Naomba sana kuelemishwa juu athari ya kupiga ng'ombe chapa. Naona ni agizo hili limetolewa na Mamlaka ya juu kuwa kila mfugaji apige ng'ombe wake wote chapa. Binafsi kwa uelewa wangu ng'ombe anapopigwa chapa ni wazi unaharibu ngozi yake na baadaye ngozi ya ng'ombe husika inapouzwa inauzwa kwa bei ndogo kwa sababu ya alama iliyopo kwenye ngozi na hasa ngozi zinazouzwa nchi za nje. Sasa basi naomba kuelemishwa ni kwa nini tunapiga chapa ng'ombe huku tukifahamu kuwa upigaji chapa unapunguza thamani ya ngozi?.