Naomba kujua mchango wa Wamisionari katika maendeleo ya elimu Afrika

Hiyo shule iko wapo kwa sasa? Au ilikuwa eneo gani?
Kinyungu,
Shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilijengwa kuanzia mwaka wa 1933 ilipoasisiwa taasisi yenyenyewe.

Waasisi wakiwa Mzee bin Sudi President, Kleist Sykes Secretary pamoja Ali Jumbe Kiro na wazee wengine wa Dar es Salaam.

Hawa wote walikuwa viongozi pia katika African Association.

Mwaka wa 1936 Aga Khan alitembelea Tanganyika na akakaribishwa kuitembelea shule hii.

Mwanafunzi aliyesoma risala ya kumkaribisha Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.

Baba yangu na watoto wengi wa miaka ile walisoma shule hii.

Aga Khan akachangia fedha shule ikamilishwe na likajengwa jengo ambalo lipo hadi leo Mtaa wa Makisi Mbwana na Lumumba Avenue.

Serikali ilipovunja EAMWS na kuunda BAKWATA mwaka wa 1968 shule hii ikaangukia mikononi kwa BAKWATA na hivi ndivyo ilivyokuwa kwa mali zote za Waislam.

Hii shule imebadilishwa jina inaitwa Lumumba.
Waislam wameomba warudishiwe jengo lao na shule lakini hadi leo hawajafanikiwa.

Naingia Maktaba kukutafutia picha.
 
Kinyungu,
Shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilijengwa kuanzia mwaka wa 1933 ilipoasisiwa taasisi yenyenyewe.

Waasisi wakiwa Mzee bin Sudi President, Kleist Sykes Secretary pamoja Ali Jumbe Kiro na wazee wengine wa Dar es Salaam.

Hawa wote walikuwa viongozi pia katika African Association.

Mwaka wa 1936 Aga Khan alitembelea Tanganyika na akakaribishwa kuitembelea shule hii.

Mwanafunzi aliyesoma risala ya kumkaribisha Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.

Baba yangu na watoto wengi wa miaka ile walisoma shule hii.

Aga Khan akachangia fedha shule ikamilishwe na likajengwa jengo ambalo lipo hadi leo Mtaa wa Makisi Mbwana na Lumumba Avenue.

Serikali ilipovunja EAMWS na kuunda BAKWATA mwaka wa 1968 shule hii ikaangukia mikononi kwa BAKWATA na hivi ndivyo ilivyokuwa kwa mali zote za Waislam.

Hii shule imebadilishwa jina inaitwa Lumumba.
Waislam wameomba warudishiwe jengo lao na shule lakini hadi leo hawajafanikiwa.

Naingia Maktaba kukutafutia picha.
Tutajie jina la hilo jengo.

Mnataka kurudishiwa shule yenu na Wakristo wakitaka kurudishiwa shule zao mtasoma wapi? Au vibarazani na mikekani?
 
Kinyungu,
Shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilijengwa kuanzia mwaka wa 1933 ilipoasisiwa taasisi yenyenyewe.

Waasisi wakiwa Mzee bin Sudi President, Kleist Sykes Secretary pamoja Ali Jumbe Kiro na wazee wengine wa Dar es Salaam.

Hawa wote walikuwa viongozi pia katika African Association.

Mwaka wa 1936 Aga Khan alitembelea Tanganyika na akakaribishwa kuitembelea shule hii.

Mwanafunzi aliyesoma risala ya kumkaribisha Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.

Baba yangu na watoto wengi wa miaka ile walisoma shule hii.

Aga Khan akachangia fedha shule ikamilishwe na likajengwa jengo ambalo lipo hadi leo Mtaa wa Makisi Mbwana na Lumumba Avenue.

Serikali ilipovunja EAMWS na kuunda BAKWATA mwaka wa 1968 shule hii ikaangukia mikononi kwa BAKWATA na hivi ndivyo ilivyokuwa kwa mali zote za Waislam.

Hii shule imebadilishwa jina inaitwa Lumumba.
Waislam wameomba warudishiwe jengo lao na shule lakini hadi leo hawajafanikiwa.

