Naogopa kulala ndani peke yangu, nahisi kuna mtu simuoni

juvenile davis

JF-Expert Member
Apr 13, 2015
4,752
4,449
Waungwana habari,hivi sasa naandika uzi huu ni saa nane na dakika 16usiku.nina usingizi ila naogopa kulala kwani nahisi kuna mtu chumbani kwangu.kibaya zaidi nakaa nyumba nzima peke yangu,nimeenda sebuleni ila napo naogopa sana,nahisi kuna mtu ananichungulia huku anacheka.hii inasababishwa na nini.maana kila nikitaka kusinzia nakwama.nashtuka nahisi kuna mtu.kwa mnajua niambieni nifanyeje ili niwe na amani,na ili nilale
 
Tatizo dogo sana. Hapo ulipo piga magoti uliite Jina la Bwana Yesu mlinzi wa walinzi. Usijali hata kama hujawahi kwenda kanisani. Wewe mweleze Mungu na sali unavyojua wewe. Sali kemea kwa jina la Yesu. Muite Mungu Akusafishie nyumba hiyo Atume malaika wake wakulinde. Halafu kwa imani kabisa Ingia kitandani ulale. Hutasikia lolote na utalala usingizi mnono ajabu.

Kwa nini nakushauri hivi? Kuna siku moja usiku kama saa nne kule Usukumani nilikuwa peke yangu. Ili kufika nyumbani kulikuwa na kamto fulani hivi lazima ukavuke halafu pembeni kuna miti mingi ya michongoma na mitunduru. Basi kufika pale nikaona mbele yangu watu kama wanne hivi wana vijinga vya moto wamesimama huko niendako. Nikataka kutimua mbio lakini nilipogeuka nikawaona tena hata huko wapo. Basi nikajua kuwa nimezingirwa na hawa siyo watu wa kawaida mpaka nikadhani pengine haya ndiyo mambo ya akina Mch. Gwajima ya kuchukuliwa msukule. Wakati ule nilikuwa Mwadventista Msabato na katika makambi tulikuwa tunafanya mashindano ya kukariri mafungu ya Biblia. Basi hapo hapo nikakumbuka Zaburi 23 na nikaanza kusali kwa sauti kubwa mpaka nasikia mwangwi: Mungu Ndiye mchungaji wangu na sitapungukiwa na kitu. Nijapopita katika bonde la mauti sitaogopa mabaya...Nikatamka kwa sauti kubwa "Yesu nakuhitaji. Shuka Mfalme wa wafalme unipiganie. Waondoe hawa kama wana nia mbaya nami. Ondokeni kwa jina la Yesu..." Yaani mpaka jasho likanitiririka. Kuja kuinua macho sikuona kitu. Huyooo nikatembea mpaka home. Ajabu kesho yake nilikuwa nimechoka balaa. Na baadaye sana nilikuja kuwafahamu wabaya wale na ambacho walikuwa wamepanga kunifanyia. Na kiongozi wao alikuwa ni shangazi yangu kabisa tumbo moja toka nitoke na baba.

Tangu siku hiyo ndiyo nikajua kuwa jina hili Yesu lina nguvu za ajabu. Na cha kushangaza zaidi kuchelewa kote huko mpaka saa nne usiku nakatisha mtoni ni kwa sababu nilikuwa nafukuzia demu. Demu mwenyewe wala hakutokea. Imagine nilikuwa natoka katika harakati za kutenda dhambi lakini Mungu Alikuwa tayari kuniokoa. Ni wema na upendo gani upitao huu?

Sorry for a long story. Mkuu sali halafu uchape usingizi. Mungu Akulinde na kukubariki. Amen!
 
Tatizo dogo sana. Hapo ulipo piga magoti uliite Jina la Bwana Yesu mlinzi wa walinzi. Usijali hata kama hujawahi kwenda kanisani. Wewe mweleze Mungu na sali unavyojua wewe. Sali kemea kwa jina la Yesu. Muite Mungu Akusafishie nyumba hiyo Atume malaika wake wakulinde. Halafu kwa imani kabisa India kitandani ulale. Hutasikia lolote na utalala usingizi mnono ajabu.

