Wateule
JF-Expert Member
- Sep 17, 2010
- 390
- 368
Huyo mnayesema "anaangushwa" ndio anayewatuma kutumia mbinu chafu za kisiasa. Na ule unaitwa "mgogoro wa CUF." Kama CUF na wao wangeweka ving'amuzi mapema ili kunasa na kuweka ushahidi hadharani, tungeona na kusikia mengi. Kwa kuwa hawa wakuu wa wilaya na wengine wana maagizo "kutoka juu", hawafanywi lolote pindi wakiharibu mambo. Sanasana mtasikia mkuu na yeye akiropoka "wewe piga kazi tu", kwani Bashite ilikuwa aje pamoja na kwamba video za CCTV zilimnasa LIVE akifanya uvamizi usiku kwenye ofisi za watu? Mpaka leo mado yupo madarakani anadunda na kuendeleza kibri.
CCM na kiongozi wao wapo tayari kufanya lolote ili mambo yao yaende, na hata mipango ikiharibika kama suala la Bashite, na sasa huyu Mnyeti, wao hawajali, maana polisi na mahakama pia wamedhibiti wao. Nafikiri wanapopewa maagizo ya kufanya uharamia kama huu wa Arusha na mengineyo, huwa wanapewa jukumu tu (kwa mfano, kuhakikisha madiwani wa CHADEMA wana hamia CCM au kuvuruga umoja na mshikamano wa wana CUF, nk), bila masharti ya utekelezaji wa jukumu hilo. Matokeo yake, kila mtu anakuja na mikakati yake ya kutimiza malengo kusudiwa, iwe uvamizi sawaaa!, iwe rushwa, sawaaa!, iwe mauaji, pia sawaaa tu!!
CCM na kiongozi wao wapo tayari kufanya lolote ili mambo yao yaende, na hata mipango ikiharibika kama suala la Bashite, na sasa huyu Mnyeti, wao hawajali, maana polisi na mahakama pia wamedhibiti wao. Nafikiri wanapopewa maagizo ya kufanya uharamia kama huu wa Arusha na mengineyo, huwa wanapewa jukumu tu (kwa mfano, kuhakikisha madiwani wa CHADEMA wana hamia CCM au kuvuruga umoja na mshikamano wa wana CUF, nk), bila masharti ya utekelezaji wa jukumu hilo. Matokeo yake, kila mtu anakuja na mikakati yake ya kutimiza malengo kusudiwa, iwe uvamizi sawaaa!, iwe rushwa, sawaaa!, iwe mauaji, pia sawaaa tu!!