Nani mkali Ally Kamwe vs George Ambangile?

tofauti na miaka ya zamani, hii kazi ya uchambuzi inachukuliwa userious zaidi kwenye kizazi hiki cha ukusanyaji wa takwimu kupitia pembe tofauti kwa kuangalia zaidi eneo la analysis na research.

dunia ya sasa mashabiki wanaojielewa hawahitaji kuhadithiwa na mchambuzi jinsi gani goli limefungwa bali wanachohitaji ni kudadavuliwa jinsi goli lilivyoanza kutengenezwa mpaka kufungwa kwake, jinsi timu X inavyocheza, kwa nini mchezaji yule amecheza vizuri na mwengine hakucheza vizuri, upi udhaifu wa timu X, kwa nini mlinzi yule ananusa harufu au mikimbio ya timu pinzani na mengineo yote yanayorekodiwa kwenye mitandao inayohusika na takwimu za kimpira.

hivyo wachambuzi aina ya george ambangile na wengineo wenye sifa hii huu ndio muda wao wa kuvuna mashabiki lukuki kupitia maeneo tofauti kwa sababu wanakupa kile ambacho wewe kama mshabiki/mtazamaji wa mechi umekikosa licha ya kujaaliwa macho mawili kama George.

sijawahi kumsikiliza au kumsoma huyo bwana Ally, kama atakuwa na sifa mfano wa hizo basi ni sahihi kumweka pamoja na george ila kama itakuwa ni kinyume chake kwa dunia hii haitokuwa sahihi kumlinganisha na george.

kwa sababu george ameshavuka kwenye dunia ya usimuliaji wa soka kama anavyofanya edo kumwembe, shaffih dauda na wachambuzi wengineo waliojijengea heshima tokea zamani ila wakashindwa kujiendeleza.

ila usisahau unaweza kuwa mchambuzi hodari wa mechi lakini ukawa kocha mbovu ndani ya touchline zinazopatikana uwanjani, mfano gary neville
 
Hao wote bado sana kwa shaffih dauda, hata page zao tu zinadhihirisha walivyo wachanga kwa shaffih dauda.

Kuna mmojawao hapo huwa anapenda sana kujiselfie na kujipost akiwa peke yake, na akiwa na mdada flani ivi,, wewe ni pundit hupaswi kuwa hivyo, shaffih huo ujinga hana.
 
Hao wote bado sana kwa shaffih dauda, hata page zao tu zinadhihirisha walivyo wachanga kwa shaffih dauda.

Kuna mmojawao hapo huwa anapenda sana kujiselfie na kujipost akiwa peke yake, na akiwa na mdada flani ivi,, wewe ni pundit hupaswi kuwa hivyo, shaffih huo ujinga hana.
Dauda ni msimuliaji wa histroria za mpira siyo mchambuzi wa mpira.
Hata wewe unaweza kusoma historia ukameza na kuja kusimulia hapa.
Ambangile anachambua mpira siyo kusimulia.
 
Kwanza George mpira anaujua. Anajua siasa ya mpira..anajua tactics za mpira. Anajua viongozi wa FIFA, CAF, TFF wa vilabu vya bongo mpaka ulaya.

Jamaa ametimia kila idara,ni full package, hakuna mchambuzi anayejulikana anamuweza George kwa sasa...Ally anajitahidi sana tu ila Ambangile ni maji marefu sana.
Umeshamsikiliza Jef reya ile ni google iliyo kichwani.
 
Hiki kitu watu wengi hawakijui...hongera kwa kutambua hilo.
Ndo hivyo mkuu watu wanasimulia mara goli Kali lilifungwa na mchezaji fulani na timu fulani ikaibuka kidedea sisi tunataka uchambue kwanini lile goli limefungwa?, Je mfungaji ametumia mbinu gani? Je aliyetoa fainal pass kwanini alimpa yule afunge? kwanini asingefunga yeye? Formation iliyotumika kupata hilo goli ni ipi?​
 
Ndo hivyo mkuu watu wanasimulia mara goli Kali lilifungwa na mchezaji fulani na timu fulani ikaibuka kidedea sisi tunataka uchambue kwanini lile goli limefungwa?, Je mfungaji ametumia mbinu gani? Je aliyetoa fainal pass kwanini alimpa yule afunge? kwanini asingefunga yeye? Formation iliyotumika kupata hilo goli ni ipi?​
Kabisa mkuu
 
Hao wote bado sana kwa shaffih dauda, hata page zao tu zinadhihirisha walivyo wachanga kwa shaffih dauda.

