Nani Msafi...?nani Mchafu....?

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,967
22,476
Wana jf....Kumekuwa na msururu wa threads mpaka sasa hujui nini ni nini na wapi ni wapi!
Kunaonekana kuna MVUTANO MKUBWA!
Ni wazi kuwa KESI IMELETWA JF!
Sasa ili wananchi wanaofuatilia mijadala hii wasichanganyikiwe...Basi sasa MIMI NIKO RADHI KUSEMA KUWA...Huu ni muda wa kuangalia ni nani safi na ni nani si safi!
Kuna Mpango mahsusi kabisa wa kujaribu kumchafua MWAKYEMBE.
Kwasababu sasa tunajuwa stories zote za EPA NA RICHMOND..ECT ECT...
Ni vizuri tukaanza kutaja majina ya watu ambao kisheria wanatakiwa mahakamani.
Pia kwa wale watakaoleta siasa...Then na sisi tutawaonyesha ni kwanini na wao wameguswa na UFISADI.
Kwa kuanzia...NASEMA MWAKYEMBE NI SAFI...Baada ya hapo...Nitaendeleza kutaja wengine walio safi na wale CHAFU!
 
Badala ya kuanza kuwalaumu watoa ripoti...Kwanini wale waliotajwa wasijibu makosa yao mbele ya bunge ama na mahakama?
HATUTAKI SIASA ZA KUSAFISHANA HAPA JF!
UKWELI WOTE UNAJULIKANA!
TUNATAKA RIPOTI ZOTE ZISOMWE...YA EPA,MADINI NK!
BAADA YA RIPOTI HIZO KUSOMWA NDIPO WANANCHI WATAJUWA KUWA NI NANI SAFI NA NI NANI MCHAFU!
KUWANZA KUTUCHAGULIA KUWA NANI NI MSAFI NA NANI NI MCHAFU NI KUTUPOTEZEA MUDA WA KUJADILI MUSTAKABALI WA NCHI!
 
Rais wangu wote tulishuhudia kujiuzulu kwa Abdallah Natepe, Peter Siyovelwa, Ali Hassan Mwinyi na wengine. Ni kikao gani kilikaa kuwasafisha watu hawa? Mbona mpaka leo wapo safi? Hawakusafishwa kwa sababu wao wenyewe hawakuchafuka.

Walijiuzulu ili kulinda ustaarabu. Walijiuzulu bila kuchafuka wangesafishwa vipi? Huwezi kupungwa mapepo kama huna mapepo. Lakini kama una mapepo, hata upungwe vipi alama ya mapepo itabaki juu yako.

Inasikitisha kuona watu wazima wanaficha maiti chumbani kwa kuipulizia marashi. Inasikitisha zaidi tunapotaarifiwa kuwa, kusafishwa huko kunakuja huku kukiwa na wingu zito la tuhuma za rushwa, ushirikina, vitisho na hata ulaghai uliogubika mikakati ya kuhakikisha watuhumiwa wote wa ufisadi wanasafishwa.

Na hiyo ndio habari yenyewe!!
 
Baada ya kuendelea kuona migogoro ya wajumbe wa mafisadi...basi nachukuwa nafasi hii kwaambia wananchi kuwa hakuna chama kisafi na pia kuna dini mbili...NAZO NI ZA WAZALENDO NA ILE YA MAFISADI!
DINI YA WAZALENDO NI ILE ITAKAYOSHINIKIZA MAFISADI WAKAMATWE!
NA DINI YA MAFISADI NI ILE YA KUSAFISHANA NA WALE WENYE KUSEMA PESA ZIRUDISHWE.
 
