Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,055
- 10,723
Katika kumbukumbu zangu tangu matumizi ya umeme kwa mfumo wa Luku yaanzishwe nchini sijawahi kusikia huduma hii kukosekana kwa siku tatu mfululizo kama ilivyokuwa kuanzia Agosti 29-2011.
Hii tarehe ilikuwa ni siku ya kuangalia mwezi baada ya mfungo wa Ramadhani 1432.Siku ya pili yake ilikuwa ni Iddi mosi kwa baadhi ya waislamu.
Matayarisho ya sikukuu hii hayakwenda vizuri kwa familia nyingi za waislamu.Msemaji wa Tanesco bi Badra Masoud alisema kulikuwa na tatizo la kiufundi na mafundi walikuwa wakiendelea na matengenezo hata hivyo maelezo yaliishia hapo tu.
Kwanini tatizo hili lilitokea msimu wa Iddi na kipi kilitokea hata mitambo hiyo ikashindwa kufanya kazi.
Jee haiwezekani kwamba ni visa vya kisiasa vilivyokusudiwa kuleta malalamiko na kuleta vurugu katika jamii?.
Hii tarehe ilikuwa ni siku ya kuangalia mwezi baada ya mfungo wa Ramadhani 1432.Siku ya pili yake ilikuwa ni Iddi mosi kwa baadhi ya waislamu.
Matayarisho ya sikukuu hii hayakwenda vizuri kwa familia nyingi za waislamu.Msemaji wa Tanesco bi Badra Masoud alisema kulikuwa na tatizo la kiufundi na mafundi walikuwa wakiendelea na matengenezo hata hivyo maelezo yaliishia hapo tu.
Kwanini tatizo hili lilitokea msimu wa Iddi na kipi kilitokea hata mitambo hiyo ikashindwa kufanya kazi.
Jee haiwezekani kwamba ni visa vya kisiasa vilivyokusudiwa kuleta malalamiko na kuleta vurugu katika jamii?.