Naomba kujua mchango wa Wamisionari katika maendeleo ya elimu Afrika

JK
BAKWATA ni katika matatizo makubwa waliyopata kukutananayo Waislam wa Tanzania.
Kwa zaidi ya nusu karne Waislam wamekataa kuikubali BAKWATA kama taasisi yao.

Naamini hili si jambo geni kwako lazima utakuwa unalijua na kwa nini wameikataa naamini sababu unazijua.

Kwa ajili hii basi Waislam wamejiweka mbai sana na BAKWATA.

Mwanzoni mwa miaka ya 1980 vijana wa Kiislam kupitia taasisi ya Warsha waliweza kujipenyeza katika uongozi wa BAKWATA kwa nia ya kuboresha shule zake, Kinondoni, Kibohehe na Jumuiya kwa kuzigeuza kuwa Seminari za Kiislam.

Shule hizi zilibadilika na kwa mara ya kwanza matokeo ya mitihani ilitia fora.

Pamoja na mabadiliko haya Warsha iliandika waraka kwa Waislam wa Tanzania kuonyesha hali yao ya elimu toka uhuru mwaka wa 1961.

Serikali ilikuwa inashutumiwa kwa kukosa uadilifu.

Waraka huu ulishtua si serikali peke yake bali hata Waislam wenyewe.
Hii ilikuwa mwaka wa 1981.

BAKWATA ikajikuta inagongana na serikali iliyounda taasisi hiyo.

Vijana wa WARSHA waliokuwa BAKWATA wakafukuzwa BAKWATA pamoja na Katibu Mkuu wa wakati ule Sheikh Mohamed Ali.

Kosa lao likiwa kuliweka jambo nyeti hadharani.
Ninakuandikia kwa kifupi kwani ni kisa kirefu.

Kuanzia wakati huo hadi hivi sasa Waislam wanajitahidi kujenga shule zao nje ya BAKWATA na kujiletea maendeleo yao hawajishughulishi na BAKWATA kwa jambo lolote sababu kubwa ni kuwa taasisi hiyo haikuasisiwa na wao wenyewe Waislam bali na serikali mwaka wa 1968.

..nimesoma historia uliyoandika kuhusu kuanzishwa kwa Bakwata.

..hata nikikubaliana na wewe 100% bado inaniumiza kuona sekondari za Bakwata zikifanya vibaya.

..na waathirika wa sekondari za Bakwata ni watoto wa imani mbalimbali, lakini mostly ni watoto wa Kiislamu.

..kwanini Waislamu msiungane ktk suala hili la ELIMU na hayo mengine mkayashughulikia baadae?

..Na ukichunguza Waislamu ni matajiri wakubwa hapa nchini, sasa inakuwaje shule za taasisi ya Kiislamu iliyopo nchi nzima kama Bakwata zikatelekezwa kiasi hiki?

..Mimi nawashauri muungane mrekebishe madhaifu yaliyoko ktk sekondari za Bakwata.
 
..nimesoma historia uliyoandika kuhusu kuanzishwa kwa Bakwata.

..hata nikikubaliana na wewe 100% bado inaniumiza kuona sekondari za Bakwata zikifanya vibaya.

..na waathirika wa sekondari za Bakwata ni watoto wa imani mbalimbali, lakini mostly ni watoto wa Kiislamu.

..kwanini Waislamu msiungane ktk suala hili la ELIMU na hayo mengine mkayashughulikia baadae?

..Na ukichunguza Waislamu ni matajiri wakubwa hapa nchini, sasa inakuwaje shule za taasisi ya Kiislamu iliyopo nchi nzima kama Bakwata zikatelekezwa kiasi hiki?

..Mimi nawashauri muungane mrekebishe madhaifu yaliyoko ktk sekondari za Bakwata.
JK,
Hatuwezi kurudi nyuma.

Kuwaambia Waislam waingie BAKWATA ni kuwashughulisha pasi na sababu.

Kitu chochote kilichoanzishwa kwa minajili ya kupambana na Allah kwa Waislam watakikalia mbali.

Shule za Kiislam ziko nyingi kwa sasa.
Katika elimu ya Waislam kuna matatizo mengi.

Nadhani ulisikia kisa cha Baraza la Mitihani lilivyokuwa linahujumu shule za Kiislam na wakuu wa shule hizi wakaandika taarifa ikapelekwa serikalini.

Waislam kwa ajili hii walifanya maandamano bila kibali na serikali ilitoa vitisho kuwa maandamano hayo ni haram.

Haya maandamano yalifanyika juu ya kuwa walitumwa askari Msikiti wa Kichangani yalipokuwa yanaanzia na helikopta zikiwa zinazunguka juu kama vitisho na Kamanda Suleiman Kova akatoa tangazo la kutisha walioazimia kuandamana kupinga dhulma.

Kisa hiki ni kirefu na maandamano haya yaliongozwa na Sheikh Ponda.

Ilikuwa mwaka wa 2012.

BAKWATA iliundwa baada ya EAMWS kupigwa marufuku na serikali wakati inajitayarisha kujenga Chuo Kikuu Cha Waislam Chang'ombe huku ikijenga shule majimboni kuanzia mwaka wa 1962 baada ya Muslim Congress mara tu baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.

Hii ni historia inayowapa shida sana serikali na viongozi wa BAKWATA waliopo madarakani.

Si jambo wanalopenda Waislam walifahamu.
 
Sasa mchango wa wazungu ni upi? au mchango wa waarabu ni upi?

Humu nasoma "waislamu" "wakristo" na "watanganyika" au "waafrika" sasa hao "waislamu" ni nani? hao "wamishionari" au wakristo ni kina nani?
 
Wamissionary mchango woa mkubwa ni kutubrainwash kupitia dini na elimu na kutufanya tuwe kondoo wa wazungu.
 
I Love Girls,
Nakuwekea hapo chini niliyoandika kuhusu Wamishionari na Elimu kama nilivyoeleza katika kitabu changu, ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...'' (1989).

Nimehariri hapa na pale kidogo ili msomaji aelewe somo tunalojadili:

''
Wajerumani walipofika Tanganyika waliwakuta Waislam wanafahamu kuandika, kusoma na walikuwa wameelimika katika hesabu.

Mmishionari Ludwig Krapf alipofika kwa Chifu Kimweri wa Usambaa mwaka 1848 alimkuta yeye na wanae wote wanajua kusoma.

Herufi walizokuwa wakitumia zilikuwa za Kiarabu.

Wajerumani kwa ajili hii basi waliwaajiri Waislam kama walimu, wakalimani na makarani serikalini. Wamisionari na wakoloni waliona wivu kwa maendeleo haya waliyoyakuta kwa Waislam.

Kubwa zaidi ni kuwa walikuwa wamekuja kustaarabisha watu ''Washenzi' badala yake wamewakuta watu walistaarabika na wanye utamaduni wa kupendeza.

Elimu hii yote na utamaduni huu wa hali ya juu ulikuwa unatokana na Uislam na shule zake za ndani ya madrasa.

Hapo ndipo zilipoaanza mbinu ya kuvunja maendeleo haya yote.

Herufi za Kiarabu zikapigwa marufuku kutumika na badala yake watu wakalazimishwa kujifunza herufi za Kirumi.

Muislam ambae jana alipoingia kulala alikuwa anaitwa ameelimika akaamka asubuhi yake mjinga, hana elimu, hajui kusoma wala kuandika.

Njama hizi zote dhidi ya Uislam ilikuwa sehemu ya makubaliano kama ilivyoandikwa katika kifungu IV cha Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884.

Kifungu hicho kilikuwa kinasema kuwa Ukristo ni lazima ulindwe dhidi ya Uislam.

Kati ya mwaka 1888 - 1892 katika kutekeleza kifungu hicho kama ilivyokubalika katia Mkutano wa Berlin, Imperial British East Africa Company ilitumia nguvu za kisiasa na kijeshi kuulinda Ukristo katika Afrika ya Mashariki.

Ombwe lililoachwa na elimu ya Kiislam ikajazwa na elimu ya iliyokuwa inatolewa na Wamishionaro katika kanisa chini ya usimamizi wa Waingereza.

Wengi wanaamini kuwa kanisa kuwa lenyewe ndilo lililoweka msingi wa kwanza wa elimu Tanganyika.

Ukweli ni kuwa Wamisionari walifuata nyayo za madrasa na walimu wa kwanza katika shule za misheni walikuwa Waislam ambao hawakusoma katika shule za kanisa bali katika madrasa.''

Hamna njama yoyote kuhusu uislamu.. Ukristu na uislamu zote ni dini za kishetani zilitumika kumfanya mtu mweusi kuwa mtumwa
 
Sasa mchango wa wazungu ni upi? au mchango wa waarabu ni upi?

Humu nasoma "waislamu" "wakristo" na "watanganyika" au "waafrika" sasa hao "waislamu" ni nani? hao "wamishionari" au wakristo ni kina nani?
Syll...
Takriban nusu ya umri wangu wa miaka 68 naingia 69 In Shaa Allah Februari nimekuwa nikiandika vitabu, ''academic papers,'' na makala nyingi zisizo na hesabu kuhusu Uislam Tanzania na nimehudhuria mikutano mingi ndani na nje ya Tanzania pamoja na kuzungumza katika vyuo mbalimbali Afrika, Ulaya na Marekani.

