Naomba kujuzwa bei ya Phantom X

Hio bei ni fake, hizo website ni bots tu za computer zinaguess bei.

Nigeria ni Naira 250k ambayo ni around 1.4m

Kenya ni Ksh 50k ambayo ni around 1.1m


Na Tanzania imewekwa link ya 1.3m huko juu.

Hivyo mkuu unapigwa Helio G95 kwa zaidi ya 1m,
Kwa hiyo hapa kwa hii simu kihalal tungetakiwa kununuwa bei gan mkuu mana mnaruambia tunapigwa mm binafs nilitaka kwenyda kununua hii sim lakin baada ya haya hapan binafsi mamb ya processa nilikuwa siyajui us long us sim ilikuwa inatamia ramu 8 na rom 256 kioo super amoled nikajuwa ni simu bora kumbe wap
 
Mambo ni mengi sana Mkuu, ila simu si kama pc, jambo muhimu kabisa la kuangalia ni soc (system on chip) hii ina include vitu kama processor, gpu, aina za ram, modem ya internet, processor ya camera, Bluetooth, wifi etc. Vitu vyote hivi vinakuwa kwenye package moja.

Mfano simu mbili zina snapdragon 865 basi ni lazima zote ziwe na processor moja, gpu moja, ram za Aina moja, wifi aina moja, modem aina moja etc.

Kama soc ni nzuri automatic Ita affect
-ukaaji chaji, soc efficient itakaa na chaji sana hata kama battery ni dogo.
-camera nzuri, Kuna simu za kichina hazina camera nzuri ila sababu zina soc nzuri unaweka Gcam na inaongeza ubora wa picha.
-speed ya storage
-resolution ya Display
-fast charging
-idadi ya network band etc.

Hivyo kwangu mimi soc kwanza, soc ikishakuwa nzuri ndio na Angalia camera, display na mambo mengine
Na ukubwa wa oamera tunapaswa tuangalie nn mega pixels au
 
Na ukubwa wa oamera tunapaswa tuangalie nn mega pixels au
Mega pixel ni ukubwa wa picha, hizi camera za siku hizi zinafanya oversampling, mfano camera ya 48mp unapiga picha 4 za megapixel 12 na kuziunganisha kupata picha moja nzuri ya 12mp.

Hivyo unless unapiga picha za Mabango ya barabara I usiangalie wingi wa megapixel kama kigezo.

Hii phantom hardware wise si mbaya hio camera ni nzuri sana, tatizo litakuja tu hio soc (processor) waliotumia ni ndogo itaikwamisha hio camera.
 
Kwa hiyo hapa kwa hii simu kihalal tungetakiwa kununuwa bei gan mkuu mana mnaruambia tunapigwa mm binafs nilitaka kwenyda kununua hii sim lakin baada ya haya hapan binafsi mamb ya processa nilikuwa siyajui us long us sim ilikuwa inatamia ramu 8 na rom 256 kioo super amoled nikajuwa ni simu bora kumbe wap
Kwa kuangalia simu zenye soc kama hii
-redmi note 10s inauzwa $199
-realme 8 around $250
-Realme Narzo 30 around $250

Hivyo ulitakiwa iuzwe around laki 5 mpaka 6 hivi, Sema sababu ina premium feature kama 8gb na 256 storage hata ingezidi laki ikawa laki 7 si mbaya.

Mkuu ukishakuwa na Budget kuanzia laki 8 kupanda ni vyema ukaanza kuangalia Flagship phone. Achana na hizi midrange.

Kwa laki 8 Kenya Avechi Unapata Oneplus 7 ama 7T yenye storage 256GB na ram 8 ama 12GB, flagship soc kama sd 855, camera nzuri, storage za kisasa za ufs, USB 3 etc.
 
Njia rahisi mkuu ni kufuatilia habari za vitu vinapotokea.
Mfano.
1. Sony walitangaza sensor yao mpya ya 50MP ambayo itatumika kwenye flagship, hivyo unaanza kuona simu kibao zinatumia.

2. Samsung Wana display mpya za LTPO Amoled simu zote mpya za kisasa zinatumia,

3.umoja wa usb umetangaza usb type C itapitisha umeme hadi watts 240

4. Samsung katangaza ram za lpddr5

5. Storage Mpya za ufs 3.1 etc.

Hivyo unapo kuwa na habari za vitu vinapotokea wewe Uta judge sasa kama hii simu imepack feature zote za kisasa?