Wana jf....Kumekuwa na msururu wa threads mpaka sasa hujui nini ni nini na wapi ni wapi!
Kunaonekana kuna MVUTANO MKUBWA!
Ni wazi kuwa KESI IMELETWA JF!
Sasa ili wananchi wanaofuatilia mijadala hii wasichanganyikiwe...Basi sasa MIMI NIKO RADHI KUSEMA KUWA...Huu ni muda wa kuangalia ni nani safi na ni nani si safi!
Kuna Mpango mahsusi kabisa wa kujaribu kumchafua MWAKYEMBE.
Kwasababu sasa tunajuwa stories zote za EPA NA RICHMOND..ECT ECT...
Ni vizuri tukaanza kutaja majina ya watu ambao kisheria wanatakiwa mahakamani.
Pia kwa wale watakaoleta siasa...Then na sisi tutawaonyesha ni kwanini na wao wameguswa na UFISADI.
Kwa kuanzia...NASEMA MWAKYEMBE NI SAFI...Baada ya hapo...Nitaendeleza kutaja wengine walio safi na wale CHAFU!

Mkuu,

Nilitegemea kuona watu tunaendeleza kampeni kuhakikisha wale wote wanaotuhumiwa kuhusika na kashfa zote hizo wanaikabili sheria na kuona mwisho wake.

Lakini hili jambo linaitwa "spinning" ndilo nilionalo linajaribu kujipenyeza kwa nguvu.

Lengo kuu la spinning ni kupoteza lengo kwa public kwa kuwa-manipulate na vijihabari mbuzi na midubwana mingine isiyo kichwa wala mkia.

Watu wanajaribu kuongelea kuhusu Mwakyembe huku wakiwapa nafasi watuhumiwa wajisafishe majimboni kwao .

Kama ni hivyo nami ntakuwa nalifuatilia.
 
Mkuu,

Nilitegemea kuona watu tunaendeleza kampeni kuhakikisha wale wote wanaotuhumiwa kuhusika na kashfa zote hizo wanaikabili sheria na kuona mwisho wake.

Lakini hili jambo linaitwa "spinning" ndilo nilionalo linajaribu kujipenyeza kwa nguvu.

Lengo kuu la spinning ni kupoteza lengo kwa public kwa kuwa-manipulate na vijihabari mbuzi na midubwana mingine isiyo kichwa wala mkia.

Watu wanajaribu kuongelea kuhusu Mwakyembe huku wakiwapa nafasi watuhumiwa wajisafishe majimboni kwao .

Kama ni hivyo nami ntakuwa nalifuatilia.

Richard naona MAFISADI WALIKUWA WAKILALAMIKA KWASABABU HABARI ZOTE MAGAZETINI ZILIKUWA ZIKITOKEA HAPA!
Na kama kawaida...Mijadala huendelea hapa na kesho yake kuandikwa gazetini!
Sasa naona wameamua kuja kwenye SOURCE ILI KU DISTORT HABARI ZA WANANCHI!
KWA HIYO KWASABABU NILITABIRI MIGAWANYIKO YOTE HII...BASI NI MUHIMU TUSIKUBALI KUYUMBISHWA!
VITA NI MOJA....WAZALENDO VS mafisadi...!
 
Kwasababu CHADEMA NA CCM WAMEAMUWA KUGOMBEA MADARAKA YA NCHI KWA KUJIPANGA KIANA...Sasa na sisi tunasema kuwa hatutaki hayo..Tunataka RIPOTI na wananchi ndio waamue nani safi na nani si safi!
Huko ccm tayari tumeshawajuwa...Na CHADEMA..Wanaaza kugombana labda kwa kukuru kakara za kujipanga ama kuvuruga mawazo ya wananchi kwenye mjadala wa UFISADI.
Sasa Naanza na CHADEMA...NANI SAFI HUMO CHADEMA?NANI MSAFI?KABLA YA HAYO MAUGOMVI YENU YA PESA ZA RUZUKU NA UKABILA...NAULIZA TENA NANI SAFI HUMO?
 