Naweza kujidai kuwa suala hili nalijua kwa kiasi changu.

Katika ujuzi huu kuna namna ya ''pattern,'' nimejenga na kwa sasa naweza kusema imekuwa sawasawa na sheria au kanuni ya aina fulani mfano wa ''Archimedes Principle.''

Mfano ni kama huu wako.

Unapoona mtu anaandika kwa staili yako kuwa liko tatizo na linajadiliwa na mtu anaandika kwa kusema kama unavyosema wewe kuwa huwajuia Waislam, Waarabu, Wakristo, Waafrika, Wamishionari nk; huyu tafuta imani yake utakuta si Muislam.

Sasa utafiti wangu haukuishia hapa ili niweze kuitengeneza hii sheria yangu au kanuni iweze kuwa na mashiko ni lazima nijue kiwango cha elimu yake.

Nitakijuaje?

Huwa namtia hamu ya kufanya majadala na mimi na kila anapoandika najaribu kupima kiwango cha elimu yake na si kazi kubwa mara moja naweza kukisia kama ni elimu ya chini, kati au juu.

Hapa nitaeleza jambo.

Uzoefu wangu unaonesha kuwa baadhi katika mjadala huu wa dhulma huwa wanapandwa na hamaki kwa kukosa hoja na huja na lugha kali na pengine matusi na vitisho au kunishambulia binafsi badala ya kujibu hoja.

Lakini haya yote yamesaidia sana katika kuelewa uzito wa suala hili.

Suala linalofuatia ni kwa nini ghafla baada ya kujua uwezo wake kuwa kiwango chake cha elimu ni kizuri anaandika kama mtu asiyejua kitu?

Sasa ili kupata ''conclusion,'' au uhakika wa kile ninachotafuta ni lazima hii ''pattern'' yangu iwe na ''sampling,'' kubwa yaani nimejadiliana na watu wengi katika jamii katika tatizo hili.

Nilichogundua ni kuwa imani ina nafasi kubwa sana katika fikra kiasi anaona kukubali ukweli anaowekewa wazi ni kushindwa kwa imani yake.

Hiki ni kitu muhali mkubwa sana kwake hawezi kukiruhusu.

Sasa ukichukua ukweli huu ukauweka katika serikali ambayo watendaji wakuu wanaoshika nafasi za maamuzi ni wa imani moja kwa mathalan uwiano wa 20:80 utaelewa bila tabu yote kwa nini hali iko hivyo ilivyo kuwa Waislam wanajaribu kueleza matatizo yao lakini hakuna aliye tayari katika serikali kusikiliza au hata kuamini kuwa liko tatizo.

Hapa ndipo linapoingia lile suala linalotisha.

Ni akina nani waliotoa uamuzi wa kuvunjwa kwa EAMWS wakati wanajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na kutekeleza mipango yao ya elimu?

Nini lilikuwa kusudio lao?

Hofu kuwa Waislam wataelimika na hivyo kushika madaraka katika serikali ya Tanganyika huru?

Ndiyo hapo ghafla unasoma mtu kama Edwayne anaandika kuwa Uislam na Ukristo zote ni dini za shetani na utumwa.

Tafuta imani yake utapata jibu.

Lakini ukiangalia mjadala si huo bali ni dhulma ambayo Waislam wanaeleza serikali kuwa wamekuwa wanafanyiwa toka uhuru upatikane mwaka wa 1961 na vielelezo vyote kama ushahidi wameweka.

Nachelea kumchosha msomaji lakini mifano ipo mingi.

Tatizo ni kuwa viongozi wetu hawako tayari kuliweka tatizo hili katika agenda lijadiiwe kwa wazi kwa hofu ambayo si tabu kuitambua.
 
Hamna njama yoyote kuhusu uislamu.. Ukristu na Uislamu zote ni dini za kishetani zilitumika kumfanya mtu mweusi kuwa mtumwa
Edwayne,
Soma hii barua hapo chini:

MK/HB. VOL.5/07/101 06/06/2012

MAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: HUJUMA ZA BARAZA LA MITIHANI DHIDI YA WAISLAM


Kila sifa njema anastahiki Allah, ambaye rehema zake zimeenea katika kila kitu katika ulimwengu bila ya kujali utii ama uasi wa kitu hicho katika amri na sharia zake.

Rehema na amani zimuendee kipenzi chetu mtume Muhammad (S.A.W) kwa kuwa kiigizo chema na rehema kwa walimwengu wote.

Ndugu waandishi kwa muda mrefu Waislam wamekuwa wakiilalamikia suala zima la utendaji wa serikali kuwa umekuwa wakibaguzi kwa kuwapendelea Wakirsto kwa kuwapa nafasi mbalimbali muhimu serikalini na katika taasisi zake.

Ndugu waandishi na Waislam mnamo tarehe 01/ 05/2012 Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya kidato cha sita, matokeo hayo yaliwashtua sana wanafunzi Waislam waliofanya mtihani wa elimu ya dini ya Kiislam (Islamic Knowledge). Takriban asilimia 70 walifeli kwa kupata daraja F, na asilimia 30 ndio waliofaulu tu.

Katika hao waliofaulu walipata alama za juu kabisa nchi nzima ni wanafunzi saba tu ambao wamepata daraja D, kwa matokeo haya somo hili likawa somo la mwisho kwa ufaulu nchi nzima (rejea kitabu cha takwimu cha Baraza la Mitihani Tanzania April 2012.

Matokeo haya yaliwashtua wazazi na walimu wa somo hili, baadhi ya wanafunzi waliamua kukata rufaa ya kutokubaliana na matokeo hayo.

Waislam kupitia Taasisi mbali mbali za Kiislam walimuandikia Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kumuomba aunde tume huru kuchunguza matokeo ya somo husika.

Kufuatia malalamiko hayo ya baadhi ya taasisi za dini, Barraza la Mitihani liliyatazama matokeo hayo na kugundua pia walikosea na hivyo Baraza la Mitihani likaidhinisha kutolewa matokeo mapya kwa somo hilo.

Mabadiliko hayo ya matokeo ufaulu kwa wanafunzi wale wale ambao awali walifeli kwa asilimia 70, sasa yakabadilika na ufaulu ukaongezeka kwa zaidi ya asilimia 70.

Kwa namna yoyote ile itakavyokuwa dosari kubwa kama hii ni kashfa kubwa kwa Baraza la Mitihani Tanzania na Serikali kwa ujumla.

Na kwa kutilia maanani muundo na historia ya utendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania kama nilivyoanza kuelezea, Waislam wanayokila sababu ya kuamini kwamba matokeo haya ni uthibitisho tosha wa hujuma ambazo wanafunzi wa kiislam walikuwa wakifanyiwa kwa muda mrefu.

Na hii inatupa picha kwamba dosari hizi zilizotokea kwenye somo la maarifa ya Kiislam, haziishii kwenye somo hili, bali uchunguzi ukifanyika kwa masomo yote waliofanya wanafunzi wa Kiislam itadhihirika kwamba hila na dhulma kama hizi zinafanyika katika masomo mengine.

Kimsingi kwa dhulma hii waliyoifanya Baraza la Mitihani dhini ya wanafunzi wa Kiislam, Bakwata na Waislam wote kwa ujumla wamepoteza imani na Baraza la Mitihani la Tanzania na hasa katibu mtendaji wake .

Bakwata, linawapongeza na kuwaunga mkono Taasisi zote za Kiislam nchini kwa jitihada ya kuligundua hili na hatua walizozichukuwa dhidi ya Baraza la Mitihani na kuhufahamisha umma wa Kiislam juu ya kadhia hii.

Tunarudia baraza tunawapongeza taasisi zote za kiislam na tunasema katika hili Bakwata tuko nyuma yao kwani kauli yao ndio kauli yetu.

Bakwata, inamshangaa Katibu Mtendaji wa Baraza la mitihani (Necta) Dk. Joyce Ndalichako, kwa kauli yake aliyoitoa kupitia vyombo mbali mbali vya habari vya jana tarehe 5/06/2012, akisema hakuna hujuma na mitihani inasahihishwa na walimu wenye sifa,wanachaguliwa na na wakuu wa shule zao, walimu wenye uzoofu na kuna mfumo wa usahihishaji aliouita “Conveyor Belt”.

Bakwata inasema hapa tatizo la msingi sio mitihani kusahihishwa na walimu wenye sifa, na nani anawachagua walimu hao wenye sifa au huo mfumo wa usahihishaji, tatizo la msingi hapa ni kufelishwa kwa makusudi kwa wanafunzi wetu wa Kiislam katika somo husika, wakati nakala za mitihani yao (Scripts) zinaonyesha wamefaulu.

Bakwata, tunahoji kwanini tatizo hili la huo mfumo (Conveyor Belt) litokee mwaka huu, mbona matokeo ya mwaka jana waislam hawakulalamika na kulikuwa hakuna dosari kama za mwaka huu iweje itokee mwaka huu, wakati mfumo ni ule ule?

Bakwata, tunaamini Waislam katika hili tumehujumiwa na Waislam hawajaridhishwa na majibu ya Dk. Ndalichako, aliyoyatoa kupitia vyombo vya habari vya hapa nchini.

Hiyo mifumo ya usahihishaji sio maneno matakatifu kwamba haiwezi kuchezewa kutokana hila za binadamu ni mifumo iliyowekwa na binadamu, na binadamu huyohuyo anaweza kuibadilishabadilisha vyovyote anavyotaka.

Sisi kama Bakwata,tunaamini ili kurudisha imani ya Waislam dhidi ya Baraza la Mitihani tunataka mambo yafuatayo yafanyike:
  • Tume huru iundwe la kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake wa kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
  • Katibu mkuu wa Baraza la Mitihani (Necta) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Baraza la Mitihani.
  • Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa kompyuta ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.
  • Hatua za kisheria na kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa baraza la mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.
  • Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha makatibu wakuu watendaji na manaibu katibu wakuu wamekuwa wakristo na wenyevyiti wa baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.
  • Pia tunaiyomba Serikali iwape nafasi wanafunzi wote ambao baada ya matokeo yao kubadilishwa wamekuwa na sifa za kujiunga na vyuo vikuu waruhusiwe kuomba mikopo bodi ya mikopo, tunalisema hili kutokana na
  • muda wa kuomba mikopo kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu kwisha.
Suala la Sensa ya watu na makazi.


Kama tunavyojua kwa mwaka huu wa 2012, kuna zoezi la sense ya watu na makazi ambayo inatarajiwa kufanyika kuanzia mwezi wa nane, 2012, na kutoka na upotoshaji ulioenea kwenye vyombo vya habari hapa nchini, kalenda iliyochapichwa na ofisi ya waziri mkuu, imetoa takwimu zinazoonyesha idadi ya watanzania ni milioni 43 ambapo kwa mujibu wa dini zao wakristo ni asilimia 52, waislam asilimia 32 na dini zingine ni asilimia 16.

Bakwata tunalaani kitendo hiki na tunasema takwimu hizi sio sahihi na zinapotosha wananchi, hii ni kwa sababu katika sense zilizofanyika hivi karibuni ikiwemo sense ya mwaka 2002 kipengele kinachobainisha dini za watanzania kiliondolewa.

Kwakuwa taarifa hizi zinaonekana kwenye kalenda zinazoonyesha zimetayarishwa na ofisi ya waziri mkuu, tunaitaka serikali kurudisha kipengele kinachobainisha dini za watanzania katika sense ya mwaka huu ili ukweli ujulikane na kuondoa kabisa sintofahamu hii.

SUALA LA MGOGORO WA HIVI KARIBUNI ZANZIBAR

Ndugu waandishi wa habari naamini nyinyi nyote kama waandishi wa habari mnajua au mmesikia vurugu zilizohusisha imani za dini zilizotokea visiwani humo na kutokana na taarifa nyingi za vyombao vya habari zilizokuwa zikitolewa tangu mgogogro huu uanze kuna kila dalili za kuchukuliwa hatua za haraka haraka na katika mazingira haya wale wote waliohusika na vurugu hizi wasijulikane tena na watu wasio na hatia wakahusishwa na hali ikawa mbaya zaidi kwa hivy o kutokana na kadhia yote hiyo na yote yaliyosemwa na makundi mbalimbali ya waisla na wasiokuwa waislam Sisi kama Bakwata tunasema yafuatayo:

Kwanza tunalaani kitendo cha uvunjifu wa amani uliotokea Zanzibar na tunaamini waliofanya vurugu zote zile sio waislam bali ni wahuni tu.

Pili tunasema Wazanzibar, wasikilizwe kwa yale ambayo wanayapigia kelele kama malalamiko yao yapo katika muungano Serikali haina budi kuyasikiliza yale yote yanayolalamikiwa na kuyarekebisha, kwani Muungano sio qur- an useme kilichomo humo hakiwezi kurekebishika.

Tatu iundwe tume huru yenye wajumbe kutoka pande zote, makanisa, Serikali na UAMSHO ili zichunguzwe tuhuma hizi kwa undani zaidi maana kwa kweli athari zinaweza zikawa za muda mrefu kwani zinapandikiza kutoaminiana baina ya Wazanzibar hasa wakristo na waislam jambo ambalo halikuwepo hapo kabla na yoyote takae bainika kuwa na hatia sheria ichukue mkondo wake bila ya kujali wadhifa alionao katika chama, dini ama Serikali.

Mwisho tunamuomba Allah atupe Imani ya kweli katika nchi yetu na kama kuna fisadi na adui Allah amdhalilishe hapahapa Duniani, amen.

Wabillah Tawfiq.

Sheikh Issah Bin Shaabani Simba.

Sheikh Mkuu na Muft wa Tanzania
 
Sasa kama wamisionari wa wajerumani walifuta nyayo za waislam Tanzania, je, ilikuwaje katika nchi ambazo hazikuqa na waislam kabla kama Namibia, Kamerun na Togo?
Nchi hizi na zenyewe zilikuwa colonized na wajerumani na walipeleka wamisionari huko pia.
Syll...
Takriban nusu ya umri wangu wa miaka 68 naingia 69 In Shaa Allah Februari nimekuwa nikiandika vitabu, ''academic papers,'' na makala nyingi zisizo na hesabu kuhusu Uislam Tanzania na nimehudhuria mikutano mingi ndani na nje ya Tanzania pamoja na kuzungumza katika vyuo mbalimbali Afrika, Ulaya na Marekani.

Naweza kujidai kuwa suala hili nalijua kwa kiasi changu.

Katika ujuzi huu kuna namna ya ''pattern,'' nimejenga na kwa sasa naweza kusema imekuwa sawasawa na sheria au kanuni ya aina fulani mfano wa ''Archimedes Principle.''

Mfano ni kama huu wako.

Unapoona mtu anaandika kwa staili yako kuwa liko tatizo na linajadiliwa na mtu anaandika kwa kusema kama unavyosema wewe kuwa huwajuia Waislam, Waarabu, Wakristo, Waafrika, Wamishionari nk; huyu tafuta imani yake utakuta si Muislam.

Sasa utafiti wangu haukuishia hapa ili niweze kuitengeneza hii sheria yangu au kanuni iweze kuwa na mashiko ni lazima nijue kiwango cha elimu yake.

Nitakijuaje?

Huwa namtia hamu ya kufanya majadala na mimi na kila anapoandika najaribu kupima kiwango cha elimu yake na si kazi kubwa mara moja naweza kukisia kama ni elimu ya chini, kati au juu.

Hapa nitaeleza jambo.

Uzoefu wangu unaonesha kuwa baadhi katika mjadala huu wa dhulma huwa wanapandwa na hamaki kwa kukosa hoja na huja na lugha kali na pengine matusi na vitisho au kunishambulia binafsi badala ya kujibu hoja.

Lakini haya yote yamesaidia sana katika kuelewa uzito wa suala hili.

Suala linalofuatia ni kwa nini ghafla baada ya kujua uwezo wake kuwa kiwango chake cha elimu ni kizuri anaandika kama mtu asiyejua kitu?

Sasa ili kupata ''conclusion,'' au uhakika wa kile ninachotafuta ni lazima hii ''pattern'' yangu iwe na ''sampling,'' kubwa yaani nimejadiliana na watu wengi katika jamii katika tatizo hili.

Nilichogundua ni kuwa imani ina nafasi kubwa sana katika fikra kiasi anaona kukubali ukweli anaowekewa wazi ni kushindwa kwa imani yake.

Hiki ni kitu muhali mkubwa sana kwake hawezi kukiruhusu.

Sasa ukichukua ukweli huu ukauweka katika serikali ambayo watendaji wakuu wanaoshika nafasi za maamuzi ni wa imani moja kwa mathalan uwiano wa 20:80 utaelewa bila tabu yote kwa nini hali iko hivyo ilivyo kuwa Waislam wanajaribu kueleza matatizo yao lakini hakuna aliye tayari katika serikali kusikiliza au hata kuamini kuwa liko tatizo.

Hapa ndipo linapoingia lile suala linalotisha.

Ni akina nani waliotoa uamuzi wa kuvunjwa kwa EAMWS wakati wanajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na kutekeleza mipango yao ya elimu?

Nini lilikuwa kusudio lao?

Hofu kuwa Waislam wataelimika na hivyo kushika madaraka katika serikali ya Tanganyika huru?

Ndiyo hapo ghafla unasoma mtu kama Edwayne anaandika kuwa Uislam na Ukristo zote ni dini za shetani na utumwa.

Tafuta imani yake utapata jibu.

Lakini ukiangalia mjadala si huo bali ni dhulma ambayo Waislam wanaeleza serikali kuwa wamekuwa wanafanyiwa toka uhuru upatikane mwaka wa 1961 na vielelezo vyote kama ushahidi wameweka.

Nachelea kumchosha msomaji lakini mifano ipo mingi.

