Nani wa kumrithi TB Joshua na kuendeleza huduma yake katika bara la wapenda miujiza na injili ya mafanikio (prosperity gospel?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,581
46,178
TB Joshua ni mtu aliyejitengenezea jina kubwa barani Africa kwa injili yake ya mafanikio. Aliwakamata wafanyakazi, maskini, matajiri, wafanyabiashara na wanasiasa wakubwa kabisa katika ngazi za Urais na wakuu wa upinzani.

Watu hawakulizungumza tu jina lake bali walisafiri hadi Nigeria katika kanisa lake alilolipa jina la Sinagogi kanisa la watu wote(SCOAN). Inasemekana kuna wakati watu 6 kati ya 10 ambao ungewakuta wakisafiri kuingia Nigeria walikuwa wanaenda kanisani kwake!

Watu mashuhuri walimwalika kwao pia. Mfano hapa Tanzania amewahi kufika na kukutana na JK, Magufuli, Mbowe na Lowassa.

Mpaka sasa nikiacha hii sababu ya hulka ya watu kupenda kuambiwa, kuhadiwa na kutabariwa mafanikio makubwa kwa yale wanayoyatamani sijui kwa uhakika hasa ni kitu gani kingine kilimfanya TB Joshua ambaye aliendesha huduma yake kwa mfumo wa Mwamposa na Mzee wa Upako kuwa maarufu mkubwa hivyo kiasi cha kuliteka bara zima na kuweza kuaminiwa hata na pande zilizokuwa mahasimu mara nyingine.

Huenda waliomuamini na kumhusudu wana sababu nyingine za msingi walizoshawishika nazo lakini sasa akiwa hayupo tena duniani ni nani watampa nafasi hiyo? Wale mlioko Mikocheni B kanisani kwa Getrude Rwakatare tuelezeni mambo yanavyoendelea kwa sasa tupate mwangaza.
 
Nigeria kuna Jerry Eze ni kijana aliyelelewa na single mother. Hakua hata na uwezo wa kumpeleka shule mpaka alipojitokeza msamaria mwema aliyeamua kumlipia gharama za masomo.

Jerry Eze ukimaliza kusikiliza ibada yake mara nyingi na wewe unakua na testimony yako.

1623123962017.png
 
Mchungaji kuliteka bara zima la Afrika na si kwingineko ni shida ya kuwa na maarifa haba juu ya maisha ya mwanadamu.
 
Nigeria kuna Jerry Eze ni kijana aliyelelewa na single mother. Hakua hata na uwezo wa kumpeleka shule mpaka alipojitokeza msamaria mwema aliyeamua kumlipia gharama za masomo.

Jerry Eze ukimaliza kusikiliza ibada yake mara nyingi na wewe unakua na testimony yako.
Na yeye anauza anointing water 90$?
 
Nigeria kuna Jerry Eze ni kijana aliyelelewa na single mother. Hakua hata na uwezo wa kumpeleka shule mpaka alipojitokeza msamaria mwema aliyeamua kumlipia gharama za masomo.

Jerry Eze ukimaliza kusikiliza ibada yake mara nyingi na wewe unakua na testimony yako.
Ni wa kiume au wa kike? Kama wa kiume, huyo msamaria ni mwema kweli? Hajatoka na huyo single mother kweli?
 
Sijui kwa nini, mimi hawa wachungaji wa makanisa ya kilokole wengi naona matapeli. Kuanzia kwa akina Gwajima, TB J na wenzake.
Wengi wao ni wapigaji.

Ukiwa masikini ukaingia haya makanisa uwezekano wa kuzidi kuwa hopeless na fukara kichwani ni mkubwa!
 
Sijui kwa nini, mimi hawa wachungaji wa makanisa ya kilokole wengi naona matapeli. Kuanzia kwa akina Gwajima, TB J na wenzake.
Wengi wao ni wapigaji.

Ukiwa masikini ukaingia haya makanisa uwezekano wa kuzidi kuwa hopeless na fukara kichwani ni mkubwa!
Ulokole sio utapeli ila WAPO WAHUNI WALIOVAMIA ULOKOLE MFANO NDIO HAO KINA MASANJA, GWAJIMA, LUSEKELO N.K
 
TB Joshua ni mtu aliyejitengenezea jina kubwa barani Africa kwa injili yake ya mafanikio. Aliwakamata wafanyakazi, maskini, matajiri, wafanyabiashara na wanasiasa wakubwa kabisa katika ngazi za Urais na wakuu wa upinzani.

Watu hawakulizungumza tu jina lake bali walisafiri hadi Nigeria katika kanisa lake alilolipa jina la Sinagogi kanisa la watu wote(SCOAN).Inasemekana kuna wakati watu 6 kati ya 10 ambao ungewakuta wakisafiri kuingia Nigeria walikuwa wanaenda kanisani kwake!

Watu mashuhuri walimwalika kwao pia. Mfano hapa Tanzania amewahi kufika na kukutana na JK, Magufuli, Mbowe na Lowassa.

Mpaka sasa nikiacha hii sababu ya hulka ya watu kupenda kuambiwa, kuhadiwa na kutabariwa mafanikio makubwa kwa yale wanayoyatamani sijui kwa uhakika hasa ni kitu gani kingine kilimfanya TB Joshua ambaye aliendesha huduma yake kwa mfumo wa Mwamposa na Mzee wa Upako kuwa maarufu mkubwa hivyo kiasi cha kuliteka bara zima na kuweza kuaminiwa hata na pande zilizokuwa mahasimu mara nyingine.

Huenda waliomuamini na kumhusudu wana sababu nyingine za msingi walizoshawishika nazo lakini sasa akiwa hayupo tena duniani ni nani watampa nafasi hiyo? Wale mlioko Mikocheni B kanisani kwa Getrude Rwakatare tuelezeni mambo yanavyoendelea kwa sasa tupate mwangaza.
Nipo tayari, mnitume mimi.
 
TB Joshua ni mtu aliyejitengenezea jina kubwa barani Africa kwa injili yake ya mafanikio. Aliwakamata wafanyakazi, maskini, matajiri, wafanyabiashara na wanasiasa wakubwa kabisa katika ngazi za Urais na wakuu wa upinzani.

Watu hawakulizungumza tu jina lake bali walisafiri hadi Nigeria katika kanisa lake alilolipa jina la Sinagogi kanisa la watu wote(SCOAN). Inasemekana kuna wakati watu 6 kati ya 10 ambao ungewakuta wakisafiri kuingia Nigeria walikuwa wanaenda kanisani kwake!

Watu mashuhuri walimwalika kwao pia. Mfano hapa Tanzania amewahi kufika na kukutana na JK, Magufuli, Mbowe na Lowassa.

Mpaka sasa nikiacha hii sababu ya hulka ya watu kupenda kuambiwa, kuhadiwa na kutabariwa mafanikio makubwa kwa yale wanayoyatamani sijui kwa uhakika hasa ni kitu gani kingine kilimfanya TB Joshua ambaye aliendesha huduma yake kwa mfumo wa Mwamposa na Mzee wa Upako kuwa maarufu mkubwa hivyo kiasi cha kuliteka bara zima na kuweza kuaminiwa hata na pande zilizokuwa mahasimu mara nyingine.

Huenda waliomuamini na kumhusudu wana sababu nyingine za msingi walizoshawishika nazo lakini sasa akiwa hayupo tena duniani ni nani watampa nafasi hiyo? Wale mlioko Mikocheni B kanisani kwa Getrude Rwakatare tuelezeni mambo yanavyoendelea kwa sasa tupate mwangaza.
Ila kwa Nigeria nazani TB Joshua ni ka number 3 hivi kama sikosei, kule wako wahubiri balaa acha kabisa na ile Nchi,
 
Nigeria kuna Jerry Eze ni kijana aliyelelewa na single mother. Hakua hata na uwezo wa kumpeleka shule mpaka alipojitokeza msamaria mwema aliyeamua kumlipia gharama za masomo.

Jerry Eze ukimaliza kusikiliza ibada yake mara nyingi na wewe unakua na testimony yako.

View attachment 1812018
Nigeria wahubiri ni wengi mno, ni Sawa na Brazili kwenye Vipaji vya mpira
 
Back
Top Bottom