Nani walikuwa viongozi wa PSRC?

Rufiji

Platinum Member
Jun 18, 2006
1,881
941
Kwa muda sasa tumekuwa tukisikia ni kwa jinsi gani viongozi mbali mbali wa serikali walivyoweza kujinunulia kampuni mbali mbali zilizokuwa zikibinafsishwa kwa bei ya chini kabisa .

Cha kushangaza sijasikia hata mtu mmoja akiuliza ni sababu gani haswa zilizopelekea hii tume ya kubinafsisha haya mashirika bila ya kufuata taratibu kitendo ambacho kinachoashiria uzembe wa hali ya juu.

Mimi ninachotaka kujua; ni nani haswa walikuwa viongozi wa hii tume na je, ni sababu gani zilizowapelekea kufanya maamuzi yasiyo na kichwa wala miguu?
 
http://www.psrctz.com/Main_Index.htm

sasa hivi ni ALI KARAVINA ndio chairman
hii cv yake

EDUCATION

Chartered Institute of Marketing -UK Marketing Courses 1991 - CERTIFICATE

University of Wales (UK) MSc.(Transport Economics, Planning and Policy) 1984 1986 MASTERS DEGREE

Chartered Institute of Transport (UK) B.A (Transport) 1982 - GRADUATE

National Institute of Transport-Dar es Salaam Diploma in Transport Management 1979 - ADV DIPLOMA


EMPLOYMENT HISTORY

Tanzania Railways Co-operation(TRC) Deputy Head of Directorate of Trade and Markets 1992 2000

Tanzania Railways Corporation Chief Costing & Pricing Manager 1986 -

Tanzania Railways Corporation-TRC Principal Traffic Manager 1981 1983

Tanzania Railways Corporation Traffic Manager 1978 1994

East African Railways Corporation Traffic Officer 1971 1978
 
Kuna mtu anaitwa Mbowe na mwingine anaitwa John Rubambe.

John Rubambe alikuwa ndiyo sorta CEO wao kipindi cha Mkapa, ajamaa alitokea Bima, alikuwa classmate wa Mkapa.Nasikia alikuwa under great scrutiny -some would even say intimidation- kwa muda mrefu kabla ya kupewa hiyo kazi na Mkapa.Ilikuwa Mpaka simu yake ya nyumbani walimuwekea tap.By the way washua kibao hawako tayari kuongea ma issue mazito kwenye simu au email wanasema bongo kuna surveillance kichizi.

So Rubambe, Mkapa pamoja na hawa viongozi wa mashirika ya umma wana a lot to answer.Wengine wanaweza kumtetea kuwa alikuwa anafanya alichoambiwa na Mkapa tu lakini still, angeweza kufanya bonge la expose kama angetaka.
 
Pundit,

Nakubalina na wewe kabisa viongozi wote wa tume hii kipindi cha Mkapa they have a lot to answer. Mimi ninachojiuliza ni kwa nini PSRC ilivurunda kila kitu ilichofanya ? Jee ni kwamba hawakuwa na wataalamu wa kutosha au ni kwa sababu hawakuweka maslahi ya taifa mbele ?

Mimi nadhani kuna haja ya kufanywa investigation kubwa kuichunguza hii tume nini haswa ilifanya kipindi cha Mkapa.
 
Mkuu waliohusika sana na hiyo kitu ya PSRC:-

1. Mkapa
2. Sumaye
3. Idd Simba
4. Kigoda
5. Yona
6. Masilingi
7. Chenge
8. Rubambe
9. Balozi Kazaura
10. Mpungwe,

Deal zote za hiyo kitu inahusisha hawa wakuu, in one way or another!
 
Kuna mtu anaitwa Mbowe na mwingine anaitwa John Rubambe.

John Rubambe alikuwa ndiyo sorta CEO wao kipindi cha Mkapa, ajamaa alitokea Bima, alikuwa classmate wa Mkapa.Nasikia alikuwa under great scrutiny -some would even say intimidation- kwa muda mrefu kabla ya kupewa hiyo kazi na Mkapa.Ilikuwa Mpaka simu yake ya nyumbani walimuwekea tap.By the way washua kibao hawako tayari kuongea ma issue mazito kwenye simu au email wanasema bongo kuna surveillance kichizi.

So Rubambe, Mkapa pamoja na hawa viongozi wa mashirika ya umma wana a lot to answer.Wengine wanaweza kumtetea kuwa alikuwa anafanya alichoambiwa na Mkapa tu lakini still, angeweza kufanya bonge la expose kama angetaka.

George Mbowe alikuwa nafikiri DG wa kwanza wakati PSRC ilipoanzishwa. Kama wengi mtakumbuka huyu alikuwa TDFL( I think) ambako alifukuzwa kazi na Nyerere pamoja na Augustine Mwingira na Lawrence Mmasi kwa zile scandal za Mawasiliano kuruhusu ATC kununua zile 707 za George Habash na Tacoshili kuuza meli kwa Lord Rajpar.

Pundit,

If there was such high level of survillance, how come both PSRC na TIC walituingiza mkenge? Don't you think you are adding more fuel to the talk of irresponsible TISS?
 
Alikuwepo mwenyekiti George Mbowe wakati wa Mwinyi, na John Rubambe wakati wa Mkapa. Sasa hivi yupo Ali Karavina.

Katika mahojiano fulani, George Mbowe aliwahi kusema yeye pia ndiye aliyepewa na Mwalimu Nyerere jukumu la kuratibu utaifishaji wakati Azimio la Arusha 1967.

Watu wamekula nchi muda mrefu mwanawane!
 
Kithuku, Pundit, Rufiji,

..George Mbowe inasemekana alikuwa rafiki mkubwa wa Cygwiyemwisi John Malecela.

..Mbowe ni mwenyeji wa Mbeya sifahamu kabila lipi though.

..Mtendaji Mkuu wa PSRC analipwa na World Bank. kuna kipindi wabunge walilalamika kwanini alipwe mshahara wa zaidi ya USD 6000 kwa mwezi.

..Mkapa basically alimfukuza kazi Mbowe. uteuzi wa Rubambe ulifanywa kwa siri kubwa na hata waziri wa fedha aliusikia redioni.

..Kikwete naye alipoingia amkampatia ulaji swahiba wake Alli Karavina. Appointment ya Rubambe imefutwa kabla hata mkataba wake haujaisha.

..sijui tatizo la PSRC ni nini. chukulia mfano wa ubinafsishaji wa TRC ulivyoborongwa, despite the fact kwamba Karavina aliwahi kuwa Mkurugenzi huku TRC kabla ya kujiunga na siasa.
 
This is dated but relevant

VIONGOZI mbalimbali wa Kanisa Katoliki Tanzania, wameelezea wasiwasi juu ya zoezi zima la ubinafsishaji linalofanywa na serikali kupitia Tume ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC).

Viongozi hao walieleza wasiwasi huo wakati wa semina ya Wajumbe wa Baraza la Maskofu wa Kanisa Katoliki ilifanyika jana katika Ukumbi wa Baraza la Maaskofu Kurasini, Dar es Salaam.
Askofu Mkuu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mathodius Kilaini, alihoji kuna uwazi gani katika zoezi zima la ubinafsihaji.

ASkofu Kilaini pia alihoji ujanja unaofanywa na baadhi ya wawekezaji ambao huja wakiwa wameweka mikono nyuma kuomba zabuni hizo na pindi wanapopewa hutumia ujanja kuhakikisha kuwa wanavuna bila jasho na kuondoka kavbla hawajalipa kodi.

"Sheraton walikuja tukawapa msamaha wa kodi lakini baada ya muda wa msamaha huo kuisha, wakafanya ujanja na sasa ni Royal Palm na si Sheraton tena," alisema ASkofu Kilaini.

Akijibu tuhuma hizo, Mwenyekiti wa PSRC, John Rubambe, alisema kuwa, PSRC inafuata uwazi katika kubinafsisha mashirika yake na kwamba mikataba yote ina nguvuisipokuwa baadhi ya wawekezaji wanakiuka masharti hayo.

Rubambe pia aliyapuuza malalamiko yanayotolewa na baadhi ya wawekezaji walioshindwa kupata zabuni, kwamba ubinafsishaji si wazi. Alisema uamuzi wa kubiinafsisha shirika la umma unapitishwa na Baraza la Mawaziri na akasema wanaodaii kuwa kuna mchezo mchafu, wana ajenda zao.

Alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, PSRC haina uwezo wa kutoa ama kumueleza mtu aliyeshindwa kwa kuwa sababu hizo hutolewa ndani ya kikao cha Baraza la Mawaziri.

Rubambe alisema kinachotokea ni kwamba Watanzania wanashindwa kupata Zabuni kutokana na uwezo mdogo wa fedha na akaitaka serikali kuwawezesha wananchi wake ili wapate uwezo wa kununua mashirika hayo.

Rais wa TEC ambaye ni Askofu wa Jimbo la Rulenge Severin Niwemwagizi, alitoa malalamiko ya baadhi ya watu kuwa Taasisi hiyo inafanya kiini macho katika utoaji wa zabuni hizo kwa kuwa wanakuwa tayari wamewapendekeza watu wao.