Tatizo ni kuwa viongozi wetu hawako tayari kuliweka tatizo hili katika agenda lijadiiwe kwa wazi kwa hofu ambayo si tabu kuitambua.
Edwayne,
Soma hii barua hapo chini:

MK/HB. VOL.5/07/101 06/06/2012

MAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: HUJUMA ZA BARAZA LA MITIHANI DHIDI YA WAISLAM


Kila sifa njema anastahiki Allah, ambaye rehema zake zimeenea katika kila kitu katika ulimwengu bila ya kujali utii ama uasi wa kitu hicho katika amri na sharia zake.

Rehema na amani zimuendee kipenzi chetu mtume Muhammad (S.A.W) kwa kuwa kiigizo chema na rehema kwa walimwengu wote.

Ndugu waandishi kwa muda mrefu Waislam wamekuwa wakiilalamikia suala zima la utendaji wa serikali kuwa umekuwa wakibaguzi kwa kuwapendelea Wakirsto kwa kuwapa nafasi mbalimbali muhimu serikalini na katika taasisi zake.

Ndugu waandishi na Waislam mnamo tarehe 01/ 05/2012 Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya kidato cha sita, matokeo hayo yaliwashtua sana wanafunzi Waislam waliofanya mtihani wa elimu ya dini ya Kiislam (Islamic Knowledge). Takriban asilimia 70 walifeli kwa kupata daraja F, na asilimia 30 ndio waliofaulu tu.

Katika hao waliofaulu walipata alama za juu kabisa nchi nzima ni wanafunzi saba tu ambao wamepata daraja D, kwa matokeo haya somo hili likawa somo la mwisho kwa ufaulu nchi nzima (rejea kitabu cha takwimu cha Baraza la Mitihani Tanzania April 2012.

Matokeo haya yaliwashtua wazazi na walimu wa somo hili, baadhi ya wanafunzi waliamua kukata rufaa ya kutokubaliana na matokeo hayo.

Waislam kupitia Taasisi mbali mbali za Kiislam walimuandikia Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kumuomba aunde tume huru kuchunguza matokeo ya somo husika.

Kufuatia malalamiko hayo ya baadhi ya taasisi za dini, Barraza la Mitihani liliyatazama matokeo hayo na kugundua pia walikosea na hivyo Baraza la Mitihani likaidhinisha kutolewa matokeo mapya kwa somo hilo.

Mabadiliko hayo ya matokeo ufaulu kwa wanafunzi wale wale ambao awali walifeli kwa asilimia 70, sasa yakabadilika na ufaulu ukaongezeka kwa zaidi ya asilimia 70.

Kwa namna yoyote ile itakavyokuwa dosari kubwa kama hii ni kashfa kubwa kwa Baraza la Mitihani Tanzania na Serikali kwa ujumla.

Na kwa kutilia maanani muundo na historia ya utendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania kama nilivyoanza kuelezea, Waislam wanayokila sababu ya kuamini kwamba matokeo haya ni uthibitisho tosha wa hujuma ambazo wanafunzi wa kiislam walikuwa wakifanyiwa kwa muda mrefu.

Na hii inatupa picha kwamba dosari hizi zilizotokea kwenye somo la maarifa ya Kiislam, haziishii kwenye somo hili, bali uchunguzi ukifanyika kwa masomo yote waliofanya wanafunzi wa Kiislam itadhihirika kwamba hila na dhulma kama hizi zinafanyika katika masomo mengine.

Kimsingi kwa dhulma hii waliyoifanya Baraza la Mitihani dhini ya wanafunzi wa Kiislam, Bakwata na Waislam wote kwa ujumla wamepoteza imani na Baraza la Mitihani la Tanzania na hasa katibu mtendaji wake .

Bakwata, linawapongeza na kuwaunga mkono Taasisi zote za Kiislam nchini kwa jitihada ya kuligundua hili na hatua walizozichukuwa dhidi ya Baraza la Mitihani na kuhufahamisha umma wa Kiislam juu ya kadhia hii.

Tunarudia baraza tunawapongeza taasisi zote za kiislam na tunasema katika hili Bakwata tuko nyuma yao kwani kauli yao ndio kauli yetu.

Bakwata, inamshangaa Katibu Mtendaji wa Baraza la mitihani (Necta) Dk. Joyce Ndalichako, kwa kauli yake aliyoitoa kupitia vyombo mbali mbali vya habari vya jana tarehe 5/06/2012, akisema hakuna hujuma na mitihani inasahihishwa na walimu wenye sifa,wanachaguliwa na na wakuu wa shule zao, walimu wenye uzoofu na kuna mfumo wa usahihishaji aliouita “Conveyor Belt”.

Bakwata inasema hapa tatizo la msingi sio mitihani kusahihishwa na walimu wenye sifa, na nani anawachagua walimu hao wenye sifa au huo mfumo wa usahihishaji, tatizo la msingi hapa ni kufelishwa kwa makusudi kwa wanafunzi wetu wa Kiislam katika somo husika, wakati nakala za mitihani yao (Scripts) zinaonyesha wamefaulu.

Bakwata, tunahoji kwanini tatizo hili la huo mfumo (Conveyor Belt) litokee mwaka huu, mbona matokeo ya mwaka jana waislam hawakulalamika na kulikuwa hakuna dosari kama za mwaka huu iweje itokee mwaka huu, wakati mfumo ni ule ule?

Bakwata, tunaamini Waislam katika hili tumehujumiwa na Waislam hawajaridhishwa na majibu ya Dk. Ndalichako, aliyoyatoa kupitia vyombo vya habari vya hapa nchini.

Hiyo mifumo ya usahihishaji sio maneno matakatifu kwamba haiwezi kuchezewa kutokana hila za binadamu ni mifumo iliyowekwa na binadamu, na binadamu huyohuyo anaweza kuibadilishabadilisha vyovyote anavyotaka.

Sisi kama Bakwata,tunaamini ili kurudisha imani ya Waislam dhidi ya Baraza la Mitihani tunataka mambo yafuatayo yafanyike:
  • Tume huru iundwe la kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake wa kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
  • Katibu mkuu wa Baraza la Mitihani (Necta) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Baraza la Mitihani.
  • Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa kompyuta ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.
  • Hatua za kisheria na kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa baraza la mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.
  • Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha makatibu wakuu watendaji na manaibu katibu wakuu wamekuwa wakristo na wenyevyiti wa baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.
  • Pia tunaiyomba Serikali iwape nafasi wanafunzi wote ambao baada ya matokeo yao kubadilishwa wamekuwa na sifa za kujiunga na vyuo vikuu waruhusiwe kuomba mikopo bodi ya mikopo, tunalisema hili kutokana na
  • muda wa kuomba mikopo kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu kwisha.
Suala la Sensa ya watu na makazi.


Kama tunavyojua kwa mwaka huu wa 2012, kuna zoezi la sense ya watu na makazi ambayo inatarajiwa kufanyika kuanzia mwezi wa nane, 2012, na kutoka na upotoshaji ulioenea kwenye vyombo vya habari hapa nchini, kalenda iliyochapichwa na ofisi ya waziri mkuu, imetoa takwimu zinazoonyesha idadi ya watanzania ni milioni 43 ambapo kwa mujibu wa dini zao wakristo ni asilimia 52, waislam asilimia 32 na dini zingine ni asilimia 16.

Bakwata tunalaani kitendo hiki na tunasema takwimu hizi sio sahihi na zinapotosha wananchi, hii ni kwa sababu katika sense zilizofanyika hivi karibuni ikiwemo sense ya mwaka 2002 kipengele kinachobainisha dini za watanzania kiliondolewa.

Kwakuwa taarifa hizi zinaonekana kwenye kalenda zinazoonyesha zimetayarishwa na ofisi ya waziri mkuu, tunaitaka serikali kurudisha kipengele kinachobainisha dini za watanzania katika sense ya mwaka huu ili ukweli ujulikane na kuondoa kabisa sintofahamu hii.

SUALA LA MGOGORO WA HIVI KARIBUNI ZANZIBAR

Ndugu waandishi wa habari naamini nyinyi nyote kama waandishi wa habari mnajua au mmesikia vurugu zilizohusisha imani za dini zilizotokea visiwani humo na kutokana na taarifa nyingi za vyombao vya habari zilizokuwa zikitolewa tangu mgogogro huu uanze kuna kila dalili za kuchukuliwa hatua za haraka haraka na katika mazingira haya wale wote waliohusika na vurugu hizi wasijulikane tena na watu wasio na hatia wakahusishwa na hali ikawa mbaya zaidi kwa hivy o kutokana na kadhia yote hiyo na yote yaliyosemwa na makundi mbalimbali ya waisla na wasiokuwa waislam Sisi kama Bakwata tunasema yafuatayo:

Kwanza tunalaani kitendo cha uvunjifu wa amani uliotokea Zanzibar na tunaamini waliofanya vurugu zote zile sio waislam bali ni wahuni tu.

Pili tunasema Wazanzibar, wasikilizwe kwa yale ambayo wanayapigia kelele kama malalamiko yao yapo katika muungano Serikali haina budi kuyasikiliza yale yote yanayolalamikiwa na kuyarekebisha, kwani Muungano sio qur- an useme kilichomo humo hakiwezi kurekebishika.