Kuna mmojawao hapo huwa anapenda sana kujiselfie na kujipost akiwa peke yake, na akiwa na mdada flani ivi,, wewe ni pundit hupaswi kuwa hivyo, shaffih huo ujinga hana.
Shaffih ndo mchambuzi wa kwanza kuanza kumsikiliza na kumkubali enzi nipo sec nilikua sipati usingizi mpk nisikilize michezo ya clouds,kiukweli nimesikiliza wachambuzi wengi wa ila baada ya kumsikiliza Geogre Ambangile ndo nimegundua wale wengine walikua wanatusimulia tu matokeo ya mechi na sio kuchambua mechi.Ambangile ni mchambuzi bora kwasasa hizo page zao zisikutishe wengine wapo muda mrefu kwenye uchambuzi tangu vipindi vya michezo havijaanza kuwa na ushindani mkubwa kama hivi sasa kwanza naamini kipindi Shaffih anaanza uchambuzi Ambangile alikua yupo shule huko anasoma.
 
Hao wote bado sana kwa shaffih dauda, hata page zao tu zinadhihirisha walivyo wachanga kwa shaffih dauda.

Kuna mmojawao hapo huwa anapenda sana kujiselfie na kujipost akiwa peke yake, na akiwa na mdada flani ivi,, wewe ni pundit hupaswi kuwa hivyo, shaffih huo ujinga hana.

Unapotoka
 
Nimejipanga kuandika makala juu ya wachumbuzi wetu wakiwemo hao. Nafikiri itawasaidia kubadilika ila kuna mapungufu mengi na unfortunately ni kama hakuna wa kuwaeleza ukweli.
 
George anaonekana bora zaidi sababu ya pamoja ya ujuzi wake lakini hajikwezi tofauti na Ally ambaye hadi macho yake yanaonesha over confidence. Hili tatizo la Ally analo pia George Job, too much know hadi uongeaji wake!

Wajifunze kwa kipenzi cha watu Dr Ricky ambaye huongea kwa unyenyekevu mkubwa huku akishusha madini mazito! Huhitaji kuvimba tukuone unajua, maneno yako ni ujumbe tosha. Body language si kitu cha kupuuza maana watu ndio wanatumia kama kioo kwako.
 
tofauti na miaka ya zamani, hii kazi ya uchambuzi inachukuliwa userious zaidi kwenye kizazi hiki cha ukusanyaji wa takwimu kupitia pembe tofauti kwa kuangalia zaidi eneo la analysis na research.

dunia ya sasa mashabiki wanaojielewa hawahitaji kuhadithiwa na mchambuzi jinsi gani goli limefungwa bali wanachohitaji ni kudadavuliwa jinsi goli lilivyoanza kutengenezwa mpaka kufungwa kwake, jinsi timu X inavyocheza, kwa nini mchezaji yule amecheza vizuri na mwengine hakucheza vizuri, upi udhaifu wa timu X, kwa nini mlinzi yule ananusa harufu au mikimbio ya timu pinzani na mengineo yote yanayorekodiwa kwenye mitandao inayohusika na takwimu za kimpira.

hivyo wachambuzi aina ya george ambangile na wengineo wenye sifa hii huu ndio muda wao wa kuvuna mashabiki lukuki kupitia maeneo tofauti kwa sababu wanakupa kile ambacho wewe kama mshabiki/mtazamaji wa mechi umekikosa licha ya kujaaliwa macho mawili kama George.

sijawahi kumsikiliza au kumsoma huyo bwana Ally, kama atakuwa na sifa mfano wa hizo basi ni sahihi kumweka pamoja na george ila kama itakuwa ni kinyume chake kwa dunia hii haitokuwa sahihi kumlinganisha na george.

kwa sababu george ameshavuka kwenye dunia ya usimuliaji wa soka kama anavyofanya edo kumwembe, shaffih dauda na wachambuzi wengineo waliojijengea heshima tokea zamani ila wakashindwa kujiendeleza.

ila usisahau unaweza kuwa mchambuzi hodari wa mechi lakini ukawa kocha mbovu ndani ya touchline zinazopatikana uwanjani, mfano gary neville

Thank you for this post.
 
Back
Top Bottom