Fatuma alimtazama Eric,,kwa muda mrefu,,alikumbuka mengi waliyopitia.Alikumbuka mara ya kwanza walipokutana na Eric..jinsi Eric alivyokuwa mpole,msikivu na mtulivu sana.Fatuma alikumbuka zaidi siku ya arusi yao,kila kitu kilionekana safi,salama na chenye matumaini.Kweli walipendana sana!
::
Fatuma alikuwa ni mwanamke mwenye akili sana.Aliweza kujadili mambo kwa busara sana.Eric aliona fahari sana kumtambulisha kwa rafiki zake.Lakini sasa mambo yanaonekana yamebadilika.Eric hafurahii tena.Hata Fatuma anapotoa maoni au shauri,Eric anajibu tu.."Je,unataka kunifundisha! Jali kazi yako!.."
::
Fatuma hakupenda ndoa yao yenye mwaka mmoja tu ikose mawasiliano.Alifikiri kwa muda,aliona kuwa madam wote wanapata mshahara mzuri,,basi wajadili juu ya matumizi ya hela yao,kwani pesa ilikuwa inatoka upesi zaidi nyumbani kuliko ilivyoingia.
::
Usiku mmoja baada ya chakula cha jioni,Fatuma alimfuata Eric akamwambia "Mume wangu,unaonaje kama tutapanga namna ya kutumia fedha tunazopokea sote wawili,ili tuweke akiba ya kutusaidia baadaye?"...Bila kuinua macho kwenye laptop yake,Eric alijibu "..Kwa nini unajiingiza katika mambo ya fedha? Shughulika na jiko lako,hiyo inatosha.Ni nani mkubwa hapa ndani?.."
::
Fatuma hakupendezwa na jibu hilo,hakusema zaidi.Alijiona ameachwa nje ya uamuzi uliowahusu wote wawili.Mwezi ulipita na Eric alikuja amenunua Kamera.Fatuma hakufurahi,aliamua kusema "Mume wangu,kamera ni yako,lakini hukukumbuka hatuna kitanda kwenye chumba cha wageni,hatuna mapazia sebuleni naona aibu wageni wakija,inaonekana sijui kutunza nyumba?"..Eric alimkata kauli Fatuma,akamjibu kwa ghadhabu "Unaanza tena kunifundisha! Kutunza nyumba,mimi ndie kichwa cha familia sio we mwanamke! Ni nani mkubwa ndani?"
::
Fatuma aliumia.Aliona hana nafasi katika nyumba ambayo alidhani ni yao wote.Alijua namba ya siri ya akaunti zao.Alijisemea "ntaenda kwa rafiki zangu,ntanunua nguo,ntapitia club nikajirushe,nile vizuri hotelini,,Eric atajifunza kwamba KAMA yeye ni mkubwa basi SI mkubwa wake Fatuma"
Naam,,Eric aliwaza "KUNIFUNZA MIMI,MWANAMKE?" Fatuma aliwaza "NANI MKUBWA?"
=
Ndugu wana Jf nani mkubwa katika nyumba hii?
::
Fatuma alikuwa ni mwanamke mwenye akili sana.Aliweza kujadili mambo kwa busara sana.Eric aliona fahari sana kumtambulisha kwa rafiki zake.Lakini sasa mambo yanaonekana yamebadilika.Eric hafurahii tena.Hata Fatuma anapotoa maoni au shauri,Eric anajibu tu.."Je,unataka kunifundisha! Jali kazi yako!.."
::
Fatuma hakupenda ndoa yao yenye mwaka mmoja tu ikose mawasiliano.Alifikiri kwa muda,aliona kuwa madam wote wanapata mshahara mzuri,,basi wajadili juu ya matumizi ya hela yao,kwani pesa ilikuwa inatoka upesi zaidi nyumbani kuliko ilivyoingia.
::
Usiku mmoja baada ya chakula cha jioni,Fatuma alimfuata Eric akamwambia "Mume wangu,unaonaje kama tutapanga namna ya kutumia fedha tunazopokea sote wawili,ili tuweke akiba ya kutusaidia baadaye?"...Bila kuinua macho kwenye laptop yake,Eric alijibu "..Kwa nini unajiingiza katika mambo ya fedha? Shughulika na jiko lako,hiyo inatosha.Ni nani mkubwa hapa ndani?.."
::
Fatuma hakupendezwa na jibu hilo,hakusema zaidi.Alijiona ameachwa nje ya uamuzi uliowahusu wote wawili.Mwezi ulipita na Eric alikuja amenunua Kamera.Fatuma hakufurahi,aliamua kusema "Mume wangu,kamera ni yako,lakini hukukumbuka hatuna kitanda kwenye chumba cha wageni,hatuna mapazia sebuleni naona aibu wageni wakija,inaonekana sijui kutunza nyumba?"..Eric alimkata kauli Fatuma,akamjibu kwa ghadhabu "Unaanza tena kunifundisha! Kutunza nyumba,mimi ndie kichwa cha familia sio we mwanamke! Ni nani mkubwa ndani?"
::
Fatuma aliumia.Aliona hana nafasi katika nyumba ambayo alidhani ni yao wote.Alijua namba ya siri ya akaunti zao.Alijisemea "ntaenda kwa rafiki zangu,ntanunua nguo,ntapitia club nikajirushe,nile vizuri hotelini,,Eric atajifunza kwamba KAMA yeye ni mkubwa basi SI mkubwa wake Fatuma"
Naam,,Eric aliwaza "KUNIFUNZA MIMI,MWANAMKE?" Fatuma aliwaza "NANI MKUBWA?"
=
Ndugu wana Jf nani mkubwa katika nyumba hii?