Nani wapo nyuma ya leseni vamizi za madini Jimbo la Mbogwe baada ya Hayati Magufuli kufariki? Je, Biteko umenunulika au ni shinikizo juu yako?

thetallest

JF-Expert Member
Oct 21, 2017
8,256
9,085
Ni leo bungeni, Bunge likimaliza vikao vyake, kaibuka mbunge wa Jimbo hilo Mheshiwa Maganga akilitaka bunge kujadili kwa dharura yanayoendelea jimboni kwake kuhusu mauaji ya watu sita akiwemo binamu yake , akidai mauaji hayo yalisababishwa na leseni vamizi baada ya hayati Magufuli kufariki.

Nimpongeze Spika kwa kulipa umuhimu suala hilo.

Mbunge huyo kaongea kwa uchungu sana,na kasema mahakama shinyanga anaamini zimenunulika na hata yeye angekuwa ana shida ya pesa angechukua ,kwani alitangaziwa dau,isipokuwa uhai wa waliokufa na binamu yake haulingani na hiyo hongo , hivyo ameikataa.

Pia kaongeza kwa kusema, kuna watu walienda eneo hilo na kujifanya maafisa usalama toka juu na ndio waliofanya uhalifu huo.

Tujiuliuze ,kama ni kweli asemayo mbunge huyo wa Mbogwe, je Waziri Biteko kawasaliti wanyonge dhidi ya wachache wenye pesa kwa kuhofia kupoteza uwaziri wake?, yaani kapiga U turn?

Mambo haya yalishamiri sana awamu ya nne ,lakini awamu ya tano wachimbaji hawa wadogo wadogo walipata utulivu sana .

Mwisho,
Amani ya nchi hii tutaivunja wenyewe kwa mikono yetu kwa tamaa za kujilimbikizia mali pasi kufuata sheria,. kwani hawa wanaodhurumiwa wanakiwango pia cha uvumilivu ,hebu changanya hawa wachimbaji wadogo+wamachinga+Mama lishe+wahitimu wasio na ajira +waliokata tamaa ya maisha ,nini matokeo yake akitokea wa kuliwasha?

 
Hii nchi mpaka ipasuke vipande ndio tutakaa sawa,wapo wanaojifanya wana akili sana kuliko wenzao ,kumbe si kweli
 
Huyu Mbunge ni tapeli kwa habari za uhakika yeye binafsi alitaka apewe eneo lake la kuchimba dhahabu ikashindikana sasa anajaribu kumtafutia lawama Kamishna wa Madini aliyeteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan hii njama Doto Biteko anajua vizuri kwani baada ya uteuzi wa Kamishna Mpya wa Madini mtandao wa Doto Biteko ulisambaa
Sidhani,the way alivyoongea naamini hana interest yoyote kwenye kadhia hii, ispokua anahitaji haki itendeke.
 
Huyu Mbunge ni tapeli kwa habari za uhakika yeye binafsi alitaka apewe eneo lake la kuchimba dhahabu ikashindikana sasa anajaribu kumtafutia lawama Kamishna wa Madini aliyeteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan hii njama Doto Biteko anajua vizuri kwani baada ya uteuzi wa Kamishna Mpya wa Madini mtandao wa Doto Biteko ulisambaa
Tuombe utulivu hayo maeneo ,kwani kamishina si anatakiwa kufuata sheria?
Issue hapa ni leseni vamizi,tujiulize zipo au hazipo,na kama zipo ni kwanini zije kipindi hiki ?
 
Mkuu, hebu kuwa serious kidogo kwenye masuala muhimu yenye maslahi kwa taifa
Ninachokizungumza kina maslah kwa taifa! Nikuoe siri moja tu kuwa hayo maisha ya watu wa hali chini ndiyo maisha halisi ya mabepali! Magufuli aliwah kusema kwenye awamu yangu kama tajiri unajiamini unaweza kufanya chochote basi ujue naww unaweza kufanywa chochote.

Magu hakuwa mtu wa ndimi mbili hasa watu wa hali chini wakitendewa maovu, nashawishika kabisa kibisa kukubali kuwa aliuwawa na aoao na nakupa siri nyingine kuwa "Ata Yesu akirudi leo mabepali watapanga njia ili wamuue tu"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni leo bungeni, Bunge likimaliza vikao vyake, kaibuka mbunge wa Jimbo hilo Mheshiwa Maganga akilitaka bunge kujadili kwa dharura yanayoendelea jimboni kwake kuhusu mauaji ya watu sita akiwemo binamu yake , akidai mauaji hayo yalisababishwa na leseni vamizi baada ya hayati Magufuli kufariki.

Nimpongeze Spika kwa kulipa umuhimu suala hilo.

Mbunge huyo kaongea kwa uchungu sana,na kasema mahakama shinyanga anaamini zimenunulika na hata yeye angekuwa ana shida ya pesa angechukua ,kwani alitangaziwa dau,isipokuwa uhai wa waliokufa na binamu yake haulingani na hiyo hongo , hivyo ameikataa.

Pia kaongeza kwa kusema, kuna watu walienda eneo hilo na kujifanya maafisa usalama toka juu na ndio waliofanya uhalifu huo.

Tujiuliuze ,kama ni kweli asemayo mbunge huyo wa Mbogwe, je Waziri Biteko kawasaliti wanyonge dhidi ya wachache wenye pesa kwa kuhofia kupoteza uwaziri wake?, yaani kapiga U turn?

Mambo haya yalishamiri sana awamu ya nne ,lakini awamu ya tano wachimbaji hawa wadogo wadogo walipata utulivu sana .

Mwisho,
Amani ya nchi hii tutaivunja wenyewe kwa mikono yetu kwa tamaa za kujilimbikizia mali pasi kufuata sheria,. kwani hawa wanaodhurumiwa wanakiwango pia cha uvumilivu ,hebu changanya hawa wachimbaji wadogo+wamachinga+Mama lishe+wahitimu wasio na ajira +waliokata tamaa ya maisha ,nini matokeo yake akitokea wa kuliwasha?


Huyu mheshimiwa huenda ana hoja lakini hiyo hoja imekuwa kioja. Hivi huwa hawafundishwi jinsi ya kujenga na kuwasilisha hoja?
 
Ndugai Kuna muda ana busara mpaka unafikiri yule aliyemtandika mwenzie bakora kwenye uchaguzi ni Ndugai rapa..
Kwahili Ndugai ameonyesha unyenyekevu, uzalendo,busara na ukomavu wa maamuzi, majibu yenye busara, hekima na unyenyekevu kama haya aliyoyatoa tumezoea kuyaona kwa Mheshimiwa Waziri wa Utumishi, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Mheshimiwa Rais.
Mungu Ibariki Tanzania
 
Mbunge kutoka jimbo la Mbogwe mh Maganga ameomba mwongozo wa spika bungeni huku akimwaga machozi hadharani kutokana na wachimbaji wadogo wa madini kutoka jimboni kwake kuanza kufukuzwa ,kunyanyaswa na wengine kuawa na wachimbaji wakubwa mara tu baada ya Dk Magufuli kufariki dunia!

Mh Maganga amesema wizara ya madini imekuwa ikitoa leseni kwa wachimbaji wakubwa wanaoenda kuwafukuza wananchi wake kwenye maeneo waliokuwa wakichimba bila usumbufu kwa miaka mitano iliyopita.
Vurugu hizo zimesababisha wananchi sita kuuawa ikiwemo binamu yake.


 
Ndugai Kuna muda ana busara mpaka unafikiri yule aliyemtandika mwenzie bakora kwenye uchaguzi ni Ndugai rapa..
Kwahili Ndugai ameonyesha unyenyekevu, uzalendo,busara na ukomavu wa maamuzi, majibu yenye busara, hekima na unyenyekevu kama haya aliyoyatoa tumezoea kuyaona kwa Mheshimiwa Waziri wa Utumishi, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Mheshimiwa Rais.
Mungu Ibariki Tanzania
Hakika alionyesha busara ya hali ya juu sana,nami nampongeza tena,hasa Jenista Muhagama ,wazri wa sera bunge alipotaka Waziri Biteko ajibu tuhuma hizo kwa kifupi
 
Huyu mheshimiwa huenda ana hoja lakini hiyo hoja imekuwa kioja. Hivi huwa hawafundishwi jinsi ya kujenga na kuwasilisha hoja?
Kwa wenye busara kaeleweka ,ni kweli hana uzoefu wa namna ya uwasilishaji,ukizingatia na mhemko aliokua nao
 
Back
Top Bottom