Uzi maalumu wa kujua gharama za ujenzi wa majengo mbalimbali

Englishman

New Member
Jul 13, 2018
2
2
Habari wadau,

Naomba msaada wa gharama za ujenzi wa nyumba ya vyumba 2(self), sitting room & kitchen.

maeneo ya Mwanza Busweru.

Habari zenu, Naomba kujuzwa rough estimate za kujenga nyumba ya maelezo hayo hapo chini;
1. Ya kisasa kidogo
2. Size: Plot ya 18x25
3. Eneo: Moshono, Arusha (kwa Laizer)

Hitaji:👇
  • 1 Master Bedroom
  • 2 Bedrooms ( Zote 2 Self Contained)
  • Sitting Room
  • Open Kitchen + Store
  • Dinning
  • Public Bathroom + Toilet
* Kupauwa napauwa na Mabati mgongo mpana.

🙏 Tafadhali naombeni makadirio ya kuanzia chini hadi nyumba kupauliwa.

NOTE: Natashukuru pia kupendekezewa mchoraji mzuri asiye na gharama... Na Mjenzi kwa maeneo ya Arusha ambye mwaminifu.

🙏 NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU.
 
Wakuu naomba ushauri wenu au uchambuzi wenu wa kujua (roughly estimates) gharama za ujenzi wa nyumba ya vyumba vitatu yenye ifuatavyo (ukubwa wa 17 kwa 12)
1.master 1 na self 2
2.sitting room
3.dining room
4.jiko na store na public toilet
Gharama ya kwa ujumla (material +ufundi) kuanzia msingi,boma, kupaua, blundering hadi kuezeka bati la royal romantile la alaf, mashimo yachimbwe kabisa na grill ziwekwe. Kabla ya plasta na jamvi. Kwa ujumla itagharimu kama kiasi gani... Naomba msaada wenu kwa ujuzi wenu.. Yaani usiwe na upungufu wa kiasi gani??
 
Uko mkoa gani? ama wilaya gani? sikia nkuambie tukikupa estimates unaweza ukajiona hujengi, Anza na fundi wako na uanze kidogo kidogo!

kiuhalisia nyumba unayotaka angalau anza na 5m, Ila kufika mpaka uliposemea angalau 45m.
Nipo dar-Goba, nataka nijue ili nisipigwe sana yaani nijue nachezea wapi.. Nimeamua kujenga ila nataka niwe na idea kidogo kuwa nitasimama wapi hadi wapi
 
Umejiminya Sana 30 million , bila stress 40-45 millions ,mziki upo kwenye finishing , unaweza itoroka nyumba Kwa mda
 
Habari Mkuu, nina fundi mzuri sana anajenga mpaka finishing zote anafanya. Kama ukimhitaji karibu nikuunganishe naye.
 
IMG_9718.jpg
 
Naomba kujua gharama za ujenzi mpaka lenta.

Urefu 18m upana 14mita
vyumba vitatu, kimoja masta, seble choo public na stoo pemben ndogo, Dar es Salaam.
 
mkuu kwa upande wangu hii nyumba ni kubwa sana ungeweza hata kutoa vyumba vinne vya kulala,bila shaka vyumba ni vikubwa na seble ni kubwa,sasa ngoja nikushauri , kama unapenda nyumba kubwa ni sawa endelea na hio ramani,ila kama sio mpenzi wa nyumba kubwa hakikisha wakati wa kuseti msingi unapunguza vipimo,kwa makadirio hapo andaa kama 15m kufikia lenta(inaweza kuzidi) ,kupaua kama utatumia bati kigae andaa 15 m ,ya kawaida migongo mipana inaweza kucheza 12m - 13m,All the best.
 
Wakuu naomba ushauri wenu au uchambuzi wenu wa kujua (roughly estimates) gharama za ujenzi wa nyumba ya vyumba vitatu yenye ifuatavyo (ukubwa wa 17 kwa 12)
1.master 1 na self 2
2.sitting room
3.dining room
4.jiko na store na public toilet
Gharama ya kwa ujumla (material +ufundi) kuanzia msingi,boma, kupaua, blundering hadi kuezeka bati la royal romantile la alaf, mashimo yachimbwe kabisa na grill ziwekwe. Kabla ya plasta na jamvi. Kwa ujumla itagharimu kama kiasi gani... Naomba msaada wenu kwa ujuzi wenu.. Yaani usiwe na upungufu wa kiasi gani??
35 hadi 45M.

Nimeona site moja hadi sasa wanapaua na shimo la choo limefunikwa, tayari imegota 20M.

Kwa hiyo kuna kazi kibao hazijafanyika.
 
Back
Top Bottom