Kuna tofauti gani kati ya Hayati na Marehemu?

kamkoda

JF-Expert Member
Sep 20, 2012
396
71
Kwa wale wajuzi wa lugha yetu tofauti ya maneno hayo ni nini hasa?

Michango ya wadau
Hayati ni neno la kiarabu likimaanisha uhai, kwa hiyo mtu aliyekufa na kuacha Legacy yaani bado kuna vitu alifanya kwa manufaa ya jamii au dunia na bado vinaishi huyu ndiye huitwa hayati kwa maana kafa lakini bado anaishi kutokana na legacy aliyoiacha wala siyo lazima kuwa maarufu au tajiri.

Hata Masikini anaweza kuacha Legacy, kwa mfano anaweza kusema ana eneo lake ligeuzwe kujengwa shule au hospitali au kisima au msikiti au kanisa na ikafanyika hivyo huyu ni hayati maana kaacha legacy kile alichokuwa akimiliki pamoja na umasikini wake bado kinaishi na kinainufaisha jamii aliyoiacha.

Mwingine anaweza kufundisha ujuzi vijana na wale vijana wakanufaika na ule ujuzi na ukanufaisha jamii, kwa hiyo elimu yake aliyoitoa bado inaishi na inainufaisha jamii huyu naye ni hayati.

Lakini ukifa na kashfa kibao za ufisadi wa mali, ufisadi wa mapenzi au dhulma au uchawi yaani kifo chako kikaleta nafuu kwa jamii, basi wewe ni marehemu tu huwezi kupewa heshma ya kuitwa hayati.

Kwa hiyo kila mtu ajitathmini kama yeye akifa ataitwa Hayati au Marehemu?
Mimi nijuavyo maneno yote mawili marehemu na hayati hutumika kwa kutangulizwa kabla ya kutaja jina la mtu aliyekwisha kufariki.

Lakini tofauti yake ni kwamba neno marehemu linatumika bila kujali kama aliyefariki amefariki leo muda mfupi uliopita, wiki iliyopita, miaka kumi, miaka hamsini au zaidi iliyopita wakati hayati linatumika pale mtu anaezungumziwa habari zake alikuwa ni mtu maarufu katika jamii tena anakuwa alifariki muda mrefu kidogo uliopita pengine miaka kadhaa nyuma mfano hayati Mwalimu Nyerere, hayati Shaaban Robert na wengineo. Pengine ndiyo maana mleta mada umekuwa ukisikia akina "hayati" wachache tofauti na marehemu kwa sababu wengi tunakufa bila umaarufu wowote au kuacha legacy yoyote nyuma yetu.

Sijawahi kusikia mtu aliyefariki mfano leo asubuhi au jana akatanguliziwa jina la hayati.
 
Ningependa kujuzwa tofauti ya vyeo hivi wanavyopewa watu walio fariki, wengne wanaitwa Hayati na wengne Marehemu..

Mfano HAYATI JULIUS K. NYERERE, MAREHEMU STEVEN KANUMBA..
 
Nijuavyo marehemu ktk uhai wake was just a mere persön mwenye maisha ya kawaida while hayati wanakuwa na title flan ktk jamii!
 
Kaaaazi kweli kweli kiongozi.Marehemu ni jina apewalo mtu YEYOTE aliyefariki.Hayati ni mwenye uhai.
 
Kaaaazi kweli kweli kiongozi.Marehemu ni jina apewalo mtu YEYOTE aliyefariki.Hayati ni mwenye uhai.

Mmh mkuu unajua mtu anapouliza sometime anakua serious anataka kujua,sasa unapomwambia kitu kama hicho hapo cjui kama unamtendea haki,anajua wote wanakuwa wamefariki sasa wewe unamwambia hayati anakuwa hai tena duuh,,ni shidaaaah
 
Mmh mkuu unajua mtu anapouliza sometime anakua serious anataka kujua,sasa unapomwambia kitu kama hicho hapo cjui kama unamtendea haki,anajua wote wanakuwa wamefariki sasa wewe unamwambia hayati anakuwa hai tena duuh,,ni shidaaaah
Kiongozi pole kama nimekukwaza, si nia yangu.Kwa ufahamu wangu,asili ya maneno haya mawili ni lugha ya kiarabu.Al marhum,marehemu,na hayyat enye uhai.

Yapo mafuta ya kula yanaitwa hayyat bila shaka umewahi kuyaona.....lakini kumbuka kiongozi elimu haina mwisho.Wengine watatuelimisha zaidi.Karibu tafadhal.
 
Marehemu ni mtu aliye kufa lakini bado hajazikwa. Ndio maana huwa tunauliza alirehemeka lini? Hayati ndio alishafukiwa 6*6. Swali zuri.

Hayati " the late"
Marehemu " late"
 
Mh, sio haki wadau, wakiwa hai waheshimiwa, wakifa mahayati mbona wanatufisadi hadi kwenye vifo mph!!!"""
 
Hayati linatumika kwa kiongozi au mtu aliyekuwa na hadhi katika jamii, ambaye amefariki.

Marehemu linatumika kwa mtu wa kawaida aliyefariki.
 
Mara nyingi mtu anapofariki jina lake hutanguliwa na neno 'marehemu'na wachache sana 'hayati' je kuna sifa maalum ambazo zinasababisha kutanguliwa na maneno hayo? Je kwa Tanzania kuna hayati mwingine zaidi ya baba wa taifa?
 
Back
Top Bottom