Naomba kujua namna sahihi ya matumizi ya maneno 'sorry' na 'excuse me'

mangonifera indica

JF-Expert Member
Dec 2, 2017
845
1,462
Naomba kujua matumizi yake,

Kwa mfano mtu anataka umpishe utasikia sorry naomba kupita. Mwingine atasema excuse me. Usahihi wake upo wapi?

Nisaidieni,

we are still learning!

MAONI YA MDAU

Sorry ni kusema unajisikia vibaya. Excuse me ni kusema niwie radhi.

Katika kuomba kupita neno sahihi ni excuse me. Kwamba, naomba radhi yako nipite.Ingawa wengine wanasema sorry, kama najisikia vibaya kukutaka unipishe nipite hapo ulipo, najisikiavibaya kukusumbua, kitu ambacho ni sawa, lakini ni Uingereza mwingi sana kuutafsiri kwenye utamaduni wetu.

Muingereza anaweza kukuambia sorry umpishe akiwa na maana ya kwamba "wewe mbona umekaa njiani?".
Siku hizi watu wanaitumia sana sorry hata pasipohusika.
 
naomba kujua matumizi yake mfano mtu anataka umpishe utasikia sorry naomba kupita mwingine atasema excuse me...usahihi wake upo wapi nisaidieni,we are still learning!
Sorry ni kusema unajisikia vibaya. Excuse me ni kusema niwie radhi.

Katika kuomba kupita neno sahihi ni excuse me. Kwamba, naomba radhi yako nipite.Ingawa wengine wanasema sorry, kama najisikia vibaya kukutaka unipishe nipite hapo ulipo, najisikiavibaya kukusumbua, kitu ambacho ni sawa, lakini ni Uingereza mwingi sana kuutafsiri kwenye utamaduni wetu.

Muingereza anaweza kukuambia sorry umpishe akiwa na maana ya kwamba "wewe mbona umekaa njiani?".
Siku hizi watu wanaitumia sana sorry hata pasipohusika.
 
Sorry huja baada ya kutenda excuse huja kabla ya kutenda. Na Mzungu anajua Zaidi
 
Sorry in pole au unajisikia vibaya kuhusu jambo fulani.

Excuse me,(tena nilazima iwe au iambatane Na 'me' maana wengine wanaikata hiyo me ) ni samahani.

Please ni Tafadhali kwa kuongezea tu.
 
Mimi nitoe maoni yangu haya,

Kuomba kupita au kuomba mhudumu: tumia "excuse me" au "pardon me". Usitumie "sorry".

Kumpa mtu pole kwa sababu amefiwa ndugu, au matatizo mengine: sema "very sorry for your loss", usiseme "excuse me".

Mtu akiangusha kitu chini: usiseme "sorry" wala "excuse me". Sema tu "oops". Ni jinsi ya kiingereza kumaanisha kwamba kosa dogo limejitokeza. Lakini! Wewe ukiangusha kitu kwenye mguu wa mwenzako, lazima umpe "sorry".

Nipe scenario nyingine, nikupe matumizi ya sorry/ excuse me.
 
Mtu akiangusha kitu chini: usiseme "sorry" wala "excuse me". Sema tu "oops". Ni jinsi ya kiingereza kumaanisha kwamba kosa dogo limejitokeza. Lakini! Wewe ukiangusha kitu kwenye mguu wa mwenzako, lazima umpe "sorry".


Hapo mkuu nadhani kuna mapungufu kidogo, mtu akiangusha kitu chini, unatakiwa uumpe pole na neno sahihi ni "sorry" na unaweza kusema; oops, sorry. Na kama utamuangushia mtu kitu mguuni kwake kwa bahati mbaya hapo utasema; oops, I am sorry.

Neno sorry lipo kwa ajili ya kutoa pole kwa tukio lisilofurahisha, msiba, ugonjwa nk.
 
Kama ni hivyo embu onesha neno "sorry"litatumikaje kwenye sentensi hizi?

1.I'm so sorry for your loss.
2. I'm sorry,please forgive me.



Hiyo sentensi ya kwanza tafsiri yake kwa kiswahili ni; "pole kwa (kupata) hasara."

Hiyo sentensi ya pili tafsiri yake ni; "ninasikitika, tafadhali nisamehe."

"Sorry" inatumika kwenye "calamities", inapotumika nje ya calamities ni makosa, mfano ni hapo ulipoitumia ambapo "kuna "pole" na "nasikitika" hizo ni ishara za calamities , wala samahani (excuse) halipaswi kutumika hapo kwenye sentesi zote.
 
Hiyo sentensi ya kwanza tafsiri yake kwa kiswahili ni; "pole kwa (kupata) hasara."

Hiyo sentensi ya pili tafsiri yake ni; "ninasikitika, tafadhali nisamehe."

"Sorry" inatumika kwenye "calamities", inapotumika nje ya calamities ni makosa, mfano ni hapo ulipoitumia ambapo "kuna "pole" na "nasikitika" hizo ni ishara za calamities , wala samahani (excuse) halipaswi kutumika hapo kwenye sentesi zote.
Naomba unipe tafsiri ya sentensi ya pili ila mimi ya kwangu nitasema "Samahani,naomba unisamehe"
 
Naomba unipe tafsiri ya sentensi ya pili ila mimi ya kwangu nitasema "Samahani,naomba unisamehe"


Mkuu hiyo sentensi ya pili, uliyoiandika, I'm sorry, please forgive me, tafsiri yake kwa kiswahili ni; "Ninasikitika, tafadhali nisamehe"

Tafsiri ya neno kwa neno:-

I'm sorry= ninasikitika.
Please= tafadhali.
Forgive me= nisamehe.

