Naomba kujuzwa sehemu ninayoweza kupata tairi za bei nafuu

Killmonger

JF-Expert Member
Jan 11, 2015
2,014
2,231
Wakuu nawasalimu,

Mimi bwana tokea ka gari kangu kaingia hapa mjini Dar es Salaam sikuwahi badilisha tairi zake. Nilikwenda mkoani kama safari nne hivi na tairi ya mbele kushoto ikapata slow pancha. Fundi umesisizita nibadili tairi zote (nakubaliana na yeye kwani zimesha expire ).

Shida wakuu ni budget imebana. Budget yangu maximum ni laki na 20 (120,000) tu. Ni wapi karibu naweza pata tairi yenye unafuu kwenye quality ( naishii maeneo ya Victoria DSM) kwa budget yangu hii? Na jina ya tairi husika!
Size ni 205 , 65 , rim 15.

Natanguliza shukrani kwa michango yenu.
 
Pole sana. Pia hongera kwakununua gari. Kwa usalama wako, usalama wa chombo chako na wengine, nakushauri jitahidi tu kununua matairi mapya bila kuangalia sana bei kwani hayo ya rahisi yana madhara yake, kwani mengi hayana viwango.
 
Pole sana. Pia hongera kwakununua gari. Kwa usalama wako, usalama wa chombo chako na wengine, nakushauri jitahidi tu kununua matairi mapya bila kuangalia sana bei kwani hayo ya rahisi yana madhara yake, kwani mengi hayana viwango.

Asante mkuu. Ni kweli ulichosema shida ni budget tu. Nimepanga kuweka hizi za bei rahisi kwanza then mambo yakikaa sawa naweka buti za JEJE.
 
Nenda kwenye sehemu za kubadili matairi maeneo ya ushuani kama Masaki au Mikocheni uongee na wale wafanyakazi wakutafutie hizo tairi wakivua kwenye gari za kampuni au matajiri.

Unaweza kwenda Cruise Inn au the wheel waambie wafanyakazi wakutafutie tairi used zilizo katika hali nzuri.
Utapata Pirelli,Good ride,Yokohama used kwako zitakuwa mpya.

Pia tafuta connection za wale vijana wanaotumwa na matajiri kubadili tairi, utapata tyre za hitaji lako.
 
Nenda kwenye sehemu za kubadili matairi maeneo ya ushuani kama Masaki au Mikocheni uongee na wale wafanyakazi wakutafutie hizo tairi wakivua kwenye gari za kampuni au matajiri.

Unaweza kwenda Cruise Inn au the wheel waambie wafanyakazi wakutafutie tairi used zilizo katika hali nzuri.
Utapata Pirelli,Good ride,Yokohama used kwako zitakuwa mpya.

Pia tafuta connection za wale vijana wanaotumwa na matajiri kubadili tairi, utapata tyre za hitaji lako.

Asante mkuu
 
Mimi ni muuzaji wa matairi ya magari kwa size ya gari lako nina kampuni zifuatazo
Dunlop made in South Africa 140000
Goodride made in China 120000
Sportrack made in China 110000
Napatikana Kariakoo mtaa wa swahili na twiga
0714360270
Duka lako lipo wapi? Hizi bei zinafikirisha. Hasa hiyo ya Dunlop.
 
Bei inaweza kuwa sawa.Mchina kawashikisha adabu.Mfano nilishanunua good year za S.Afrika kwa 180k ila kwa sasa ni 120k
 
Back
Top Bottom