Nani kachora Nembo ya Taifa kati ya Ngosha, Kabati au Farahani?

Kanyunyu

JF-Expert Member
May 2, 2012
335
495
Nani Kachora Nembo ya Taifa: Mzee Farahani (Farhan), Ngosha, au Jeremiah Wisdom Kabati?

Kuna wanaosema Mzee Jeremiah Wisdom Kabati kachora nembo ya Taifa. Wengine wanasema Mzee Ngosha kachora. Kwa sasa mimi nipo upande wa Professor Elias Jengo anayesema nembo ilichorwa na Mzee Abdallah Farahani kutoka Zanzibar. Professor Jengo aliandika kwenye kitabu kwamba Mzee Farahani ndio aliyechora nembo ya Taifa.

Inasemekana mtoto wa Mzee Farahani, Iddi Farahani alikuwa na sketches za baba yake za hii nembo. Mzee Farahani alisoma na Mwalimu Nyerere Makerere. Professor Elias Jengo kutoka Chuo Kikuu anaandika kwenye kitabu “East Africa Art Biennale” kwamba “As a designer, Abdallah Farahani will be remembered for his design of the national emblem. The emblem was recently criticized by a legislator for depicting barefooted human figures.” Ukurasa 44.

Kaka Dominicus Makukula, msanii na mwalimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anaamini kwamba Mzee Furahani ndio aliyechora ile nembo ya taifa. Anasema mjukuu wa Mzee Farahani yupo Music Academy Zanzibar na pengine anaweza kutoa majibu kama kuna atayeweza kwenda kuongea nae zaidi. Mpaka tutapopata habari zaidi, inaonenaka kwamba Mzee Farahani kutoka Zanzibar ndio aliyechora ile nembo. Tusubiri tuone kama serikali itafuta mavumbi na kufungua maboksi yenye nyaraka husika.

FACT NUMBER 2

Tukiangalia nembo hii ya Tanganyika 1961, ile ya Tanzania 1964 na ule mchoro usio na rangi uliopo katika nyaraka ya National Flag and Coat of Arms Act ya 1971, tunapata nafasi na sababu ya kudhani kuwa mchoraji na mbunifu halisi wa nembo ya Taifa si Ngosha wala marehemu mzee Jeremiah Kabati. Familia ya kabati inasema mzee alichora nembo hiyo mwaka 1960 na katika mahojiano na TBC Taifa, Ngosha alisema kuwa alisanifu nembo hiyo na mwenzake mwaka 1957.

Prof. Jengo anathibitisha kuwa mchoro wa Farahani kwa ajili ya Tanganyika uliandaliwa mwaka 1961 na kuboreshwa 1964 wakati wa maandalizi ya nembo ya Jamhuri ya muungano. Swali la msingi, je yawezekanaje pasiwe na kumbukumbu hali miaka kumi baadae, marehemu Mwl. Nyerere alipatiwa mswada wa sheria ya nembo ya Taifa ileile ya mwaka 1961 pia 1964 (isiyonakshiwa kwa rangi) kwa ajili ya kuisaini ili iwe sheria kamili. Je walioandaa mswada walitoa wapi blue print ya nembo halisi mwaka 1971?

Tatizo si kukosekana kwa nyaraka wala kumbukumbu, bali tatizo ni kukosekana watu wenye weledi kweye eneo la historia ya sanaa katika kuhifadhi amali hizi za Taifa katika mamlaka za kusimamia sanaa na utamaduni wa Taifa. mzee Mbughuni Sr. alifanya kazi kama Promoter of national arts miaka ya 1960s na hatimaye kuwa mkurugenzi wa idara ya sanaa miaka ya 1970s mwishoni, alianzisha Chuo cha Sanaa Bagamoyo mwaka 1981 baada ya kuvunja kikundi cha sanaa cha Taifa mwaka 1979 (Kelly Askew 2005:304-309), hawa ndio aina ya watu tuliowakosa katika miaka hii Tanzania.

Imechukuliwa kutoka bandiko la Azaria Mbughuni

May 26, 2017
 
Watanzania ccm sijui imeturogaje yani kuhusu swala la kumbukumbu hatuna kabisa. Mfano kuna mchezaji kumbukumbu ya kupigwa kadi tatu mpaka leo imekuwa kitendawili? Maisha chini ya serekali ya ccm ni magumu ila siku ya kupiga kura watu watapotezaa kumbukumbu ya njaa wataipa kura ccm tena dah!
 
Tanzania tunatia aibu kila kitu kwetu ni tatizo.

Hata kumbukumbu muhimu kama hizi hatuna.
 
Sasa hivi babu anaenjoy matibabu bure toka kwa serikali. Sishangai serikali kutokuwa na kumbu kumbu kwani hata hati ya Muungano haijulikani ilipo
Ilipotolewa kwenye bunge la katiba ulikuwa kuzimu. Sijui nalijibu litoto? Ngoja nisubiri majibu huenda yatakuwa ya kikubwa.
 
Manikia ya nembo inaaslimia ngapi ya dhahabu
Maana iyo nembo haieleweki kama mchanga wa buzwagi
 
Nani Kachora Nembo ya Taifa: Mzee Farahani (Farhan), Ngosha, au Jeremiah Wisdom Kabati?

