Naomba Majibu Tafadhali: 'Mfumo imara' ni nini?

Naona kwenye mfumo mnajikita kwenye mifumo inayolinda taasisi za chini zisiingiliwe na rais. Hamtaki kujishughulisha kwamba hizo taasisi za chini zinaweza kutumia hiyo mifumo inayowakingia kifua kufanya mambo ya ovyo kwa kisingizio cha kwamba ni wao ni mihimili inayojitegemea wasiingiliwe.

Kama mnaogopa kwamba katiba inampa rais madaraka makubwa sana na kwa udhaifu wa kibinadamu anaweza akayatumia vibaya, kwa nini msiogope pia kwamba uhuru wa mihimili mingine nao unaweza kutumika vibaya?

Kama inshu ni kuweka sheria kwamba yeyote atakayetumia vibaya ashtakiwe bila kujali yeye ni mhimili gani, swali litabaki nani atamfunga paka mwenzake kengele. Na ikumbukwe sisi raia hatujui kinachoendelea jikoni, tunalishwa tu matango pori na hayo mamihimili. CAG anapokuletea mareport kwamba shirika hili na lile limepata hasara, hatuwezi kujua uhalisia wa kile kilichoendelea nyuma ya pazia wakati akifanya hayo mahesabu.

Wape watu heshima wanayostahili, nayo ni kwamba mifumo inategemea watu.
Unapoambiwa mifumo imara maana yake ni kwamba nchi inakua ya wananchi na wote kuanzia rais na taasisi nyingine zote za serikali watawajibika kwa wananchi kupitia taratibu zilizowekwa na kama kuna kasoro au mianya yoyote yakuenenda tofauti na miongozo hatua zinachukulika automatic.
 
Taifa halijawahi na haliwezi kupata hasara kwa kumpoteza kiongozi wa aina yoyote mkuu,
no one is indispensable under the sun.(JFK)
Na ndiyo maana Mama anasema "Kazi iendelee.
Nakubali kama taifa we are stronger, na katikati yetu tuna hazina ya watu bora na wanaotufaa/watakaotufaa sana kama taifa kwa nafasi zao, uwezo wao na potential zao.

Lakini hilo halimaanishi kwamba you can just do away with anybody however you like eti kisa no one is dispensable. Hiyo ni model mbaya sana, na ndio maana nchi huwa zina vipindi vya prosperity na vipindi vya depression. Tanzania iliyoongozwa na Nyerere ni tofauti na Tanzania iliyoongozwa na Mwinyi ni tofauti na Tanzania iliyoongozwa Mkapa ni tofauti na Tanzania iliyoongozwa na JK ni tofauti na Tanzania iliyoongozwa na JPM. Kama katiba ni ile ile kwa nini ladha za uongozi ziwe tofauti? Kuignore impact ya mtu ni willfull ignorance, na ni hatari sana, maana inajenga tabia kwamba mtu yeyote anaweza kuwa eti kwa vile kuna katiba na job descriptions.
 
Nyerere ndiye aliyewaloga Watanzania waone kuwa ni bora watawaliwe kidikteta badala ya kufata mfumo wa kidemokrasia. Lazima ukubali Nyerere alikuwa ni genius. Na Watanzania walikubali. Wachache waliompinga walipotezwa au walikimbia nchi. Kwa hiyo kutawaliwa kidikteta ndiyo msingi wa nchi hii aliotuachia baba wa taifa na mpaka leo upo. Mfumo imara unapingwa kwa sababu msingi uliojengewa nchi hii ni kutawaliwa kidikteta.
 
Watu ni muhimu katika mfumo. Bila wao hakuna mfumo imara. Shida ni pale anapopewa mtu mmoja madaraka makubwa sana. Hata CAG office sio perfect, lakini tunaweza kuongeza uimara wake kwa mfano kutafuta kampuni ya nje nayo iwe inafanya random audits za kule alikopita CAG. Ndio mfumo wenyewe unavyojengwa, kwamba wewe kama ni mkaguzi kutoka CAG office unajua kabisa kuna mfumo wa watu kuja kujiridhisha kuhusu kazi yangu.

