Naomba kuju tiba sahihi au sababu ya huu ugonjwa

Lelloh

Member
May 6, 2015
53
9
Kitendo cha MTU kutoka damu puanii ni sababu ipi inasababisha au madhara yake ni nini

Maana niko na mtu anatokwa na damuu nyingii alafu analia anajua anaweza kufaaa,
Ila watu wengine wameniambia kuwa sio Ugonjwa sasa naomba kujua zaidiiiiii

Asantee
 
Kitendo cha MTU kutoka damu puanii ni sababu ipiiii inasababisha au madhara yake ni nini

Maana niko na mtu anatokwa na damuu nyingii alafu analia anajua anaweza kufaaa,
Ila watu wengine wameniambia kuwa sio Ugonjwa sasa naomba kujua zaidiiiiii

Asantee
images-1.jpg

DAMU KUTOKA PUANI

Kutokwa na damu puani ni hali inayotokea watu wengi hasa wakati wa utoto na uzee. Damu hii hutoa kwenye kuta za ndani za pua. Kuta hizi zimejaa mishipa ya damu iliyo membamba na kufunikwa na kiasi kidogo cha seli laini. Kwa hali hii huwa ni rahisi kupasuka pale inapoguswa au kukutana na hali ya ukavu mkali. Inapopasuka damu humwagika na kutoka puani hali inayojulikana kwa kitaalamu kama epistaxis.
Mara nyingi hali hii huisha yenyewe bila kuhitaji matibabu, ingawa mara chache inaweza kuwa ya kuhatarisha maisha kiasi cha kuhitaji matibabu ya haraka.
Damu inaweza kutoka sehemu ya mbele au nyuma ya ndani ya pua. Mara nyingi damu hutokana sehemu ya mbele ya ndani ya kuta za pua (anterior nose bleeding).
Sababu

Kutokwa damu puani ni dalili inayoweza kusababishwa na magonjwa au hali mbalimbali zifuatazo :

  • Kuingiza vidole puani
  • Kupiga chafya au kupenga mafua kwa nguvu sana
  • Shinikizo la damu la kupanda
  • Saratani ya damu
  • Matatizo ya damu kushindwa kuganda
  • Kuumia puani kwa kujigonga, au kuvunjika mfupa wa pua
  • Kutumia dawa za kuzuia damu kuganda kama aspirin, clopidogrel na warfarin.
  • Saratani ya pua
  • Magonjwa ya ini au figo
  • Maambukizi ya bakteria au virusi kwenye pua
  • Matumizi ya madawa ya kuvuta puani
  • Kukauka kwa kuta za ndani za pua
Namna Inavyotokea

Kutokwa na damu puani hutokea hasa kwa watoto wa umri wa miaka 2-10 na watu wazima wenye umri wa miaka 50-80.
Hali hii hutokea ghafla damu ikianza kutoka puani polepole. Inaweza ikatoka kwenye tundu moja la pua au yote mawili. Wakati mwingine damu inaweza kutoka baada ya kutembea kwenye jua kali au kufanya mazoezi.
Damu inaweza kutoka wakati wa usiku ukiwa umelala na ukaimeza, kisha ikaonekana kwa kutapika damu au mabonge ya damu, au kupata choo chenye damu damu au cheusi sana.
Nini cha Kufanya

Mara nyingi kutokwa damu puani huacha baada ya muda mfupi bila kuhitaji matibabu. Unapotokwa damu puani fanya yafuatayo;

  • Tulia, usihangaike hangaike.
  • Inua kichwa chako kiwe juu ya usawa wa moyo
  • Inamisha kichwa chako kuelekea mbele kidogo kuzuia kumeza damu
  • Minya sehemu laini ya pua kwa vidole vyako kwa dakika 10 mpaka 15.
Unaweza ukatumia dawa za kupuliza puani ili kusimamisha damu isitoke.
Ikiwa damu inaendelea kutoka licha ya kuibana pua kwa dakika 15 au kupulizia dawa ya kuzuia damu kutoka, unatapika damu au kama hali hii inajirudia mara kwa mara basi onana na daktari haraka iwezekanavyo.
Matibabu ya hospitali hujumuisha;

  • Kuziba mshipa wa damu uliopasuka kwa umeme
  • Kuweka pamba zenye kemikali za kuzuia damu kutoka ndani ya pua. Hizi hukandamiza mishipa ya damu na kuzuia damu kuvuja. Hukaa kwa siku 1 mpaka 3 kabla ya kuondolewa. chanzo.http://www.afyamd.co.tz/dalili/damu-kutoka-puani/


Mwambie akitaka dawa ninayo anaweza kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
 
Back
Top Bottom