Taarifasahihi
Senior Member
- May 24, 2019
- 170
- 157
Makamu wa kwanza wa Raisi wa SMZ kwa mujibu wa katiba, ni Lazima atoke chama kingine, kilichoshika nafasi ya pili kwenye uchaguzi mkuu. NI LAZIMA. ndiyo maaana awamu ya pili ya Mh Sheni hapakuwa na Makamo wa Kwanza kwa vile CUF (Chama kilichokuwa kimeshika nafasi ya pili) iligoma kuutambua uchaguzi na matokeo yake.Twende kikatiba zaidi...
Katiba ya zanzibar ya mwaka 1984 na mabadiliko yake toleo la 2010 .
Ibara ya 40 ,Ibara ndogo ya kwanza(i) inasema,
40.(1) Endapo nafasi ya Makamo wa Kwanza wa Rais au Makamo
wa Pili wa Rais itakuwa wazi:
(a) kwa sababu ya kufariki au kujiuzulu; au
(b) ikiwa Rais amefuta uteuzi huo; au
(c) kwa sababu nyengine yoyote itakayomfanya ashindwe
kuwa na sifa za Makamo wa Kwanza wa Rais au
Makamo wa Pili wa Rais;
Rais atamteua Makamo wa Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa
Rais kutegemeana na nafasi iliyo wazi.
Hivyo utaratibu unarudi kama awali alivyoteuliwa maalim seif.
Kuhusu nani ata fit kuwa makamu wa kwanza hilo tuwe na subira msiba uishe.
Hivyo Makamo wa kwanza hawezi kuteuliwa na Raisi wa Zanzibar bali chama (ACT) kwa maana ya mwaka huu, ndio wanaotakiwa kuteua jina la mtu anayefaa kuwa makamo wa kwanza, Rais wa Znz anamwapisha tu, wala hamteui, ila anateua makamo wa pili.
Tuelewane vizuri hapo, Rais wa Zanzibar hawezi kuteua Makamo wa Kwanza wa Rais, ACT wasipopeleka jina, nafasi itabaki wazi siku zote.