Ila kuwa na mtu mmoja anaamua nani achunguzwe nani aachwe sio sawa. Angalia hata hili la Mama Samia kuagiza special audit BOT, mamlaka zilikuwa wapi kuona shida? Ina maana kila siku tutahitaji rais ambaye anashida kuzunguka kila kona, no wonder hearts zao zinapata shida.
Sidhani kama inawezekana mtu kuwa na control kwa kila kitu katika uongozi wa taasisi yoyote hata ngazi ya familia, achilia mbali ngazi ya taifa. Tunaposema mtu ni nguzo hatumaanishi mtu awe omnipotent, omniscient na omnipresent. Mtu hawezi kuwa hivyo, mtu si Mungu.

Ila tunachomaanisha ni kwamba mtu anapaswa kufanya intervention katika mifumo ya binadamu pale inapobidi. Watu wana talanta zao, wana maarifa yao, wana utashi wao, na wana gut insticts zao. Kuzizuia zisifanye kazi eti aache mfumo ufanye kazi ni kuzuia ubunifu, ni kuzuia potential za mtu zisifanye kazi.

Mama Samia kuagiza BOT ifanyiwe special audits inadhihirisha jinsi usivyoweza kuachia tu mifumo ijifanyie mambo yao yaliyopo kikanuni. Kwa nini ameagiza BOT ifanyiwe special audit? Hatuwezi kujua kwa uhakika, lakini kwangu mimi it is OK, namtegemea mama asikalie kile kiti kama robot. Kama kuna taarifa kazipata, kama ana gut insticts kwamba kuna mambo hayaendi ndivyo sivyo, kama kuna namna nyingine iliyomtuma afanye hivyo, wacha afanye. Anautendea haki ubinadamu wake, anaitendea haki nafasi yake, kama mtu binafsi.
 
Unapoambiwa mifumo imara maana yake ni kwamba nchi inakua ya wananchi na wote kuanzia rais na taasisi nyingine zote za serikali watawajibika kwa wananchi kupitia taratibu zilizowekwa na kama kuna kasoro au mianya yoyote yakuenenda tofauti na miongozo hatua zinachukulika automatic.
Si ndivyo mfumo wetu ulivyo? Kipi kimebadilika? Katiba yetu inamtaja Rais anachaguliwa na wananchi na anawajibika kwa wananchi. Kama akienda ndivyo sivyo wananchi kupitia bunge letu linaweza kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, na bunge likavunjwa na kurudi kwenye uchaguzi.

Huo sio mfumo? Una shida yoyote?
 
Nyerere ndiye aliyewaloga Watanzania waone kuwa ni bora watawaliwe kidikteta badala ya kufata mfumo wa kidemokrasia. Lazima ukubali Nyerere alikuwa ni genius. Na Watanzania walikubali. Wachache waliompinga walipotezwa au walikimbia nchi. Kwa hiyo kutawaliwa kidikteta ndiyo msingi wa nchi hii aliotuachia baba wa taifa na mpaka leo upo. Mfumo imara unapingwa kwa sababu msingi uliojengewa nchi hii ni kutawaliwa kidikteta.
Mkuu, ukichunguza uzi huu utagundua ninafuatilia kila bandiko linalowekwa hapa. Lengo, nipate majibu nijifunze. Mwisho wa siku kwa pamoja tuamue kipi kinatufaa kama taifa, kwa msingi ule ule wa kuendeleza umoja, amani, ushirikiano,na ustawi katika nyanja zote za nchi yetu Tanzania. Binafsi nina imani na nguvu ya JF kufikisha ujumbe panapohusika.

Kwa msingi huo, bandiko lako limenichanganya hasa ukizingatia swali la msingi la uzi huu. 'Mfumo imara' ni nini?

Kwa hiyo, Mkuu naomba udadavue tena hoja yako. Natanguliza shukrani.
 
Naweza kupendekeza hivi: kwamba tupalilie watu bora watakaotengeneza mifumo bora itakayosimamiwa na watu bora. "Standing on the shoulders of giants" wao wanasema. Inapotokea mtu imara na akaonyesha umahiri huyo ni asset , na hata akifa, kama tulivyompoteza JPM, we build on his legacy. Mfumo imara kuliko yote kwangu mimi si sheria na wala si katiba. Mfumo imara ninavyouona mimi ni mila, desturi na utamaduni. Vitu, dhana, legacies na practices zikiwa codified hadi zikawa sehemu ya mila, desturi na utamaduni wa watu fulani au taifa fulani ni vigumu sana kuvifuta. Kama kuna kitu ni kizuri na tunadhani ni vizuri tukijengee mfumo imara ili isiwe rahisi kupotea, basi kitafutuwe namna kiwe sehemu ya mila, desturi na utamaduni wetu. Na kuna njia kadha wa kadha za kufanya hivyo.
 
Mfumo imara ni muunganiko wa watu, rasilimali, sera na sheria tofautitofauti wanaofanya kazi kwa umoja na uhuru ili kufikia lengo la taasisi husika kwa ufanisi na weledi wa hali ya juu; kama tulivyoona katika kipindi cha Rais bora wa nchi yetu, Hayati Dr. JPM.
Hovyoo...!!

Jiwe hajawahi kua na mfumo imala.
Badala yake.alikua anafanya mambo anavyota.

Nakumbuka zama za kizazi kile kabla ya watu hasa watanzania kwenye sehemu zao za kazi akiingua meneja au mkurugenzi watu wanatetemeka.

Tofauti na sasa watu wanasomea uongozi wanajua haki na wajibu wa kila mmoja ktk sehemu yake ya kazi kwenye ofice yake.

H.R.
Atampa mkataba mfanyakazi kuanzia muda wa kuingia kazini ,muda wa kula,muda wa kufunga kazi na hata mavazi.
Na ili mtu asizalilishwe kwenye ofisi yake kwa kufokewa kama alivyokua anafanya jiwe kwa wasaidizi wake sheria(mfumo imara wa H.R) Unambana mfanyakazi hadi mkuruenzi ndani ya ofisi.
Hapa tunaona sasa mfumo imala unambana kuanzia mfanyakaz wa chini kabisa hadi mkurugenzi mwenye idara,ofisi,au kampuni hasa kwa mfano muda wa kufika kazini au mavazi bila ya ugomvi au kofokeana.

Kiongozi na mfanyakazi wanacheka na wanafulahi pamoja lakini mwisho wa siku mmoja wapo atabanwa na mfumo imara ana anaweza kutolewa au kutoka kazi kutokana na sheria (mfumo uliowekwa.

Mfano:-
Mkataba ,sheria(mfumo )unakwambia uingie kazini saa 2 kamili asubuhi utakuta daftari la kusini muda ulifika.
Ikifika saa saa2 na robo HR anachukua daftari anapiga mstar mwisho wa.kolamu ya wafanyakazi.wanaoingia hivyo wewe uliochelewa utakua nje ya mstari,HR haongei na wewe.

Mwisho wa mwezi tunakaa kikao cha.mwez tunakuona wewe ulikua nje ya msatar kalibu mala 10.
Maana yake mchelewaji sugu kazini.
HR anakuandikisha maelezo ya uchelewaji kama onyo.
Ukirudia mala 2 au 3 utakua umejifukuzisha

Ndio hivyohivyo kwa mkurugenzi nae akilewa madaraka kila siku anafika ofisini sa 4 na menejiment inasubili mafaili yalioko mezani.yasainiwe ili kazi ziende yeye hayupo maanayake nayeye anahatari ya kujihalibia hazi au kutaka kujifiris.

Hivyo MFUMO IMARA NI KATIBA IMARA INAYOWEZA KUMBANA KILA MMOJA KUANZIA MFANYAKAZI WA CHINI KABISA HADI MKURUGENZI, BIRA YA KUSUKUMANA.

Nakumbuka jk nyerere aliwahi kusema kwenye hotuba zake kua.
Katiba hii ya sasa akitokea mtu mwenye roho mbaya atawaburuza sana wananchi.

Hivi tujiulize hii leo Rais akisema hela zote zilizokuwemo benk kuu ni zangu na hata akizichukua hakuna wa kumshitaki.

Huu ni ujinanga na upuzi wa hali yajuu kabisa.

