Nani hasa aliyesababisha Zimbabwe kudorora mpaka kufikia hali hii ya sasa

Uko sahihi sana, ilikuwa ni rahisi sana, ukweli ni kuwa wenye uwezo wa kulima walikuwa ni wazungu, hao waafrika walikuwa ni wakuna ardhi hamna mkulima. Ungewekwa utaratibu mzuri wa mfuko maalum ambao kila mzungu anayemiliki ardhi akatwe kiasi walipwe wanaodai, au hizo pesa zianzishe viwanda na watakaopewa ajira kipaombele ni waliokua wameondolewa kwenye ardhi. Ila mihemko ya viongozi kujifanya wazalendo na kusaka kiki za kisiasa ndio matokeo yake. Je hao wafrika waliporudishiwa hizo ardhi walitoka kwenye umasikini au ndio walirudi rasmi kwenye umasikini wakiwa wanamiliki ardhi?

Kibaya zaidi huyo rais aliyekuwa anajifanya rais mzalendo akaishia kukaa madarakani kwa mrefu tena kwa mbinu chafu kuliko hata hizo za hao wazungu, huku akitumia ardhi alizowapa hao weusi kama kete ya kuendelea kukaa madarakani hata mambo yalipokuwa mabaya. Huu ni mchezo wa viongozi wengi wa kiafrika kujifanya wazalendo huku wakichezea box la kura ili wabaki madarakani. Mchezo huo wa kiongozi kujifanya mzalendo ili akae madarakani kwa kisingizio cha uzalendo uko hata hapa nchini, na tunaona kabisa chaguzi zenye dhuluma na matendo machafu kwa kisingizio cha kuleta maendeleo na uzalendo wa kuigiza.
Wakishindwa na kufirisika akili wanakimbilia kujificha kwenye kivuli cha uzalendo
Wananchi wanaimbiwa pambio za uzalendo kwa kiki wanashangilia huku wanaumia wanasiasa wanazidi kitumbua
Ifike mahala rais asiwe muamuzi wa kila akitakacho ona makinikia yalikoishia hamna kitu zaidi ya hasara sasa hivi wanataka walete malumbano yasiyo na msingi na mabeberu afu tunaumia saizi hakuna condom za jero hospitali dawa za kutafutiza sasa uzalendo njaa hautusaidii
 
Mkuu kwani ardhi ndio inayotoa ajira? Hata ukipewa ardhi kama huna mtaji utafanya nini zaidi ya kugeuka kuwa masikini? Kwa mfano hapa Tanzania wengi wetu wanamiliki ardhi, mbona ndio masikini zaidi? Robo 3 ya watu walioko huku mjini wamekimbia ardhi huko vijijini, sasa hivi wengi wao wanaishi kwenye room za kupanga huku mijini, kama ardhi ni mali hivyo kipi kimewafanya watu waziache huko vijijini na kuja kulundikana huku mijini?
Of course haitoi ajira moja kwa moja lakini ni msingi mkubwa wa ajira hasa pale mnapokuwa na jamii ambayo haina maarifa ya uvumbuzi kama ilivyo kwa waafrika wengi wataponea hapo japo kwa chakula na kukodisha
 
Waafrica kila siku wanalalamikia Mzungu wakati Mzungu alikuja akawatawala wakakataa kutawaliwa akaondoka akaziacha nchi zote huru lakini zote mpaka sasa zimeshindwa kujikwamua kivyovyote vile na bado zinapewa misaada na huyo Mzungu..

China, Singapore, Taiwan, Hong Kong, Malyasia, Indonesia,India, Brazil, Mexico, Australia nk hawa wote walitawaliwa lakini huwasikii wakilia lia zaidi zaidi wanapambana na kustawisha mataifa yao na hata kuwakaribia na kuwazidi hao wazungu..

Kiufupi WaAfrica tunamatatizo tuache blahblah ujinga mwingi tulionao..
 
Waafrica kila siku wanalalamikia Mzungu wakati Mzungu alikuja akawatawala wakakataa kutawaliwa akaondoka akaziacha nchi zote huru lakini zote mpaka sasa zimeshindwa kujikwamua kivyovyote vile na bado zinapewa misaada na huyo Mzungu..