Tatu iundwe tume huru yenye wajumbe kutoka pande zote, makanisa, Serikali na UAMSHO ili zichunguzwe tuhuma hizi kwa undani zaidi maana kwa kweli athari zinaweza zikawa za muda mrefu kwani zinapandikiza kutoaminiana baina ya Wazanzibar hasa wakristo na waislam jambo ambalo halikuwepo hapo kabla na yoyote takae bainika kuwa na hatia sheria ichukue mkondo wake bila ya kujali wadhifa alionao katika chama, dini ama Serikali.

Mwisho tunamuomba Allah atupe Imani ya kweli katika nchi yetu na kama kuna fisadi na adui Allah amdhalilishe hapahapa Duniani, amen.

Wabillah Tawfiq.

Sheikh Issah Bin Shaabani Simba.

Sheikh Mkuu na Muft wa Tanzania
Sheikh Mohamed Saidi: naona wajumbe wamekukaba koo huku mwenziyo nimetulia tuli! Miecsikutoka kwa khasr wala jazba ila ni kutoa nafasi kwa wajumbe tuache kuimonopolize mada.

Nina mawili matatu, nipe majibu hey presto kama una ubavu.

La kwanza umemtaja Mmisionari Ludwig Krapf, kafa, Mtemi Kimweri, he is dead too. aarabu bado wapo Tanga, na sisi tupo, hati za Kiarabu zipo, hati za Kirumi zipo. Kwa nini hatujaona usitawi wa hati za Kiarabu zitumike kufundisha IFM na SUA? I bet hata wewe hapo ulipo hujui Kiarabu. Kakangu, unawasakama Wamisionari hadi leo?

La pili, kumbuka Wajerumani na Waarabu wote majizi, walIkuja kuiba ninihii zetu na hadi leo bado wananyemelea makanikia yetu. Mtemi Kimweri alijua Kiarabu kutoka kwa mkoloni mkongwe Mwarabu, tena baada ya kusomba Wazigua alfu kwenda utumwani. Angekuwa si Manyema mwenziyo Karume tungelikuwa watumwa wa kukaanga karafuu hadI leo. Shame on you, mate!

Tatu, niwasaidie wasomaji wako, najua weye unajua. Hapa tuna vitabu viwili tafauti ingawa mtunzi huyo huyo. Cha kwanza, in Queen's English, ni sahihi, objective, kinauma na kupuliza lakini kinatanguliza ukweli. Mwandishi wetu alipata nafasi kwenda kusoma IFM kawa Mhasibu, in the process akatekwa na Mujaheedeen, waislamu wenye siasa kali. Ghafla bin vuu, Mody wetu, mwenzetu, ndugu yetu, mwanetu, katoa translation ya Kiswahili yote imejaa urongo mtupu! Anasifia Waarabu, anasifia Wamanyema, yaani utadhani walitapakaa mpaka Iramba na Tandahimba. Mie ningekuwa ndiye publisher wa The and Times of AWS, wallahi ningekuburuza mahakamani kwa kosa la kuchakachua copyright ya kitabu kizuri kabisa.

Kabla hujalialia sana niseme tu kuwa AboudJumbe, Shujaa wa Nji hii, naye alifanya kosa hilo alipotranslate kitabu chake murua. That makes 2 of you.

La mwisho, umemleta Mufti. Mie na Watanzania wengi sana tunaamini kuwa dua la Mufti (alianza yeye, nadhani mwishoni alilia kwa uchungu!) limetuokoa na janga la corona. Kama kuna mtu mmoja anayanyanyua Utanzania wetu na Mungu wetukatika umoja wetu, ni huyo Baba.

Naishia hapo, ngoja njemba wakugaragaze kwanza nitajarudi kukuokoa yakikufija hapa. Abdulwahi tawfiq.
 
Edwayne,
Soma hii barua hapo chini:

MK/HB. VOL.5/07/101 06/06/2012

MAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: HUJUMA ZA BARAZA LA MITIHANI DHIDI YA WAISLAM


Kila sifa njema anastahiki Allah, ambaye rehema zake zimeenea katika kila kitu katika ulimwengu bila ya kujali utii ama uasi wa kitu hicho katika amri na sharia zake.

Rehema na amani zimuendee kipenzi chetu mtume Muhammad (S.A.W) kwa kuwa kiigizo chema na rehema kwa walimwengu wote.

Ndugu waandishi kwa muda mrefu Waislam wamekuwa wakiilalamikia suala zima la utendaji wa serikali kuwa umekuwa wakibaguzi kwa kuwapendelea Wakirsto kwa kuwapa nafasi mbalimbali muhimu serikalini na katika taasisi zake.

Ndugu waandishi na Waislam mnamo tarehe 01/ 05/2012 Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya kidato cha sita, matokeo hayo yaliwashtua sana wanafunzi Waislam waliofanya mtihani wa elimu ya dini ya Kiislam (Islamic Knowledge). Takriban asilimia 70 walifeli kwa kupata daraja F, na asilimia 30 ndio waliofaulu tu.

Katika hao waliofaulu walipata alama za juu kabisa nchi nzima ni wanafunzi saba tu ambao wamepata daraja D, kwa matokeo haya somo hili likawa somo la mwisho kwa ufaulu nchi nzima (rejea kitabu cha takwimu cha Baraza la Mitihani Tanzania April 2012.

Matokeo haya yaliwashtua wazazi na walimu wa somo hili, baadhi ya wanafunzi waliamua kukata rufaa ya kutokubaliana na matokeo hayo.

Waislam kupitia Taasisi mbali mbali za Kiislam walimuandikia Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kumuomba aunde tume huru kuchunguza matokeo ya somo husika.

Kufuatia malalamiko hayo ya baadhi ya taasisi za dini, Barraza la Mitihani liliyatazama matokeo hayo na kugundua pia walikosea na hivyo Baraza la Mitihani likaidhinisha kutolewa matokeo mapya kwa somo hilo.

Mabadiliko hayo ya matokeo ufaulu kwa wanafunzi wale wale ambao awali walifeli kwa asilimia 70, sasa yakabadilika na ufaulu ukaongezeka kwa zaidi ya asilimia 70.

Kwa namna yoyote ile itakavyokuwa dosari kubwa kama hii ni kashfa kubwa kwa Baraza la Mitihani Tanzania na Serikali kwa ujumla.

Na kwa kutilia maanani muundo na historia ya utendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania kama nilivyoanza kuelezea, Waislam wanayokila sababu ya kuamini kwamba matokeo haya ni uthibitisho tosha wa hujuma ambazo wanafunzi wa kiislam walikuwa wakifanyiwa kwa muda mrefu.

Na hii inatupa picha kwamba dosari hizi zilizotokea kwenye somo la maarifa ya Kiislam, haziishii kwenye somo hili, bali uchunguzi ukifanyika kwa masomo yote waliofanya wanafunzi wa Kiislam itadhihirika kwamba hila na dhulma kama hizi zinafanyika katika masomo mengine.

Kimsingi kwa dhulma hii waliyoifanya Baraza la Mitihani dhini ya wanafunzi wa Kiislam, Bakwata na Waislam wote kwa ujumla wamepoteza imani na Baraza la Mitihani la Tanzania na hasa katibu mtendaji wake .

Bakwata, linawapongeza na kuwaunga mkono Taasisi zote za Kiislam nchini kwa jitihada ya kuligundua hili na hatua walizozichukuwa dhidi ya Baraza la Mitihani na kuhufahamisha umma wa Kiislam juu ya kadhia hii.

Tunarudia baraza tunawapongeza taasisi zote za kiislam na tunasema katika hili Bakwata tuko nyuma yao kwani kauli yao ndio kauli yetu.

Bakwata, inamshangaa Katibu Mtendaji wa Baraza la mitihani (Necta) Dk. Joyce Ndalichako, kwa kauli yake aliyoitoa kupitia vyombo mbali mbali vya habari vya jana tarehe 5/06/2012, akisema hakuna hujuma na mitihani inasahihishwa na walimu wenye sifa,wanachaguliwa na na wakuu wa shule zao, walimu wenye uzoofu na kuna mfumo wa usahihishaji aliouita “Conveyor Belt”.

Bakwata inasema hapa tatizo la msingi sio mitihani kusahihishwa na walimu wenye sifa, na nani anawachagua walimu hao wenye sifa au huo mfumo wa usahihishaji, tatizo la msingi hapa ni kufelishwa kwa makusudi kwa wanafunzi wetu wa Kiislam katika somo husika, wakati nakala za mitihani yao (Scripts) zinaonyesha wamefaulu.

Bakwata, tunahoji kwanini tatizo hili la huo mfumo (Conveyor Belt) litokee mwaka huu, mbona matokeo ya mwaka jana waislam hawakulalamika na kulikuwa hakuna dosari kama za mwaka huu iweje itokee mwaka huu, wakati mfumo ni ule ule?

Bakwata, tunaamini Waislam katika hili tumehujumiwa na Waislam hawajaridhishwa na majibu ya Dk. Ndalichako, aliyoyatoa kupitia vyombo vya habari vya hapa nchini.