Kwa nini nakushauri hivi? Kuna siku moja usiku kama saa nne kule Usukumani nilikuwa peke yangu. Ili kufika nyumbani kulikuwa na kamto fulani hivi lazima uvuke. Basi kufika pale nikaona mbele yangu watu kama wanne hivi wana vijinga vya moto wamesimama huko niendako. Nikataka kutimua mbio lakini nilipogeuka nikawaona tena hata huko wapo. Basi nikajua kuwa hawa siyo watu wa kawaida na nikadhani pengine haya ndiyo mambo ya kuchukuliwa msukule. Wakati ule nilikuwa Mwadventista Msabato na katika makambi tulikuwa tunafanya mashindano ya kukariri mafungu ya Biblia. Basi hapo hapo nikakumbuka Zaburi 23 na nikaanza kusali kwa sauti kubwa mpaka nasikia mwangwi: Mungu Ndiye mchungaji wangu na sitapungukiwa na kitu. Nijapopita katika bonde la mauti sitaogopa mabaya...Nikatamka kwa sauti kubwa "Yesu nakuhitaji. Shuka Mfalme wa wafalme unipiganie. Waondoe hawa kama wana nia mbaya nami. Ondokeni kwa jina la Yesu..." Yaani mpaka jasho likanitiririka. Kuja kuinua macho sikuona kitu. Huyooo nikatembea mpaka home. Ajabu kesho yake nilikuwa nimechoka balaa. Na baadaye sana nilikuja kuwafahamu wabaya wale na ambacho walikuwa wamepanga kunifanyia. Na kiongozi wao alikuwa ni shangazi yangu kabisa tumbo moja toka nitoke na baba.

Tangu siku hiyo ndiyo nikajua kuwa jina hili Yesu lina nguvu za ajabu. Na cha kushangaza zaidi kuchelewa kote huko mpaka saa nne usiku nakatisha mtoni usiku ni kwa sababu nilikuwa nafukuzia demu. Demu mwenyewe wala hakutokea. Imagine nilikuwa natoka katika harakati za kutenda dhambi lakini Mungu Alikuwa tayari kuniokoa. Ni wema na upendo gani upitao huu?

Sorry for a long story. Mkuu sali halafu uchape usingizi mkuu. Mungu Akulinde na kukubariki. Amen!

Uliwajuaje wabaya wako, walijitokeza kuomba msamaha, au?
 
Waungwana habari,hivi sasa naandika uzi huu ni saa nane na dakika 16usiku.nina usingizi ila naogopa kulala kwani nahisi kuna mtu chumbani kwangu.kibaya zaidi nakaa nyumba nzima peke yangu,nimeenda sebuleni ila napo naogopa sana,nahisi kuna mtu ananichungulia huku anacheka.hii inasababishwa na nini.maana kila nikitaka kusinzia nakwama.nashtuka nahisi kuna mtu.kwa mnajua niambieni nifanyeje ili niwe na amani,na ili nilale
Pole sana nlishawah kuandika kuhusu hilo soma huu uzi

