Nani mkali Ally Kamwe vs George Ambangile?

Fohadi

JF-Expert Member
Jul 24, 2020
770
2,408
Vijana wawili wanaokuja juu katika sekta ya uchambuzi wa soka nchini. Wote wamebahatika na wanafanya kazi katika taasisi ambazo ni miongoni mwa brand kubwa ukizungumzia nyanja ya michezo na habari kwa ujumla hapa nchini. Napenda sana kuwasoma na kuwasikiliza lakini hadi leo sijaweza kuwatofautisha na kugundua nani anajua zaidi ya mwenzie.

Je, yupi ni mkali zaidi ya mwenzake. Ningependa hoja na facts zitawale katika mjadala huu.​
 
Vijana wawili wanaokuja juu katika sekta ya uchambuzi wa soka nchini. Wote wamebahatika na wanafanya kazi katika taasisi ambazo ni miongoni mwa brand kubwa ukizungumzia nyanja ya michezo na habari kwa ujumla hapa nchini. Napenda sana kuwasoma na kuwasikiliza lakini hadi leo sijaweza kuwatofautisha na kugundua nani anajua zaidi ya mwenzie...​
Too private and also too personal, wasifie kwenye page zao ndio inafaa zaidi
 
Si mfuatiliaji saana wa hawa wachambuzi wetu uchwara, wachambuzi wa mchele..

Kila mmoja nimebahatika kutembelea page yake.

George anajua zaidi ya ally.

Ally anajua jua, ila anajiona anajua saana, mjivuni mjivuni.. Kuna makala moja mwanaspoti ile ya zamani edo kumwembe alikuwa anaandika vizuri sana, ally anatembea mule mule.
 
Ambangile mkali ingawa Ali kamwe na yeye yupo vizuri ila kwa sasa Ambangile yupo juu zaidi, halafu akichambua mapenzi yake na team anayoshabikia anayeka pembeni.
anashabikia timu gani huyu jamaa ndani na nje?
 
Ally Kamwe yupo vizuri zaidi,, George ubishi ubishi mwingi mpk anaboa
 
Kwanza George mpira anaujua. Anajua siasa ya mpira..anajua tactics za mpira. Anajua viongozi wa FIFA, CAF, TFF wa vilabu vya bongo mpaka ulaya.

Jamaa ametimia kila idara,ni full package, hakuna mchambuzi anayejulikana anamuweza George kwa sasa...Ally anajitahidi sana tu ila Ambangile ni maji marefu sana.
 
Back
Top Bottom