Hiyo mifumo ya usahihishaji sio maneno matakatifu kwamba haiwezi kuchezewa kutokana hila za binadamu ni mifumo iliyowekwa na binadamu, na binadamu huyohuyo anaweza kuibadilishabadilisha vyovyote anavyotaka.

Sisi kama Bakwata,tunaamini ili kurudisha imani ya Waislam dhidi ya Baraza la Mitihani tunataka mambo yafuatayo yafanyike:
  • Tume huru iundwe la kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake wa kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
  • Katibu mkuu wa Baraza la Mitihani (Necta) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Baraza la Mitihani.
  • Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa kompyuta ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.
  • Hatua za kisheria na kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa baraza la mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.
  • Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha makatibu wakuu watendaji na manaibu katibu wakuu wamekuwa wakristo na wenyevyiti wa baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.
  • Pia tunaiyomba Serikali iwape nafasi wanafunzi wote ambao baada ya matokeo yao kubadilishwa wamekuwa na sifa za kujiunga na vyuo vikuu waruhusiwe kuomba mikopo bodi ya mikopo, tunalisema hili kutokana na
  • muda wa kuomba mikopo kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu kwisha.
Suala la Sensa ya watu na makazi.


Kama tunavyojua kwa mwaka huu wa 2012, kuna zoezi la sense ya watu na makazi ambayo inatarajiwa kufanyika kuanzia mwezi wa nane, 2012, na kutoka na upotoshaji ulioenea kwenye vyombo vya habari hapa nchini, kalenda iliyochapichwa na ofisi ya waziri mkuu, imetoa takwimu zinazoonyesha idadi ya watanzania ni milioni 43 ambapo kwa mujibu wa dini zao wakristo ni asilimia 52, waislam asilimia 32 na dini zingine ni asilimia 16.

Bakwata tunalaani kitendo hiki na tunasema takwimu hizi sio sahihi na zinapotosha wananchi, hii ni kwa sababu katika sense zilizofanyika hivi karibuni ikiwemo sense ya mwaka 2002 kipengele kinachobainisha dini za watanzania kiliondolewa.

Kwakuwa taarifa hizi zinaonekana kwenye kalenda zinazoonyesha zimetayarishwa na ofisi ya waziri mkuu, tunaitaka serikali kurudisha kipengele kinachobainisha dini za watanzania katika sense ya mwaka huu ili ukweli ujulikane na kuondoa kabisa sintofahamu hii.

SUALA LA MGOGORO WA HIVI KARIBUNI ZANZIBAR

Ndugu waandishi wa habari naamini nyinyi nyote kama waandishi wa habari mnajua au mmesikia vurugu zilizohusisha imani za dini zilizotokea visiwani humo na kutokana na taarifa nyingi za vyombao vya habari zilizokuwa zikitolewa tangu mgogogro huu uanze kuna kila dalili za kuchukuliwa hatua za haraka haraka na katika mazingira haya wale wote waliohusika na vurugu hizi wasijulikane tena na watu wasio na hatia wakahusishwa na hali ikawa mbaya zaidi kwa hivy o kutokana na kadhia yote hiyo na yote yaliyosemwa na makundi mbalimbali ya waisla na wasiokuwa waislam Sisi kama Bakwata tunasema yafuatayo:

Kwanza tunalaani kitendo cha uvunjifu wa amani uliotokea Zanzibar na tunaamini waliofanya vurugu zote zile sio waislam bali ni wahuni tu.

Pili tunasema Wazanzibar, wasikilizwe kwa yale ambayo wanayapigia kelele kama malalamiko yao yapo katika muungano Serikali haina budi kuyasikiliza yale yote yanayolalamikiwa na kuyarekebisha, kwani Muungano sio qur- an useme kilichomo humo hakiwezi kurekebishika.

Tatu iundwe tume huru yenye wajumbe kutoka pande zote, makanisa, Serikali na UAMSHO ili zichunguzwe tuhuma hizi kwa undani zaidi maana kwa kweli athari zinaweza zikawa za muda mrefu kwani zinapandikiza kutoaminiana baina ya Wazanzibar hasa wakristo na waislam jambo ambalo halikuwepo hapo kabla na yoyote takae bainika kuwa na hatia sheria ichukue mkondo wake bila ya kujali wadhifa alionao katika chama, dini ama Serikali.

Mwisho tunamuomba Allah atupe Imani ya kweli katika nchi yetu na kama kuna fisadi na adui Allah amdhalilishe hapahapa Duniani, amen.

Wabillah Tawfiq.

Sheikh Issah Bin Shaabani Simba.

Sheikh Mkuu na Muft wa Tanzania
Mbona baada ya kuamuliwa kutumika namba badala ya majina bado shule zenu ni ZERO ZERO ZERO TUPU?
 
Syll...
Takriban nusu ya umri wangu wa miaka 68 naingia 69 In Shaa Allah Februari nimekuwa nikiandika vitabu, ''academic papers,'' na makala nyingi zisizo na hesabu kuhusu Uislam Tanzania na nimehudhuria mikutano mingi ndani na nje ya Tanzania pamoja na kuzungumza katika vyuo mbalimbali Afrika, Ulaya na Marekani.

Naweza kujidai kuwa suala hili nalijua kwa kiasi changu.

Katika ujuzi huu kuna namna ya ''pattern,'' nimejenga na kwa sasa naweza kusema imekuwa sawasawa na sheria au kanuni ya aina fulani mfano wa ''Archimedes Principle.''

Mfano ni kama huu wako.

Unapoona mtu anaandika kwa staili yako kuwa liko tatizo na linajadiliwa na mtu anaandika kwa kusema kama unavyosema wewe kuwa huwajuia Waislam, Waarabu, Wakristo, Waafrika, Wamishionari nk; huyu tafuta imani yake utakuta si Muislam.

Sasa utafiti wangu haukuishia hapa ili niweze kuitengeneza hii sheria yangu au kanuni iweze kuwa na mashiko ni lazima nijue kiwango cha elimu yake.

Nitakijuaje?

Huwa namtia hamu ya kufanya majadala na mimi na kila anapoandika najaribu kupima kiwango cha elimu yake na si kazi kubwa mara moja naweza kukisia kama ni elimu ya chini, kati au juu.

Hapa nitaeleza jambo.

Uzoefu wangu unaonesha kuwa baadhi katika mjadala huu wa dhulma huwa wanapandwa na hamaki kwa kukosa hoja na huja na lugha kali na pengine matusi na vitisho au kunishambulia binafsi badala ya kujibu hoja.

Lakini haya yote yamesaidia sana katika kuelewa uzito wa suala hili.

Suala linalofuatia ni kwa nini ghafla baada ya kujua uwezo wake kuwa kiwango chake cha elimu ni kizuri anaandika kama mtu asiyejua kitu?

Sasa ili kupata ''conclusion,'' au uhakika wa kile ninachotafuta ni lazima hii ''pattern'' yangu iwe na ''sampling,'' kubwa yaani nimejadiliana na watu wengi katika jamii katika tatizo hili.

Nilichogundua ni kuwa imani ina nafasi kubwa sana katika fikra kiasi anaona kukubali ukweli anaowekewa wazi ni kushindwa kwa imani yake.

Hiki ni kitu muhali mkubwa sana kwake hawezi kukiruhusu.

Sasa ukichukua ukweli huu ukauweka katika serikali ambayo watendaji wakuu wanaoshika nafasi za maamuzi ni wa imani moja kwa mathalan uwiano wa 20:80 utaelewa bila tabu yote kwa nini hali iko hivyo ilivyo kuwa Waislam wanajaribu kueleza matatizo yao lakini hakuna aliye tayari katika serikali kusikiliza au hata kuamini kuwa liko tatizo.

Hapa ndipo linapoingia lile suala linalotisha.

Ni akina nani waliotoa uamuzi wa kuvunjwa kwa EAMWS wakati wanajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na kutekeleza mipango yao ya elimu?

Nini lilikuwa kusudio lao?

Hofu kuwa Waislam wataelimika na hivyo kushika madaraka katika serikali ya Tanganyika huru?

Ndiyo hapo ghafla unasoma mtu kama Edwayne anaandika kuwa Uislam na Ukristo zote ni dini za shetani na utumwa.

Tafuta imani yake utapata jibu.

Lakini ukiangalia mjadala si huo bali ni dhulma ambayo Waislam wanaeleza serikali kuwa wamekuwa wanafanyiwa toka uhuru upatikane mwaka wa 1961 na vielelezo vyote kama ushahidi wameweka.

Nachelea kumchosha msomaji lakini mifano ipo mingi.

Tatizo ni kuwa viongozi wetu hawako tayari kuliweka tatizo hili katika agenda lijadiiwe kwa wazi kwa hofu ambayo si tabu kuitambua.
Unaweza kuwa umepata fursa ya kwenda kokote au kuzungumza kokote lakini bado ukawa na USHAMBA WA UDINI, UONGO na Kulialia kama mwanamke mjane
 
JK,
Hatuwezi kurudi nyuma.

Kuwaambia Waislam waingie BAKWATA ni kuwashughulisha pasi na sababu.

Kitu chochote kilichoanzishwa kwa minajili ya kupambana na Allah kwa Waislam watakikalia mbali.

