mchezo mbaya
JF-Expert Member
- Feb 11, 2017
- 242
- 235
Nilishinda kesi ya jinai katika Mahakama ya mwanzo (kuvunjiwa na kuibiwa). Baadae nikashauriwa nifungue kesi ya madai ili nilipwe haki zangu yaani pesa inayolingana na thamani ya vitu nilivyoibiwa. Naombeni msaada wa kisheria au ushauri ili nipate haki haraka na iliyokamilika. Pesa ninayoidai in TShs 3,000,000/= inayoendana na vitu vilivyoibwa. Kingine ni nyaraka ambazo ni hati za nyumba. Naomba kujua ni Mahakama IPI inaweza kunipa haki vizuri?. Na je, Nakala ya hukumu pekee inatosha kuwa ushahidi bila kuwahusisha tena mashahidi?.Maana nasikia kuwa Mahakama za mwanzo zina mipaka yake kimaamuzi ambayo ni tofauti na za Wilaya. Natanguliza shukurani.