Askofu Niwemwagizi apia alihoji kwanini wawekezaji wengi wanatoka Afrika Kusini na kuongeza kuwa hata wakija hapa, huwaajiri watu wao na kuwalipa mishahara mikubwa tofauti na wazalendo wanaofanya kazi ziinazofanana.

Mshauri Mkuu wa masuala ya sheria katika PSRC, Buhari Minja alisema kinachotokea ni kwamba watu hawakubali kushindwa palewanapopoteza zabuni na hivyo huanzisha maneno kuwa kuna upendeleo.

"Mtu anayeshindwa kesi hawezi kukubaliana na maamuzi yaliyotolewa na hakimu dhidi yake na badala yake anaona ameonewa," alisema Minja.

Kamishina wa PSRC, Dk. Damas Mbogoro akitoa mada ya ushirikishwaji wa wananchi wa Tanzania katika Ubinafsishaji, alisema pamoja na nia nzuri ya wawekezaji wa ndani, bado kuna kikwazo katika kufikia lengo hilo.

Dk. Mbogoro aliyataja matatizo hayo kuwa ni pamoja na kukosa uwezo wa kifedha na kitaalamu wa kutayarisha zabuni zinazobainisha vizuri mipango ya uwekezaji na uendelezaji na namna itakayotekelezeka.

"Sasa hivi kuna malumbano kuhusu mchezo mchafu, kama fedha yako haitoshi kutuambia mchezo mchafu ni kutuonea, sasa uwezo wako ni mdogo utaweza kulipa madeni kweli? Kama mtu wa nje anakuja na fedha nyingi lazima achaguliwe kwani vigezo ni pamoja na kuwa na uwezo kifedha."

Hata hivyo Kamishina mwingine wa PSRC, Beata Swai, alisema umefika wakati wa Tanzania kuachana na imani za kishetani na mizimu na kumwamini Mungu.

Swai alisema kuwa pamoja na Tanzania kuwa na mali nyingi, bado watu wake ni maskini na wameshindwa kuongoza wenyewe mali hizo kutokana na watu wake kupendelea zaidi nguvu za giza.

"Hii ni laana! Kiongozi akichaguliwa tu anakimbilia kwa mganga, ukijiuliza wanakwenda kufanya nini huko unakosa jibu. Wote hawajiamini hata muda wa kufanya kazi unakuwa mdogo wote wanaenda kwa waganga," alisema
 
Kithuku,Pundit,Rufiji,

..George Mbowe inasemekana alikuwa rafiki mkubwa wa Cygwiyemwisi John Malecela.

..Mbowe ni mwenyeji wa Mbeya sifahamu kabila lipi though.

..Mtendaji Mkuu wa PSRC analipwa na World Bank. kuna kipindi wabunge walilalamika kwanini alipwe mshahara wa zaidi ya USD 6000 kwa mwezi.

..Mkapa basically alimfukuza kazi Mbowe. uteuzi wa Rubambe ulifanywa kwa siri kubwa na hata waziri wa fedha aliusikia redioni.

.

It is true kuwa wabunge walilalamika sana. Lakini WB si ndio walikuja na kutuambia tuache kuendesha mashirika na hivyo mzigo wa kuundwa taasisi hii ukawa mabegani mwao?

As far as I know PSRC is no longer functioning. Kazi yao ya mwisho ilikuwa ni mkataba wa Karamagi wa TICTS!
 
Rev. Kishoka,

Ni kweli kwamba PSRC ai-function tena na ndio maana swali nililouliza lilukuwa katika wakati uliopita , " Nani walikuwa viongozi wa PSRC ? ". Lakini hata kama aifunction aituzuii sisi kuuliza maswali haswa pale tunapoona ya kuwa tume hii ilifanya makosa makubwa sana katika mikataba mingi.

Jee ni nini haswa kilichowapelekea kuextend mkataba na Karamagi (TICTS) kwa miaka 25 huku wakijua wazi ya kuwa serikali imepoteza mabilioni ya shilingi pale Bandari, Jee yalikuwa kwa manufaa ya taifa au manufaa binafsi .

Mimi nadhani ni muhimu kuichunguza hii tume kwani hawa watu wanajua vitu vingi na kama kweli tunataka kujua undani wa ufisadi basi hawa watu ni lazima wajibu maswali mazito.
 
Mkuu waliohusika sana na hiyo kitu ya PSRC:-

1. Mkapa, 2. Sumaye, 3. Idd Simba, 4. Kigoda, 5. Yona, 6. Masilingi, 7. Chenge, 8.Rubambe 9. Balozi Kazaura, 10. Mpungwe,

Deal zote za hiyo kitu inahusisha hawa wakuu, in one way or another!