Shule za Kiislam ziko nyingi kwa sasa.
Katika elimu ya Waislam kuna matatizo mengi.

Nadhani ulisikia kisa cha Baraza la Mitihani lilivyokuwa linahujumu shule za Kiislam na wakuu wa shule hizi wakaandika taarifa ikapelekwa serikalini.

Waislam kwa ajili hii walifanya maandamano bila kibali na serikali ilitoa vitisho kuwa maandamano hayo ni haram.

Haya maandamano yalifanyika juu ya kuwa walitumwa askari Msikiti wa Kichangani yalipokuwa yanaanzia na helikopta zikiwa zinazunguka juu kama vitisho na Kamanda Suleiman Kova akatoa tangazo la kutisha walioazimia kuandamana kupinga dhulma.

Kisa hiki ni kirefu na maandamano haya yaliongozwa na Sheikh Ponda.

Ilikuwa mwaka wa 2012.

BAKWATA iliundwa baada ya EAMWS kupigwa marufuku na serikali wakati inajitayarisha kujenga Chuo Kikuu Cha Waislam Chang'ombe huku ikijenga shule majimboni kuanzia mwaka wa 1962 baada ya Muslim Congress mara tu baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.

Hii ni historia inayowapa shida sana serikali na viongozi wa BAKWATA waliopo madarakani.

Si jambo wanalopenda Waislam walifahamu.
UONGO MWINGINE

Mzee huna aibu weyee????

Shule zote maarufu za zamani zilijengwa na Wamisionary wakikristo kisha baadae Serikali ikataifisha ili na waislam ambao walikuwa wanatawadha tu na kucheza bao wapate angalau elimu

Hata wasomi maarufu wachache wakiislam walisoma katika seminary za kikristo ndio maana wana akili timamu na wanajielewa, kama:-

Rais mstaafu J.M KIKWETE, Prof Ibrahim LIPUMBA na wengine.

Shule hizo ni kama Pugu, Ilboru n.k

Huo ndio ukweli ulio wazi na ushahidi upo.

Hizo zingine unazoandika ni kutokana na Udini uliokujaa na Uzushi uliyojitungia


TAKIBIIIIR..........!
 
..nimesoma historia uliyoandika kuhusu kuanzishwa kwa Bakwata.

..hata nikikubaliana na wewe 100% bado inaniumiza kuona sekondari za Bakwata zikifanya vibaya.

..na waathirika wa sekondari za Bakwata ni watoto wa imani mbalimbali, lakini mostly ni watoto wa Kiislamu.

..kwanini Waislamu msiungane ktk suala hili la ELIMU na hayo mengine mkayashughulikia baadae?

..Na ukichunguza Waislamu ni matajiri wakubwa hapa nchini, sasa inakuwaje shule za taasisi ya Kiislamu iliyopo nchi nzima kama Bakwata zikatelekezwa kiasi hiki?

..Mimi nawashauri muungane mrekebishe madhaifu yaliyoko ktk sekondari za Bakwata.
Yaani ni sawa na kuwalazimisha waislam wale kitimoto au wabatizwe, kukubali na kupokea Ilim sio jambo jepesi kwa Waumin wa Mwamedi shekhe

Wabillah Tawfiq,
 
Sheikh Mohamed Saidi: naona wajumbe wamekukaba koo huku mwenziyo nimetulia tuli! Miecsikutoka kwa khasr wala jazba ila ni kutoa nafasi kwa wajumbe tuache kuimonopolize mada.

Nina mawili matatu, nipe majibu hey presto kama una ubavu.

La kwanza umemtaja Mmisionari Ludwig Krapf, kafa, Mtemi Kimweri, he is dead too. aarabu bado wapo Tanga, na sisi tupo, hati za Kiarabu zipo, hati za Kirumi zipo. Kwa nini hatujaona usitawi wa hati za Kiarabu zitumike kufundisha IFM na SUA? I bet hata wewe hapo ulipo hujui Kiarabu. Kakangu, unawasakama Wamisionari hadi leo?

La pili, kumbuka Wajerumani na Waarabu wote majizi, walIkuja kuiba ninihii zetu na hadi leo bado wananyemelea makanikia yetu. Mtemi Kimweri alijua Kiarabu kutoka kwa mkoloni mkongwe Mwarabu, tena baada ya kusomba Wazigua alfu kwenda utumwani. Angekuwa si Manyema mwenziyo Karume tungelikuwa watumwa wa kukaanga karafuu hadI leo. Shame on you, mate!

Tatu, niwasaidie wasomaji wako, najua weye unajua. Hapa tuna vitabu viwili tafauti ingawa mtunzi huyo huyo. Cha kwanza, in Queen's English, ni sahihi, objective, kinauma na kupuliza lakini kinatanguliza ukweli. Mwandishi wetu alipata nafasi kwenda kusoma IFM kawa Mhasibu, in the process akatekwa na Mujaheedeen, waislamu wenye siasa kali. Ghafla bin vuu, Mody wetu, mwenzetu, ndugu yetu, mwanetu, katoa translation ya Kiswahili yote imejaa urongo mtupu! Anasifia Waarabu, anasifia Wamanyema, yaani utadhani walitapakaa mpaka Iramba na Tandahimba. Mie ningekuwa ndiye publisher wa The and Times of AWS, wallahi ningekuburuza mahakamani kwa kosa la kuchakachua copyright ya kitabu kizuri kabisa.

Kabla hujalialia sana niseme tu kuwa AboudJumbe, Shujaa wa Nji hii, naye alifanya kosa hilo alipotranslate kitabu chake murua. That makes 2 of you.

La mwisho, umemleta Mufti. Mie na Watanzania wengi sana tunaamini kuwa dua la Mufti (alianza yeye, nadhani mwishoni alilia kwa uchungu!) limetuokoa na janga la corona. Kama kuna mtu mmoja anayanyanyua Utanzania wetu na Mungu wetukatika umoja wetu, ni huyo Baba.

Naishia hapo, ngoja njemba wakugaragaze kwanza nitajarudi kukuokoa yakikufija hapa. Abdulwahi tawfiq.
LGF,
Ungefanya kwanza utafiti lau mdogo unifahamu ili uandikayo yawe ya kweli.

Hapa tungefanya mjadala wa kupendeza.

Vinginevyo nitakuwa nakanusha kila jambo lako kuhusu mie.
 
Waislamu hawajapuuza elimu, hili ni kweli. Kinachogombewa ni sawa tu nz maongezi ya siku hizi kuwa haiwatayarishi vijana kujitegemea, inawadumiza kusubiri wapewe kazi, walishwe na kuhudumiwa. Wamisionari wameleta shule zao watu wamesoma bila ubaguzi (soma kwanza, batizwa baadaye, shule za waislami ni za waislam zilifundisha uislamu).

Kumbuka kuwa Tanganyika haijawahi kuwa nchi ya Waislamu, wala ya Wakristo, hii ilikuwa nchi ya Wapagani. Sensa 1965 ilikuta Wapagani 35% Wauslamu 33% Wakristu 31%. Ukihesabu leo (Nyerere alifuta) utakuta Waislamu bado ni 33% lskini Wapagani wamebaki 20% (sanasana Serengeti, Usukunani na Wakinga).


Nitajie shule za Waislamu zilizoelimisha Watanganyika? Hakuna, labda utaje za Aga Khan (Usagara, Tambaza, Kisutu, lakini hizi zilikuwa hazifundishi uislam). Na Wamisionari? St Francis (Pugu), St Michael & St George (Mkwawa), Rosary College (Ngaza), Marian College (Kilakala) hizi zinewasonesha "wapagani".

Kusifia Wamisionari si kudogosha Waislam, kila mmoja alifanya alichoweza Inshaallah.

Umemtaja Aga Khan na EAMWS hapo ni manati yenyewe. Soma kitabu cha Abdulwaheed Sykes mtunzi Mohamed Said. Soma kile cha Kiingereza kimeelezea vizuri (cha Kiswahili kilichakachuliwa kwenye translation baada ya mwandishi kuwa siasa kali ). Itoshe tu kuwa makao makuu ya EAMWS yalikuwa Nairobi, (kusiko na Waislamu) na CEO wake alikuwa Mhasibu (CPA, si Imam). Kazi yake kuu ilikuwa ni kutunza biashara za Aga Khan (Riddoch Motors, Motor Mart, Landrover, Sugar Plantations).

EAMWS kilikataliwa na wazee wetu Waislam masheikh, kupitia baraza la Ulamaa na Viongozi wetu naarufu wakiwamo Rashidi Kawawa, Abedi Karume, Adam Naseeb, Hamis Masasi, Ali Bawazir, na wengineo wengi. Wakaanzisha BAKWATA, kwani ulishwahi kusikua BAKWAKE hadi leo? Kwa nini walimkataa Aga Khan? Alitaka kuivunja Tanganyika kwa udini kama alivyoibomoa India na Pakistan akaanzisha chama kinaitwa AMNUT (All Muslim National Union of Tanganyika) kuipinga TANU (Tanganyika African National Union).

Haya yote soma kitabu cha Mohamed Said, kipo wanauza pale Faya.