Kuna wanaosema Mzee Jeremiah Wisdom Kabati kachora nembo ya Taifa. Wengine wanasema Mzee Ngosha kachora. Kwa sasa mimi nipo upande wa Professor Elias Jengo anayesema nembo ilichorwa na Mzee Abdallah Farahani kutoka Zanzibar. Professor Jengo aliandika kwenye kitabu kwamba Mzee Farahani ndio aliyechora nembo ya Taifa. Inasemekana mtoto wa Mzee Farahani, Iddi Farahani alikuwa na sketches za baba yake za hii nembo. Mzee Farahani alisoma na Mwalimu Nyerere Makerere. Professor Elias Jengo kutoka Chuo Kikuu anaandika kwenye kitabu “East Africa Art Biennale” kwamba “As a designer, Abdallah Farahani will be remembered for his design of the national emblem. The emblem was recently criticized by a legislator for depicting barefooted human figures.” Ukurasa 44. Kaka Dominicus Makukula, msanii na mwalimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anaamini kwamba Mzee Furahani ndio aliyechora ile nembo ya taifa. Anasema mjukuu wa Mzee Farahani yupo Music Academy Zanzibar na pengine anaweza kutoa majibu kama kuna atayeweza kwenda kuongea nae zaidi. Mpaka tutapopata habari zaidi, inaonenaka kwamba Mzee Farahani kutoka Zanzibar ndio aliyechora ile nembo. Tusubiri tuone kama serikali itafuta mavumbi na kufungua maboksi yenye nyaraka husika.

FACT NUMBER 2

Tukiangalia nembo hii ya Tanganyika 1961, ile ya Tanzania 1964 na ule mchoro usio na rangi uliopo katika nyaraka ya National Flag and Coat of Arms Act ya 1971, tunapata nafasi na sababu ya kudhani kuwa mchoraji na mbunifu halisi wa nembo ya Taifa si Ngosha wala marehemu mzee Jeremiah Kabati. Familia ya kabati inasema mzee alichora nembo hiyo mwaka 1960 na katika mahojiano na TBC Taifa, Ngosha alisema kuwa alisanifu nembo hiyo na mwenzake mwaka 1957. Prof. Jengo anathibitisha kuwa mchoro wa Farahani kwa ajili ya Tanganyika uliandaliwa mwaka 1961 na kuboreshwa 1964 wakati wa maandalizi ya nembo ya Jamhuri ya muungano. Swali la msingi, je yawezekanaje pasiwe na kumbukumbu hali miaka kumi baadae, marehemu Mwl. Nyerere alipatiwa mswada wa sheria ya nembo ya Taifa ileile ya mwaka 1961 pia 1964 (isiyonakshiwa kwa rangi) kwa ajili ya kuisaini ili iwe sheria kamili. Je walioandaa mswada walitoa wapi blue print ya nembo halisi mwaka 1971? Tatizo si kukosekana kwa nyaraka wala kumbukumbu, bali tatizo ni kukosekana watu wenye weledi kweye eneo la historia ya sanaa katika kuhifadhi amali hizi za Taifa katika mamlaka za kusimamia sanaa na utamaduni wa Taifa. mzee Mbughuni Sr. alifanya kazi kama Promoter of national arts miaka ya 1960s na hatimaye kuwa mkurugenzi wa idara ya sanaa miaka ya 1970s mwishoni, alianzisha Chuo cha Sanaa Bagamoyo mwaka 1981 baada ya kuvunja kikundi cha sanaa cha Taifa mwaka 1979 (Kelly Askew 2005:304-309), hawa ndio aina ya watu tuliowakosa katika miaka hii Tanzania...
Kwenye hii Mechi Mzee Ngosha ataibuka Kidedea
Kabila litambeba
 
Huyu wa mwaka 1957 yaani Ngosha na Mwenzie wa Tanga ndio wabunifu wa mchoro huo. Hao wengine walionekakana wakiuboresha tu. Si kila kitu alichokifanya Mwal Nyerere kimewekwa kwenye kumbukumbu. Ngosha na Nyerere kukutana hayakuwa makutano ya kiserikali. Ni wazi ilikuwa ni harakati za ukombozi huko kwenye mashamba ya mkonge. Je mwaka huo Nyerere hakufika huko? Je Mzee Ngosha hakuwahi kuwa mchoraji?
 
Huyu wa mwaka 1957 yaani Ngosha na Mwenzie wa Tanga ndio wabunifu wa mchoro huo. Hao wengine walionekakana wakiuboresha tu. Si kila kitu alichokifanya Mwal Nyerere kimewekwa kwenye kumbukumbu. Ngosha na Nyerere kukutana hayakuwa makutano ya kiserikali. Ni wazi ilikuwa ni harakati za ukombozi huko kwenye mashamba ya mkonge. Je mwaka huo Nyerere hakufika huko? Je Mzee Ngosha hakuwahi kuwa mchoraji?
Watz ni roho mbaya daima!! Mzee Ngosha kalamba dume, ukoo wa Kabati unaibuka kutaka kutia vumbi kitumbua cha Mzee Ngosha, mwacheni Mzee ale kuku wakati wake umefika
 
Back
Top Bottom