Kuna tofauti gani kati ya Hayati na Marehemu?

Kwa muda mrefu sana nilikua nikisikia toka kwa ndugu na watu wengine wakimuita merehemu mtu alie kufa siku nyingi zilizopita.

Hivo ilinijengea mimi pia mazoea ya kumuita marehemu, mtu alie kufa mda mrefu.

Pia nimekuwa nikisikia katika vyombo vya habari wakimuita hayati mtu ambae amekufa muda mrefu lakini akiwa na cheo fulani.

Kwa hivo katika fikra zangu zimeweza kufikiri kuwa huenda kuna makundi mawili ambalo kundi la kwanza ni la wale wasio na cheo chochote katika taifa ndio huitwa marehemu lakini pia kundi la pili ni la wale wenye vyeo katika taifa ndio huitwa hayati, sina uhakika na fikra zangu.

Kwahivo nimeona ni bora niilete huku mada ili niweze kupata uhakika wa tofauti kati ya marehemu na hayati.

JamiiForums great thinker.
Hayati hutumika kwa watu waliokuwa na nafasi kubwa katika taifa kwa mfano mwalimu Nyerere huwezi kusema tu marehemu mwl. JK Nyerere bali yeye huwa tunasema Hayati mwl. JK au Karume huwa tunasema Hayati Abeid Aman Karume. Lakini akifa hohe hahe kama Bwana Kaduga tutasema Marehemu Bwana Kaduga!!
 
Mimi ni Kapuku flani tu, ila naomba nikifa mnipe cheo cha hayati kama hayati Bob Marley na hayati Tupac...:):):)
 
Mimi ni Kapuku flani tu, ila naomba nikifa mnipe cheo cha hayati kama hayati Bob Marley na hayati Tupac...:):):)
Hilo neno hayati waswahili wa mwanzo walilielewa vibaya,ni neno la kiarabu lenye maana hai milele,sasa mtu kafa anakuwaje hayati!?
 
Hilo neno hayati waswahili wa mwanzo walilielewa vibaya,ni neno la kiarabu lenye maana hai milele,sasa mtu kafa anakuwaje hayati!?
Ina maana wewe hujui kwamba kuna watu wamekufa lakini wanaishi?

Ni kwa nini kila siku kwenye tv zenu mnaweka nukuu za Nyerere?

Bob Marley muziki wake kuna mtu ameweza kumpiku mpaka leo? Jiulize mwenyewe marehemu kwa miaka karibu 30 waluo hai wanashindwa kumbeat.

Hayati ni neno sahihi kwa watu hao.
 
Ina maana wewe hujui kwamba kuna watu wamekufa lakini wanaishi?

Ni kwa nini kila siku kwenye tv zenu mnaweka nukuu za Nyerere?

Bob Marley muziki wake kuna mtu ameweza kumpiku mpaka leo? Jiulize mwenyewe marehemu kwa miaka karibu 30 waluo hai wanashindwa kumbeat.

Hayati ni neno sahihi kwa watu hao.
Hayati sokoine,hayati kolimba
 
Ni nani anatakiwa aitwe Marehemu na ni nani anatakiwa aitwe Hayati na ni wakati gani haya Maneno mawili yanatakiwa Kutumika hasa 'Kiuwasilishaji' pale linapotakiwa Kuelekezwa kwa Mhusika ( aliyeaga ) dunia?

Ni maneno ambayo kwa muda mrefu yananichanganya na Kunifikiisha mno hivyo ni matumaini yangu leo hii wana JamiiForums ( Great Thinkers ) na Wabobezi Waandamizi wa Lugha adhimu ya Kiswahili mtanielimisha.

Ahsanteni.
 
Aliyefariki anaweza kuitwa hayati kama alikua kiongozi wa juu kabisa wa serikali
Aliyekufa hawezi kuitwa hayati huyu ni marehemu tu..

Kuna ku-dead na ku-pass away

Shukran kwa Elimu yako ya awali na ngoja niwasubiri wengine ili niweze kuelimika zaidi juu ya haya maneno mawili ' sumbufu ' Kwangu ya Marehemu na Hayati.
 
Kufa hutumika kwa wanyama wasio binadamu na kufariki kwa binadamu.

Hayati hutumika kwa waliokuwa au viongozi wajuu kisiasa waliofariki. Nijuavyo mimi hayati laweza kutumiwa kwa Waziri mkuu na Rais.

Marehemu ni kwa wengine wote,mfano wafanya biashara wakubwa, watu mashuhuri na cheap labour wengine.

Kwamujibu wa kamusi ya TUKI

Marehemu - mtu aliyefariki

Hayati - si mfu si mzima

Yaani mtu ambaye amefariki lakini anaishi katika ulimwengu uliopo kwa mchango wake katika nchi. Wakimaanisha kuwa yale aliyoyafanya marehemu yanaishi.
 
GENTAMYCINE, p



Mkuu maneno yote hayo yametokana na lugha ya kiarabu, Marehemu (Marhum/ مرحوم) ni sifa inayotangulia kutajwa kabla ya jina la mtu aliyefariki/ kufa, ni sawa na neno la kiingereza "late".

Hayati (Hayah/حياة) maana yake kwa kiswahili ni maisha (life), sasa ni kwa namna gani limeingia katika kiswahili na kutumika sawa na maana ya neno Marehemu (Marhum) waje wataalamu watujuze, ila neno safi, kwa maoni yangu, linalofaa kutajwa kabla ya kutaja jina la mtu aliyefariki ni jina Marehemu.
 
Hakuna utofauti hapo katika lugha tunaita visawe yani maneno yenye matamshi na uandikwaji tofauti ila maana yake ni moja tu,

Hii inatokana na nini hutokana na tabia ya lugha kukua hasa ukopaji wa maneno na utohoaji ndio hupelekea haya kutokea mfano hayati ni kiarabu, marehemu imetokana na kngereza neno late
 
mfano hayati ni kiarabu, marehemu imetokana na kngereza neno late



Hayati na marehemu yote yametokana na lugha ya kiarabu, na kwa mujibu wa lugha ya kiarabu neno Marhum (marehemu kwa kiswahili) ndio lina maana ya "late" katika kiingereza.

Neno hayati kwa kiarabu maana yake ni maisha., sasa limeingiaje katika kiswahili kwa maana ya marehemu, hilo ni suala la kupeleleza.
 



Hoja yangu ipo katika jambo hili kwamba maneno yote hayat / hayati na marehemu yametokana na maneno ya kiarabu (lugha ya kiarabu), ama kwa kiswahili yawe visawe (synonym) au vyovyote sio hoja yangu.

الحياة في الدنيا (alhayaat fii duniya)= maisha duniani
الحياة (alhayaah)= maisha
حياتي (hayaati)= maisha yangu.

مرحوم (marhuum)= marehemu.


Kwahiyo utaona neno hayati la kiswahili limetokea humo kwenye kiarabu, because it has got something to do with life and life is related to death, nadhani ndipo waswahili wakalichukua kimakosa na likawa loosely used todate.
 
Ni nani anatakiwa aitwe Marehemu na ni nani anatakiwa aitwe Hayati na ni wakati gani haya Maneno mawili yanatakiwa Kutumika hasa 'Kiuwasilishaji' pale linapotakiwa Kuelekezwa kwa Mhusika ( aliyeaga ) dunia?

Ni maneno ambayo kwa muda mrefu yananichanganya na Kunifikiisha mno hivyo ni matumaini yangu leo hii wana JamiiForums ( Great Thinkers ) na Wabobezi Waandamizi wa Lugha adhimu ya Kiswahili mtanielimisha.

Ahsanteni.
Marehemu ni maiti. Na maiti ni mwili wa mfu. Ule mwili unaoubeba kwenda kuuzika ndio marehemu. Hayati pengine kwa makusudio ya kiswahili ni mtu aliyewahi kuishi. Kwasababu muda ukishapita mwili hupotea hubakia sifa tu kwamba fulani aliishi. Na pengine pia hutumika neno hayati kama kwamba mtu huyo bado yuko pamoja nanyi
 
Marehemu ni maiti. Na maiti ni mwili wa mfu. Ule mwili unaoubeba kwenda kuuzika ndio marehemu. Hayati pengine kwa makusudio ya kiswahili ni mtu aliyewahi kuishi. Kwasababu muda ukishapita mwili hupotea hubakia sifa tu kwamba fulani aliishi. Na pengine pia hutumika neno hayati kama kwamba mtu huyo bado yuko pamoja nanyi


Mkuu, hapo siyo sahihi kwamba Marehemu ni maiti??!!.

Marehemu ni jina la sifa linalotangulia jina halisi la mtu kumtambulisha kwamba mtu huyo kisha fariki.

Mfano, unaposema; Marehemu Julius Nyerere, hapo maana yake huyo Julius Nyerere kishafariki.

Na labda watu wakitaka kujua mahala alipofariki, watauliza; alifia wapi??, jibu litakuwa; alifia London, labda watauliza; mwili wake (maiti) uliletwa vipi??, jibu litakuwa uliletwa (ulisafirishwa) kwa ndege.

Hivyo, ni kwamba Marehemu siyo maiti, maiti ni corpse na marehemu ni late katika kiingereza, nadhani hata katika lugha zingine, mfano Kiarabu nk, kuna maneno tofauti katika maiti na marehemu.


Hayo maelezo yako kuhusu neno "hayati" yameniingia akilini kwa mbali nitayafanyia kazi.

Shukrani.
 
Hayati ni marehemu, lakini sio kila marehemu anaweza kuwa hayati, Hayati ni mtu aliyekuwa na mchango mkubwa kwa jamii na taifa lake kwa ujumla, marehemu ni mtu yoyote aliyefariki
 
Kwa wenye bahati ya kuingia uchumi wa kati, kuna tofauti kati ya maiti, hayati na marehemu? Inachukua muda gani aliyefariki kuitwa hayati na kwa mazingira gani?
 
Back
Top Bottom