Nikutakie Mwaka Mpya lakini umechagua ajenda dhaifu.
Asante sana leo kwa mara ya kwanza nimesoma mtu anayeweza kumjibu Sheikh Mohamed Said kwa facts
 
Sheikh Mohamed Saidi: naona wajumbe wamekukaba koo huku mwenziyo nimetulia tuli! Miecsikutoka kwa khasr wala jazba ila ni kutoa nafasi kwa wajumbe tuache kuimonopolize mada.

Nina mawili matatu, nipe majibu hey presto kama una ubavu.

La kwanza umemtaja Mmisionari Ludwig Krapf, kafa, Mtemi Kimweri, he is dead too. aarabu bado wapo Tanga, na sisi tupo, hati za Kiarabu zipo, hati za Kirumi zipo. Kwa nini hatujaona usitawi wa hati za Kiarabu zitumike kufundisha IFM na SUA? I bet hata wewe hapo ulipo hujui Kiarabu. Kakangu, unawasakama Wamisionari hadi leo?

La pili, kumbuka Wajerumani na Waarabu wote majizi, walIkuja kuiba ninihii zetu na hadi leo bado wananyemelea makanikia yetu. Mtemi Kimweri alijua Kiarabu kutoka kwa mkoloni mkongwe Mwarabu, tena baada ya kusomba Wazigua alfu kwenda utumwani. Angekuwa si Manyema mwenziyo Karume tungelikuwa watumwa wa kukaanga karafuu hadI leo. Shame on you, mate!

Tatu, niwasaidie wasomaji wako, najua weye unajua. Hapa tuna vitabu viwili tafauti ingawa mtunzi huyo huyo. Cha kwanza, in Queen's English, ni sahihi, objective, kinauma na kupuliza lakini kinatanguliza ukweli. Mwandishi wetu alipata nafasi kwenda kusoma IFM kawa Mhasibu, in the process akatekwa na Mujaheedeen, waislamu wenye siasa kali. Ghafla bin vuu, Mody wetu, mwenzetu, ndugu yetu, mwanetu, katoa translation ya Kiswahili yote imejaa urongo mtupu! Anasifia Waarabu, anasifia Wamanyema, yaani utadhani walitapakaa mpaka Iramba na Tandahimba. Mie ningekuwa ndiye publisher wa The and Times of AWS, wallahi ningekuburuza mahakamani kwa kosa la kuchakachua copyright ya kitabu kizuri kabisa.

Kabla hujalialia sana niseme tu kuwa AboudJumbe, Shujaa wa Nji hii, naye alifanya kosa hilo alipotranslate kitabu chake murua. That makes 2 of you.

La mwisho, umemleta Mufti. Mie na Watanzania wengi sana tunaamini kuwa dua la Mufti (alianza yeye, nadhani mwishoni alilia kwa uchungu!) limetuokoa na janga la corona. Kama kuna mtu mmoja anayanyanyua Utanzania wetu na Mungu wetukatika umoja wetu, ni huyo Baba.

Naishia hapo, ngoja njemba wakugaragaze kwanza nitajarudi kukuokoa yakikufija hapa. Abdulwahi tawfiq.
LGF,
Kitabu cha Abdul Sykes kimechapwa matoleo manne tunakwenda toleo la tano.
Tafasiri ilichapwa na Phoenix Publishers, Nairobi 2002.

Tafsiri ya Kiswahili ya Phoenix (Nairobi) haipo hapo chini hiyo unayoiona rangi ya blue ni kutoka India:

1612020172113.png
 
Asante sana leo kwa mara ya kwanza nimesoma mtu anayeweza kumjibu Sheikh Mohamed Said kwa facts
Kinyungu,
Mimi huwa sina kawaida ya kupinga fikra za mwenzangu ila kama kuna makosa huandika lile lililo sawa.

Hati za Kiarabu zifundishwe katika shule na vyuo ilhali Tanganyika inatawaliwa na Muingereza.

Fikra nzuri sana hii.
Waingereza walifanya ''abrogation,'' ya hati hizi yaani walipiga marufuku.

Maana ya abrogation:
repeal or abolition of a law, right, or agreement.

Anasema mbona hazikufundishwa.
Hati zimepigwa marufuku kisha zisomeshwe.

Hizi ndizo unaita ''facts.''

Imetajwa SUA.

Mimi huyo hapo SUA mwaka wa 2004 nilialikwa kufanya mhadhara hicho kitabu mkononi ni Toleo la Kwanza la kitabu cha Sykes, London, (1998) :

1612021209969.png


Ungependa niendelee au hapa panakutosha?
 
Kinyungu,
Mimi huwa sina kawaida ya kupinga fikra za mwenzangu ila kama kuna makosa huandika lile lililo sawa.

Hati za Kiarabu zifundishwe katika shule na vyuo ilhali Tanganyika inatawaliwa na Muingereza.

Fikra nzuri sana hii.

Waingereza walifanya ''abrogation,'' ya hati hizi yaani walipiga marufuku.

Maana ya abrogation:
repeal or abolition of a law, right, or agreement.

Anasema mbona hazikufundishwa.

Imetajwa SUA.
Mimi huyo hapo SUA mwaka wa 2004 nilialikwa kufanya mhadhara hicho kitabu mkononi ni Toleo la Kwanza la kitabu cha Sykes, London, (1998) :

View attachment 1690042

Ungependa niendelee au hapa panakutosha?
Inatosha. Wacha niendelee kufuatilia mjadala.

Pia nilichogundua ni kwamba LGF alikuwa bado hajajua kama weww ni Mohamed Said mwandishi kwa kitabu alichokuwa akikifangia rejea. Nadhani sasa atakuwa ameshajua kuwa anajadiliana na mtunzi wa kitabu anachokizungumzia
 
Inatosha. Wacha niendelee kufuatilia mjadala.

Pia nilichogundua ni kwamba LGF alikuwa bado hajajua kama weww ni Mohamed Said mwandishi kwa kitabu alichokuwa akikifangia rejea. Nadhani sasa atakuwa ameshajua kuwa anajadiliana na mtunzi wa kitabu anachokizungumzia
Kinyungu,
Hapana haitoshi.

Hiki kitabu yeye anasema nimekichakachua katika tafasiri.

Anasema maneno yasiyo na ithibati.

Nichakachue kwa kutafuta kitu gani ambacho sikuwanacho katika toleo la kwanza?

Kinachomghadhibisha na kwa hakika wengi kiliwashangaza ni tofauti ya historia niliyoandika mimi ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Wengi pamoja na yeye wakiamini kuwa historia ya TANU inaanza 1954 na Julius Nyerere.

Mimi nimeanza 1924 Kleist Abdallah Sykes alipokutana na Dr. Kwegyr Aggrey.

Nimeyaandika haya kwa ushahidi wa kalamu ya Kleist mwenyewe katika mswada wa kitabu alioandika kabla hajafariki mwaka wa 1949.

Lakini kubwa na ndilo linalochoma nafsi ni kueleza mchango wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika chama alichasisi Kleist Sykes 1933 baada ya kuasisi African Association 1929 kufuatia ushauri wa Dr. Aggrey aliompa 1924 katika harakati za kudai uhuru.

Katika historia rasmi iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni haya yote hayapo.

Historia ya TANU inaanza na Julius Nyerere 1954 inamalizikia na Julius Nyerere.

Mimi nilikasirishwa sana na historia hii yao kwa sababu wazee wangu walikuwa wamefutwa.

1612032250103.png


Kinyungu,
Unasemaje.

Niendelee na huyu ndugu yetu?
 
Kinyungu,
Hapana haitoshi.

Hiki kitabu yeye anasema nimekichakachua katika tafasiri.
Anasema maneno yasiyo na ithibati.

Nichakachue kwa kutafuta kitu gani ambacho sikuwanacho katika toleo la kwanza?

Kinachomghadhibisha na kwa hakika wengi kiliwashangaza ni tofauti ya historia niliyoandika mimi ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Wengi pamoja na yeye wakiamini kuwa historia ya TANU inaanza 1954 na Julius Nyerere.
Mimi nimeanza 1924 Kleist Abdallah Sykes alipokutana na Dr. Kwegyr Aggrey.

Nimeyaandika haya kwa ushahidi wa kalamu ya Kleist mwenyewe katika mswada wa kitabu alioandika kabla hajafariki mwaka wa 1949.

Lakini kubwa na ndilo linalochoma nafsi ni kueleza mchango wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika chama alichasisi Kleist Sykes 1933 baada ya kuasisi African Association 1929 kufuatia ushauri wa Dr. Aggrey aliompa 1924 katika harakati za kudai uhuru.

Katika historia rasmi iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni haya yote hayapo.
Historia ya TANU inaanza na Julius Nyerere 1954 inamalizikia na Julius Nyerere.

Mimi nilikasirishwa sana na historia hii yao kwa sababu wazee wangu walikuwa wamefutwa.

View attachment 1690198

Kinyungu,
Unasemaje.

Niendelee na huyu ndugu yetu?
Endelea naye. Ni kwa faida yetu sote.

Hujanijibu swali shule ya Kiislam uliyoitaja iko wapi? Hakuna hata masalia ya majengo yake?
 
Back
Top Bottom