Naomba mchanganuo wa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza Toothpick

Habari zenu wadau wa JF.!

Naam wadau wa JF naombeni mwenye uelewa wa hichi kiwanda ashushe Nondo Hapa kwa faida yetu sote. Maana nasikia hiz Toothpicks bado zinatoka China Aisee kama ni kweli inatia huruma.

Napenda kujua Gharama zake mpaka kinakamilika kiwanda katika Mazingira mazuri na rafiki kwa kazi. Gharama za mashine yenyewe vpi nitapata Malighafi zake na soko lake kiujumla.

Naombeni yeyote mwenye ufahamu na hichi kiwanda anipange vizuri. Hapa JF tupo watu wengi na wenye mawazo Tofauti tofauti, naimani nitapata mawazo mazuri.

Asanteni karibuni katika Hoja.
Malighafi ni mambazi yanayotokana baada ya kuchana mbao.au mianzi .kiwanda bila jengo ni Tzs 80.000.000.kama unataka technical proposal na bei na idadi ya mashine nnazo ni PM
 
Hakikisha unatengeneza toothpicks za bamboo trees ndo utapambana na ushindani wa mchina
Kwa Tanzania Bamboo ni shida kuzipata za kutosheleza production.labda awe na shamba lake mwenyewe.Malighafi ambayo ipo ya kutosha ni mabanzi ya mbao
download (1).jpeg
download (1).jpeg
IMG_20171206_160038.jpg
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom