Naomba kujuzwa gharama za msingi kwa nyumba ya ghorofa moja

Sihitaji polee, najitambua na najua ninachokifanya, pole unahitaji wewe unayejidai Engineer halafu kichwani mtupu, unajisifu ujenzi umeanza zamani, hujui hata wahuni pia wanazeeka?
Endelea kudhihirisha uzito wa kichwa chako kwa kuingilia taaluma za watu. Napiga kazi, wateja wanaridhika na maisha yangu yanaenda swaaafi kabisa. Endelea kubwabwaja kujiona unajua kila kitu kumbe wanaojua wanakuchora tu.
 
Ni kweli chuma iko juu Sana, Ila 50M ni mbali Sana mkuu. Hiyo ramani yake hata sio kubwa kivile.
Nimejenga msingi mkubwa kuzidi huo kwa size na ugumu wa mazingira. Ila umekula around 22M, tena ni mkoa wenye vitu bei juu zaidi.
Kaka unaweza niunganisha na jamaa waliokujengea msingi
 
MREJESHO: Nakaribia kumaliza msingi wa ki GHOROFA, lakini 10M haijaisha bado. Nadhani wakadiriaji wengi au makampuni ya ujenzi yanatukatisha tamaa sana wananchi, niliogopa waliponiambia 50M kuweka msingi

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile ap
MREJESHO: Nakaribia kumaliza msingi wa ki GHOROFA, lakini 10M haijaisha bado. Nadhani wakadiriaji wengi au makampuni ya ujenzi yanatukatisha tamaa sana wananchi, niliogopa waliponiambia 50M kuweka msingi

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
Mkuu unaweza niunganisha na mafundi wako msaada
 
ushauri tu awe na hiyo kitu. kuna chuma zinasukwa chini (base) na kuzunguka msigi wote, kuna tofali zinazikwa kozi zaidi ya saba za kulaza, kuna mkanda unapigwa mzunguko wote, kuna zege chini kwenye base na huo mkanda, kuna kifusi cha kujaza, kuna framework za kufunga na mambo ya mafundi. Basically, ata cement. mchanga, na kokoto zote zimepanda
Duuu
 
Kumbe bado nilikuwa sijafika kwenye ujenzi wa ghorofa, Muda huu nipo Kwa slab inataka kunitoa roho, nitaleta mrejesho.
Nimeanza kusoma tokea mwanzo, comment kwa comment. Nimejifunza mengi. Hongera kwa uthubutu mkuu. Na pia usiache kutupa mrejesho, inatusaidia kujipima kwa sisi tunaojipanga kujenga
 
Mkuu ulitutia moyo kule kwenye msingi wa 10m, sasa inakuwaje tena. Tupe vitu slab imekunyuka bei gani. Weka ramani yako hapa vizuri tuigilizie
Endeleeni na ujuaji wenu na kujenga misingi ya ghorofa kwa 10M
Screenshot_2022_1219_175429.jpg
 
MREJESHO

Hatimaye sasa nimekuja kureta mrejesho hapa,kaa kitako na ujiandae kujenga ghorofa.

1. Msingi nimetumia 8,528,200
2.Shimo la choo ni 1,237,500
3.Boma ni 5,029,200
4.Kumwaga slab ni 16,537,000
5. Kulaza Bomba za umeme kwenye slab ni 220,000
Asante kwa mrejesho mkuu.
1. Slab ni mita ngapi za mraba?
2. Vipi nguzo ni ngapi na umetumia kiasi gani.
3. Boma ni full kwa floor 2 au ni ya floor ya kwanza tu?
 
Back
Top Bottom