TATIZO NI KUNA MAMLUKI KUTOKA BOTH ccm na chadema wanaovuruga mijadala ya upinzania kwa maslahi yao binafsi!
Wananchi kama mnataka tuwatajie nani ni safi na nani si safi tutafanya hivyo!
maana hapa kuna vita kati ya watu binafsi ndani ya vyama vyao!
HAKUNA ATAKAYE CHAGUA VYAMA...WANANCHI WATAWACHAGUA WAZALENDO!
NINGEPENDELEA HOJA YA MGOMBEA BINAFSI IPEWE KIPAUMBELE AMA ULE MUUNGANO ALIOUTANGAZA MTIKILA AMBAO UNADHAMIRIA KUFUNGUA KESI YA EPA!
HAO NDIO WA KUSIKILIZWA! NA SI MAMBO YA VYAMA!
 
Health people sleep for how many hours? beware of JF addiction and take take of ur mental health
 
TATIZO NI KUNA MAMLUKI KUTOKA BOTH ccm na chadema wanaovuruga mijadala ya upinzania kwa maslahi yao binafsi!
Wananchi kama mnataka tuwatajie nani ni safi na nani si safi tutafanya hivyo!
maana hapa kuna vita kati ya watu binafsi ndani ya vyama vyao!
HAKUNA ATAKAYE CHAGUA VYAMA...WANANCHI WATAWACHAGUA WAZALENDO!
NINGEPENDELEA HOJA YA MGOMBEA BINAFSI IPEWE KIPAUMBELE AMA ULE MUUNGANO ALIOUTANGAZA MTIKILA AMBAO UNADHAMIRIA KUFUNGUA KESI YA EPA!
HAO NDIO WA KUSIKILIZWA! NA SI MAMBO YA VYAMA!

Mushi jaribu kupanga vizuri maandishi ya aya zako unazoandika,inakatika mtu tamaa kusoma kilichoandikwa..
 
Ndugu zangu kwasababu nimeshaisoma ripoti ya EPA...Basi pia nitahitaji ushirikiano wa wale wazalendo.

Mimi nitaleta majina ya makampuni na vyeo vya wale walioidhinisha uoza huo na Wananchi wengine mlioko Tanzania naomba muweke majina ya hao waliokuwa na vyeo hivyo wakati scandal hiyo...Kwa mfano DDDD,DF,NK.

Watu kama kina MGONJA NA MWENGINEO TAYARI TUNAJUWA VYEO VYAO.

Ila kuna watu kama hao DF,DDD, na wengineo ambao nitahitaji msaada wenu.

Hivyo basi sasa hivi najiandaa kutaja watu wote walioguswa na ripoti hizo ili mjadala sasa uwe ni UFISADI NA SI UKABILA NA UDINI!

Mijadala ambayo inatufanya tudharaulike na wananchi na pia kushangazwa kwa wananchi na namna ambavyo issue ya UFISADI Iliyokuwa ikipigwa sana vita hapa jf imepoteza mwelekeo na kuwa udini na ukabila!

Sasa kama kweli jf ni chombo huru...Kwanini wengine haturuhusiwi kuzipinga hoja hizo zinazopewa kipaumbele na mafisadi kwa hali na mali ili vita vitokee na wao wapone na kukimbia nchi kwenda ughaibuni huku wananchi wakifa kwa kuuwana?

Nani hajui kama vita ya ukabila na udini ikianza hata hao walioianzisha hawatakuwa na tabu kwani PESA ZOTE WANAZO NA WANAWEZA KUISHI POPOTE DUNIANI?

Wananchi msikubali kuuwana wenyewe kwa wenyewe kwa chuki za mafisadi wanaotumia pesa nyingi kupanda mbegu mbaya ya machafuko ili tu wao wapone!

Msikubali kabisa! ADUI YENU SI KILA MCHAGGA WA KILA MUISLAM NA PIA SI KILA MKRISTO!

Mkizingatia HOJA YA UFISADI BASI MTAPONA NA KUPATA UHURU WENU NA KUTAJIRIKA! KAMWE MSIKUBALI KUCHUKIANA WENYEWE KWA WENYEWE NA KUANZA KUPIGANA KAMA WANAVYOTAKA ccm NA BAADHI YA chadema!

Mwenye macho na aone...Na MWENYE MASIKIO NA ASIKIE!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom