ekibira_ishengo
Member
- Oct 31, 2016
- 37
- 15
Miaka inakwenda siku zinapita , Maisha yana zidi kuwa magumu kisa yaweza kuwa mambo mengine lakini kwa kuwa tuliwekeza kwenye kupanda mbegu DECI miaka ya 2007,2008,na 2009 nalaani kuwa walioizuia DECI ndio wanaosababisha maisha haya kuwa magumu. Tena niwambie heri mimi kwani sikujiunga mwanzo! Niliingia mwishoni! Wako Watumishi wa Serikali (Walimu, Manesi, Waganga Wahudumu na wengine wengi), Wafanya Biashara, Wakulima ambao wameuza nyumba, magari mashamba na mali nyinginezo nyingi na wako hata ambao pengine waliishia mahakamani kutokana na kusimamishwa ghafla mpango huo. Nawaomba nguvu wana Jamii Forum saidia kupaza sauti ili watu wapate fedha hizi hali ni mbaya! Serikali ilizuia mpango huo na ikafunga kesi ambayo hivi sasa imekwisha yapata miaka miwili iliyopita. Kwa fununu fedha hizi zilikuwapo Je Serikali na Mahakama mnataka wale Jamaa wa DECI wapotee na fedha hizo?