China, Singapore, Taiwan, Hong Kong, Malyasia, Indonesia,India, Brazil, Mexico, Australia nk hawa wote walitawaliwa lakini huwasikii wakilia lia zaidi zaidi wanapambana na kustawisha mataifa yao na hata kuwakaribia na kuwazidi hao wazungu..

Kiufupi WaAfrica tunamatatizo tuache blahblah ujinga mwingi tulionao..
Unajua kitu kiitwacho athari? Walivyoondoka waliacha mapungufu makubwa.
Pili kila kiongozi aliyetaka kuleta mapinduzi ya kweli walumuua ama walim sabotage hivyo hswakutoa uhuru kamili. Kama vile wamarekani weusi wanavyodai malipo ya utumwa japo wazungu waliwauza mababu zao hawapo ila ile legacy bado inawafanya waonekane kama second citizen.

Kuwatetea wazungu ni kutojua historia yako
 
Unajua kitu kiitwacho athari? Walivyoondoka waliacha mapungufu makubwa.
Pili kila kiongozi aliyetaka kuleta mapinduzi ya kweli walumuua ama walim sabotage hivyo hswakutoa uhuru kamili. Kama vile wamarekani weusi wanavyodai malipo ya utumwa japo wazungu waliwauza mababu zao hawapo ila ile legacy bado inawafanya waonekane kama second citizen.

Kuwatetea wazungu ni kutojua historia yako

Hizo nchi nilizokutajia walivyoondoka hawakuacha athari zozote??

Vietnam ilipigwa sana mabomu na USA lakini leo hii inawatu ambao wanaweza hata kuwekeza ulaya na kwingine, Iran imepiga hatua pamoja na kuwa kwenye mizozo na Wazungu kila kukicha toka enzi za mfalme shaha..Brother Japan ilipigwa mabomu ikasambaa lakini leo kila mtu anajua wapi ilipo..

Unataka kuniambia hizo nchi nyingine zilizoendelea hata baada nazo kutoka kutawaliwa hazihujumiwi ila Africa pekee ndio inahujumiwa kila kukicha, Africa ina nini ambacho duniani kwingineko haviko?
 
Kwanini unaniambia nitaje nchi tatu? Unajua tangu Ujerumani ishindwe vita kuu haijawa na siasa za kimataifa kama hao wawili. Switzerland pia hawajatawala watu na wala hawana siasa za nje zinazofanana na hao wawili. Ya tatu tafuta msenyewe. Huwezi kumkemea mwizi wakati wewe ni mwizi utakua unachekesha
😜😜😜😜 Umenikoti mambo ambayo sijayangea mkuu
 
Hahaha hivi kule CHADEMA hawapo enhee?!
Hapa kwetu kila government failure ni CHADEMA kasababiaha, hao ndio denominator.
 
Mbase1970 ,

..kabla hatujafunga mjadala, ningeomba ututajie nchi tatu ambazo zina moral authority ya kukemea ukatili na ukikwaji wa haki unaoendelea hapa Tz.

Cc tindo
Kwanini unaniambia nitaje nchi tatu? Unajua tangu Ujerumani ishindwe vita kuu haijawa na siasa za kimataifa kama hao wawili. Switzerland pia hawajatawala watu na wala hawana siasa za nje zinazofanana na hao wawili. Ya tatu tafuta msenyewe. Huwezi kumkemea mwizi wakati wewe ni mwizi utakua unachekesha
 
Kwanini unaniambia nitaje nchi tatu? Unajua tangu Ujerumani ishindwe vita kuu haijawa na siasa za kimataifa kama hao wawili. Switzerland pia hawajatawala watu na wala hawana siasa za nje zinazofanana na hao wawili. Ya tatu tafuta msenyewe. Huwezi kumkemea mwizi wakati wewe ni mwizi utakua unachekesha

..kwa hiyo Ujerumani na Uswizi wangekemea usingekuwa na tatizo.
 
Back
Top Bottom