ukitaka kumjua mchawi mahali unapoishi au unapofanyia kazi, mara nyingi anakuwa na tabia isiyofanana na wengine. Mfano, asubuhi ukiamka, ukiwa unakwenda chooni, ukikutana na jirani yako ukamsalimia lakini akaitikia kwa sauti ya chini sana tena huku akiangalia ukutani, tambua huyo ni mchawi.<br />Au, unakwenda kazini, kufika unakutana na mfanyakazi mwenzako, unamsalimia kwa kumpa mkono yeye anaitikia salamu lakini hakupi mkono tambua huyo ni mchawi. hakuna mchawi asiyekuwa na dalili kwenye jamii, sema tu macho ya watu yamefungwa kuona yaliyo sirini kutokana na wingi wa dhambi zetu sisi wanadamu.<br />Mitaani tunapotembea, kuna viumbe vingi sana tunapishana navyo, vinatuona lakini sisi hatuvioni. Mbaya zaidi, viumbe hivi wakati mwingine vinaingia kulala kwenye majumba yetu baada ya kuchoka kwa shughuli zao za mchana kutwa.<br />Sema usiri wake ni kwamba, baadhi ya viumbe havina ubaya na binadamu, hata vikiingia ndani kwako vinataka hifadhi ya malazi tu asubuhi zinaondoka.<br />Umewahi kuwa peke yako usiku chumbani halafu ukajisikia hali ya kuogopa sana kiasi kwamba hutaki hata kulala na giza, unawasha taa mpaka kuna kucha? Basi tambua kwamba, kuna viumbe visivyoonekana vimeingia kulala chumbani kwako. Unaposhtuka na kuangalia dirishani vyenyewe vinakuona na kukucheka.<br />Kifupi kila unachofanya vinaona ila havina dhamira ya kukuzuru.<br />Sasa utajuaje kuwa ulilala na viumbe? Mara nyingi hivi viumbe humsababishia hali ya kwenda chooni mtu kila wakati. Unaweza kutoka chooni usiku mara nne, wakati si kawaida yako, jua ulilala na viumbe.<br />Kikubwa, kama unahisi hatari hiyo, ukilala usifunge mlango, yaani ukae wazi. Viumbe hawa huwa hawana ubavu wa kuingia kwenye chumba au nyumba yenye mlango wazi.<br />Umewahi kutembea usiku peke yako ukafika mahali kwa mbele kama kuna watu au mtu lakini ukifika hakuna? Jua maeneo hayo kuna viumbe visivyoonekana. Na mara nyingi ukikutana na hali hii lazima itaambatana na hisia za nywele kusisimka kichwa kizima.<br />unaweza ukahisi nywele zinanyonyoka kwa jinsi zinavyosisimka, ujue ni maeneo yenye viumbe.<br />Tabia ya viumbe hivi ambavyo asili yake ni kutoka Nchi ya Wachawi, ni kupenda maeneo yenye watu wengi, mfano, sokoni, stendi ya mabasi na vituo vya daladala. Hakuna maeneo Dar es Salaam yana viumbe wa ajabu kwa wingi kama stendi ya mabasi, pale Ubungo na katikati ya mitaa ya Kariakoo.<br />Kwa Ubungo, unapoona watu wengi wakiingia na kutoka huku wamebeba mizigo, nyuma yao kuna viumbe hao, ndiyo maana huwa tunasema watu wengi, lakini ukweli ni kwamba tunawachanganya na viumbe.<br />Sasa ubaya wao hawa viumbe ni pale wanapoamua wakati mwingine kujitokeza na kuwa watu wanaoweza kuonekana kwa macho.<br />Hapo ndipo wanapoweza kuharibu eneo. Mfano, usidhani kilio cha mara kwa mara cha foleni jijini Dar es Salaam ni cha kweli, foleni nyingine tunaongezewa na hawa viumbe baada ya kujigeuza na kuwa binadamu.<br />Wana uwezo wa kufanya magari yao, wakatoka Kariakoo kwenda Kimara, kwenda Mwenge au Kibamba na wanapokuwa Magomeni na wao wanakuwa kwenye foleni wakati wana uwezo wa kufika wanakokwenda bila kuwepo kwenye foleni wala kuwa kwenye magari.<br />Tatizo ni kwamba, hata ukiliona gari la kiumbe kisichoonekana huwezi kulijua, lina namba za kawaida, kila kitu cha kawaida.<br />Ila, mara zote abiria wa magari haya hawazidi watatu ikiwa na pamoja na dereva. Na mara zote ndani ya gari kunakuwa na utulivu, hakuna anayeongea wala kucheka, mwanzo wa safari yao hadi mwisho.<br />Hatari iliyopo ni kwa wale wafanyabiashara wanaouza maji, juisi, sabuni au bidhaa nyingine kwa wenye magari.<br />Naamini hapa nimeeleweka, yaani ni kwamba, ukifika Magomeni Mapipa, si kuna foleni halafu kuna vijana wanauza vitu kwa watu waliomo ndani ya magari? Basi wale vijana wako hatarini zaidi.<br />Kwanini? Kwa sababu baadhi ya watu wanaowauzia ni wale viumbe wasioonekana ambao siku hiyo wanakuwa ndani ya gari.<br />Wana tabia ya kuchukua damu ya vijana kama hao na kwenda kuichafua, baada ya muda utakuta kijana anakuwa mdhaifu, hana maendeleo, mwili unakuwa umechoka, yaani anakuwa binadamu ilimradi anaishi lakini kwa upande mwingine si binadamu kamili.
 
