 2 tupe mafuta tukamfate unawapa..wanakaa hata wiki kimya ukiuliza wanasema amehama yuko singida tupe hela madame tumfate . Nikasema nhiii!
Nimewaeleza wazazi wake ama zangu ama zake
Kama Polisi huna mtu wa kukusaidia wala kukurahisishia kazi, bora mmalizane...
Sijui watu wakishika pesa wanaingiwa na nini, huwezi mzania.
 
Bora kutia ndani majitu kama hayo..mie bro toto la aunt limekimbia na 19m ! Nikaenda police geita uwii nikawatoa mpunga mzuri tu..mara wakuambia ndug yako yuko tabora anatumia mtambo no 2 tupe mafuta tukamfate unawapa..wanakaa hata wiki kimya ukiuliza wanasema amehama yuko singida tupe hela madame tumfate . Nikasema nhiii!
Nimewaeleza wazazi wake ama zangu ama zake
Aise nikikopa kulipa kwa riba chafu hadi leo nalipa deni kubwa yanu inauma vibaya sanaaa maisha hayaa
 
Back
Top Bottom