Naingia Maktaba kukutafutia picha.
Sorry sijaelewa ni wapi? Au unamanaisha hii hapa kwenye makutano ya Mkunguni na Lumumba ave? Mbele yake kidogo penye Shopping Mall kubwa ambayo nasikia majengo ni ya Bakwata?
 
Sorry sijaelewa ni wapi? Au unamanaisha hii hapa kwenye makutano ya Mkunguni na Lumumba ave? Mbele yake kidogo penye Shopping Mall kubwa ambayo nasikia majengo ni ya Bakwata?
Kinyungu,
Jengo lipo kona ya Mtaa wa Makisi Mbwana na Lumumba Avenue.

1612090773559.png


Katika miaka ya 1930s Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika walikuwa wanajenga shule ambayo sote tunaijua lakini hela zilikuwa tatizo jengo likawa linachukua muda mrefu kukamilika.

Sababu ya kujenga shule hii ni kuwa wazee wetu na wao walitaka wawe na mahali pa kuwasomesha watoto wao kuepuka vijana wao kubatizwa katika shule ambazo serikali ya kikoloni iliziweka mikononi kwa Kanisa.

Kleist akiwa kiongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika alitambua mapema sana kuwa tatizo kubwa lililokuwa likiwakabili Waislam ilikuwa ni kukosa elimu ambayo serikali ya kikoloni iliwaachia wamishionari waisimamie.

Si kama Waislam hawakuwa wanatambua faida ya elimu kwa watoto wao.

Wazazi wengi walichelea kuwapeleka watoto wao shule kwa sababu wamishionari walichukua fursa hiyo kuwabatiza.

Kuliko kwa watoto wao kutolewa katika Uislam na kuwa murtad, wazazi wengi waliamua kuisamehe elimu yenyewe kabisa.

Kleist aliona kuwa ufunguo wa tatizo hilo kwa Waislam ilikuwa ni kuanzisha shule zao wenyewe ambazo zitasomesha Qur’an pamoja na masomo mengine.

Wakati ule, na hata hivi sasa, Qur’an ilikuwa ikisomeshwa kwa mtindo wa asili ambapo mwanafunzi anakaa chini sakafuni mbele ya maalim akiwa na ubao wake na juzuu.

Kleist hakuona sababu kwa nini Qur’an nayo isisomeshwe kama elimu nyingine, wanafunzi wakiwa madarasani wakikaa katika madawati.

Alilitoa wazo hili kwa rafiki zake akashauri madrasa ipanuliwe ili masomo mengine yasomeshwe pamoja na Uislam.

Ushauri huu ulijadiliwa kati ya Kleist, Ali Kiro, Maalim Popa Saleh na Shariff Salim.

Wakitambua kazi kubwa iliyokuwa ikiwakabili, waliamua waanze hiyo shule kwa kidogo kidogo kwa awamu.

Nyumba itakayokuwa shule ya muda ilitafutwa na wanafunzi wakaanza kusoma.

Kati ya walimu wa mwanzo wa shule hiyo walikuwa Mzee Ali Comorian na Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo ambao walikuwa kati ya wasomi wa Kiislam waliokuwa wakiheshimika.

Wazazi wa Kiislam waliombwa wachange fedha ili jengo la kudumu lijengwe.

Al Jamiatul Islamiyya ikawa inapita nyumba hadi nyumba ikikusanya michango kutoka kwa Waislam.

Bahati nzuri mwaka wa 1936 Aga Khan alitembelea Tanganyika na akafahamishwa kuhusu ujenzi wa shule ile.

Katika hafla ile mtoto aliyesoma risala kwa Aga Khan alikuwa Abdul Sykes akiwa na umri wa miaka 12.

Marehemu Kanyama Chiume amenihadithia kuwa wakati huu alipofika Aga Khan Tanganyika yeye alikuwa anasoma Shule ya Kitchwele na alikuwa katika bendi ya shule iliyompokea yeye akipiga, ‘’triangle,’’ na alinieleza kuwa picha yake yeye akipiga, ‘’triangle,’’ ilitokea katika gazeti.