I'm sorry =ninasikitika na siyo samahani, samahani ni "Excuse me".

Excuse inatumika, kwa mfano, pale ambapo unataka kuwatoa watu katika shughuli zao ili ufanye shughuli yako, mfano kama watu wapo katika mkutano na wewe unataka wavunje mkutano wao kwa muda na wakusikilize wewe juu ya jambo lako linalohusu mkutano huo au lisilohusu.

Mfano umewakuta watu wamekaa na wewe unataka wainuke kwanza ili upite hapo walipo, unapo waomba njia ya kupita hapo utaanza na neno "Excuse me, may I -------", Excuse me hapo maana yake ni "Samahani".

Jambo hili watu wengi wanachanganya sana kati ya "sorry" na "Excuse"---Sorry ni kuomba radhi kwa hasara, majonzi nk, yaliyokwisha tokea na Excuse ni kuomba ridhaa ya "kuwasumbua" watu (inconvenience/disturbance ). na hapo neno Excuse ndipo hutumika ambalo kwa kiswahili ni Samahani, neno Sorry halina maana ya samahani bali lina maana kadhaa kulingana na lilivyotumika katika sentensi, mfano, linaweza kuwa na maana hasa hizi mbili "pole na ninasikitika,"
 
According to Macmillan Dictionary,excuse me is used fo:
  1. politely getting someone's attention
  2. showing you are sorry for interrupting someone
  3. asking someone to move so that you can get past them
  4. politely telling someone you are leaving

Sorry is used for :
  1. emphasizing how bad,stupid,or embarrassing something is
  2. feeling sadness or sympathy because something bad has happened to them
  3. disappointed about a situation,and wishing you could change it

1. We usually say excuse me before we interrupt or disturb somebody;
we say sorry after we disturb or trouble somebody.
Compare:
  • Excuse me, could I get past?… Oh, sorry, did I step on your foot?
  • Excuse me, could you tell me the way to the station?
I beg your pardon is a more formal way of saying sorry.
  • I beg your pardon. I’m afraid I didn’t realize this was your
2. If we do not hear or understand what people say, we usually say Sorry?What? (informal) or (I beg your) pardon?
Americans also say Pardon me?
  • “Mike’s on the phone.” ” Sorry?” I said “Mike’s on the phone”
  • “See you tomorrow”. “What?” I said “See you tomorrow”.
  • “You’re going deaf”.” I beg your pardon?”
 
Mkuu hiyo sentensi ya pili, uliyoiandika, I'm sorry, please forgive me, tafsiri yake kwa kiswahili ni; "Ninasikitika, tafadhali nisamehe"

Tafsiri ya neno kwa neno:-

I'm sorry= ninasikitika.
Please= tafadhali.
Forgive me= nisamehe.

I'm sorry =ninasikitika na siyo samahani, samahani ni "Excuse me".

Excuse inatumika, kwa mfano, pale ambapo unataka kuwatoa watu katika shughuli zao ili ufanye shughuli yako, mfano kama watu wapo katika mkutano na wewe unataka wavunje mkutano wao kwa muda na wakusikilize wewe juu ya jambo lako linalohusu mkutano huo au lisilohusu.

Mfano umewakuta watu wamekaa na wewe unataka wainuke kwanza ili upite hapo walipo, unapo waomba njia ya kupita hapo utaanza na neno "Excuse me, may I -------", Excuse me hapo maana yake ni "Samahani".

Jambo hili watu wengi wanachanganya sana kati ya "sorry" na "Excuse"---Sorry ni kuomba radhi kwa hasara, majonzi nk, yaliyokwisha tokea na Excuse ni kuomba ridhaa ya "kuwasumbua" watu (inconvenience/disturbance ). na hapo neno Excuse ndipo hutumika ambalo kwa kiswahili ni Samahani, neno Sorry halina maana ya samahani bali lina maana kadhaa kulingana na lilivyotumika katika sentensi, mfano, linaweza kuwa na maana hasa hizi mbili "pole na ninasikitika,"
Hii kwa mujibu wa kamusi ya TUKI kuwa "sorry" ni "samahani"
Screenshot_20191107-063749.png
 
Hiyo sentensi ya kwanza tafsiri yake kwa kiswahili ni; "pole kwa (kupata) hasara."

Hiyo sentensi ya pili tafsiri yake ni; "ninasikitika, tafadhali nisamehe."

"Sorry" inatumika kwenye "calamities", inapotumika nje ya calamities ni makosa, mfano ni hapo ulipoitumia ambapo "kuna "pole" na "nasikitika" hizo ni ishara za calamities , wala samahani (excuse) halipaswi kutumika hapo kwenye sentesi zote.
Vile vile kwa mujibu wa google translate neno "sorry" ni "samahani"
Screenshot_20191107-063848.png
 
Haya maneno kwa juu juu yanaonekana mepesi, ila ni magumu sana kuyatofautisha kwa usahihi wake.
 
If we do not hear or understand what people say, we usually say Sorry?What? (informal)



Hayo maelezo ya hiyo kamusi ni sahihi kabisa juu ya matumizi ya sorry na excuse.

Pia zingatia hapo niliponukuu matumizi ya "Sorry" yanapokuwa (informal) --- matumizi yasiyo rasmi.

maneno rasmi hapo, kama kamusi ilivyoeleza ni, I beg your pardon, au pardon me, na hata Excuse me say it again.

Pia angalia kamusi mbalimbali, usiangalie kamusi moja tu.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom