Naomba kuijua kura ya turufu inayoamua rais Amerika

Beira Boy

JF-Expert Member
Aug 7, 2016
17,895
25,944
Aman iwe nanyi wakuu

Naomba kuijua kura ya turufu ambayo ndo nasikia huwa ina amua nani awe rais hata kama wananchi hawaja mchagua

Je kura hiyo huwa inapigwa na nan na akina nan

Nawasilisha

BOY FROM LONDON

Sent using Jamii Forums mobile app



=======================================

Kura ya turufu (Veto) ni haki ya kukataza Azimio lisipite wala kutekelezwa hata kama limekubaliwa na wengi. Katika nchi nyingi Rais au Kiongozi wa Taifa kwa manufaa ya Taifa ana haki ya kukataza maazimio au sheria zilizokubaliwa na Bunge akiona kasoro au hasara ndani yake

Mfano; nchini Marekani Rais ana haki ya kukataza sheria iliyokubaliwa na Bunge katika kipindi cha siku 10 baada ya Azimio la Bunge. Akipiga Veto Aheria inarudi Bungeni na hapo Bunge linaweza kufuta Veto kwa theluthi mbili za kura au kubadilisha sheria

Mataifa matano yanaweza kutumia kura ya Turufu (Veto) katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa: China, Marekani, Ufaransa, Uingereza na Urusi. Kila moja kati ya hayo linaweza kuzuia maazimio ya Baraza la Usalama
 
Country: United States of America (USA)

Houses of parliament/Congress( aina za mabunge): Two chambers

Ambayo ni:

Upper house/Bunge la juu: Senate (maseneta)
Lower house/Bunge la chini: Representatives (Bunge la wawakilishi)

Katika USA kuna:

States: 50
Non-states:
-washington D.C (hii sio state, ni wilaya)
-Guam Island
-Puerto Rico
-Mariana islands

Katika states 50 za USA, jumla ya counties (majimbo) ya states hizi ni 435 (voting + nonvoting members ) Kwahiyo hapa unapata namba ya wambunge la chini (lower chamber house/ Congress representatives) kua 435 Sawa na majimbo ya USA

Kila state inatoa maseneta 2 ambapo kwa states 50 unapata jumla ya maseneta wa Bunge la juu/ house senate kua 2x50 =100.

Electoral college/votes ni Sawa na electrors: Congress +senate
= 435+100
=535 Electoral college/votes

Lakini jumla ya Electoral votes zilizopo ni 538

Je 3 zinatoka wapi?

Washington DC sio states though ndo capital ya USA

Kwahiyo Washington DC Wana mbunge/Congress representative 1 ambaye hapigi kura bungeni pia Washington DC ina maseneta 2 ambapo nao hawana nguvu kwenye bunge la Senate

Kwahiyo Washington DC ina electoral votes 3: 2 shadow senates + 1 Shadow Congress representative

Total USA Electoral votes inafikia 535+3=538 votes

States huongozwa na magavana/Sawa na wakuu wa mikoa
Washington DC sio state ni wilaya thus why DC= District of Columbia. States za karibu zilichanga ardhi kupata independent region likaitwa Washington DC.

Puerto Rico sio state lakini huongozwa na gavana na iko chini ya USA though karibuni walipiga Kura ili wawe na seneta na Congress bungeni. Kwahiyo Puerto Rico haina seneta wa Congress bungeni. USA na Puerto Rico ni sawa na Tanzania na Zanzibar. Gavana wa Puerto Rico Yuko chini ya Trump na USA.

Pia islands hazina maseneta wala Congress bungeni



MFUMO WA UCHAGUZI

Uchaguzi wao huhusisha President , vice President, senators na house representatives

Achana na Senate na Congress:

President na vice President huchaguliwa Kwa Electoral votes

Electoral votes (538) ndo huchagua Rais na Vice wake

Ili ushinde Urais inabidi ufikishe electoral votes 270 and above unakua rais. Mkilingana 270 and 270 kuna other case utaisoma mwenyewe.

Mfano:
California ina majimbo 58 lakini ina Electoral votes 55. Kuna system ambayo inafanya kwanini hao 3 hawahesabiwi kwenye EV.

California inawatu karibia 40milion

Rais atakayeshinda popular votes hizo California anabeba Electoral votes zote 55 hata kama kazidi Kwa Kura ya mtu mmoja
Inakua hivo hivo hadi states zote

Na ndomana unaeza kuta Aliyeshinda urais Kwa electoral votes kazidiwa Kwa popular votes, inatokana na states inawatu wengi majimbo machache au watu wachache majimbo mengi

Mfano: wilaya ya Washington DC ina Electoral votes 3 lakini ina population ya watu hata zaidi ya mastates baadhi.
Kwahiyo wewe ukitegemea upige kampeni usiku kucha Washington DC ili upate hizo Electoral votes 3 utafika lini 270 hata kama utashinda Kwa watu wote hao??


Kwanini waliweka Electoral votes na sio population ndo iamue Rais?
Ilitokega kwamba ma states yenye watu wengi na yenye nguvu kama California, Texas, Florida, etc yalikua yanaamua nani awe president Kwa popular votes iwe Presidential candidate kapiga kampeni au laa ni uchama Tu. Mfano Democrats kuna ma states ambayo hata wasipopiga kampeni wanashinda. Ikatokea Civil war katika USA sababu ni hiyohiyo, California wanamchagua president Kwa nguvu ya popular hatafu ni jina moja wakati states nyingine haimtaki, Sasa wazee wa nchi wakale wakakaa kwamba haya ma states yenye nguvu yanawaburuza ma states yasio na nguvu kwahiyo tuweke Electoral votes ili Rais apige kampeni nchi nzima asikie shida sio ku target sehemu sehemu Tu ili ashinde.

.....


Forget the typos, got little light?
Sijui ulisoma shule gani,hata ya Kata ina nafuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui ulisoma shule gani,hata ya Kata ina nafuu.

Sent using Jamii Forums mobile app


Veto power - nations votes at UN assembly ili kupitisha maazimio

Electoral votes - USA election system ambayo ndo huamua nani awe Rais hatakama wananchi hawajamchagua wengi

Swali lina sema

"Naomba kuijua kura ya turufu ambayo ndo nasikia huwa ina amua nani awe rais hata kama wananchi hawaja mchagua"

Bila shaka alitaka kuujua electoral vote na sio veto power.

Hakuna nchi ambayo inatumia Veto kuamua nani awe Rais bali USA ndo hutumia Electoral votes ambayo huamua nani awe Rais na sio Veto

Kwahiyo nafikiri na muuliza swali naye nikama kachanganya either anataka kujua Veto au Electoral votes

Aseme mwenyewe alimaanisha Veto au Electoral votes?
Ili nifute jibu langu ambalo ni USA election system, Electoral votes.
 
Swali lina sema

"Naomba kuijua kura ya turufu ambayo ndo nasikia huwa ina amua nani awe rais hata kama wananchi hawaja mchagua"

Bila shaka alitaka kuujua electoral vote na sio veto power.

Hakuna nchi ambayo inatumia Veto kuamua nani awe Rais bali USA ndo hutumia Electoral votes ambayo huamua nani awe Rais na sio Veto

Kwahiyo nafikiri na muuliza swali naye nikama kachanganya either anataka kujua Veto au Electoral votes

Aseme mwenyewe alimaanisha Veto au Electoral votes?
Ili nifute jibu langu ambalo ni USA election system, Electoral votes.
Hujui kuandika kitu kikaeleweka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom