Naomba kwenye mfano wa cover letter

malifimbo

Senior Member
Apr 2, 2013
127
29
Samahani kama una mfano wa cover letter naomba msaada nitumie kwenye hii email,msigwab@gmail.com

asanteni
 
Kizazi cha google hadi barua unataka copy an paste... changamsha akili fikiria unataka andika jambo gani kuhusu hiyo barua then labda kwa msaada wa format wa barua za kuombea kazi watu tukusaidie. Mambo mengne tusibweteke vijana EAC inakuja epuka kuwa tegemezi hadi kula mwenyewe baadae utashindwa kwa kusema hujui mdomo upo wapi.
 
Ni uvivu au? yaani barua tumejifunza kuandika tangu tukiwa primary...... sasa ata kama mimi HR nataka kukuajiri wewe inawezekana kweli... kama barua ni shida report utaweza kweli.... ni mawazo tu, barua ni kitu cha kuandika mwenyewe
 
ndio maana nimesema sample sio wote wanaojua kama ww na akili yako uliyo nayo bwana DAVION DELMONTE Jr
 
Google utapata sample unayoitaka then edit........ila angalia usicopy mpaka jina la mwenye hiyo sample kwani itakula kwako
 
format na maanisha bwana HEKIMA na GKM

Okay format yake huwa kama hivi ifuatavyo. Nitaweka namba kuashiri ndio kinachoanza mpaka mwisho na natumai itakuwa msaada kwako kaka mkuu.

1. Utaanza na anuani yako (adddress) ambayo hii itakaa upande wa kuliwa wa karatasi yako ya barua ya kazi. Na vitu vya kuzingatia ni jin lako kamili, sanduku la posta, mjini, nchi, na utamaliza na namba zako za simu pamoja na barua pepe kama utakuwa nayo.

2. Utaandika anuani ya sehemu unayopeleka hiyo barua yako. Kwa mfuatano kama wa namba 1 ila kumbuka tu kuwa hapo utaiandika barua inaenda kwa nani kwa kuandika cheo chake HR, GM, CEO nk. NB: hii itakaa upande wa kushoto

3. Utafungua barua kwa kuandika Dear sir/ madam / ambayo utaandika chini ya anuani ya ofisi chini japo ruka mstari mmoja.

4. Kichwa cha habari ambayo inakuwa na YAH: au ref: kwa lugha ya kiingereza na utaandika dhumuni lako katika kichwa hicho cha habari.

5. Utaandika barua yenyewe chini ya kichwa cha habari. Kumbuka kuanza kwa aya kwa kila jambo lenye uzito aidha unaelezea sifa yako au elimu au jambo lolote lile.

6. Ni Saini yako ambayo itakaa upande wa kushoto wa aratasi yako

Nadhani kwa uchache utakuwa na official letter nit and clear kwa maudhui uliyolenga. Hope itakiwa msaada japo kwa uchache. Asante.
 
...duuuh
tapatalk_1561310695681.jpeg
 
Back
Top Bottom