Aga Khan alitoa fedha na shule ikajengwa New Street si mbali sana na ilipokuwa ofisi ya African Association.

Kleist akawa katika kamati ya ujenzi akikagua kazi hadi ujenzi ulipokamilika.

Hii ni moja kati ya shule za mwanzo kujengwa na Waislam wa Tanganyika.

Jengo la Al Jamiatul Islamiyya lipo limesimama hadi leo kama ushahidi na kumbukumbu za juhudi za Waislam katika kujiletea maendeleo yao.

Serikali katika kuthamini mchango wa Kleist katika kupeleka mbele elimu kwa ajili ya watoto wa Kiislam ikamchagua kuwa katika Provincial Education Committee of Tanganyika Education.

Mwanae Abdulwahid na yeye vilevile akaja kuwa katika Aga Khan Education Committee.
 
Don't be daft. Chuo Kikuu cha Waislamu kimejengwa na Benjamin William Mkapa, Mkiristo, kawanyanganyaTANESCO shule ymao ya Engineering pale Msanvu Morogoto. Naona wewe ni mbux3 hujui mambo. Njoo ofisini pale Faya nitakupa kitabu cha Mohamed Said. Unajua Kiingrezq? Kinaitwa THE LIFE AND TIMES OF ABDUKWZHEED SYKES. Kinaeleza jinsi gani Agha Khan alitaka kutuuzia mbuzi guniani kama alivyovunja India na Pakistan ila Wazee wetu Waislamu wakakataa. Hujui historia, kama kimya.

Nipe Dunihaji.

Mkuu unayejibizana nae ndio Mohamed Said,mwanahistohisia wa Tanganyika.
 
Syll...
Takriban nusu ya umri wangu wa miaka 68 naingia 69 In Shaa Allah Februari nimekuwa nikiandika vitabu, ''academic papers,'' na makala nyingi zisizo na hesabu kuhusu Uislam Tanzania na nimehudhuria mikutano mingi ndani na nje ya Tanzania pamoja na kuzungumza katika vyuo mbalimbali Afrika, Ulaya na Marekani.

Naweza kujidai kuwa suala hili nalijua kwa kiasi changu.

Katika ujuzi huu kuna namna ya ''pattern,'' nimejenga na kwa sasa naweza kusema imekuwa sawasawa na sheria au kanuni ya aina fulani mfano wa ''Archimedes Principle.''

Mfano ni kama huu wako.

Unapoona mtu anaandika kwa staili yako kuwa liko tatizo na linajadiliwa na mtu anaandika kwa kusema kama unavyosema wewe kuwa huwajuia Waislam, Waarabu, Wakristo, Waafrika, Wamishionari nk; huyu tafuta imani yake utakuta si Muislam.

Sasa utafiti wangu haukuishia hapa ili niweze kuitengeneza hii sheria yangu au kanuni iweze kuwa na mashiko ni lazima nijue kiwango cha elimu yake.

Nitakijuaje?

Huwa namtia hamu ya kufanya majadala na mimi na kila anapoandika najaribu kupima kiwango cha elimu yake na si kazi kubwa mara moja naweza kukisia kama ni elimu ya chini, kati au juu.

Hapa nitaeleza jambo.

Uzoefu wangu unaonesha kuwa baadhi katika mjadala huu wa dhulma huwa wanapandwa na hamaki kwa kukosa hoja na huja na lugha kali na pengine matusi na vitisho au kunishambulia binafsi badala ya kujibu hoja.

Lakini haya yote yamesaidia sana katika kuelewa uzito wa suala hili.

Suala linalofuatia ni kwa nini ghafla baada ya kujua uwezo wake kuwa kiwango chake cha elimu ni kizuri anaandika kama mtu asiyejua kitu?

Sasa ili kupata ''conclusion,'' au uhakika wa kile ninachotafuta ni lazima hii ''pattern'' yangu iwe na ''sampling,'' kubwa yaani nimejadiliana na watu wengi katika jamii katika tatizo hili.

Nilichogundua ni kuwa imani ina nafasi kubwa sana katika fikra kiasi anaona kukubali ukweli anaowekewa wazi ni kushindwa kwa imani yake.

