Elections 2010 Nani kuukwaa uwaziri mkuu?

Status
Not open for further replies.
Okoa muda wako............Waziri Mkuu atakuwa yuleyule Pinda Mizengo Peter..............JK siyo mtu wa mageuzi.............
 
Habari kutoka Dodoma zinasema kuwa kati ya Tibaijuka na Magufuli mmojawapo atateuliwa kuwa Waziri Mkuu. Awali kulikuwa na candidates watatu mezani kwa Kikwete; akiwemo Mwandosya, ambaye sasa jina lake limeondolewa.
Akitambua bayana kuwa serikali yake haina haiba wala mvuto wa kutosha kuungwa mkono na wananchi, Kikwete amesema anataka waziri Mkuu "kukuru-kakara" atakayeweza kuburuza hybrid policy katika kilimo, viwanda (manufacturing) kwa ajili ya kuleta impact katika ajira. Huu ni mkakati wa ku-mobilize vijana amabo wanaonekana kuitupa mkono CCM, hasa kutokana na uzoefu wa CCm kutoungwa mkono na vijana wengi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010.
Nwasilisha. Tuendelee kutega masikio yetu.

JK hata ukimpatia Obama kama PM wake hataweza kumsaidia. Kwa hiyo I really don't care nani atakuwa PM kwa sababu tuna miaka mingine 5 ya kupoteza bure!
 
Hapo kati ya hayo majina mawili ukinipa niotoe uamuzi moja kwa moja nitakwambia ni Magufuli. Mimi ninashagazwa sana wanaomshabikia Tibaijuka. Je kuna political history yoyote inayomwonyesha mama huyu kuwa ni wa shoka kama wengine mnavyodiriki kumtukuza. Wengi tu wamefanya kazi katia mashirika makubwa, wengi tu ni maprofesa lakini wakishaingia humo ndani ya baraza ndio inakuwa hoi na vituko.

So far mama huyu hajaifanyia tanzania chochote kwa kupitia kale kacheo kake. Labda waje na hoja ya kijinga ya 'mwanamke' tena
 
yetu macho tu ngoja tusubiri tujionee watakavyofanya tena,maana maamuzi yao huwa si ya kutabilika sana :bowl::bowl::bowl::bowl:
 
Mtembezi katika tembea tembea yangu kama ilvyo ada nimefanikiwa kunusa KIGOGO mmoja aliyekaribu na IKULU anadai jina la waziri mkuu mpya ni SHAMSI VUAI NAHODHA wana jamvi mpo?
 
mmmh kwa sasa niko:doh::tape::bowl:,nchi yangu inazidi kunichanganya
 
Hawezi kuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania maana haijui Tanganyika ikoje. Lakini sishangai kama watamweka maana CCM na JK wote lao moja kuhaikisha mafisadi wanang'aa.
 
No tatizo lazima awe "mkristu" ili kubalansi pale juu.

Kwa hiyo sio kweli ... god forbid.
 
Hivi Mzanzibari anaweza kuwa PM wa JMT? Samahani kwa kuuliza hivi.
Suala la udini vipi kwenye nafasi hii maana Kingunge aliwahi kumconfront BWM mwaka 2005 kuwa sasa ni "zamu ya Waislamu"?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom