Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza sana wana JF, you are real a home of GREAT THINKERS,huwa napenda sana kusoma mambo mbalimbali kutoka kwa wadau na nimejifunza mambo mengi sana,hatimaye nimeona na mimi nijiunge na wana JF rasmi ili niweze kutoa maoni yangu kuhusu mambo mbalimbali, na kubadilishana mawazo pamoja na uzoefu.
Kwa mara ya kwanza napenda wadau mnisaidie katika suala hili.nani wanahusika kubadilisha mtaala wa elimu hapa nchini na kwa vigezo gani? Ni jambo muhimu sana kubadilisha mtaala huu ili kuenda sambamba na mazingira halisi ya wakati husika sambamba na mabadiliko yanayotokea kila kukicha.Hata hivyo mabadiliko ya mara kwa mara yanaweza kuathiri kukua kwa elimu na kusababisha wanafunzi kukosa mwelekeo.
Napata utata kidogo kama kweli wale wote wanaohusika na masuala haya huwa wanashirikishwa kikamilifu,mfano walimu na wanafunzi ambao ndio wanaotendea kazi mabadilika hayo. Na kama hawashirikiswi,hasa walimu watawezaje kufundisha kwa kufuata mtaala mpya?na wanafunzi wataelewa nini?
Wadau nipenio mwanga katika hili.
Kwa mara ya kwanza napenda wadau mnisaidie katika suala hili.nani wanahusika kubadilisha mtaala wa elimu hapa nchini na kwa vigezo gani? Ni jambo muhimu sana kubadilisha mtaala huu ili kuenda sambamba na mazingira halisi ya wakati husika sambamba na mabadiliko yanayotokea kila kukicha.Hata hivyo mabadiliko ya mara kwa mara yanaweza kuathiri kukua kwa elimu na kusababisha wanafunzi kukosa mwelekeo.
Napata utata kidogo kama kweli wale wote wanaohusika na masuala haya huwa wanashirikishwa kikamilifu,mfano walimu na wanafunzi ambao ndio wanaotendea kazi mabadilika hayo. Na kama hawashirikiswi,hasa walimu watawezaje kufundisha kwa kufuata mtaala mpya?na wanafunzi wataelewa nini?
Wadau nipenio mwanga katika hili.