Naomba kujua tiba sahihi kwa mtoto aliezaliwa bila kulia

Africa Tanzania

JF-Expert Member
Jun 13, 2015
1,504
2,261
Habari za muda huu madaktari,

Napenda kupokea ushauri wa kitabibu kutoka kwenu maana kuna mtoto wa Dada yangu alipitia yafuatayo wakati wa kuzaliwa:-

1.UJAUZITO zile tarehe za makadirio zilivuka, mtoto alizaliwa baada ya wiki mbili mbele zaidi. (zaidi ya wiki halali)

2.KUTOKULIA alipozaliwa hakulia, na madaktari walimuwekea oxygen kupumua baada ya muda wakaitoa na akawa vizuri.

3.KUMEZA MAJI wakati wa kuzaliwa kuna maji alikunywa(yale ya uzazi) na madaktari waliyanyonya kwa awamu kisha yakaisha..

Baada ya kutokea hayo, Madaktari walisema ukuaji wake utachelewa sana, pia anaweza kupata degedege au kifafa kutokana na kukosa hewa kwenye ubongo.

~mtoto alikuwa anashtuka mara kwa mara na kulia sana, alivyopelekwa tena hospital madaktari walisema ni degedege na wakampa dawa ya phenobarbital,

Hiyo dawa mpaka sasa anaitumia na usipo mpa mtoto analia sana,

Mpaka sasa mtoto anamiezi 9, hawezi kukaa. Shingo haijakaza na ukimuangalia hatofautiani na mtoto wa miezi mitatu.

Je...Tufanyaje mtoto huyu apate awe vizuri?
Ni tiba gani mwarobaini kwa case kama hii?
Hospital gani hapa Tz wanaweza kumsaidia mtoto huyu?

Nb: mtoto anahudhuria mazoezi kwrnye Center maalum, huu ni ushauri wa baadhi ya madaktari.

Tunaomba msaaada wa mawazo, ushauri au lolote neno hapo.

Nawasilisha.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Africa Tanzania,
Pole kwa madhila yanayomkumba mtoto na familia kwa ujumla. Ni kweli kwamba kulingana na mazingira yaliyozunguka kuzaliwa kwa mtoto wako, anaweza kuwa amepata matatizo kwenye cell za.ubongo wake kutokana na kutopata chakula na oxygen.

Kiasi cha madhila yanaweza kuelezwa vyema.na daktari aliyrhusika wakati wa uzazi kwa ndiye aliyefanya tathimini baada ya zoezi zima la kujifungua.

Lakini pia daktari bingwa wa.watoto anaweza kumwona mtoto na kufamya tathimini upya kulingana na umri wa mtoto na kulinganisha anaweza kufanya nini kulingana na umri wake na nini yawe matarajio ya baadaye na nini unaweza kufanya ili kumsaidia.

Hivyo:
1: Afanyiwe tahimini pale alipozaliwa kama kuna madaktari bingwa.
Au

2: Mpeleke kwa daktari wa watoto ili amfanyie tathimini.
 
Kesi yako inafanana na yangu mtoto wangu hakulia akawekwa kwenye oxygen.Alikunywa maji ya uzazi na alivutwa na vyuma.

Aliugua sana kwenye makuzi yake. Kwa sasa ana miaka 25 na alimaliza form six ila sasa ana tatizo la ugonjwa wa akili japo si taahira lakini anajitambua.

Hata hivyo wakati tunatoka hospitali Dr alituambia huyu mtoto atawasumbua kidogo. Nashauri nendeni kwa Dr wa watoto apate clinic ya mara kwa mara.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante mkuu.
Kesi yako inafanana na yangu mtoto wangu hakulia akawekwa kwenye oxygen.Alikunywa maji ya uzazi na alivutwa na vyuma.

Aliugua sana kwenye makuzi yake. Kwa sasa ana miaka 25 na alimaliza form six ila sasa ana tatizo la ugonjwa wa akili japo si taahira lakini anajitambua.

Hata hivyo wakati tunatoka hospitali Dr alituambia huyu mtoto atawasumbua kidogo. Nashauri nendeni kwa Dr wa watoto apate clinic ya mara kwa mara.


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Africa Tanzania,
Pole kwa madhila yanayomkumba mtoto na familia kwa ujumla. Ni kweli kwamba kulingana na mazingira yaliyozunguka kuzaliwa kwa mtoto wako, anaweza kuwa amepata matatizo kwenye cell za.ubongo wake kutokana na kutopata chakula na oxygen.

Kiasi cha madhila yanaweza kuelezwa vyema.na daktari aliyrhusika wakati wa uzazi kwa ndiye aliyefanya tathimini baada ya zoezi zima la kujifungua.

Lakini pia daktari bingwa wa.watoto anaweza kumwona mtoto na kufamya tathimini upya kulingana na umri wa mtoto na kulinganisha anaweza kufanya nini kulingana na umri wake na nini yawe matarajio ya baadaye na nini unaweza kufanya ili kumsaidia.

Hivyo:
1: Afanyiwe tahimini pale alipozaliwa kama kuna madaktari bingwa.
Au

2: Mpeleke kwa daktari wa watoyo ili amfanyie tathimini.
Ni kwel KABISA ushaur mzur afu pia wa kutoa ushaur mzur ni pale alipojifungulia maana , ukianza kujifikria kitaalam sababu za mtoto kutokulia ni zip , lazima tujiuloze wakat wa uchungu (labour)ya mama ilikua vip , wenda mtoto alichoka sana (foetal distress), kwa sababu tofaut tofaut au difficult labour during pushing stage ) hatuwez kujua , ama mtoto alikua ana tatizo la kuzaliwa kwa hyo ni vema kwenda kwa mabingwa wa watoto ila n vizur ukienda na maelezo (medical notes)za apo alipojifungulia awali kuwasaidia ktk ubora wa kumtibu mtoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu fuata ushauri waliotoa baadhi ya wana JF kwamba mpeleke kwa mtaalamu wa watoto(Dr).
 
P
Pole sana mkuu fuata ushauri waliotoa baadhi ya wana JF kwamba mpeleke kwa mtaalamu wa watoto(Dr).
Pia ushauri kwa wamama, endapo watahisi kunamatatizo karibu na wakati wa labour ni vizuri waombe wawekewe mashine za oxygen ili kuongeza kiwango cha oxygen kwenye damu ya mama ambayo itakwenda pia kwa mtoto, hii itasaidia endapo itachukua muda kupush mtoto ubongo wake utakuwa na oxygen ya kutosha kwa muda hivyo kupunguza madhara ubongoni maana wakati wa kupush mishipa ya kumpelekea mtoto damu ya oxygen kutoka kwa mama inakuwa imekatika tayari hivyo oxygen ya akiba ubongoni mwake itasaidia kwa muda hadi kutoka maana katika kipindi hicho mtoto anatakiwa aanze kutumia pua na mapafu kujipatia oxygen mwenyewe ni muhimu kumonitor mapigo ya moyo ya mama kabla na pamoja na mtoto huyo baada ya kujifungua hadi hali itakapohakikiwa ni stable
 
P

Pia ushauri kwa wamama, endapo watahisi kunamatatizo karibu na wakati wa labour ni vizuri waombe wawekewe mashine za oxygen ili kuongeza kiwango cha oxygen kwenye damu ya mama ambayo itakwenda pia kwa mtoto, hii itasaidia endapo itachukua muda kupush mtoto ubongo wake utakuwa na oxygen ya kutosha kwa muda hivyo kupunguza madhara ubongoni maana wakati wa kupush mishipa ya kumpelekea mtoto damu ya oxygen kutoka kwa mama inakuwa imekatika tayari hivyo oxygen ya akiba ubongoni mwake itasaidia kwa muda hadi kutoka maana katika kipindi hicho mtoto anatakiwa aanze kutumia pua na mapafu kujipatia oxygen mwenyewe ni muhimu kumonitor mapigo ya moyo ya mama kabla na pamoja na mtoto huyo baada ya kujifungua hadi hali itakapohakikiwa ni stable
Kweli mtaaalamu umetoa madini ya maana.
 
ooh pole sana mkuu,iyo hali kitabibu inatwa cerebral palsy(mtindio wa ubongo) moja katika sababu zinazopelekea mtoto kupata shida hii ni kunywa maji ya uzazi(meconium aspiration) hivo kupelekea kukosa hewa ya oxygen na hatimaye mtoto hupata madhara katika mfumo wa neva na kupelekea kuwa na maendeleo hafifu katka ukuaji wa ubongo wa mtoto .kitu kikubwa naweza kukushauri jitahidi kumepeleka mtoto katika kitengo cha mazoez .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ooh pole sana mkuu,iyo hali kitabibu inatwa cerebral palsy(mtindio wa ubongo) moja katika sababu zinazopelekea mtoto kupata shida hii ni kunywa maji ya uzazi(meconium aspiration) hivo kupelekea kukosa hewa ya oxygen na hatimaye mtoto hupata madhara katika mfumo wa neva na kupelekea kuwa na maendeleo hafifu katka ukuaji wa ubongo wa mtoto .kitu kikubwa naweza kukushauri jitahidi kumepeleka mtoto katika kitengo cha mazoez .

Sent using Jamii Forums mobile app
👏
 
Kesi yako inafanana na yangu mtoto wangu hakulia akawekwa kwenye oxygen.Alikunywa maji ya uzazi na alivutwa na vyuma.

Aliugua sana kwenye makuzi yake. Kwa sasa ana miaka 25 na alimaliza form six ila sasa ana tatizo la ugonjwa wa akili japo si taahira lakini anajitambua.

Hata hivyo wakati tunatoka hospitali Dr alituambia huyu mtoto atawasumbua kidogo. Nashauri nendeni kwa Dr wa watoto apate clinic ya mara kwa mara.


Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba tuwasiliane tafadhari, najaribu ku pm inashindikana
 
Back
Top Bottom