Arafat
JF-Expert Member
- Nov 17, 2009
- 2,581
- 758
Jamani, nchni inaenda wapi? Petrol Bei bado ipo juu zaidi, Umeme bei juu na haupo, Kodi zote zimepanda ya Duka ndio husiseme, Kodi ya nyumba inazidi Mishahara, mchele na nyama bei yake ni zaidi robo ya mshahara wa kima cha chini, starehe sasa wanafanya RA, JK, Chenge na EL na watoto wao peke yao, Serikali inategemea bia kupata kodi wakati Quaran na Biblia hairuhusu kunywa pombe, Msikitini na Kanisani sadaka imepandishwa hawataki silver wanataka noti lasivyo watanamwita EL na RA kuzindua kanda na kufungua majendo ya ibada, mahari ndio husijaribu manaa wana hasira ya mwanao kufukuzwa shule kwa ajili ya ada,rate ya dola haishikiki, school fee utadhani unanunua majengo ya shule, Polisi wana uwa raia kama panzi sasa hii ni maisha bora kwa kila Mtanzania jamani au ni maisha bora kwa Kikwete na familia yake! Jamani huyu Bwana kashindwa kadorora kazeeka akili tuingie mtaani kudai nchni yetu imetekwa.