Ama kweli maisha kitu kingine. Wote hawa ni wastaafu au kama bado kwenye system ndo hivo wako ukingoni. Imagine mtu kama Sumaye ..na madudu yoooote aliyoyafanya, leo shamelessly anakuja kukwambia kwamba ameokoka and he can deliver us to the promised land.

Ila Kiukweli nchi nyingi za Kiafrika umasikini wetu umesababishwa na viongozi wetu. Kwa mda mrefu tumekosa uongozi bora.

Inabidi tuwe na mjadala wa kitaifa tusioneane aibu..waliotufikisha hapa..hata kama hawatafungwa..basi watubu!
 
Ama kweli maisha kitu kingine. Wote hawa ni wastaafu au kama bado kwenye system ndo hivo wako ukingoni. Imagine mtu kama Sumaye ..na madudu yoooote aliyoyafanya, leo shamelessly anakuja kukwambia kwamba ameokoka and he can deliver us to the promised land.

Ila Kiukweli nchi nyingi za Kiafrika umasikini wetu umesababishwa na viongozi wetu. Kwa mda mrefu tumekosa uongozi bora.

Inabidi tuwe na mjadala wa kitaifa tusioneane aibu..waliotufikisha hapa..hata kama hawatafungwa..basi watubu!

..kama umeshindwa ku-reconcile na Sumaye umeweza vipi na Magu?

..haswa ukizingatia kashfa ya kuuza nyumba za serikali nchi nzima na nyingine kwa ndugu zake.

..au kashfa ya ununuzi wa meli mkweche na sasa hivi imefichwa mahala na ni jinai kuhoji suala hilo.

NB.

..psrc ili-deal na wizara zote. Kwasababu kila wizara ilikuwa na shirika ambalo lilitakiwa kubinafsishwa.
 
JokaKuu,

Endapo ndugu yetu Masanja atakupa jibu la kukuridhisha basi naomba uni-tag ili nami nipate ilmu kidogo!!!

Halafu hebu nikumbushe hao #9 (Balozi Kazaura) na #10, Mpungwe! Ni nani kati yao alikuwa ndie Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini.

Moja ya watu ambao sitakuja kuwasamehe ni yule aliyekuwa Balozi wetu SA wakati wa Mkapa!!! Yule jamaa aliitendea "haki" kweli kweli economic diplomacy kwa kutuletea mabeberu ya kiuchumi kutoa SA; kuanzia kwenye sekta ya madini, mabenki hadi viwanda!!
 
Alikuwepo mwenyekiti George Mbowe wakati wa Mwinyi, na John Rubambe wakati wa Mkapa. Sasa hivi yupo Ali Karavina!

Enzi za Mkapa Mbowe alikuwa Chairman. Manyika huyu wa Acacia Gold alikuwa Legal Secretary. Then kulikuwa na ma kamishna wa PSRC kutia ndani kina Prof Mwandosya nk.
 
JokaKuu,

Endapo ndugu yetu Masanja atakupa jibu la kukuridhisha basi naomba uni-tag ili nami nipate ilmu kidogo!!!

Halafu hebu nikumbushe hao #9 (Balozi Kazaura) na #10, Mpungwe! Ni nani kati yao alikuwa ndie Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini.

Moja ya watu ambao sitakuja kuwasamehe ni yule aliyekuwa Balozi wetu SA wakati wa Mkapa!!! Yule jamaa aliitendea "haki" kweli kweli economic diplomacy kwa kutuletea mabeberu ya kiuchumi kutoa SA; kuanzia kwenye sekta ya madini, mabenki hadi viwanda!!
Ni Ami Mpungwe
 
George Mbowe enzi za mwinyi. Huyu alijitahidi kiasi na hakuhusika kurajisi mali na mashirika mengi ya umma.

John Rubambe alikuwa wakati wa Mkapa. Huyu alineemeka sana kwani wakati wake ndio sera ya ubinafsishaji migodi na mali nyingi. Wakati huo ubalozi wetu Afrika kusini tukiwakilishwa na Ndg Mpungwe hapa ndio uporaji mkubwa na mikataba mibovu yote ililala.
 
Deo mwanyika vice president wa Acacia ndio alikuwa chief legal secretary wa PSRC. Baadae Barrick waliona anawafaa wamchukue sababu aliwasaidia kupata lions share kwenye mikataba kwa kigezo cha kuvutia wawekezaji in Ngeleja's insight
 
Back
Top Bottom