MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Dalili zote unaonyesha upo katika Kundi la Wagonjwa wa Akili na unahitaji Tiba ya haraka sana.Naomba kwa wataalamu humu mniambie Mimi ni mtu wa Aina gani kwa izi sifa zangu;
- Mimi ni mkorofi (tokea utotoni napenda Sana ugomvi na sehemu zenye ugomvi na shari)
- Mimi ni mkimya (yaani sipendi kuongea na pia sipendi mtu aniongeleshe kwa muda mrefu nachukia sana yaani natak nikiwa na wewe ukae kimya usiniulze maswali mengi)
- Ninapenda kampani au watu wasio wapole wapole yaani napenda watu waliochangamka(wahuni wahuni)
- Nayachukia mahusiano(ya kimapenzi) naweza kumtongoza msichana ila baada ya kukubali nkikaa nae kidogo nachoka na naachana nao.
- Mara nyingne Ni muongeaji Sana kwa watu nisiowajua ama ninaowajua ila wakati mwingne nakuwa mkimya Sana naweza maliza muda sijaongea na mtu
- Sinaga aibu.
- Napenda Sana kuishi/kukaa pekeangu pekeangu muda mwingne natamani dunia nzima ningebaki mwenyewe.
- Nina huruma Sana.
- Sipendi sehemu zenye starehe starehe (hii sjui kutokana na malezi) mf birthday party izi ama sehemu za kuchanganyika na watu, napenda Mambo ya fujofujo.
- Nikimbembeleza mtu au mpenzi wangu roho inaniuma Sana najiona Kama sjui Nini yaani kiufupi sipendi maswala ya kubembelezana (ata Mimi sipendi kubembelezwa.
- Napenda Sana uadui na pia kuwa kwenye mazingira magumu(waga ninakuwaga na mawazo Sana ) na bila kuwa na mawazo sifanyagi vitu vizuri(malezi nilokulia).
- Sipendi kufatilia mtu na Mimi sipendi kufatiliwa Mambo yangu.
- Story zangu waga haziko romantic napenda story za matukio matukio ya ajabu na ya kiume sinaga story za kuvutia za mapenzi
Hayo ni machache tu, je me ni mtu wa aina gani maana yake nashindwa kuelewa! Msaada tafadhali🙏