Ndio maana jiwe alijua amelewa madalaka hadi ananunua kuku au muhindi wa.kuchoma kwa elf50 hadi laki.
Na kugawa au kutumia hela vile anavyoona inafaa yeye kama yeye.
 
Mkuu, ukichunguza uzi huu utagundua ninafuatilia kila bandiko linalowekwa hapa. Lengo, nipate majibu nijifunze. Mwisho wa siku kwa pamoja tuamue kipi kinatufaa kama taifa, kwa msingi ule ule wa kuendeleza umoja, amani, ushirikiano,na ustawi katika nyanja zote za nchi yetu Tanzania. Binafsi nina imani na nguvu ya JF kufikisha ujumbe panapohusika.

Kwa msingi huo, bandiko lako limenichanganya hasa ukizingatia swali la msingi la uzi huu. 'Mfumo imara' ni nini?

Kwa hiyo, Mkuu naomba udadavue tena hoja yako. Natanguliza shukrani.
Kwa kifupi sana
Mfumo imara ni pale ambapo nchj inakuwa na katiba imara inayozipa nguvu na uhuru taasisi zake kutekeleza majukumu ya kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi bila kuingiliwa kwa namna yoyote ile.Ili serikali iweze kuwajibika ipasavyo kwa wanachi walioiweka madarakani.(Social accountability and right based approach).
Taasisi hizo ni pamoja na;
1.tume huru ya uchaguzi
2.Bunge
3.Mahakama
4.CAG
5.Baraza la madiwani.
Maana yake ni kwamba taasisi hizi zikiwa imara na zikatekeleza majukumu yake bila kuingiliwa,Serikali itawajibika vilivyo kwa wananchi walioiweka madarakani,kwa kuogopa kuondolewa madarakani na hata kushitakiwa na kufungwa bila kujali nafasi aliyonayo kiongozi yeyote awae, pale watakapo shindwa kutimiza wajibu wao au kufanya ubadhilifu wa Mali ya umma au kutoa maamuzi yanayoweza kuisabishia nchi hasara ya Mali na watu.
Misingi imara ya kitaasisi inapelekea kuwa na Serikali inayowajibika kwa umma badala ya umma kuwajibika kwa serikali.
 
Mama Samia kuagiza BOT ifanyiwe special audits inadhihirisha jinsi usivyoweza kuachia tu mifumo ijifanyie mambo yao yaliyopo kikanuni
Maana yake mfumo umefeli, imagine kama rais mwenyewe angekuwa anahusika. Maana yake asingetoa hiyo order, na hakuna kile kingefanyika.

Kunatakiwa kuwe na layers nyingi zinazotazama uwajibikaji. US wana office za Inspector General kwenye key institutions. Kazi yake ni kudeal na misconducts za taasisi, mfanyakazi wa taasisi akiona issue ya hovyo inataka au inafanyika, na kama yeye hawezi kuzuia, anareport kwa IG. Na IG anatakiwa achunguze na analazimika kupeleka taarifa kwenye kamati ya sekta yake bungeni kuhusu malalamiko ya mfanyakazi. Akishindwa, mfanyakazi anaruhusiwa kuifuata kamati ya bungeni kuhusu IG kutofikisha report yake.

Kamati zao za bunge zina viongozi wa chama tawala na upinzani. Kukiwa na uchafu, sio kila mtu anavumilia, swali ni je kuna mfumo wa mtu mdogo kama junior accountant kwenye wizara au taasisi kujaribu kirekebisha? Wenzetu hapa wamekwenda mbali na kulihusisha hata bunge, maana vitu vingine serikali itaminya kwa sababu ni aibu yao. Accountability haitakiwi kuwa hisani ya kiongozi mmoja, jana Kakoko anaonekana wa maana, leo anaonekana hafai, nani anajua kesho itakuwaje.
 
Maana yake mfumo umefeli, imagine kama rais mwenyewe angekuwa anahusika. Maana yake asingetoa hiyo order, na hakuna kile kingefanyika.

Kunatakiwa kuwe na layers nyingi zinazotazama uwajibikaji. US wana office za Inspector General kwenye key institutions. Kazi yake ni kudeal na misconducts za taasisi, mfanyakazi wa taasisi akiona issue ya hovyo inataka au inafanyika, na kama yeye hawezi kuzuia, anareport kwa IG. Na IG anatakiwa achunguze na analazimika kupeleka taarifa kwenye kamati ya sekta yake bungeni kuhusu malalamiko ya mfanyakazi. Akishindwa, mfanyakazi anaruhusiwa kuifuata kamati ya bungeni kuhusu IG kutofikisha report yake.

Kamati zao za bunge zina viongozi wa chama tawala na upinzani. Kukiwa na uchafu, sio kila mtu anavumilia, swali ni je kuna mfumo wa mtu mdogo kama junior accountant kwenye wizara au taasisi kujaribu kirekebisha? Wenzetu hapa wamekwenda mbali na kulihusisha hata bunge, maana vitu vingine serikali itaminya kwa sababu ni aibu yao. Accountability haitakiwi kuwa hisani ya kiongozi mmoja, jana Kakoko anaonekana wa maana, leo anaonekana hafai, nani anajua kesho itakuwaje.
Umejaribu kuwaza kuhusu hizo cost implications za hizo layers za uwajibikaji? Tayari Tanzania ina changamoto ya kuwa na serikali kubwa, na kubuni layers za checks and balances za ziada ndani ya serikali isije ikawa ni kuiongezea uzito wa kibudget serikali, na hilo maana yake ni kutengeneza serikali yenye matumizi oversize.

Tanzania tuna tabia ya kusolve tatizo moja kwa kutengeneza tatizo jingine. Kama kuna tatizo la rushwa, basi unda taasisi uiite PCCB, PCCB ikienda kumkamata mla rushwa au mpokea rushwa, rushwa zaidi inafanyika hili mtuhumiwa asikamatwe. Perpertual cycle of corruption!

Kumodel kile wanachokifanya Marekani hapa Tanzania haiwezi kuwa bila na changamoto zake. Changamoto ya kwanza ninayoiona ni kwamba Marekani wanaishi kwenye social-economic climate tofauti na Tanzania. Kule private-sector ina nguvu na inainfluence kile kinachofanyika serikalini. Checks and balances, na levels za uwajibikaji zinazooperate kwenye private corporations kama microsoft zimekuwa modeled hata ndani ya public institutions za Marekani. Bosi wako immediate asiporidhika na utendaji anakufire tu, na ile inaleta discipline ya hali ya juu. Ila kwa nchi yetu iliyojengwa kwenye misingi ya kijamaa, ukiintroduce hiyo model utayasikia hayo mayowe. JPM si ndicho alichokuwa akifanya? Kwake aliichukulia Tanzania kama kampuni na yeye akiwa kama CEO, alitaka matokeo, tena matokeo sasa. Alipoanza kutumbua tumbua (private sector huwafire waajiriwa namna hii hii) nadhani uliyasikia mayowe. In short JPM alioperate bila kujijua kama maCEO wa big corporations wanavyooperate.
 
Nina wasiwasi hapa kuna watu wanajadili lakini hata maana ya neno lenyewe mfumo hawaijui.

Mfumo kwa kiingereza ni system, ikiwa na maana ni mchanganyiko wa vitu vinavyofanya kazi kwa pamoja ili kukikamilisha, mfano mfumo wa lugha unaunganisha vitu kama sauti, silabi, sentensi na tungo, au music system inaunganisha vitu kadhaa ili kuunda kimoja kinachoeleweka ndio maana tunaenda dukani kununua subwoofer.

Mpak kufikia hapa utaona wale wanaoamini mfumo unaundwa na individual person wanakosea, hakuna mfumo unaoundwa na mtu au kitu kimoja, lazima viungane vitu kadhaa ili kufanya kimoja kilicho kamili, hiyo ndio maana ya mfumo.
 
Umejaribu kuwaza kuhusu hizo cost implications za hizo layers za uwajibikaji? Tayari Tanzania ina changamoto ya kuwa na serikali kubwa, na kubuni layers za checks and balances za ziada ndani ya serikali isije ikawa ni kuiongezea uzito wa kibudget serikali, na hilo maana yake ni kutengeneza serikali yenye matumizi oversize.

Tanzania tuna tabia ya kusolve tatizo moja kwa kutengeneza tatizo jingine. Kama kuna tatizo la rushwa, basi unda taasisi uiite PCCB, PCCB ikienda kumkamata mla rushwa au mpokea rushwa, rushwa zaidi inafanyika hili mtuhumiwa asikamatwe. Perpertual cycle of corruption!

Kumodel kile wanachokifanya Marekani hapa Tanzania haiwezi kuwa bila na changamoto zake. Changamoto ya kwanza ninayoiona ni kwamba Marekani wanaishi kwenye social-economic climate tofauti na Tanzania. Kule private-sector ina nguvu na inainfluence kile kinachofanyika serikalini. Checks and balances, na levels za uwajibikaji zinazooperate kwenye private corporations kama microsoft zimekuwa modeled hata ndani ya public institutions za Marekani. Bosi wako immediate asiporidhika na utendaji anakufire tu, na ile inaleta discipline ya hali ya juu. Ila kwa nchi yetu iliyojengwa kwenye misingi ya kijamaa, ukiintroduce hiyo model utayasikia hayo mayowe. JPM si ndicho alichokuwa akifanya? Kwake aliichukulia Tanzania kama kampuni na yeye akiwa kama CEO, alitaka matokeo, tena matokeo sasa. Alipoanza kutumbua tumbua (private sector huwafire waajiriwa namna hii hii) nadhani uliyasikia mayowe. In short JPM alioperate bila kujijua kama maCEO wa big corporations wanavyooperate.
Kuhusu cost, kila kitu kina gharama. Ingawa kuna vingine tayari vipo kama kamati za bunge. Shida ni kuzitoa meno. Hata kufanya kazi zake zinashindwa
 
Nafikiri humaanisha kwamba kiongozi awepo pale kama robot, afu nchi, taasisi na idara zake vijiendeshe automatic kulingana na sheria mama ya nchi na sheria zinginezo. Kazi ya rais iwe ni kupewa taarifa, kushauriwa na kutoa maamuzi kulingana na alivyoshauriwa.

Mashabiki wa "mfumo imara" wanapenda nchi iongozwe hivi ili wafanye watakavyo. Ni wapigaji balaa, maana ndani ya "mfumo" ni kama serikali ndani ya serikali. Hawakumpenda JPM maana alivuruga hiyo "mifumo imara" yao, akatengeneza mfumo imara wake. Stuka mtu anayekwambia hatutaki kiongozi imara tunataka mifumo imara. Ni mafisi kwenye ngozi ya kondoo.
Wewe ulipenda 'Mtu imara', yupo wapi sasa..analiwa na mafunza huko. Utakaa unamlilia mpaka lini?
 
Mkuu, ukichunguza uzi huu utagundua ninafuatilia kila bandiko linalowekwa hapa. Lengo, nipate majibu nijifunze. Mwisho wa siku kwa pamoja tuamue kipi kinatufaa kama taifa, kwa msingi ule ule wa kuendeleza umoja, amani, ushirikiano,na ustawi katika nyanja zote za nchi yetu Tanzania. Binafsi nina imani na nguvu ya JF kufikisha ujumbe panapohusika.

Kwa msingi huo, bandiko lako limenichanganya hasa ukizingatia swali la msingi la uzi huu. 'Mfumo imara' ni nini?

Kwa hiyo, Mkuu naomba udadavue tena hoja yako. Natanguliza shukrani.
Hakuna mfumo wa namna nyingine utakaowezekana kwa nchi hii. Nchi hii msingi wake ulichimbwa na Nyerere ili tuongozwe kidikteta. Na huo ndiyo mfumo mpaka leo tunaufata na ni imara hapa. Na ukijaribu kuubadilisha mfumo tulionao, nchi itasambaratika halafu tutaanza upya tena. Ndiyo maana nchi nyingi zinazoongozwa kiditekta zikibadilisha mfumo zinasambaratika. Mfano mzuri ni nchi kama Iraq baada ya Wamarekani kumtoa Saddam na kuwaletea demokrasia.
 
Back
Top Bottom