Mfano hii phantom X, ina flagship camera 50mp, ina maana imetick kwenye camera lakini soc sio flagship material, haina ddr5, fast charging ya kawaida, haina ltpo display etc.

Na njia nyengine ni kuangalia reviews online, toka website maarufu.
Hiz taarifa za kina sumsung na song tunaweza kuzipata kweny platform mana ukiangalia kweny page ya sumsung Twitter wanatoa habar za simu tu
 
Kwa kuangalia simu zenye soc kama hii
-redmi note 10s inauzwa $199
-realme 8 around $250
-Realme Narzo 30 around $250

Hivyo ulitakiwa iuzwe around laki 5 mpaka 6 hivi, Sema sababu ina premium feature kama 8gb na 256 storage hata ingezidi laki ikawa laki 7 si mbaya.

Mkuu ukishakuwa na Budget kuanzia laki 8 kupanda ni vyema ukaanza kuangalia Flagship phone. Achana na hizi midrange.

Kwa laki 8 Kenya Avechi Unapata Oneplus 7 ama 7T yenye storage 256GB na ram 8 ama 12GB, flagship soc kama sd 855, camera nzuri, storage za kisasa za ufs, USB 3 etc.
Je hiz simu tunazouziwa bongo ambazo ni refurbish na used kutoka uk na korea ni nzuri mana naona watu wanauza sumsung s10+ kwa 700k
Na je nawezaje kununuwa simu kutoka kenya na nikaipata bongo bila shaka mana wakenya siku hiz wamekuwa wapigaj sana
 
Hiz taarifa za kina sumsung na song tunaweza kuzipata kweny platform mana ukiangalia kweny page ya sumsung Twitter wanatoa habar za simu tu
Hawawezi kutangaza kwenye page za Twitter, Tafuta site ya habari za Tech kama Gsmarena, neowin, Engadget, the verge, Arstechnica etc ambayo unaona inafit taste zake visit Mara kwa Mara kupata habari.
 
Je hiz simu tunazouziwa bongo ambazo ni refurbish na used kutoka uk na korea ni nzuri mana naona watu wanauza sumsung s10+ kwa 700k
Na je nawezaje kununuwa simu kutoka kenya na nikaipata bongo bila shaka mana wakenya siku hiz wamekuwa wapigaj sana
Avechi wanatuma ni Kampuni kubwa, usinunue mtaani matapeli wengi. Kama una mtu unamjua vyema akununulie kule akutumie na Basi.

Kuhusu Refurbished kama hufahamu simu vyema uka kaa nazo mbali, zina matatizo mengi sana.
 
Je hiz simu tunazouziwa bongo ambazo ni refurbish na used kutoka uk na korea ni nzuri mana naona watu wanauza sumsung s10+ kwa 700k
Na je nawezaje kununuwa simu kutoka kenya na nikaipata bongo bila shaka mana wakenya siku hiz wamekuwa wapigaj sana
Wenzenu siku hizi tunachofanya bongo,unaanza kuzoeana na mmiliki wa duka la simu kwanza.
Ukivuka kizingiti hicho ni rahisi sana kukuacha ukague simu pale pale mpaka uridhike kabla hujachukua ni rahisi pia kuirudisha kama ina shida.

Kinyume na hapo bro,ongeza 40% ya bei ya simu husika kisha nenda kwa wajamaa wanaoitwa dealers.
 
Haipo tigo shop
avechi 4GB/64GB version ni 324,000, 128gb version ni 361,000. kama una mtu unamjua itaongezeka kama 20,000 mpaka kukufikia. Avechi wenyewe kukutumia wanachrage 2500 (53,000).

hivyo kivyovyote haifiki laki 4, Tigo wanauza laki 5.
 
Avechi wanatuma ni Kampuni kubwa, usinunue mtaani matapeli wengi. Kama una mtu unamjua vyema akununulie kule akutumie na Basi.

Kuhusu Refurbished kama hufahamu simu vyema uka kaa nazo mbali, zina matatizo mengi sana.
Hawa nitawapataje mkuu wana website??
 
Wenzenu siku hizi tunachofanya bongo,unaanza kuzoeana na mmiliki wa duka la simu kwanza.
Ukivuka kizingiti hicho ni rahisi sana kukuacha ukague simu pale pale mpaka uridhike kabla hujachukua ni rahisi pia kuirudisha kama ina shida.

Kinyume na hapo bro,ongeza 40% ya bei ya simu husika kisha nenda kwa wajamaa wanaoitwa dealers.
Kama sijakuelewa bro yan niongeze 40% kivip
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom