Nani Kichaa Zaidi

Sam GM

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
535
28
Katika matukio ya siku hizi mbili zilizopita kuna kitu ambacho kila nikikisikia na kukifikiria naona kama vile sielewi vizuri labda wenye upeo zaidi watusaidie kuelewa. Huyu mtanzania mgonjwa wa akili alikuwa kalazwa Muhimbili, basi kichaa chake kikamtuma achukue stand ya kutundikia maji yanayoongezwa kwa wagonjwa, basi akaitumia hiyo stand kuwapiga wagonjwa wengine, wawili kwa bahati mbaya wakafariki papo hapo na wengine wanne wakachukuliwa kwa matibabu zaidi pamoja na upasuaji.

Katika Maendeleo ya tukio hili, mgonjwa huyu wa akili kapelekwa mahakamani na kashitakiwa kwa kesi za mauaji. Kwa utaratibu wa kawaida na katika sheria za utetezi (sanity) au kuwa na ugonjwa wa akili ni tetezi moja wapo inayotumika sana kuwatetea hata walio na akili na wakaachiliwa huru. Watanzania na akili zetu tena professionals kama huyu hakimu aliyeisoma na kusikiliza kesi, waziri wa afya aliyekimbilia kuteua tume ya kuchunguza hili jambo na huyu kichaa aliyefanya haya yote, ni nani mwenye ukichaa zaidi hapa?

Source: bbcswahili.com/08/14/08
 
Kuna yeyete mwenye taarifa kesi ya kichaa wa muhimbili imeisha vipi??
 
sijasikia lolote, na wala fidia kwayule aliyeumizwa sijui kama atalipwa. Lakini kwa uzoefu wangu kidogo nillionao najua kila chumba cha wagonjwa WARD kinakuwa na incharge na anatakiwa awepo muda wote akiwa duty, je kwa hizo ward za vichaa haiwi hivyo????? kama ndio alikuwa wapi hadi yote hayo yanatokea? na adhabu yake je imewahi kusikika popote? kama yupo aliyesikia aniambie jamani
 
sijasikia lolote, na wala fidia kwayule aliyeumizwa sijui kama atalipwa. Lakini kwa uzoefu wangu kidogo nillionao najua kila chumba cha wagonjwa WARD kinakuwa na incharge na anatakiwa awepo muda wote akiwa duty, je kwa hizo ward za vichaa haiwi hivyo????? kama ndio alikuwa wapi hadi yote hayo yanatokea? na adhabu yake je imewahi kusikika popote? kama yupo aliyesikia aniambie jamani

Wakwetu,

Tuvute subira kidogo may be tutapata taarifa, ila inasikitisha kama mgonjwa anaweza kuuwa hadi watu wanne wasimamizi sijui wanakuwa wapi, pia ukiangalia nature ya kesi ni kuwa jamaa kweli hakuwa anajua anachokifanya, kupelekwa mahakamani na kushitakiwa imekaa kushoto kidogo kwangu. Nafikiri ni mambo ya sheria wengine sio fani kabisa!
 
Mgonjwa wa akili kushitakiwa ni utaratibu wa haki wa sheria, ni lazima mahakama imuone hana hatia bila shaka yoyote, baada ya kujiridhisha kuwa ni kweli kuwa ni mgonjwa wa akili, wataalamu watatoa ushahidi wao ili mahakama iweze kutoa maamuzi, kumtia au kutomtia hatiani, kwa sababu si wote wanaolazwa ktk wodi ya vichaa ni kweli vichaa, wengine wanaingizwa huko kimakosa au wakisubiri hatima ya uchunguzi, na inatokea mtu kuwekwa huko kwa kubambikizwa ugonjwa wa akili.hakuna anayejua kilichotokea, kuna uwezekano wa yeye kuwa alikuwa anajibu mashambulizi ya vichaa waliomshambulia wakati yeye akiwa SANE, ktk kujihami na kujiokoa ilimbidi afanye hivyo, hapo inakuja verdict ya mansloughter vs Mauaji ya makusudi, huo ni ufahamu wangu mdogo , labda wanasheria watusaidie.
 
Back
Top Bottom