Tatizo dogo sana. Hapo ulipo piga magoti uliite Jina la Bwana Yesu mlinzi wa walinzi. Usijali hata kama hujawahi kwenda kanisani. Wewe mweleze Mungu na sali unavyojua wewe. Sali kemea kwa jina la Yesu. Muite Mungu Akusafishie nyumba hiyo Atume malaika wake wakulinde. Halafu kwa imani kabisa India kitandani ulale. Hutasikia lolote na utalala usingizi mnono ajabu.

Kwa nini nakushauri hivi? Kuna siku moja usiku kama saa nne kule Usukumani nilikuwa peke yangu. Ili kufika nyumbani kulikuwa na kamto fulani hivi lazima uvuke. Basi kufika pale nikaona mbele yangu watu kama wanne hivi wana vijinga vya moto wamesimama huko niendako. Nikataka kutimua mbio lakini nilipogeuka nikawaona tena hata huko wapo. Basi nikajua kuwa hawa siyo watu wa kawaida na nikadhani pengine haya ndiyo mambo ya kuchukuliwa msukule. Wakati ule nilikuwa Mwadventista Msabato na katika makambi tulikuwa tunafanya mashindano ya kukariri mafungu ya Biblia. Basi hapo hapo nikakumbuka Zaburi 23 na nikaanza kusali kwa sauti kubwa mpaka nasikia mwangwi: Mungu Ndiye mchungaji wangu na sitapungukiwa na kitu. Nijapopita katika bonde la mauti sitaogopa mabaya...Nikatamka kwa sauti kubwa "Yesu nakuhitaji. Shuka Mfalme wa wafalme unipiganie. Waondoe hawa kama wana nia mbaya nami. Ondokeni kwa jina la Yesu..." Yaani mpaka jasho likanitiririka. Kuja kuinua macho sikuona kitu. Huyooo nikatembea mpaka home. Ajabu kesho yake nilikuwa nimechoka balaa. Na baadaye sana nilikuja kuwafahamu wabaya wale na ambacho walikuwa wamepanga kunifanyia. Na kiongozi wao alikuwa ni shangazi yangu kabisa tumbo moja toka nitoke na baba.

Tangu siku hiyo ndiyo nikajua kuwa jina hili Yesu lina nguvu za ajabu. Na cha kushangaza zaidi kuchelewa kote huko mpaka saa nne usiku nakatisha mtoni usiku ni kwa sababu nilikuwa nafukuzia demu. Demu mwenyewe wala hakutokea. Imagine nilikuwa natoka katika harakati za kutenda dhambi lakini Mungu Alikuwa tayari kuniokoa. Ni wema na upendo gani upitao huu?

Sorry for a long story. Mkuu sali halafu uchape usingizi mkuu. Mungu Akulinde na kukubariki. Amen!
Ni huyo mchumba wa huyo demu ndio aliyekuletea hayo maluwe luwee
 
on the other hand,yesu alikufa saa tisa alasiri,saa tisa usiku ni wakati wachawi na shetani kufanya kazi.......

mie niliambiwa,msinishushue,
 
Waungwana habari,hivi sasa naandika uzi huu ni saa nane na dakika 16usiku.nina usingizi ila naogopa kulala kwani nahisi kuna mtu chumbani kwangu.kibaya zaidi nakaa nyumba nzima peke yangu,nimeenda sebuleni ila napo naogopa sana,nahisi kuna mtu ananichungulia huku anacheka.hii inasababishwa na nini.maana kila nikitaka kusinzia nakwama.nashtuka nahisi kuna mtu.kwa mnajua niambieni nifanyeje ili niwe na amani,na ili nilale
Ulitakiwa kupiga magoti na kumuomba Mungu akukinge na adui anaekutia hofu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom