Naomba kufahamishwa taratibu za kukomboa mafao NSSF

sungura23

Member
Apr 1, 2013
52
73
Habari wakuu? Natumaini wote ni wazima.

Wakuu naomba kwa mwenye kufahamu taratibu za kukomboa (to claim) mafao ya NSSF iwapo mtu ulikuwa unafanya kazi na mwajiri alikuwa akipeleka michango.

Mwaka 2017 hadi 2019 nilipata fursa ya kufanya kazi kwenye sekta ya masuala ya hospitality. Mwajiri wangu alikuwa akipeleka michango yangu na baada ya mkataba wangu kumalizika nikarejea dar. Baada ya kurejea dar sikuwahi kuwa na ajira rasmi ambayo inapeleka michango yangu NSSF. Hvyo tangu 2019 hadi mwaka huu uanachama wangu una akiba ileile ya miaka miwili ya mwajiri wangu kwenye sekta ya hospitality niliyofanya 2017 mpaka 2019.

Jana nimeingia kwenye portal ya NSSF kwa namba yangu ya uanachama nimeona installment zangu zote pamoja na akiba ambayo bado sijaikomboa (unclaimed balance). Vyote viko sahihi na mwajiri wangu aliwasilisha michango yangu yote ya mkataba wangu wa miaka miwili.

Maswali yangu:
1. Je ninaweza kuiokomboa hii akiba?
2. Je taratibu zake ni zipi?
3. Kuna madai kuwa huko NSSF kuna usumbufu mno, je ni kweli? Yaani hata kama una akiba yako lakini ni shughuli mpaka wakupatie chako. Haya madai ya kuwa kuna usumbufu nimepewa na watu wasiopungua watatu, ikiwa mmojawapo nilikuwa nae huko kwenye hyo kazi tuliyofanya miaka miwili.
4. Na iwapo wakikulipa kuna makato yoyote?
5. Na wanalipa kwa which mode of payment? Wanakuwekea kwenye akaunti? Au bank cheque?

Naomba msaada wenu wakuu

Ahsanteni
 
Nijuavyo mimi Nssf wanatoa mafao yote kwa wazee waliostaafu au kwa makundi ya watu wasio na profession yeyote mfano walinzi, cleaners nk.
2. Kama wewe una profession yako utapata kwa mkupuo tu fedha iitwayo fao la kukosa ajira ambalo ni 30% ya mshahara wako wa mwisho(net) mara miezi sita.
3. Baada ya hapo kama bado huna kazi then unaruhusiwa kureclaim fedha iliyopo NSSF.
Kumbuka, ni mchakato unaohitaji uvumilie kwani una chukua muda sana na ufuatiliaji. Wengi hutumia mlango wa jikoni ila sikushauri.
 
Habari wakuu? Natumaini wote ni wazima.

Wakuu naomba kwa mwenye kufahamu taratibu za kukomboa (to claim) mafao ya NSSF iwapo mtu ulikuwa unafanya kazi na mwajiri alikuwa akipeleka michango.

Mwaka 2017 hadi 2019 nilipata fursa ya kufanya kazi kwenye sekta ya masuala ya hospitality. Mwajiri wangu alikuwa akipeleka michango yangu na baada ya mkataba wangu kumalizika nikarejea dar. Baada ya kurejea dar sikuwahi kuwa na ajira rasmi ambayo inapeleka michango yangu NSSF. Hvyo tangu 2019 hadi mwaka huu uanachama wangu una akiba ileile ya miaka miwili ya mwajiri wangu kwenye sekta ya hospitality niliyofanya 2017 mpaka 2019.

Jana nimeingia kwenye portal ya NSSF kwa namba yangu ya uanachama nimeona installment zangu zote pamoja na akiba ambayo bado sijaikomboa (unclaimed balance). Vyote viko sahihi na mwajiri wangu aliwasilisha michango yangu yote ya mkataba wangu wa miaka miwili.

Maswali yangu:
1. Je ninaweza kuiokomboa hii akiba?
2. Je taratibu zake ni zipi?
3. Kuna madai kuwa huko NSSF kuna usumbufu mno, je ni kweli? Yaani hata kama una akiba yako lakini ni shughuli mpaka wakupatie chako. Haya madai ya kuwa kuna usumbufu nimepewa na watu wasiopungua watatu, ikiwa mmojawapo nilikuwa nae huko kwenye hyo kazi tuliyofanya miaka miwili.
4. Na iwapo wakikulipa kuna makato yoyote?
5. Na wanalipa kwa which mode of payment? Wanakuwekea kwenye akaunti? Au bank cheque?

Naomba msaada wenu wakuu

Ahsanteni
Kama ulikuwa unafanya hotel wewe unachukua pesa yako yote...labda kama ulikuwa mhasibu au any skilled work ila kama hizi zingine za profession za veta sijui cleaner, cookery, bartender nk hela yako unachukua yote ni haki yako kisheria.
Wai uchukue pesa yako ila usilewee, usigongee fanyia ya maana fungua hata kiduka cha mpesa.
 
Kama ulikuwa unafanya hotel wewe unachukua pesa yako yote...labda kama ulikuwa mhasibu au any skilled work ila kama hizi zingine za profession za veta sijui cleaner, cookery, bartender nk hela yako unachukua yote ni haki yako kisheria.
Wai uchukue pesa yako ila usilewee, usigongee fanyia ya maana fungua hata kiduka cha mpesa.
Nashukuru sana kwa taarifa mkuu... na ushauri pia hahaha nmeupenda ushauri wako mkuu ubarikiwe sana.
 
Nijuavyo mimi Nssf wanatoa mafao yote kwa wazee waliostaafu au kwa makundi ya watu wasio na profession yeyote mfano walinzi, cleaners nk.
2. Kama wewe una profession yako utapata kwa mkupuo tu fedha iitwayo fao la kukosa ajira ambalo ni 30% ya mshahara wako wa mwisho(net) mara miezi sita.
3. Baada ya hapo kama bado huna kazi then unaruhusiwa kureclaim fedha iliyopo NSSF.
Kumbuka, ni mchakato unaohitaji uvumilie kwani una chukua muda sana na ufuatiliaji. Wengi hutumia mlango wa jikoni ila sikushauri.
Aisee nimekupata mkuu.

Nimepewa mwongozo na kweli nimeambiwa hili jambo linahitaji uvumilivu.

Ubarikiwe
 
Nijuavyo mimi Nssf wanatoa mafao yote kwa wazee waliostaafu au kwa makundi ya watu wasio na profession yeyote mfano walinzi, cleaners nk.
2. Kama wewe una profession yako utapata kwa mkupuo tu fedha iitwayo fao la kukosa ajira ambalo ni 30% ya mshahara wako wa mwisho(net) mara miezi sita.
3. Baada ya hapo kama bado huna kazi then unaruhusiwa kureclaim fedha iliyopo NSSF.
Kumbuka, ni mchakato unaohitaji uvumilie kwani una chukua muda sana na ufuatiliaji. Wengi hutumia mlango wa jikoni ila sikushauri.
mlango wa nyuma huo nautaka mm. nimekwama
 
Back
Top Bottom