Hiki ni kitu muhali mkubwa sana kwake hawezi kukiruhusu.

Sasa ukichukua ukweli huu ukauweka katika serikali ambayo watendaji wakuu wanaoshika nafasi za maamuzi ni wa imani moja kwa mathalan uwiano wa 20:80 utaelewa bila tabu yote kwa nini hali iko hivyo ilivyo kuwa Waislam wanajaribu kueleza matatizo yao lakini hakuna aliye tayari katika serikali kusikiliza au hata kuamini kuwa liko tatizo.

Hapa ndipo linapoingia lile suala linalotisha.

Ni akina nani waliotoa uamuzi wa kuvunjwa kwa EAMWS wakati wanajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na kutekeleza mipango yao ya elimu?

Nini lilikuwa kusudio lao?

Hofu kuwa Waislam wataelimika na hivyo kushika madaraka katika serikali ya Tanganyika huru?

Ndiyo hapo ghafla unasoma mtu kama Edwayne anaandika kuwa Uislam na Ukristo zote ni dini za shetani na utumwa.

Tafuta imani yake utapata jibu.

Lakini ukiangalia mjadala si huo bali ni dhulma ambayo Waislam wanaeleza serikali kuwa wamekuwa wanafanyiwa toka uhuru upatikane mwaka wa 1961 na vielelezo vyote kama ushahidi wameweka.

Nachelea kumchosha msomaji lakini mifano ipo mingi.

Tatizo ni kuwa viongozi wetu hawako tayari kuliweka tatizo hili katika agenda lijadiiwe kwa wazi kwa hofu ambayo si tabu kuitambua.
Mkuu,
Asante sana kwa elimu endelevu kwangu na kwa wale wote wenye "imani" hiyo.
Hakika, bandiko langu na maswali yamejaa upungufu wa " imani" na elimu...walakin. Mtu yeyote asiyejua kitu anapaswa kujua kama itampatia umuhimu katika maisha yake, na hii ni maoni yangu. Hivyo basi, nakutangulizia asante, kwani, nina faraja. Naelimika.

Mkuu, kwa vile suala hili la "mchango wa wamishionari katika maendeleo ya elimu Afrika"ni pana na nina uhakika bado wapo watu kama wewe na wengine ambao wanajua na kuona umuhimu wa "elimu" huu wa "mchango"
Basi mie ninatakujua hivi vitu...au tukubaliane
"Wamishionary" walikuwa na "mission" na moja ni kuleta na kutangaza dini wanazoamini.
Na katika mlolongo huo walileta "elimu" ya kutuwezesha kuelewa hayo? au?
Mkuu, kutoka vyombo husika na masuala ya definition...Elimu ni mchakato wa kujifunza vitu?Naomba nielemishwe.


Mkuu, kutoka mission hizo tukubaliane tulielimika, tulijuwa then na bado tunaendelea kuelimika now kuwa walikuwa na mission tofauti ya maendeleo ya elimu then na hata sasa kwa vile makusudi yao ya kale na labda hata ya sasa yamejaa uhaini.

Sasa nirudi hapa na kuhusu marginalization of islamic teachings and or instututions.


Wapo wengi wenye ujuvi wa haya na wewe mmoja wapo. Tukiweka historia mbele mimi kama muafrika -I really have nothing to do with the ongoing scramble for dominance by either party for control of mind and soul of African peoples." And these parties divinely so, holy and sacred are being handled by the grand and sanctity of the you know who!
That aside, mimi naona mpasuko wa dini ya kikristo uliukiritimba dini ya kiislamu, ilikuwa siasa ni wa kisiasa-neno lenye asili ya uislamu- na bado ni kisiasa, walakin wakristo na waislamu wanaishi bega kwa bega na kuonana ana kwa ana, nafikiri kama wahumini aidha wa kikristo, uislaam n.k kama watu, wanaweza kuungana na kukemea maovu ya wachache katika dhuluma na kujaribu kutenganisha dini katika mandhari za kisiasa Duniani, Ni ndoto zangu hizi.
 
Back
Top Bottom